Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 6 Julai 2018

UBALOZI WA JAPAN YAMUUNGA MKONO MHE. UMMY KUJENGA MADARASA MKOANI TANGA



PICHA ZINAZOONYESHA TUKIO LA UTIAJI SAINI MAKUBALIANO YA UJENZI WA MADARASA 6 KATIKA SHULE YA MSINGI MWAKIDILA MKOANI TANGA KATI YA UBALOZI WA JAPAN NA TAASISI YA MAENDELEO YA WANAWAKE  TANGA ( TAWODE).

NA WAMJW-DAR ES SALAAM.

Serikali ya Japan kupitia ubalozi wa Japan nchini Tanzania imetoa kiasi cha shilingi miliioni 188 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 6 ya shule ya msingi Mwakidila kata ya Tangasisi iliyopo Jijini Tanga
Fedha hizo zimetolewa leo jijini hapa kupitia  Shirika la Maendeleo ya Wanawake wa Mkoa wa Tanga (TAWODE) chini ya Mwenyekiti wake Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu .
Ubalozi wa Japan nchini imetoa fedha hizo ikiwa  ni kuunga mkono  jitihada za Serikali za kuboresha  miundombinu ya elimu ya Msingi na Sekondari katika jiji la Tanga.
Akiongea wakati wa hafla ya kutia saini mkataba wa ujenzi wa madarasa hayo Balozi wa Japan Nchini Tanzania Mhe. Masaharu Yoshida  alisema Serikali ya japan imetoa fedha hizo  ili kusaidia maendeleo ya elimu kwa Jiji la Tanza ili kutatua  tatizo la mrundikano wa wanafunzi madarsani
Aidha, Balozi Yoshida  ameitaka TAWODE kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kikamilifu  na kukamilisha ujenzi huo wa madarasa kwa wakati.
Akiongea wakati wa kutiana saini mkataba huo Mwenyekiti wa TAWODE, Waziri Ummy Mwalimu ameushukuru Ubalozi wa Japan nchini kwa kukubali ombi la kufadhili ujenzi wa madarasa  ya shule hiyo ya Msingi  Mwakidila ambayo ina wanafunzi zaidi ya 1,400 kulinganisha na madarasa yaliyopo.
“Sisi kama sehemu ya wanajamii wa Jiji la Tanga tuliona tuna wajibu wa kuunga mkono Serikali kwa kutafuta vyanzo vingine vya fedha ili kuwezesha elimu ya Msingi na ile ya sekondari hususan changamoto ya madarasa itatuliwe hivyo fedha hizi ni za jamii ya Wana Tanga hivyo TAWODE tutahakikisha zinatumika ipasavyo”.Alisema Waziri Ummy.
Hata hivyo alisema hivi sasa kumekuwa na changamoto ya madarasa kwenye halmashauri mbalimbali nchini  kutokana na ongezeko la wanafunzi  kutokana na  Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt.John Magufuli ya kutoa elimu bure .
Kwa upande wake Meya wa Jiji la Tanga Mhe.Selebosi Mhina ameushukuru Ubalozi wa japan pamoja na kumpongeza Mhe.Ummy mwalimu kwa kuwa bega kwa bega katika kusukuma  mbele maendeleo ya wananchi wa Tanga katika sekta ya Elimu na Afya.

0 on: "UBALOZI WA JAPAN YAMUUNGA MKONO MHE. UMMY KUJENGA MADARASA MKOANI TANGA"