Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 13 Novemba 2017

WIZARA YA AFYA YAUOMBA UONGOZI WA TIBA ASILI KUTOKA CHINA KUISAIDIA KUJENGA KITUO CHA UENDESHAJI WA TIBA ASILI.



Na WAMJWW
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto yauomba ugeni wa Viongozi wa masuala ya Tiba Asili na Tiba Mbadala kutoka China kuisaidia kujenga kituo cha uendeshaji wa Tiba Asili ambacho kitakuwa kinatoa mafunzo ya muda mrefu na mfupi, utafiti wa kina na kuwa na eneo la kumbu kumbu la kutunza miti dawa.
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya mapema leo wakati apokea ugeni wa Viongozi wa masuala ya Tiba Asili na Tiba Mbadala kutoka China uliofika nchini tangu Novemba 12, huku ugeni huo ukitarajia kuwepo nchini mpaka Novemba 16.
Pia Dkt. Mpoki ameuomba ugeni huo kuwekeza zaidi katika uanzishwaji wa viwanda vya kuzalisha Dawa, sambamba na kuiruhusu Tanzania kuuza Dawa zake za Asili katika nchi ya China  jambo litalosaidia Tanzania kuwa na mashamba makubwa ya kuzalisha Dawa.
Nae Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohhamad Bakar Kambi ameahidi kushirikiana bega kwa bega na jopo la uongozi huo hususani katika kuboresha huduma za Afya nchini , huku akitia mkazo kuimarisha zaidi ushirikiano katika kufanya tafiti na kubadilishana ujuzi kupitia mafunzo.
Nae kaimu Mkurugenzi msaidizi wa Tiba Asili na Tiba Mbadala Dkt. Peter Mhane amefurahishwa na ujio wa huo huku akiamini kwamba ushirikiano huu ni faida kwa nchi ya Tanzania kwani itasidia kuondokana na umasikini na kuondokana na upungufu wa Dawa.

0 on: "WIZARA YA AFYA YAUOMBA UONGOZI WA TIBA ASILI KUTOKA CHINA KUISAIDIA KUJENGA KITUO CHA UENDESHAJI WA TIBA ASILI."