Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 2 Agosti 2018

MAAGIZO 12 YA DKT. NDUGULILE WAKATI WA ZIARA YAKE YA MIKOA 6 YA KANDA YA ZIWA


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza juu ya kuitambua Dawa ya Serikali iliyo na Nembo ya MSD GOT wakati akiwa katika ziara yake ya mikoa 6 ya kanda ya ziwa.

Msafara wa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile  akiwa katika ziara yake ya kukagua hali ya utoaji wa huduma za Afya katika mikoa 6 ya kanda ya ziwa.

MAAGIZO 12 YA DKT. NDUGULILE WAKATI WA ZIARA YAKE YA MIKOA 6 YA KANDA YA ZIWA

#Kusimamishwa kazi Mganga mkuu wa mji wa Bunda Dkt. Nikodemas Masosota 

#kusimamisha ujenzi wa jengo la upasuaji katika kituo chá Áfya chá Katoro Geita kutokana na kukosa misingi ya kitaalamu ya ujenzi

# Kupewa Ripoti ya ujenzi wa jengo la chuo chá Waganga wasaidizi Musoma kutokana na ubadhirifu wa pesa aliouona. 

# Waganga Wafawidhi wa hospitali kuhakikisha wanaagiza dawa  MSD na si mahala pengine. 

#Kamati za ulinzi za mikoa kulinda dawa za Serikali (Dawa zote za Serikali zina nembo ya MSD GOT) 

# Waganga wakuu wa mikoa kusimamia kikamilifu ujenzi wa hospitali mpya za Wilaya na Mikoa ili kuharakisha huduma za afya kwa wananchi.

# Watoa huduma za afya wote kuhakikisha wanaandika muda halisi wakati mgonjwa anapopokelewa hadi anatibiwa. Mfano wa muda ni saa 12: 06 jioni, saa 01: 01 asubuhi na siyo mazoea ya kuandika saa 12PM, saa 11AM 

# Wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya Afya na ule  wa afya ya jamii (CHF iliyoboreshwa) ili kuzishinda gharama za matibabu pindi wanapopata ugonjwa.

# Kuwekwa mikakati thabiti ili kukabiliana na tatizo la Lishe duni hususan kwa Watoto walio chini ya Miaka 5. 

#Akina mama wajawazito kuhudhuria kliniki walau mara nne ndani ya kipindi chá ujauzito na kuhakikisha wanajifungulia katika vituo vya kutolea huduma za Áfya

#Wananchi kujitokeza kuwapa watoto wao chanjo, hususan chanjo mpya  Saratani ya mlango wa kizazi (HPV) kwa wasichana wenye umri wa miaka 9 - 14.
 
#Amepiga marufuku kwa vituo vyote vya kutolea huduma za Afya nchini zenye Runinga kuonesha muziki katika maeneo yote ya kutolea huduma bali kuweka jumbe zinazohusu Elimu ya Afya kwa umma.

0 on: "MAAGIZO 12 YA DKT. NDUGULILE WAKATI WA ZIARA YAKE YA MIKOA 6 YA KANDA YA ZIWA"