Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 15 Novemba 2018

SERIKALI YAJIPANGA KUTOKOMEZA MAAMBUKIZI YA VVU KWA WATOTO WACHANGA.

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na wadau mbalimbali wa maendeleo na sekta ya afya hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma.

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akikata utepe kuashiria kuzindua chapisho la uchambuzi  wa masuala ya lishe wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma, wa pili kushoto ni Naibu Waziri OFisi ya Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara .

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akionesha moja ya chapisho la uchambuzi  wa masuala ya lishe wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma, wa pili kushoto ni Naibu Waziri OFisi ya Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara .

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akifuatilia mada iliyokuwa inawasilishwa na moja ya wawasilishaji hayupo pichani  wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma, wa pili kulia ni Naibu Waziri OFisi ya Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara .

Baadhi ya  wadau mbalimbali wa maendeleo na sekta ya afya wakifuatilia kwa makini hotuba ya Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma.


NA WAMJW-DODOMA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema serikali ina mpango madhubuti wa kuhakikisha wamama wajawazito hawawaambukizi watoto walio tumboni Virusi vya Ukimwi na kipindi wanapozaliwa.

Waziri Ummy amesema hayo leo wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya maendeleo ya jamii ikiwa ni pamoja na masuala ya lishe, uliofanyika katika ukumbi wa Hazini, Jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema hadi hivi sasa asilimia 99 ya wajawazito wenye maambukizi ya VVU wanapewa huduma za kumkinga mtoto asipate maambukizi hayo huku la serikali ifikapo mwaka 2020 ni kuhakikisha  hakuna mtoto atakayezaliwa na maambukizi ya VVU.

“Sasa hivi asilimia 99 ya wanawake wajawazito wote wenye maambukizi  ya VVU tumewaingiza katika mpango wa dawa, na hiyo asilimia moja bado hatujawafikia ila kwa nguvu na msukumo tuliouweka juzi wa kuwasainisha Wakuu wa Mikoa kwenda kufuatilia masuala ya afya ya mama na mtoto, tunaamini hakuna mtoto yeyote Tanzania atakayezaliwa na maambukizi ya UKIMWI”. Amesema Waziri Ummy.

Katika Uzinduzi huo, Waziri Ummy ameipongeza Wizara ya Fedha na Mipango kupitia kwa Waziri wake Mhe. Dkt. Philipo Mpango  inavyojikita katika mipango ya kuendeleza wanawake na watoto kwa kutoa huduma bora za afya, elimu, maji na masuala ya maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na Shirika la Watoto Duniani (UNICEF) imefanya uchambuzi wa bajeti katika sekta mtambuka ya jamii, hususani katika elimu, afya, Virusi vya Ukimwi, maji, usafi wa mazingira na lishe kwa lengo la kuboresha upangaji na utekelezwaji wa masuala ya mama na mtoto.

Pamoja na hayo, uzinduzi wa machapisho hayo umelenga kupunguza tatizo la lishe linalosababisha udumavu kwa watoto walio katika umri mdogo. Ambapo katika ripoti iliyotolewa katika mkutano wa IMF na Benki ya dunia uliofanyika nchini Indonesia mwezi Oktoba mwaka 2018, inaonesha Tanzania inashika nafasi ya 128 kati ya nchi 157 duniani katika kipimo cha ubora wa nguvukazi  katika uwekezaji wa rasilimali watu hususani katika sekta ya afya na elimu ya lishe.

Kufuatia hali hiyo, Tanzania inaonekana kuwa na matatizo ya udumavu, elimu ya lishe na afya kwa watoto wenye umri mdogo ambapo serikali inafanya kazi kubwa ya kuhakikisha elimu ya lishe inawafikia wazazi na jamii kwa ujumla ili kupambana na tatizo la udumavu. Na kufikia mwaka 2015 tatizo la udumavu limeshuka kutoka asilimia 34 kutoka asilimia 42 mwaka 2010. Alisema Waziri huyo.

Tatizo la lishe limeonekana kupungua nchini huku viashiria vya tatizo hilo vikipungua ambavyo ni uzito pungufu umeshuka kutoka asilimia 16 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 14 mwaka 2015/16, pamoja na ukondefu wa mwili kuendelea kubakia chini ya asilimia 5 kwa mwaka 2015/16.


0 on: "SERIKALI YAJIPANGA KUTOKOMEZA MAAMBUKIZI YA VVU KWA WATOTO WACHANGA."