Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 30 Oktoba 2017

UTAALAMU WA KUPANDIKIZA FIGO UPEWE KIPAUMBELE NCHINI, ASEMA DKT. NDUGULILE





Na WAMJW-DODOMA
UTAALAMU wa huduma ya kupandikiza figo kwa wagonjwa wenye magonjwa hayo upewe kipaumbele hapa nchini ili kuweza kuokoa watanzania wengi wenye matatizo hayo kwa muda mfupi na kupunguza gharama kubwa ya rufaa za kwenda nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uzinduzi wa mkutano wan ne wa chama cha wataalamu wa figo nchini uliofanyika leo mjini Dodoma.
“Serikali imekuwa ikipeleka wastani wa wagonjwa 35  kwa mwaka nje ya nchi ikiwa ni pamoja na India kwa ajili ya kupandikiza figo ambapo inagharimu takribani shilingi milioni 75 hadi 77 kwa mtu mmoja ikiwa ni gharama za malazi na kupandikiza figo” alisema Dkt. Ndugulile.
Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa ikiwa  Tanzania itazalisha wataalamu wengi wa kupandikiza na kusafisha figo itafanikiwa kupunguza gharama hizo na kufanya huduma hiyo ipatikane kwa shilingi milioni 20.3 ikiwa huduma hiyo itapatikana hapa nchini.
Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kuwekeza huduma ya kupandikiza figo Serikali imefunga mashine katika maeneo yafuatayo, UDOM 10, 5Hospitali ya Taifa ya Muhimbili  42, Hospitali ya Rufaa Mbeya 5, Hospitali ya Rufaa Bugando 10, KCMC 10, Hospitali ya Misheni Serian  10, Hospitali ya NSK Arusha 5, TMK 10,Regency 15, Hurbert Kairuki 5, Aga Khan 10 na Access 10 ambapo takwimu zinaonyesha mashine hizi zina uwezo wa kuhudumia wagonjwa 783 kupitia huduma ya NHIF na 391 kwa huduma malipo ya papo kwa papo.
Kwa upande wake Makamu wa Rais wa chama cha Wataalam wa Figo Tanzania Dkt. Paschal Rugajjo amesema kuwa wamepiga hatua kubwa katika kuongeza madaktari wa figo hapa nchini kwani mpaka sasa wapo madaktari 12 kutoka daktari mmoja miaka kumi iliyopita.
Mbali na hayo Dkt. Rugajjo amesema kuwa ushirikiano unahitajika kati ya chama hicho pamoja na Serikali kutoa kipaumbele kwenye elimu juu ya ugonjwa huo ili kuweza kupambana na tatizo hilo kuanzia ngazi ya wananchi mpaka kwenye taasisi za afya nchini.

0 on: "UTAALAMU WA KUPANDIKIZA FIGO UPEWE KIPAUMBELE NCHINI, ASEMA DKT. NDUGULILE"