Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 17 Agosti 2018

DKT. SUBI AWAHASA WANAWAKE KUWAI KLINIKI PINDI WANAPOHISI WANAUJAUZITO.

Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na  Watoto Dkt.Leonard Subi

Na.WAMJW - Dodoma

Akina Mama wajawazito wametakiwa  kuwahi kliniki mara wanapohisi wana ujauzito na kufuata ushauri wa wataamu wa afya  ili kuwakinga watoto wanaotarajia kujifungua dhidi ya maabukizi ya Virus vya UKIMWI
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na  Watoto Dkt.Leonard Subi mjini Dodoma hivyo kuwataka wananchi kuchukua hatua katika kujikinga na maradhi mbalimbali ikiwemo Virusi Vya Ukimwa (VVU).
Amesema Utafiti uliofanywa mwaka 2010 maambukizi ya Virus yalikua  asilimia 26  kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto huku utafiti uliofanywa mwaka  2016/2017 unaonesha kuwa maambukizi haya yamepungua na kufikia asilimia 7.6 ambapo Serikali imesema inatarajia maambukizi haya yapungue mpaka asilimia 2 ifikapo 2020-2021.
“Ni  muhimu kwa wajawazito kuhudhuria kliniki na kupima VVU hii itasaidia kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, malezi na makuzi  mzuri ya Mtoto yanategemea wazazi wote wawili yaani baba na mama wazazi wote wanaaswa kushirikiana hasa katika kupima afya afya ili mtoto atakaezaliwa asiwe na maambukizi ya VVU”Alisema Dkt.Subi. 
Aliongeza kuwa  moja ya changamoto inayokwamisha mpango huu ni  wanaume kukumbatia mila na destuli za kutoandamana na wenzi wao kliniki wakati wa kipindi cha ujauzito,
“hivyo familia au makabila ambayo bado yanaona kwamba mwanaume kumsindikiza mwenzi wake kliniki ni kujishushia hadhi waachane nazo”.
Aidha, Dkt.Subi amewataka vijana kuchukua hatua za kwenda katika vituo vya afya kupata elimu ya uzazi na kupima afya zao maana wao ndio mama au baba wanaotarajiwa,mimba za utotoni ni hatari kwa afya zao na kama kuna tatizo lolote wafike katika vituo vya afya ili kupata msaada wa kitalaamu.
Alisisitiza kuwa vituo vya kutolea huduma za afya vyote nchini hivi sasa vinatoa huduma ya elimu bure kuhusiana na afya ya uzazi na endapo mama mjamzito atagundulika ana maambukizi ya VVU ataanzishiwa dawa ambazo zitamkinga mtoto asizaliwe na maambukizi ya  Virus vya UKIMWI.


0 on: "DKT. SUBI AWAHASA WANAWAKE KUWAI KLINIKI PINDI WANAPOHISI WANAUJAUZITO."