Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 2 Novemba 2017

BAROZI WA JAPAN NCHINI AFANYA MAZUNGUMZO NA MH. UMMY MWALIMU (MB).



Na WAMJWW 
Barozi wa Japan nchini Tanzania Mh.Masaham Yoshida  mapema leo amefanya mazungumzo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam, lengo likiwa ni kuimarisha ushirikiano wa nchi hizo mbili hususani katika masuala za huduma ya Afya.
Mh.Masaham Yoshida  ameahidi kuisaidia Sekta ya Afya kupitia mradi wa “SUMITOMO CHEMICAL PROJECT” wenye lengo la kuangamiza mazalia ya mbu kwa kutumia Viuwadudu, mradi huo umeanza kufanya kazi katika maeneo ya Nyanja ya juu Kusini katika Mkoa wa Mbeya. Hata hivyo Mh.Masaham Yoshida ameahidi kuendeleza ushirikiano huo na Serikali ya Tanzania.
Nae Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu ameshukuru ugeni huo kutoka Japan ulio na tija kwa taifa la Tanzania katika Sekta ya Afya  huku akisisitiza na kuweka  mkazo katika ushirikiano huo ili kusukuma gurudumu la maendeleo ya Sekta ya Afya nchini.



0 on: "BAROZI WA JAPAN NCHINI AFANYA MAZUNGUMZO NA MH. UMMY MWALIMU (MB)."