Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 31 Desemba 2018

SERIKALI YAAPA KUWACHUKULIA HATUA WAMILIKI WA MAABARA BINAFSI ZOTE ZISIZOKIDHI VIGEZO





Mkurugenzi wa Tiba, Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.  Dorothy Gwajima akisisitiza jambo katika mkutano na Waandishi wa Habari kuhusu utekelezaji wa sheria ya umiliki wa maabara binafsi za Afya.

Kaimu Msajili wa Bodi ya Maabara Binafsi za Afya akijibu maswali ya Waandishi wa habari wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari uliohusu  utekelezaji wa sheria ya umiliki wa maabara binafsi za Afya.

Wajumbe wa Sekretariet ya Maabara binafsi pamoja na kamati ya Afya ya msingi za manispaa za jiji la Dar es salaam wakifuatilia maelekezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Tiba, Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.  Dorothy Gwajima kuhusu utekelezaji wa sheria ya umiliki wa maabara binafsi za Afya katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam


SERIKALI YAAPA KUWACHUKULIA HATUA WAMILIKI WA MAABARA BINAFSI ZOTE ZISIZOKIDHI VIGEZO


Na WAMJW - DSM
 
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema kuwa ifikapo Januari 15 mwaka 2019 Wamiliki wote wa Maabara binafsi ambao hawajatimiza vigezo vya uendeshaji vya Bodi ya usimamizi wa Maabara binafsi.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Tiba Dkt. Dorothy Gwajima leo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam.

Dkt. Gwajima alisema kuwa kipindi cha  kuelimishana juu ya umuhimu wakutimiza sheria na vigezo vya uendeshaji wa Maabara umekwisha hivyo Wamiliki wa Maabara hizo wanapaswa kufuata vigezo hivyo kabla ya Januari 15 mwaka 2019.
 
 'Wako wamiliki wa maabara binafsi ambao, wameamua kuamini kwenye kufuatiliwa kila siku, sasa ufuatiliaji na uelimishaji uliokwisha fanyika awali unatosha, wakati wa kuelewa somo umepita sasa ni saa ya KAZI TU !. Imefika zamu ya wamiliki wa maabara binafsi kwenda kutimiza wajibu wao bila shurti tena pasipo kuendelea kuisababishia Serikali gharama za ziada" alisema Dkt.Gwajima

Aidha, Dkt. Gwajima amesema kuwa kutimiza wajibu wa matakwa ya kisheria kwa wamiliki husika wa mabaara binafsi ni pamoja na;- 
 
1. Kila mmiliki kuhakikisha amekidhi vigezo vyote vya kumiliki maabara binafsi kama ambavyo amekuwa akielekezwa na wataalamu walioko kila halmashauri na mikoa husika,

2. Kuhakikisha amelipa ada na tozo stahiki zikiwemo malimbikizo ya nyuma na faini zote stahiki.

3. Amepata risiti halali za malipo hayo

4. Anaendelea kulipa tozo stahiki kila mwaka ili, kuwezesha bodi husika kutimiza wajibu wake wa kufanya uhakiki wa ubora wa huduma kwa kila kituo kila mwaka na kufanya ukaguzi maalumu wa vituo husika kama vinaendelea kuwa katika viwango  stahiki kama siku vilipopewa kibali cha kutoa huduma husika.
 
Mbali na hayo Dkt Gwajima amesema kuwa Bodi imeendelea kuimarisha ushirikiano wake na vyombo vyote vya Serikali ngazi zote kuanzia OR TAMISEMI na ngazi zake zote za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na sasa, huku ikiandaa orodha ya maabara binafsi nchi nzima na itaweka katika vyombo vya habari na itasambaza kwa wadau wote.
 
Dkt Gwajima aliendelea kusema kuwa yeyote ambaye hayumo katika orodha hiyo asithubutu kutoa huduma hizo maana, mamlaka za Serikali za mitaa zitambaini na taarifa zitafika mahali sahihi mara moja na hatua kali zitachukuliwa.
 
Sambamba na hayo Dkt Gwajima ametoa wito kwa mamlaka zote za Serikali ngazi zote kuendelea kupeana taarifa kwa haraka zaidi na kujipanga vema zaidi katika kuhakikisha hakuna mvunja sheria anathubutu kutoa huduma za kijamii bila kibali.
 
MWISHO.

0 on: "SERIKALI YAAPA KUWACHUKULIA HATUA WAMILIKI WA MAABARA BINAFSI ZOTE ZISIZOKIDHI VIGEZO"