Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumapili, 9 Desemba 2018

HOSPITALI MPYA 67 ZA WILAYA KUJENGWA NCHINI

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile (wakati kati) akishuhudia makabidhiano ya mabenchi yakukalia, wakwanza kulia ni Meneja wa NMB kanda ya Dar es salaam Bw. Badru Idd  akimpa mkono Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. John Rwegasha katika tukio la makabidhiano ya mabenchi yakukalia 52 lililofanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akiteta jambo na Meneja wa NMB kanda ya Dar es salaam Bw. Badru Idd katika tukio la makabidhiano ya mabenchi yakukalia 52 yenye thamani ya Mikioni 10, lililofanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akikagua mabenchi hayo baada ya makabidhiano leo, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akimuaga Meneja wa NMB kanda ya Dar es salaam Bw. Badru Idd  baada ya tukio la makabidhiano ya mabenchi yakukalia 52 yenye thamani ya shilingi Milion 10, lililofanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es salaam.

Jengo la mahala pakupimzikia la Kitengo cha Dharura, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili


HOSPITALI MPYA 67 ZA WILAYA KUJENGWA NCHINI

Na WAMJW - Dar es salaam.

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee ma Watoto inatarajia kujenga Hospitali za Wilaya 67, ikiwa ni mkakati na jitihada za Serikali kuboresha Huduma za Afya na kupunguza adha kwa wananchi kupata huduma za afya.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile leo wakati akipokea viti kwaajili yakupumzikia hospitalini, kutoka benki ya NMB katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa kwa sasa zipo Hospitali za Wilaya 80, hivyo Serikali imeamua kuongeza hospitali za Wilaya takribani 67 ikiwa ni mkakati wa kuboresha huduma za Afya hususani huduma za mama na mtoto.

"Mwaka huu tunajenga Hospitali za Rufaa, Mikoa ambayo haina, tunajenga Hospitali za Wilaya 67, na tunahospitali kama 80 za Wilaya," alisema Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa Serikali imeboresha vituo vya Afya takribani 200 ili kusaidia kutoa huduma za upasuaji, hivyo kusaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa kupata huduma katika Hospitali za Wilaya na za Rufaa za Mkoa.

Sambamba na hayo Dkt. Ndugulile ameishukuru Benki ya NMB kwa kutenga Asilimia 1 ya mapato yanayotoka kwenye faida kuelekeza kwenye Jamii ya Watanzania hususani katika huduma za Afya.

"Niwashukuru sana NMB bank, kwa kutenga mapato yenu na faida yenu kuielekeza kwenye jamii, na nimefurahi zaidi, kusikia kwamba mmewekeza zaidi katika huduma za Jamii, Sisi kama Serikali tunawapongeza" alisema Dkt Ndugulile

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa vitawasaidia sana wagonjwa ambao wanatoka sehemu mbali mbali ya nchi kupata maeneo mazuri yakuweza kukaa wakati wagonjwa wao wakipata huduma za Afya, hivyo niwaombe sana msiishie hapo kwani bado kuna maeneo mengi yanahitaji msaada.

Nae Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam Bw. Badru Idd amesema kuwa benki ya NMB huwa inalipa fadhira kwa Jamii baada ya kupata faida, kwa kuleta maendeleo, ikiwemo kujenga miundombinu, na kuboresha huduma za Jamii ili watanzania waweze kunufaika na kutoka Benki yao ya NMB.

"Kwa mujibu wa taratibu za Benki ya NMB huwa tunatoa Asilimia 1% kwenye pato ambalo tumepata kwa mwaka huo, mathalani mwaka Jana tumeingiza milioni 94, hivyo tunatoa Asilimia 1% ya Milioni 94 na kuirudisha kwa Jamii" alisema Bw. Badru Idd.

Bw. Badru Idd aliendelea kusema kuwa hiyo Asilimia 1% ipo kwenye mafungu makubwa 3, kundi la kwanza NMB inapenda sana kutoa huduma kwenye sekta ya Afya, kundi la pili ni Sekta ya Elimu na kundi la tatu ni huduma kwenye majanga yanayotokea.

Mwisho.

0 on: " HOSPITALI MPYA 67 ZA WILAYA KUJENGWA NCHINI"