Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 28 Agosti 2018

SERIKALI IMETENGA BILIONI 30 KUJENGA HOSPITALI ZA RUFAA ZA MIKOA

Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati wa uwasilishwaji wa taarifa ya uendeshaji wa hospitali za rufaa za mikoa mbele ya kamati ya kudumu ya bunge ya huduma na maendeleo ya jamii jijini Dodoma.





Naibu waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwasilisha ripoti ya uendeshaji wa Hospitali za rufaa za mikoa mbele ya wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge huduma na maendeleo ya jamii jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Ummy Mwalimu akiteta jambo na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uwasilishwaji wa taarifa ya uendeshaji wa hospitali za rufaa za mikoa mbele ya kamati ya kudumu ya bunge ya huduma na maendeleo ya jamii jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge ya huduma na maendeleo ya jamii Mhe. Peter Selukamba akitoa neno wakati wa kuwasilisha kwa taarifa za uendeshaji wa hospitali za rufaa za mikoa kutoka wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto jijini Dodoma.

Wajumbe wakifuatilia mjadala uliokua unaendelea katika kikao cha mawasilisho ya taarifa za uendeshaji wa Hospitali za rufaa za mikoa kutoka wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto katika kamati ya kudumu ya Huduma na maendeleo ya jamii jijini Dodoma


SERIKALI IMETENGA BILIONI 30 KUJENGA HOSPITALI ZA RUFAA ZA MIKOA
Na.WAMJW-Dodoma
Serikali imetenga shilingi bilioni 30 kwa ajili ya kujenga  na kukarabati miundombinu ya hospitali zaRufaa za Mikoa  kila mkoa  ili kuweza kuwawezesha wananchi kupata huduma za rufaa za kibingwa karibu na wanapoishi na hivyo kupunguza adha ya kusafiri  umbali mrefu  kufuata huduma hizo
Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile wakati akiwasilisha  taarifa za uendeshaji wa hospitali za rufaa za Mkoa kwa kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Jijini Dodoma.
Dkt. Ndugulile amesema kuwa  fedha hizo zimetengwa kwa ajili ya kukamilisha hospitali za Rufaa za Mikoa ya Geita, Katavi, Simiyu, Njombe na Songwe ambapo zipo katika hatua za ujenzi wa  hospitali hizo hivyo itafanya idadi ya hospitali hizo kuwa 28 pindi zitakapokamilika.
“Serikali ilifanya mabadiliko ya kuzihamishia hospitali za Rufaa za Mikoa  Wizarani ili kuboresha huduma za kibingwa  ikiwemo kutoa fursa nzuri  ya udhibiti ,usimamizi na mgawanyo wenye tija zaidi wa rasilimali chache zilizopo”alisema Dkt.Ndugulile.
Alisema kuwa baada ya Wizara kukabidhiwa hospitali hizo ilifanya tathimini  ya awali ya hali halisi na kubaini  changamoto  mbalimbali zilizoathiri utoaji wa huduma za afya katika maeneo yote ambayo ni nguzo ya msingi  katika kuwezesha upatikanaji wa huduma bora.
“Hospitali za Rufaa za Mikoa zinapaswa kutoa huduma za kibingwa ambazo hazitolewi   katika hospitali ngazi ya Halmashauri,Huduma za kibingwa ambazo ni lazima kupatikana katika  hospitali za Rufaa”.Alisema Naibu Waziri Dkt. Ndugulile
Alitaja huduma za kibingwa ambazo zinatakiwa kutolewa katika hospitali hizo za Rufaa za Mikoa ni pamoja na upasuaji wa jumla,magonjwa ya uzazi na yanayoathiri wanawake, magonjwa ya watoto,magonjwa ya ndani ,magonjwa ya kinywa na meno na Radilojia.
Kwa upande wa ubora wa huduma zinazotolewa Naibu Waziri huyo alisema Wizara ilifanya kaguzi za kuzitambua hali halisi ya ubora wa huduma za afya zinazotolewa katika hospitali hizo  na jumla ya hospitali  za rufaa ishirini na moja zilifanyiwa tathimini na kupewa nyota kutokana na vigezo vilivyowekwa na kupewa  mpango kazi wa kuboresha huduma .
“Ni hospitali 9 zilipata nyota mbili, hospitali kumi na moja zilipata nyota moja na hospitali moja ilipata nyota sifuri,hivyo hakuna hospitali yeyote iliyopata nyota 3 hapa nchini.Alimalizia Dkt.Ndugulile

0 on: "SERIKALI IMETENGA BILIONI 30 KUJENGA HOSPITALI ZA RUFAA ZA MIKOA"