Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 28 Septemba 2018

HUDUMA ZA MRI NA CT SCAN ZAANZA KUTOLEWA MOI.

Naibu Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua Mkono wa Bandia uliotengenezwa katika Taasisi hiyo, Kulia ni Mtaalamu wa viungo Bandia Bw. Deus David.

Naibu Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimsalimia mtoto, aliyefika na mzazi wake kupata matibabu katika Taasisi ya mifupa ya MOI, alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma na kusimikwa kwa Mitambo ya MRI,CT Scan na X-Ray

Mkuu wa Kitengo cha Fiziotherapia Bw. Lucas Machage akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile, alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma na kusimikwa kwa Mitambo ya MRI,CT Scan na X-Ray MOI.

Naibu Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na mmoja kati ya wanufaika wa Vifaa vya Bandia katika Taasisi ya Mifupa MOI aliowekewa baada ya kukatwa Mkono wake.

Naibu Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua Cheti cha moja kati ya Wagonjwa waliofika kupata huduma za Afya katika Taasisi ya Mifupa ya MOI.

Naibu Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua moja kati ya mtambo wa kisasa uliosimikwa tayari kuanza kufanya kazi, katika Taasisi ya Mifupa ya MOI, Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dkt. Respicious Bonface.

Wataalamu mbali mbali kutoka Taasisi ya Mifupa ya MOI wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma na kusimikwa kwa Mitambo ya MRI,CT Scan na X-Ray.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua kitabu cha Kusaini Wataalamu wa Maabara, Kushoto ni Muuguzi wa Kitengo cha Dharura MOI Levlin Masama.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiendelea na Ziara katika Taasisi ya Mifupa ya MOI, Kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dkt. Respicious Bonface.


HUDUMA ZA MRI NA CT SCAN ZAANZA KUTOLEWA MOI.

Na WAMJW-Dar es Salaam.

Huduma za kupima magonjwa mbalimbali kwa kutumia Mashine  za kisasa ya CT Scan na MRI sasa zimeanza kutolewa kwa ufanisi baada ya kusimikwa na kuanza kufanya kazi  katika Hospitali ya Mifupa ya MOI.

Hayo yamesemwa leo na  Naibu Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,JiAnsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipotembelea  na kukagua hali ya utoaji wa huduma na usimikaji wa mitambo ya kisasa katika kitengo cha radiolojia yenye thamani ya zaidi ya Tsh Bilioni 5.6 Hospitalini hapo .

"Lengo la ziara yangu ni kukagua maendeleo ya usimikaji wa mitambo hii ya kisasa  ya MRI, CT SCAN, Xray, Ultra sound, mitambo mingine , nimeona na kujiridhisha imekamilika kwa asilimia 99% " Alisema Dkt.Ndugulile.

Aidha ,  Dkt. Ndugulile ameuagiza uongozi wa Hospitali hiyo kuhakikisha unakamilisha  mambo machache yaliyobaki ndani ya wiki hii ili wiki ijayo wagonjwa waanze kupata huduma hapa.

 Mbali na hayo Dkt Ndugulile ameupongeza uongozi wa MOI kwa kuhakikisha usimikaji wa Mitambao unafanyika kwa wakati na hali ya utoaji huduma ni nzuri na ya kuridhisha kwani wagonjwa wamekuwa wakipata changamoto ya kwenda nje ya MOI kufuata vipimo hivi.

Mbali na hayo Dkt.  Ndugulile amesema ni adhma ya Serikali kuhakikisha huduma zote zinapatikana hapa nchini hivyo ni vyema kama kuna kifaa chochote kinachohitajika taarifa ikatolewa Wizarani ili kifaa hicho kiwekwe kwenye mpango na bajeti na kununuliwa kwani utaalamu na weledi upo wakutosha.

Dkt Ndugulule ametembelea vitengo vya mazoezi tiba pamoja na utengenezaji wa viungo bandia ambapo amekagua na kujiaone hali ya utoaji huduma na kujiridhisha kwamba huduma zimeboreka katika kipindi cha miaka 3 tangu Serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani  na kwa sasa watanzania wanapata huduma kwa wakati licha ya kuwa  kuna changamoto ya ununuzi wa vifaa tiba nje ya nchi.

Akitoa taarifa ya hali ya utoaji huduma na usimikaji wa mitambo hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface amesema kwamba hali ya utoaji wa huduma ni nzuri, wagonjwa wanapata huduma stahiki kwa wakati na idadi ya wagonjwa wanaopata huduma imeongezeka maradufu baada ya eneo la kutolea huduma kuboreshwa na kupanuliwa .

"Mh Naibu Waziri, hali ya utoaji huduma katika taasisi yetu ni nzuri, idadi ya wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji imeongezeka na kufikia 700-900 kwa mwezi kutoka 500 na ongezeko la vyumba 2 vya upasuaji katika jengo hili, awali tulikua na vyumba 6 sasa vimekuwa 8, hii nikutokana na uwekezaji uliofanywa na Serikali hii ya awamu ya 5 inayoongozwa na Dkt John Pombe Magufuli" alisema Dkt Boniface. 

0 on: " HUDUMA ZA MRI NA CT SCAN ZAANZA KUTOLEWA MOI."