Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 31 Oktoba 2017

LISHE BORA KWA WATANZANIA BADO NI TATIZO, ASEMA MH. PETER SERUKAMBA



Na.WAMJW.Dodoma

Taasisi ya Chakula na lishe nchini imetakiwa kujikita katika kutoa elimu kwa umma ili wananchi waweze kujua faida ya kula chakula bora na kuepukana na utapiamlo na udumavu
Hayo yamesemwa na Mwenyeketi wa kamati ya Bunge ya huduma na maendeleo ya jamii  Mhe. Peter Serukamba wakati wa uwasilishaji wa taarifa ya utendaji wa shughuli za taasisi hiyo mjini Dodoma leo.
Mhe.Serukamba alisema bila elimu kwa umma wananchi watakuwa wanatumia fedha nyingi kwa ajili ya matibabu kwa kuwa hali ya udumavu ni mkubwa ,”watu wakiwa na chakula na lishe bora unakuwa na uhakika hutougua hovyo na kupoteza fedha nyingi kwa ajili ya matibabu,lakini wakijua wale mlo gani ambao ni sahihi hii itasaidia kutokomeza kabisa tatizo hili”
Aidha, alisema Tanzania haina tatizo la chakula ila hawafahamu ni mlo gani sahihi wanapaswa kula hivyo kwa kutoa zaidi elimu itakua ni kinga na itasaidia wananchi wasiugue
“Taasisi hii iboreshwe na mkishirikiana na Tamisemi,wakulima na wasafirishaji wa mazao kupitia maofisa maendeleo ya jamii mtawafikia wananchi wengi na hakutokuwa na vizazi vyenye udumavu na matatizo ya akili.
Awali akiwasilisha taarifa ya utendaji wa taasisi hiyo Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto dkt.Faustine Ndugulile alisema zaidi ya asilimia 35 ya vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano nchini vinachangiwa na matatizo ya lishe duni na  katika kipindi cha mwaka 199 hadi 2015/2016 vifo vya watoto vimepungua  kutoka 147 hadi 67 kwa kila vizazi hai 1000.
“Serikali inafanya jitihada kubwa  katika kumjenga mtoto ili akue vizuri kimwili na kiakili kuanzia siku elfu moja za mwanzo za mtoto ambazo ni muhimu kwa makuzi ya mtoto”.
Hata hivyo dkt.Ndugulile alisema hali ya lishe nchini inaendelea kuimarika kutokana na kupungua kwa viwango vya utapiamlo nchini kati ya mwaka 1992 na 2015.
Alisema udumavu (urefu wa umri) umepungua kutoka asilimia 49.7 hadi 34.4 na mikoa inayoongoza ni Rukwa (56%) na Ruvuma (44%) ,kwa upande wa ukondefu (uzito kwa urefu) kutoka asilimia 7.8 hadi 4.5 na mikoa inayoongoza ni Zanzibar-Kusini Pemba na Kaskazini Pemba(9%),Manyara (6.4%),Geita (6.2%),Kigoma (6%) na Morogoro (6.0%)
Kwa upande wa uzito pungufu alisema (uzito kwa umri) kutoka asilimia 25.1 hadi 13.7 na mikoa inayoongoza ni Rukwa (23%),Arusha (20%) pamoja na Kigoma (20%).
Vilevile,mwanamke mmoja kati ya kila wanawake 10 walio katika umri wa kuzaa ana uzito pungufu (underweight) wakati asilimia 18 wana uzito mkubwa (over weight) na asilimia 10 wana kiribatumbo(obesity).Mikoa inayoongoza kwa kiribatumbo ni Zanzibar mjini Magharibi kwa 22%,Unguja Kusini 19%,Dar es Salaam 21%,Kilimanjaro 19% na Tanga 17%.
Naibu Waziri huyo aliahidi kuwa watajipanga katika kutoa elimu ya afya kwa umma na kuwafikia wananchi wengi zaidi “bado Watanzania hawajui kula lishe iliyokamilika na matumizi bora ya chakula.

0 on: "LISHE BORA KWA WATANZANIA BADO NI TATIZO, ASEMA MH. PETER SERUKAMBA"