Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 10 Oktoba 2018

VIJANA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA ILI KUEPUKA ATHARI ZA AFYA YA AKILI

Mganga Mkuu wa Serikali  Prof. Mohamed Bakari Kambi  akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati akitoa tamko la kuadhimisha siku ya afya ya akili ambayo huadhimishwa duniani kote kila ifikapo Oktoba 10.

Mtaalamu wa magonjwa ya akili kutoka hospitali ya Milembe Dodoma Dkt. Mwombeki akifafanua jambo juu ya magonjwa ya afya akili mbele ya waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa tamko la kuadhimisha siku ya afya ya akili ambayo huadhimishwa duniani kote kila ifikapo Oktoba 10.

Na WAMJW-DODOMA
Vijana wametakiwa kujiepusha na matumizi  ya madawa ya kulevya , makosa ya kimtandao, kucheza kamali na kukaa katika magenge ambayo yanaweza kupelekea kupata fikra mbaya zinazoweza kusababisha kuathirika kwa afya ya akili.

Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Serikali  Prof. Mohamed Bakari Kambi  Jijini Dodoma wakati akitoa tamko la kuadhimisha siku ya afya ya akili ambayo huadhimishwa duniani kote kila ifikapo Oktoba 10.
“Utumiaji wa mihadarati kuwa ni changamoto kubwa inayowakabili vijana katika mataifa yote pia utumiaji wa madawa ya kulevya na pombe vimehusishwa kwa kiasi kikubwa na tabia hatarishi ya ngono zembe na ajali za barabarani” alisema Prof. Kambi.
Prof Kambi amesema kuwa  sambamba na elimu kwa Umma  Wizara itaendelea kutoa matibabu ya afya ya akili katika hospitali zote za Umma nchini pamoja na kuendelea kutoa dawa za Methadone kwa watumiaji wa madawa ya kulevya katika mikoa ya Dar es salaam,Mbeya,Mwanza na Dodoma  hivi karibuni.
Aidha Prof. Kambi amesema kutokana na tafiti za shirika la afya duniani (WHO) zinaonesha vijana wanaoathirika na kupata matatizo ya akili ni wale walio katika umri wa kuanzia miaka 14, lakini wengi wao hawapati nafasi ya kutambulika na kupata matibabu katika wakati muafaka.
“Tafiti za shirika la afya duniani (WHO) zinaonesha takribani nusu ya magonjwa yote ya akili huanzia katika umri wa miaka 14 ambapo magonjwa ya akili na matumizi ya vilevi ni miongoni mwa changamoto kubwa sana za kiafya na kiusalama zinazoathiri rika hili la binadamu”. Amesema Prof. Kambi.
Prof. Kambi amesema kuwa  kujiua kunaaminika kuwa ni chanzo kikuu cha pili cha vifo vyote vinavyowakabili vijana wengi duniani ambapo Ugonjwa wa Sonona (Depression) umetajwa kushika nafasi ya tatu duniani katika magonjwa yote yanayoathiri vijana duniani.
Kwa mujibu wa Prof. Kambi amesema kuwa Takwimu za mwaka 2015 hapa nchini zinaonesha  vijana kuanzia miaka  13 hadi 17 walioko katika shule za misingi na sekondari zinaonesha kuwepo na dalili za Sonona, ambapo vijana zaidi ya asilimia 7 walionyesha kuwa na dalili hizo
Kwa upande wake mtaalamu wa magonjwa ya akili kutoka Hospitali ya Milembe Dkt. Damas Andrew  kuwa  matatizo ya unywaji pombe na uvutaji wa sigara yalitaarifiwa kwa kiwango sawa cha asilimia 5, huku asilimia 3.1 wakiripotiwa  kuvuta bangi katika maisha yao huku utafiti huo ulionesha kuwa robo ya vijana wote waliohojiwa waliripoti kufanyiwa uonevu na wenzao.
“Vijana wote waliohojiwa waliripoti kufanyiwa uonevu na wenzao ama kwa kupigwa, kusukumwa au kufungiwa madarasani kunakopelekea kupata athari ya akili”. Amesema Dkt. Damas
Dkt. Damas amesema utafiti umeripoti kuwepo kwa matukio mbalimbali ya ukatili kwa vijana kutoka kwa wazazi na walezi yanayosababisha kuzorotesha ya akili kwa watoto na vijana wanaowalea. Vilevile kiwango kikubwa cha unyanyasaji kimeripotiwa kufanyika katika mitandao ya kijamii dhidi ya watoto na vijana na kufanya changamoto hizi kuathiri kwa kiasi kikubwa afya ya akili.

0 on: "VIJANA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA ILI KUEPUKA ATHARI ZA AFYA YA AKILI"