Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 26 Septemba 2018

OCEAN ROAD YAOKOA ZAIDI YA BILIONI 7.5 KWA MWAKA

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimsikiliza moja kati ya Wataalamu wa Picha za Mionzi kwenye jengo la Mionzi katika Taasisi ya Saratani Ocean Road jijini Dar Es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwajulia hali Wagonjwa waliofika kupata Huduma za Afya katika Taasisi ya Kansa ya Ocean Road Jijini Dar es salaa.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile  akiongea na Mgonjwa aliyetoka nchi ya Jirani ya Kenya kupata matibabu Kansa nchini katika Taasisi ya Ocean Road Jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua vifaa ambavyo vimenunuliwa na Serikali kwa gharama ya shilingi Bilion 9.5, alipofanya Ziara katika Taasisi ya Ocean Road jijini Dar es salaam. Wakwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Ocean Road Dkt. Julius Mwaiselage.
 Baadhi ya Mitambo ya Mionzi katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road iliyogharimu jumla ya kiasi cha shilingi Bilioni 9.5.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongoza msafara wa kukagua hali ya utoaji huduma za Afya, na kukagua vifaa ambavyo vimenunuliwa na Serikali kwa gharama ya shilingi Bilion 9.5. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dkt. Julius Mwaiselage.
OCEAN ROAD YAOKOA ZAIDI YA BILIONI 7.5 KWA MWAKA.

Na WAMJW-DSM

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imefanikiwa kuokoa zaidi ya Bilion 7.5 zilizokuwa zikitumika kwaajili ya matibabu ya Wagonjwa wa Saratani nje ya nchi.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma katika Taasisi ya Ocean Road na kukagua vifaa ambavyo vimenunuliwa na Serikali kwa gharama ya shilingi Bilion 9.5.

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa vifaa hivi (Linac Mashine na CT Similator) vinaifanya nchi ya Tanzania kuwa moja kati ya Nchi chache barani Afrika ambayo inavifaa vya kisasa katika kutibu wagonjwa wa Saratani.

“Mashine hizi ambazo zipo ndani ya majengo haya yamenunuliwa na Serikali ya awamu ya Tano kwa gharama ya Shilingi Bilion 9.5, Vifaa hivi vinaitwa Linac Mashine na CT Similator vinaifanya Tanzania kuwa moja kati ya nchi chache sana Barani Afrika ambazo zinavifaa vya kisasa zaidi kwaajili ya matibabu ya Saratani” Alisema Dkt. Ndugulile

Pia, Dkt. Ndugulile alisema kuwa Vifaa hivi vyenye ufanisi mkubwa vinasaidia sana katika kuongeza idadi ya Wagonjwa kupata matibabu kutoka wagonjwa 170, mpaka 270 kwa siku, huku ikipunguza muda wa wagonjwa kusubiria matibabu kutoka wiki 6 mpaka chini ya wiki 2.

Aidha, Dkt. Ndugulile alisema kuwa Serikali inajipanga kufunga kifaa kikubwa cha Pate Scan ambacho kitasaidia kwa kiasi kikubwa wagonjwa wa Saratani.

Akisoma Risala ya Taasisi hiyo Mkurugenzi wa Ocean Road Dkt. Julius Mwaiselage alisema kuwa gharama za ujenzi wa jengo la vifaa vifaa hivo ni shilingi Bilion 2.3 ambazo zote zilitolewa na Serikali.

“Gharama ya ujenzi huu ni shilingi Bilion 2.33 ambapo zilitolewa zote na Serikali, Jengo hili limekwishakamilika, na liliweza kufanyiwa uhakiki na Tume ya Nguvu za Atomic Tanzania, pamoja na shilika la kimataifa la nguvu za Atomic walilipitia na kuliangalia vigezo vyake kama vimefikiwa na waliona vinafaa”. Alisema Dkt. Mwaiselage.

Mbali na hayo Dkt. Mwaiselage alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kugharamia Mradi huo uliogharimu jumla ya shilingi Bilion 9.5, zilizojumuhisha gharama za kupeleka Wataalamu kwaajili ya kupata mafunzo nje na ndani ya nchi.

“Mradi ulikuwa na sehemu ya Mafunzo kwa Wataalamu nje na ndani ya nchi, jumla ya gharama ya mradi huu ilikuwa ni Bilion 9.5, na fedha zote hizi, ziligharamiwa na Serikali chini ya Raisi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na tunamshukuru sana kwa kuweza kutoa fedha kwaajili ya mradi huu”. Alisema Dkt. Mwaiselage.

0 on: "OCEAN ROAD YAOKOA ZAIDI YA BILIONI 7.5 KWA MWAKA"