Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 22 Septemba 2018

WAKUU WA MIKOA NCHINI WATAKIWA KUTENGA VITUO MAALUM VYA KUHUDUMIA WAGONJWA WA EBOLA.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,  Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongoza Matembezi ya Hiari ya kuelimisha na kuhamasisha Jamii kuzuia ugonjwa wa Ebola usiingie nchini yalipoanzia katika viwanja vya Mnazi Mmoja na kuishia viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhamad Bakari Kambi (Wakwanza Kulia) akiwa na Mwakilishi Mkazi kutoka Shirika la Afya la Kimataifa (WHO) na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,  Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakiwa katika matembezi ya Hiari ya kuelimisha na kuhamasisha Jamii kuzuia ugonjwa wa Ebola usiingie nchini yalipoanzia katika viwanja vya Mnazi Mmoja na kuishia viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam. 

Kikundi Shupavu cha Vijana wa Skauti kikiwa kimeshika Bango lenye maandishi ya kutoa Elimu kuhusu ugonjwa wa Ebola wakati wa matembezi ya Hiari ya kuelimisha na kuhamasisha Jamii kuzuia ugonjwa wa Ebola usiingie nchini yalipoanzia katika viwanja vya Mnazi Mmoja na kuishia viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam. 

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,  Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Mwongozo utaosaidia jinsi ya kukabiliana na ugonjwa wa Ebola katika nchi yetu endapo utainia nchini.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,  Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa ameshika Mwongozo utaosaidia jinsi ya kukabiliana na ugonjwa wa Ebola katika nchi yetu endapo utaingia nchini.
 
WAKUU WA MIKOA NCHINI WATAKIWA KUTENGA VITUO MAALUM VYA KUHUDUMIA WAGONJWA WA EBOLA. 

Na WAMJW - DSM 

WAZIRI  wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,  Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amewataka Wakuu wa mikoa wote kutenga vituo maalumu katika kila halmashauri cha kuhudumia na  kuhifadhi wagonjwa wa Ebola endapo wataingia nchini.

Waziri Ummy Ameyasema hayo mapema leo katika Matembezi ya Hiari ya kuelimisha na kuhamasisha Jamii kuzuia ugonjwa wa Ebola usiingie nchini yalipoanzia katika viwanja vya Mnazi Mmoja na kuishia viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam. 

"Lazima kila mikoa, Halmashauri kutenga kituo maalumu cha kuhudumia wagonjwa wa Ebola endapo watatokea, katika kila mkoa, kila Wilaya lazima wawe na chumba maalumu kwaajili ya kuhifadhi wagonjwa wa Ebola endapo wataingia "alisema Waziri Ummy Mwalimu. 

Aidha, Waziri Ummy aliwaomba Viongozi wa Dini kutumia majukwaa yao katika Maubiri yao kutoa tahadhari kwa wananchi kuhusu ugonjwa huu wa Ebola,  huku akiwaomba wasanii na viongozi wa Siasa nchini kutumia majukwaa yao ili kutoa madaraja kufikisha taarifa kwa wananchi.

Kwa mujibu wa Waziri  Ummy  amesema kuwa licha ya ugonjwa wa Ebola kutoingia nchini, bado tupo katika hatari kubwa ya kuupata ugonjwa huu kutokana na muingiliano wa wananchi baina ya nchi ya Tanzania na eneo la Kivu Kaskazini ambalo ni karibu na nchi ya Tanzania.

"Ebola bado haijaingia nchini Tanzania, lakini ni Kweli Kwamba tupo katika hatari kubwa zaidi kupata Ugonjwa huu wa Ebola, hii inatokana Na mlipuko wa ugonjwa huu kuwepo katika eneo la Kivu Kaskazini ambalo ni karibu na nchi ya Tanzania na kutokana na muingiliano wa wavuvi baina ya nchi hizi", Alisema Waziri Ummy. 

Aidha Waziri Ummy alisema kuwa Tanzania inaweza   kuzuia ugonjwa wa Ebola usiingie nchini kwa vitengo vinavyihusika  kutoa elimu na uelewa wananchi kuhusu ugonjwa wa Ebola, itakuwa ni moja ya njia kubwa ya kuzuia ugonjwa huu usiingie. 

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa kwa mujibu wa taarifa kutoka WHO watu 111 wametolewa taarifa kuugua ugonjwa huu wa Ebola na watu 75 sawa na Asilimia 67% wamefariki kutokana na ugonjwa huu, vifo ni zaidi ya Asilimia 50%. Maana yake kukiwa na wagonjwa 100, tunapoteza wagonjwa 50.

"Kwa mujibu wa Takwimu za shirika la Afya Duniani (WHO) Mpaka sasa, watu 111 wametolewa taarifa ya kuugua ugonjwa huu wa Ebola, watu 75 sawa na Asilimia 67% wamefariki, ndiomaana tunaogopa sana kama tutaruhusu ugonjwa huu utaingia nchini, vifo ni zaidi ya Asilimia 50%, maana yake tukiwa na wagonjwa 100 , tunaweza kupoteza wagonjwa 50, kwakweli tusikubali ugonjwa huu kuingia nchini "Alisema Waziri Ummy . 

.


0 on: "WAKUU WA MIKOA NCHINI WATAKIWA KUTENGA VITUO MAALUM VYA KUHUDUMIA WAGONJWA WA EBOLA."