Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 23 Novemba 2017

LINDI WATAKIWA KUSHIRIKI KATIKA ZOEZI LA UMEZAJI KINGATIBA YA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE, ASEMA DKT. FAUSTINE NDUGULILE

Naibu Waziri wa Afya Dkt.Faustine Ndugulile akikata utepe kuashiria uzinduzi wa upasuaji wa mabusha na ngirikokoto kwa wagonjwa wapatao 200 wa Manispaa ya Lindi. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Statoil Bw.Oyotein Michelsen na kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Kinga toka Wizara ya Afya Dkt.Neema Rusibamayila.

  Naibu Waziri wa Afya Dkt.Faustine Ndugulile akimjulia hali mmoja ya wagojwa wakati wa ziara yake katika hospitali ya rufaa ya Mkoa Sokoine mkoani Lindi. pembeni yake ni Mkurugenzi wa Statoil Bw.Oyotein Michelsen.

  Mkurugenzi wa Statoil Bw.Oyotein Michelsen akisoma hotuba kwenye ufunguzi wa kambi ya upasuaji inayofanyila kwenye hospitali ya rufaa ya Mkoa Sokoine mkoani Lindi

 Baadhi ya wananchi wanaotarajia kufanyiwa upasuaji wa magonjwa hayo.

 Naibu Waziri wa Afya akimkabidhi Mkurugenzi wa Kinga toka Wizara ya Afya Dkt.Neema Rusibamayila ambapo Mpango wa Taifa wa kutokomeza Magonjwa yaliyokuwa hayapewi Kipaumbele ndiye mratibu wa upasuaji huo.

 Dkt.Faustine Ndugulile akipokea mashine ambayo ina kisu cha moto ambacho kinazuia damu wakati wa upasuaji kutoka kwa Mkurugenzi wa Statoil.

 Dkt.Faustine Ndugulile akihutubia wananchi waliofika kwenye uzinduzi wa upasuaji wa mabusha na ngirikokoto kwa wagonjwa wapatao 200 wa Manispaa ya Lindi.

Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto akipokea hundi yenye thamani ya shilingi milioni 264 toka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya utafiti na uchimbaji wa mafuta ya Statoil bw.Oyotein Michelsen .Fedha hizo ni kwa ajili ya kambi za upasuaji wa mabusha na ngirikokoto kwa watu wapatao 400 kwa mwaka 2017 na 2018.





Na WAMJW-LINDI

WAKAZI wa Lindi na vitongoji vyake wametakiwa kushiriki katika kampeni ya kutokomeza magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele kwa kumeza kingatiba za kutokomeza magonjwa hayo pamoja na kutunza mazingira kwa kuondoa mazalia ya mbu wanaenezao magonjwa hayo.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uzinduzi wa kambi ya upasuaji wa Mabusha na Ngirikokoto(Henia) unaofanyika mkoani Lindi.

"Wakazi wa Lindi na Vitongoji vyake tunatakiwa kushiriki katika zoezi la kumeza dawa za kukinga  magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele pamoja na kufanya usafi wa mazingira ili kuondoa mazalia ya mbu"alisema Dkt. Ndugulile

Aidha, Dkt. Ndugulile amewataka wananchi wa Lindi  kuondoa dhana potofu ya kuwa kila mwenye mabusha au ngirimaji basi atakuwa amerogwa ila ajue ugonjwa huo unasababishwa na vimelea vinavyotokana na mbu na kuzingatia umezaji wa dawa hizo.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kuhakikisha wanapambana kutokomeza ugonjwa huo Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya Utafiti ya uchimbani mafuta na gesi ya Statoil wamepata fedha za kuwafanyia upasuaji wagonjwa 200 wa mabusha na ngirikokoto kwa awamu ya kwanza ya mwaka 2017 na wagonjwa 200 kwa awamu ya pili ya mwaka 2018.

Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amesema kuwa wananchi wa Lindi wanatakiwa kutoa taarifa sehemu husika pindi wanapoambiwa kuwa dawa muhimu hakuna kwenye vituo vya afya vya Serikali kwani dawa hizo zipo kwa asilimia 90 Mkoani humo.

Kwa upande wake   Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi Bw. Ramadhani Kaswa amesema kuwa umezajii wa kingatiba ya magonjwa hayo umefikia asilimia 70 kwa mwaka 2016/2017.

Aidha, Bw. Kaswa amesema kuwa kutokana na zoezi la kuwatambua wagonjwa wenye mabusha na ngirikokoto wamejiandikisha wagonjwa 1294 kwa mkoa wa Lindi ikiwemo Manispaa ya Lindi wagonjwa 67,Wilaya ya Nachingwea wagonjwa 101,Halmashauri ya Lindi wagonjwa 633, Wilaya ya Liwale wagonjwa 387 na Wilaya ya Luongo wagonjwa 106.

Uzinduzi huo uliambatana na zoezi la kumeza Kingatiba za  magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ikiwemo mabusha na matende,usubi,minyoo,trakoma(vikope) na vichocho.

0 on: "LINDI WATAKIWA KUSHIRIKI KATIKA ZOEZI LA UMEZAJI KINGATIBA YA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE, ASEMA DKT. FAUSTINE NDUGULILE "