Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 20 Agosti 2018

TAARIFA KWA UMMA

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VYETI VYA WAHITIMU WA KADA ZA AFYA

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inapenda kuwajulisha kuwa imepokea vyeti vya wahitimu kutoka Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).Vyeti hivyo ni kwa wahitimu waliofanya mitihani  2016, mwezi Septemba na Oktoba 2017 kwa Mafunzo ya Astashada na Stashahada ya Uuguzi na Ukunga, Mafunzo ya Astashahda ya Wahudumu wa Afya ya Jamii na Mafunzo ya Sayansi Shirikishi za Afya (Utabibu, Wateknolojia wa Maabara, Famasia, Sayansi ya Afya ya Mazingira, Utunzaji kumbukumbu za Afya, Mazoezi ya viungo ,Utabibu wa Meno na Wateknolojia Macho).
Wizara inawajulisha wahitimu wa mafunzo hayo kuwasiliana na Wakuu wa Vyuo kuanzia tarehe 20/08/2018 ili kuweza kupewa utaratibu wa kwenda kuchukua vyeti vyao kwenye vyuo walivyopatia mafunzo hayo.
Imetolewa na,
KATIBU MKUU (AFYA)
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
20 Agosti, 2018.

0 on: "TAARIFA KWA UMMA"