Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 30 Oktoba 2018

SERIKALI YAAHIDI KUPELEKA GARI YA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA MANYONI

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile  akikagua cheti cha mgonjwa katika wodi ya akina mama wakati alipotembelea Hospitali ya wilaya ya Manyoni kuona hali ya utoaji huduma za afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akikagua madaftari ya wagonjwa waliolazwa katika wodi ya akina mama wakati alipotembelea Hospitali ya wilaya ya Manyoni kuona hali ya utoaji huduma za afya. kulia ni Mkuu wa wilaya hiyo Bi. Rahabu Solomon.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (Kulia) akifafanua jambo wakati alipotembelea kitengo cha kuzalisha chakula cha lishe kwa mama wajawazito na watoto katika Hospitali ya Mtakatifu Gasper. Kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali hiyo Fr. Seraphine Lesiriam.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na wananchi waliokuwa wakisubiri huduma Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Singida wakati alipofanya ziara hospitalini hapo kuona hali ya utoaji wa huduma za afya.


SERIKALI YAAHIDI KUPELEKA GARI YA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA MANYONI

NA WAMJW-SINGIDA

Serikali imetangaza neema ya kupeleka gari ya  wagonjwa (Ambulance)  katika Hospitali ya Wilaya ya Manyoni ili kutatua tatizo linaloikabidi Wilaya hiyo hususan ya vifo vitokanavyo na uzazi.

Ahadi hiyo imetolewa jana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati alipoitembelea hospitali hiyo kwa lengo la kutazama utoaji wa huduma za afya ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu katika mkoa wa Singida.

Dkt. Ndugulile amefikia uamuzi huo baada ya kusikiliza kero kutoka kwa wananchi wanaotumia hospitali hiyo ambapo wengi walisema kungekuwepo na gari ya wagonjwa kungeepusha vifo vya akina mama wajawazito na watoto pamoja na wagonjwa wanaohitaji huduma za dharura.

"Naomba niwaahidi wananchi wa Manyoni, Serikali imeagiza magari ya kubebea wagonjwa ambayk yanaweza kufika mwezi Disemba mwaka huu,hivyo nitahakikisha katika mgao wa magari hayo basi na hospitali hii ya Wilaya  inapata gari moja kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wa hapa. Alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha, Dkt.Ndugulile aliahidi kuwatafutia wataalam wa Afya watakaoweza kwenda  kupunguza uhaba wa watumishi wanaokabiliana nayo hospitali hiyo

Naye Mganga mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Atupele Mohamed alisema hospitali hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa majengo ikiwemo chumba cha huduma za uzazi ambapo uwezo wake kwa mwezi ni  kuzalisha akina mama 90 lakini kwa sasa huzalisha  wastani wa akina mama 400.

Aidha, Dkt. Atupele alisema Hospitali hiyo ina upungufu mkubwa wa watumishi wenye sifa, ambapo ina jumla ya watumishi 107 sawa na asilimia 53 ya watumishi wanaohitajika.

Dkt. Atupele alitaja   uhaba mkubwa wa watumishi hao  ni Madaktari, Wauguzi, Wataalamu wa mionzi na wataalamu wa kutoa huduma za usingizi.

Katika Wilaya hiyo Naibu Waziri huyo aliweza kutembelea  kutembelea kituo cha kulea wazee na wasiojiweza cha Sukamahela pamoja na Hospitali ya rufaa ya Mtakatifu Gasper iliyopo  Itigi na  kuridhika na hali ya utoaji wa huduma za afya katika Hospitali hiyo.

0 on: " SERIKALI YAAHIDI KUPELEKA GARI YA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA MANYONI"