Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 6 Desemba 2018

OCEAN ROAD KUTUMIA MIONZI YA NYUKLIA KUCHUNGUZA AFYA YA MOYO WAGONJWA WA SARATANI

Mteknolojia Tiba ya Mionzi (Nuclear Medicine) wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dk. Faraji Sabaya akimuandaa mgonjwa kwa ajili ya uchunguzi huo.

Daktari Bingwa wa Uchunguzi na Tiba ya magonjwa mbalimbali kwa kutumia Mionzi ya Nyuklia wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Tausi Maftah akiwafafanulia jambo waandishi wa habari (hawapo pichani)

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dk. Julius Mwaiselage akifafanua jambo kuhusu huduma hiyo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani)

Na Mwandishi wetu - Dar Es Salaam.

TAASISI ya Saratani Ocean Road (ORCI) imezidi kuimarisha huduma zake za uchunguzi na tiba kwa wagonjwa wa saratani ambapo awamu hii imeanzisha huduma mpya ya uchunguzi wa afya ya moyo kwa kutumia mionzi ya nyuklia.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dk. Julius Mwaiselage amesema huduma hiyo imelenga zaidi kutolewa kwa wagonjwa wa saratani nchini.

Amesema kabla ya kuanzisha huduma hiyo wagonjwa wengi walilazimika kupatiwa rufaa kwenda kuifuata nje ya nchi.

“Serikali ilipoanzisha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ilitusaidia mno, tunashirikiana nao kwa ukaribu lakini kwa upande wa uchunguzi kwa kutumia mionzi bado tulikuwa tunawapa rufaa wagonjwa kwenda nje ya nchi,” amesema.

Ameongeza “Kwa mara ya kwanza nchini ORCI inaanzisha huduma ya uchunguzi wa afya ya moyo kwa kutumia mionzi ya nyuklia, inasaidia kujua afya ya moyo kwa ujumla na iwapo dawa tunazompatia mgonjwa zinamuathiri au la, ili kuboresha zaidi matibabu yake.

“Hivyo, tutatoa huduma hii lakini pia tutaendelea kushirikiana na wenzetu wa JKCI kufanya uchunguzi kwa tiba ya namna hii (ya mionzi),” amebainisha.

Dk. Mwaiselage amesema uchunguzi huo unafanyika kwa kutumia kipimo kiitwacho kitaalamu Myocardiac Perfusion Scan na kingine Multigated Acquisition Scan na mashine maalum ya mionzi iitwayo kitaalamu Gamma Camera.

Dk. Mwaiselage amesisitiza taasisi hiyo inazidi kuboresha huduma zake na kwamba hivi karibuni Rais John Magufuli atakwenda kuzindua rasmi mashine zingine mpya za uchunguzi zilizofungwa.

Awali  Daktari Bingwa wa Uchunguzi na Tiba ya Magonjwa mbalimbali kwa kutumia mionzi ya nyuklia (nuclear medicine physician) ORCI, Tausi Maftah amesema huduma hiyo itasaidia kuimarisha matibabu kwa wagonjwa hao

Naye, Mtaalamu wa Tiba hiyo, Profesa Raphael Giubbini kutoka Italia amesema huduma hiyo ni muhimu mno kwa wagonjwa wa saratani na ndiyo inayotumika katika nchi nchi mbalimbali hivi sasa hasa zile zilizoendelea.

 MWISHO

0 on: "OCEAN ROAD KUTUMIA MIONZI YA NYUKLIA KUCHUNGUZA AFYA YA MOYO WAGONJWA WA SARATANI"