Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 13 Agosti 2018

WAZIRI UMMY AMSHUKURU BALOZI WA CANADA NCHINI TANZANIA KWA KUBORESHA SEKTA YA ÁFYA.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiagana na Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles mapema leo katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam baada ya mazungumzo juu ya Maboresho katika Sekta ya Afya.

Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles (Wapili kushoto) akimweleza jambo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu mapema leo wakati alipotembelea katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam. Wakwanza kushoto ni ofisa wa Ubalozi wa Canada Susan Steffen.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimsikiliza kwa makini Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles (Hayupo kwenye picha)

Picha ya Pamoja ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles baada ya kikao cha kumuaga Balozi huyo kilichofanyika mapema leo katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam.

WAZIRI UMMY AMSHUKURU BALOZI WA CANADA NCHINI TANZANIA KWA KUBORESHA SEKTA YA ÁFYA. 

Na WAMJW - DSM 

Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ameishukuru Serikali ya Canada kupitia Balozi wake nchini Tanzania kwa ushirikiano walioonesha katika kuboresha sekta ya Áfya hususani katika Kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Ameyasema hayo mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Áfya jijini Dar es salaam wakati akiagana na Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles anayetarajia kuondoka hivi karibuni hapa nchini.

Nae Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe Ian Myles  ameishukuru Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Áfya kwa kuendelea kutatua changamoto za sekta ya Áfya nchini.

0 on: "WAZIRI UMMY AMSHUKURU BALOZI WA CANADA NCHINI TANZANIA KWA KUBORESHA SEKTA YA ÁFYA."