Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 6 Novemba 2018

Makamu wa Rais Mama  Samia Suluhu  Hassan wakibadilishana mawazo  na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee  na Watoto  Mhe.Ummy Mwalimu tayari kwa UzinduZi wa Kampeni ya Tuwajushe  Salama kwenye  ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma leo

Makamu wa Rais akipitia  Ratiba  ya uzinduzi  wa Kampeni hiyo na MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge.Kampeni hiyo ina  lengo la kuhamasisha viongozi wa Serikali,Dini,Mashirika  yasiyo  ya kiserikali,wadau wa  Maendeleo na datos huduma za afya kuchangia katika juhudi za  kitaifa za kupunguza  vifo vitokanavyo  na uzazi  na watoto  wachanga


Baadhi ya Wakuu wa Mikoa wakifurahia Mambo wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimuelezea Makamu wa Rais vinavyoonesha ubora na mapungufu ya utoaji wa huduma za afya ya uzazi kwa mama na mtoto wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Jiongeze, Tuwavushe Salama.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizindua rasmi kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama yenye lengo la kuhamasisha viongozi wa Serikali, Dini, Mashirika yasiyo ya kiserikali, Wadau wa Maendeleo, Watoa huduma za afya, Familia na jamii kwa ujumla ili kuchangia katika juhudi za taifa za kupunguza vifo vinyotokana na uzazi na vifo vya watoto wachanga.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ahadi ya makubaliano ya uwajibikaji katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wachanga.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe wa kitabu cha muongozo wa pili wa kuzuia maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati uzinduzi huo.



MAMA SAMIA  AWASAINISHA WAKUU WA MIKOA AHADI YA MAKUBALIANO YA UWAJIBIKAJI WAKUPUNGUZA  VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI. 

NA WAMJ-DODOMA

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasainisha Wakuu wa mikoa yote nchini AHADI ya makubaliano ya uwajibikaji katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo cha Watoto wachanga nchini. 

Hayo yamefanyika leo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kitaifa inayolenga kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi nchini inayojulikana kwa jina la "JIONGEZE TUWAVUSHW SALAMA "  jijini Dodoma. 

"Leo nawasainisha makubaliano haya wakuu wa mikoa mkaifanyie kazi na kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga ntahitaji taarifa ya viashiria vya afya ya uzazi kila baada ya miezi 6 katika ofisi yangu", alisema Mhe. Samia. 

Aidha,Mhe. Samia amesema kuwa mbali na wakuu wa mikoa kuwasilisha taarifa hizo  kwake pia  kila baada ya miezi 3 wawasilishe Wizara ya Afya ili kuzifanyia kazi taarifa hizo na kutatua changamoto za vifo vitokanavyo na uzazi. 

Kwa mujibu wa Mhe. Samia amesema kuwa mbali na vikwazo vingine vinavyosababisha vifo vitokanavyo na uzazi tunatakiwa kuzingatia lishe bora wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua. 

Mbali na hayo Mhe. Samia Suluhu amesema kuwa mapambano haya zidi ya vifo vitokanavyo na uzazi ni la kila mtu kuanzia, Viongozi wa Serikali,  Jamii nzima inaotuzunguka, watumishi wa sekta ya afya, wanahabari pamoja na viongozi wa dini. 

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa takwimu ya mwaka  2017 za Wizara ya Afya zinaonesha kuwa wanawake milioni 2. 2 kila mwaka wanapata ujauzito na asilimia 85 hujifungua bila ya shida na asilimia 15 sawa na laki 3. 3 hupata matatizo mbalimbali yatokanayo na uzazi. 

"Kuna sababu mbalimbali zinazochangia vifo vitokanavyo na uzazi ikiwa kutokwa na damu nyingi kabla na baada ya kujifungua, asilimia 28, kifafa cha mimba asilimia 17, uchungu pingamizi asilimia 11, uambukizo asilimia 11 na mengineyo asilimia 11" alisema Waziri Ummy. 

Aidha,Waziri Ummy amesema kuwa wajawazito wanatakiwa kuhudhuria kliniki kwani ni asilimia 60 ndio wanaohudhuria kliniki angalau mara nne . 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binirith Mahenge amesema kuwa mkoa wake umepiga hatua katika ujenzi wa vituo vya afya mpaka kufikia 21 ndani ya miaka 3. 

"Licha ya ujenzi huo pia Serikali imeongeza bajeti ya dawa kwa upande wa mkoa wa Dodoma kutoka milioni 900 mpaka kufikia bilioni 4 kwa mwaka wa fedha 2018" alisema Dkt. Mahenge.

0 on: " "