Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 29 Agosti 2018

SERIKALI YASOGEZA HUDUMA ZA KIFUA KIKUU SUGU KARIBU NA WANANCHI





Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Ummy Mwalimu akiteta jambo na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uwasilishwaji wa taarifa ya uendeshaji wa hospitali za rufaa za mikoa mbele ya kamati ya kudumu ya bunge ya huduma na maendeleo ya jamii jijini Dodoma.

Wajumbe wakifuatilia mjadala uliokua unaendelea katika kikao cha mawasilisho ya taarifa za uendeshaji wa Hospitali za rufaa za mikoa kutoka wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto katika kamati ya kudumu ya Huduma na maendeleo ya jamii jijini Dodoma




SERIKALI YASOGEZA HUDUMA ZA KIFUA KIKUU SUGU KARIBU NA WANANCHI 

Na.WAMJW,Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya afya imefanya ugatuaji kwa kusogeza karibu na wananchi huduma ya kifua kikuu sugu (TB) ili kupunguza adha ya kusafiri umbali mrefu kwa wananchi  katika ngazi ya vituo vya afya  sabini na nane nchini.

Hayo yamesemwa jana na Waziri wa fya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto  ummy mwalimu wakati akiwasilisha  taarifa ya utekelezaji wa hospitali ya magonjwa ambukizi Kibong’oto kwa kamati ya huduma za jamii ya Bunge jijini hapa.

Waziri Ummy alisema wamefanya ugatuaji  wa vituo hivyo vya afya ili kuwezesha wagonjwa kupata tiba jirani na jamii inayowazunguka na hivyo  kujenga uelewa wa wananchi juu ya ugonjwa  na kushiriki kikamilifu katika kumhudumia mgonjwa hasa katika chakula,masuala ya kijamii na kisaikolojia.

Alitaja mikoa ambayo vituo hivyo vipo ni pamoja na Kagera, Mtwara, Kilimanjaro, Dar es Salaam, Dodoma, Geita,  Mbeya, Pwani,Mrorgoro,Njombe,Iringa, Tanga, Mwanza , Lindi na Pemba na kuongeza kuwa hadi sasa wagonjwa wapatao 112 wamepata huduma  za tiba ya TB sugu.

“Takwimu zinaonesha kuwa kati ya watu laki moja, watu 287 wana TB na kati ya watu 100 kati yao 40 tunawagundua wana  TB hapa nchini”alisema Waziri Ummy.

Hata hivyo mnamo  mwaka 2017 Serikali ilizindua kituo bora katika hospitali hiyo kwa kutoa huduma za afya kwa wachimbaji wa migodi wanaougua magonjwa ya TB, Mapafu na usikivu unaosababishwa na ulipuaji wa baruti migodini kwa kushirikiana na mfuko wa fidia kwa wafanyakazi (WCF).

Tangu kuanzishwa kwa kituohicho  jumla ya wagonjwa 863 wamepata huduma,wagonjwa 614 walipima makohozi na 116(19%) waligundulika kuwana TB na 123(15%) walikuwa na magonjwa ya mapafu yanayosababishwa na vumbi na 125(15.3%) walikuwa na upotevu wa usikivu.



0 on: "SERIKALI YASOGEZA HUDUMA ZA KIFUA KIKUU SUGU KARIBU NA WANANCHI"