Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 18 Desemba 2018

TFDA YAFIKIA NGAZI YA TATU YA UDHIBITI WA DAWA KIMATAIFA.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu (kulia) akipokea waraka wa utambuzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa-TFDA ya kufikia ngazi ya nne ya udhibiti wa bidhaa za dawa kutoka kwa Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Tigest Ketsela Mengestu (kushoto).

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu (kulia) akipokea waraka wa utambuzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa-TFDA ya kufikia ngazi ya nne ya udhibiti wa bidhaa za dawa kutoka kwa Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Tigest Ketsela Mengestu (kushoto).
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu hali ya udhibiti wa bidha za dawa chini ya TFDA.


Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Tigest Ketsela Mengestu akisoma taarifa ya hali ya udhibiti wa dawa nchini kwenye kikao na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika ofisi za Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA)

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini Bw. Adam Fimbo (aliyesimama) akisema jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kupokea waraka wa utambulisho wa mamlaka hiyo kufikia ngazi ya nne ya udhibiti wa dawa nchini.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akisoma waraka kwa utambuzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa-TFDA ya kufikia ngazi ya nne ya udhibiti wa bidhaa za dawa. aliye upande wa kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Tigest Ketsela Mengestu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akisikiliza maoni toka kwa mteja Bw. Fareh Abdul mkazi wa Dar es Salaam aliyefika katika ofisi za Mamlaka ya Chakula na Dawa kupata huduma.

Picha ya pamoja Mgeni Rasmi, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliye meza kuu katikati akiwa na viongozi mbali mbali pamoja na wajumbe wa mkutano.


Na WAMJW - Dar Es Salaam.


Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) imetambuliwa rasmi na Shirika la Afya Duniani (WHO) kufikia ngazi ya tatu ya ubora wa mifumo ya udhibiti wa dawa na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kufikia hatua hiyo.

Hayo yamejiri leo wakati Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wakati upokeaji wa waraka wa utambulisho wa ngazi ya tatu kwa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) toka WHO.

“Tunaposema ngazi ya tatu ya udhibiti wa bidhaa za dawa maana yake ni kuwa Tanzania sasa tumepiga hatua katika upatikanaji wa dawa bora, zilizo salama na zenye ufanisi pale tuu ambapo zitakapo kuwa zimethibitishwa na TFDA” amesema Waziri Ummy.

Waziri huyo amesema kuwa dawa yoyote ambayo imetengenezwa aidha ndani au nje ya Tanzania na kuthibitishwa, kukaguliwa na kupewa cheti na TFDA maana yake dawa hiyo ni bora, salama na yenye ufanisi uliokusudiwa kwa matumizi ya binadamu.
 “Kama ni dawa ya kutibu ugonjwa wa malaria basi ni dawa ya kutibu malaria kweli na si vinginevyo” alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy ameipongeza TFDA kwa kufikia hatua hiyo na kusema serikali itaendelea kuboresha mifumo iliyopo ili kuondoa dawa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu.

Naye Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzaina Dkt. Tingest Ketsela Mengestu amesema kuwa ni jambo la kujivunia kwa Tanzania kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuwa na mfumo mzuri wa udhibiti wa bidhaa za dawa.

“Nachukua nafasi hii kuipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kuweka mazingira mazuri yaliyoleta mafanikio haya. TFDA imefanya maboresho makubwa kwa kuhakikisha dawa zilizopo katika soko ndani ya Tanzania zina usalama, ubora na ufanisi wa hali ya juu kwa matumizi ya binadamu” amesema Dkt. Tingest.

Tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 2003, Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) imekuwa ikijiwekea mikakati ya kuboresha mifumo ya utendaji ili kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Bw. Adam Fimbo amesema kuwa Tathimini mbalimbali zimefanyika kutoka taasisi tofauti duniani kukagua mifumo ya umahiri katika ukaguzi wa vyakula na dawa hivyo kupelekea mamlaka hiyo kufikia ngazi ya tatu.

“Nchi nyingi bado zinasita kuwaita WHO kuwafanyia tathimini lakini sisi tuliamini tunaweza kufanyiwa tathimini kutokana na mifumo mizuri tuliyoiweka” alisema Bw. Fimbo na kuendelea kwa kusema kuwa “hatua hii ni kubwa, sasa Tanzania imeingia katika kundi la nchi chache duniani ambazo zimefikia ngazi ya tatu”

Mwisho

0 on: "TFDA YAFIKIA NGAZI YA TATU YA UDHIBITI WA DAWA KIMATAIFA."