Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 10 Oktoba 2018

DKT. NDUGULILE AAGIZA KUBORESHWA KWA MFUMO WA UKUSANYAJI TAKWIMU NCHINI

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo mbele ya Wadau mbali mbali wa masuala ya Afya baada ya kufungua mkutano wa masuala mbali mbali ya Afya uliofanyika jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akifungua Mkutano wa Wadau mbali mbali wa masuala ya Afya uliofanyika jijini Dar es salaam.

Naibu Katibu Mkuu anaeshughulikia masuala ya Afya TAMISEMI Dkt. Zainabu Chaula akiongea na Wadau mbali mbali wa masuala ya Afya katika mkutano uliofanyika jijini Dar es salaam.

Kiongozi Mkuu wa Mkutano wa Masuala ya Afya, hususani katika mfumo wa upatikanaji na usambazaji wa Dawa, Vifaa tiba na Vitendanishi Bw. Mavelle Tukai akiwakaribisha Wadau wa masuala ya Afya waliofika katika Mkutano huo uliofanyika jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea jambo na Mkurugenzi wa Bohari kuu ya Dawa nchini Bw. Laurean Bwanakunu, katikati ni Afisa mfamasia kutoka Wizara ya Afya Siana Mapunjo.

Wadau mbali mbali wa masuala ya Afya wakifuatilia kwa makini mgeni rasmi Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Faustine Ndugulile (hayupo kwenye picha)


DKT. NDUGULILE AAGIZA KUBORESHWA KWA MFUMO WA UKUSANYAJI TAKWIMU NCHINI.

Na WAMJW - Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameagiza kuboreshwa kwa mfumo wa ukusanyaji wa Takwimu nchini utaosaidia upatikanaji wa takwimu sahihi na zinazifanana katika taasisi zote.

Ameyasema hayo mapema wakati akifungua Mkutano wa masuala ya Afya, hususani katika mfumo wa upatikanaji na usambazaji wa Dawa, Vifaa tiba na Vitendanishi leo jijini Dar es salaam.

Dkt. Ndugulile alisema kuwa Serikali inataka kuona mifumo yote ya ukisanyaji Takwimu inaboreshwa mara moja huku akisisitiza kuwa mifumo hiyo ni lazima iweze kuwasiliana jambo litalosaidia kupata Takwimu sahihi na zinazofanana kwa mifumo yote.

"Tunataka kuona mnaboresha mfumo wa ukusanyaji Takwimu, Takwimu bado ni changamoto kubwa sana katika utoaji wa huduma za Afya na katika mfumo mzima wa usambazaji, na ni lazima kuhakikisha kuwa mifumo hii inawasiliana na inakuwa endelevu" Alisema Dkt. Ndugulile.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile amewaonya watumishi wa Serikali hususani kutoka Wizara ya Afya wanaokwamisha mawazo endelevu yanayopelekea kupiga hatua kwa Sekta ya Afya, na kuahidi kuwachukulia hatua endapo yeyote atabainika kufanya hivo.

" Muda wowote, mtu yeyote mwenye Mawazo mazuri na Endelevu kwaajili ya Maendeleo ya Sekta yetu ya Afya, njoo unione Mimi au Waziri wangu, milango yetu ipo wazi, wengine sisi hatuna urasimu, Serikali hii ya awamu ya tano haitaki ubabaishaji" Alisema Dkt Ndugulile.

Aidha, amewaagiza Waganga Wafawidhi wote nchini kuhakikisha wanaandaa orodha ya Dawa zilizopo kila mwanzo wa wiki ili kusaidia kufahamu orodha ya Dawa zilizopo na zinazohitajika kwa kipindi hicho, huku akisisitiza kumchukulia hatua yeyote ataebainika.

"Tumepata taarifa baadhi ya makampuni ya Dawa yanapita katika Hospitali zetu, hususani Hospitali kubwa na wanawarubuni Madaktari wetu kuandika kwa MSD orodha ya Dawa ambazo hazipo katika mwongozo wetu wa Serikali, tutachukua hatua Kali" Alisema Dkt Ndugulile.

Mbali na hayo Dkt Ndugulile amepiga marufuku Madaktari wote nchini kuandika Dawa kwa kutumia majina ya bishara na kuwataka kutumia majina ya asili ya Dawa hizo.

"Jukumu la Serikali sio kufanya Bishara ya kumtangazia mtu, mfano Panaldo sio jina lake kitaalamu, ukienda baadhi ya nchi unaweza usikute Panaldo jina lake halisi ni Parasetamo na ndio linatakiwa litumike" Alisema Dkt Ndugulile.







0 on: "DKT. NDUGULILE AAGIZA KUBORESHWA KWA MFUMO WA UKUSANYAJI TAKWIMU NCHINI"