Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 1 Novemba 2017

WAWEKEZAJI WA NDANI WANAOTAKA KUJENGA VIWANDA VYA DAWA WAHIMIZWA KUFUATA VIGEZO VYA UZALISHAJI





Na WAMJWW 

Wawekezaji wa ndani wanao taka kujenga viwanda vya dawa wahimizwa kuhakikisha wanakidhi  vigezo vya uzalishaji wa dawa ili kuweza kuruhusiwa kufanya shughuli hiyo ya uzalishaji wa dawa.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakati  AKIZINDUA MAABARA HAMISHIKA  ZAKUDHIBITI UBORA NA USALAMA WA DAWA MAPEMA leo katika viunga vya mamlaka ya dawa, chakula na Vipodozi (TFDA)
Aidha Mh. Ummy ameahidi kuongeza jitihada za kudhibiti ubora, usalama, na ufanisi wa bidhaa hasa dawa kwa kuimarisha mpango mahususi wa uchunguzi wa awali wa Dawa  mbao ulianza 2002 unaohusu uchunguzi wa Dawa muhimu za Kifua kikuu, Dawa za ARV, Dawa za Maleria pamoja na Viuwa sumu.
Kwa upande mwingine  Mh. Ummy amesisitiza athari za uwepo wa dawa zisizo na ubora katika jamii ikiwepo kuhathiri  uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na taifa kiujumla kutokana na kmanunuzi ya  Dawa zisizo na uwezo wa uwezo wa kutibu mwisho hupelekea usugu wa Dawa katika mwili.
Waziri Ummy hakusita kuipongeza Bodi , Uongozi na wafanyakazi  wa TFDA kwa utendaji  mzuri wa  kazi huku akiahidi kuendelea mkuwaunga mkono kwa kushirikiana nao kwa ukaribu katika safari ya kumsaidia Raisi wa Jamhuri ya Tanzania Dkt. John Magufuli.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi (TFDA)  Hiiti Sillo alisema kuwa kutokana na kuongezeka kwa Maabara hamishika itasaidia kuwabaini na kuwakamata wahalifu wanaofanya biashara hiyo ambayo inahathiri jamii na uchumi kiujumla.
“Mwaka 2005 wastani wa dawa bandia ulikuwa 3.7 wa dawa zilizokuwepo huku takwimu za 2017 imeshuka  kwa chini ya 1%” , alisema Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi (TFDA)  Hiiti Sillo,  huku akisema mafanikio hayo yanatokana na ufuatiliaji wa umakini unaofanywa na taasisi hiyo.
Bw. Hiiti Siilo aliendelea kwa kusema kwamba katika utekelezaji wa majukumu yake TFDA imepanga kupeleka maabara hizo katika ofisi za kanda ambazo hazikuwa na huduma hiyo ikiwemo ofisi ya Tabora, Hospitali ya Mbeya na  Mtwara huku nyingine zitapelekwa katika vituo vya Forodha Namanga,KIA mpakani, Silali (Tarime) na Mutukula (Kagera) bila kusahau Geita na Katavi, alisisitiza Bw. Sillo.

0 on: "WAWEKEZAJI WA NDANI WANAOTAKA KUJENGA VIWANDA VYA DAWA WAHIMIZWA KUFUATA VIGEZO VYA UZALISHAJI"