Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 20 Julai 2018

DKT. NDUGULILE AHAIDI KUZIWAJIBISHA MAMLAKA HUSIKA ENDAPO KITUO CHA AFYA KITAFUNGIWA.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akikagua cheti chá mmoja kati ya wagonjwa waliofika kupata huduma za Afya katika hospitali ya Mkoa wa Mwanza ya Sokotoure wakati akiendelea na Ziara yake Mkoani hapo.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile (katikati) akikagua chumba chá Dawa katika hospitali ya kanda ya Bugando pindi alipofanya ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika Mkoa wa Mwanza.

Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akikagua incubator katika Zahanati ya Nyamizeze wakati alipofanya ziara yake ya kukagua hali ya utoaji huduma za afya katika Mkoa wa Mwanza.

Mwakilishi kutoka Zahanati ya Ihayabuyaga iliyo katika Wilaya ya Magu Mkoa wa Mwanza akipokea zawadi ya cheti kutoka kwa Naibu Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (MB) baada ya kushinda nafasi ya tatu katika kutoa huduma bora za Afya.

DKT. NDUGULILE AHAIDI KUZIWAJIBISHA MAMLAKA HUSIKA ENDAPO KITUO CHA AFYA KITAFUNGIWA. 

Na WAMJW-Mwanza

NAIBU Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii ,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile amesema kuwa hatosita kuziwajibisha mamlaka husika endapo kituo chá kutolea Huduma za Afya kitafungwa kutokana na uzembe wa aina yoyote. 

Amesema hayo wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua hali ya utoaji wa huduma za Afya na kutoa vyeti na ngao kwa Halmashauri zilizofanya vizuri katika utoaji wa huduma za afya leo jijini Mwanza.

"Na Bahati nzuri tunapopita tunawapa na maelekezo wa nini chakufanya, tukishakamilisha hili zoezi letu lá kuweka mifumo ya usajili , ithibati, na utoaji wa leseni tutaanza kufungua visivyokidhi vigezo, Sasa tutapofungia kituo chá Afya Mamlaka husika,  iwe ni Rass, Mganga mkuu wa mkoa au wa Wilaya, Mkurugenzi utawajibika, Vingine ni uzembe wa baadhi ya mamlaka kutosimamia vizuri majukumu yake"Alisema Dkt Ndugulile. 

Aliendelea kusema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeendelea kuweka mikakati thabiti katika kuboresha hali ya utoaji huduma za Afya nchini ili wananchi wanufaike zaidi na hali hiyo. 

"Tunaongeza rasilimali watu, tumetangaza ajira mpya 8000 katika sekta ya Áfya,  ambapo na ninyi mtapata,  pia Vituo vyote tutavisajili, kiwe cha umma Au chá binafsi, kitu chá pili tutaweka ithibati kama usipofikisha kigezo katika ngazi husika tutakushusha kigezo unaenda kuanza hatua upya" Alisema Dkt Ndugulile

Aidha Dkt.  Ndugulile alimtaka Mganga mkuu wa mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa kuyasimamia vizuri ili kuhakikisha huduma za afya zinatolewa kwa Ubora unaostahili kwa wananchi .

Nae Mganga Mkuu wa mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa alisema kuwa Mkoa unatarajia kuanza uboreshaji wa miundombinu ya huduma za afya hususani eneo lá uzazi na Mtoto kupitia mradi wa "Improving access to maternal and Newborn health (IMPACT)  umaotekelezwa na Aga Khan Development Network  (AKDN)  chini ya Ufadhili wa Serikali ya Canadá pamoja na Agriteam kupitia mradi wa Mama na Mtoto ambapo zaidi ya Bilioni 2.8 zinatarajiwa kutolewa na kutumika katika vituo 30

Dkt. Thomas Rutachunzibwa aliendelea kusema kuwa mkoa wa Mwanza Unaendelea kuimarishwa ambapo madirisha maalum 35 yameanzishwa katika hospitali zote 7 za Serikali, vituo vya Áfya 11 na Zahanati 17 ili kuhakikisha wazee wanapata huduma kwa haraka na Ubora unaotakiwa, jumla ya wazee 43,046 wamepatiwa vitambulisho na mabaraza ya wazee 172 yameundwa 

0 on: "DKT. NDUGULILE AHAIDI KUZIWAJIBISHA MAMLAKA HUSIKA ENDAPO KITUO CHA AFYA KITAFUNGIWA. "