Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 13 Julai 2018

TAARIFA KWA UMMA




JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO


KUITWA  KAZINI

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inapenda kuwataarifu wote walioomba nafasi mbalimbali za Ajira za Kada ya Afya tarehe  11 Mei  hadi  26  Mei, 2018  kuwa  walioorodheshwa  katika tangazo hili wamechaguliwa na kupangiwa vituo vya kazi kama jedwali linavyoonyesha kwenye Tovuti ya Wizara ya  Afya  www.moh.go.tz.

Waombaji  waliochaguliwa wanatakiwa kuzingatia kwa ukamilifu maelekekezo yafuatayo:

1).   Kuripoti  Ofisi  za Wizara  ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Dodoma katika  muda  wa  siku  kumi  na  nne (14) kuanzia tarehe ya tangazo hili, kwa ajili ya kukamilisha taratibu za Ajira Serikalini.  Ambao hawataripoti ndani ya siku kumi na nne (14) nafasi zao zitajazwa na waombaji wengine wenye sifa.  Aidha, wakati wa kuripoti kila aliyechaguliwa atapaswa kuwasilisha vyeti halisi (Original Certificates) ambavyo nakala zake zilitumiwa wakati wa kuomba ajira zao, ikiwa pamoja na:-

a)      Vyeti halisi vya Elimu ya Sekondari, Vyeti vya Taaluma, Usajili wa Baraza/Bodi ya Kitaaluma na cheti cha kuzaliwa.

b)     Nakala ya picha mbili ndogo (passport size). Picha ziwe na muonekano kamili wa sura na ziwe zimepigwa si zaidi ya miezi mitatu iliyopita.

2)      Waombaji  wote  ambao  majina  yao  hayakuonekana  katika  tangazo  hili  watambue  
kuwa hawakupata nafasi hiyo, hivyo wanashauriwa  wasisite  kuomba  mara  nafasi  nyingine za  kazi zitakapotangazwa.

3)  Waombaji waliopangiwa  Kada ya Uhudumu wa Afya majina yao yatatangazwa baadae.


Imetolewana:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini - Afya
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
13 Julai, 2018

0 on: "TAARIFA KWA UMMA"