Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 21 Desemba 2018

WAZIRI UMMY AWAASA WATOA HUDUMA ZA AFYA KUZINGATIA MAADILI NA WELEDI WA TAALUMA YAO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiteta jambo na mbunge wa Nachingwea Mhe. Elias Hassan Masala wakati wa kikao na viongozi wa vyama vya vya Ushirika vya Wakulima (AMCOS), kutoka Wilaya ya Nachingwea Mkoa wa Lindi.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Viongozi wa vyama vya Ushirika vya Wakulima (AMCOS), kutoka Wilaya ya Nachingwea Mkoa wa Lindi, pindi alipokutana nao ili kuwahamasi kujiunga na Bima ya Afya.


Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bw. Benard Konga akitoa maelekezo mbele ya mgeni rasmi Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu na Viongozi wa vyama vya ushirika (Hawapo kwenye picha) kuhusu namna mfuko huo unavyofanya kazi katika kuwahudumia wananchi hususani Wakulima kupitia kifurushi cha Ushirika Afya.
WAZIRI UMMY AWAASA WATOA HUDUMA ZA AFYA KUZINGATIA MAADILI NA WELEDI WA TAALUMA YAO

Na WAMJW – NACHINGWEA,LINDI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amewaasa Watoa huduma za Afya wote nchini kuzingatia Sheria, Maadili na Weledi wa taaluma yao pindi wanapotoa huduma kwa wagonjwa.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya utoaji Ubora wa Huduma za Afya na uhamasishaji kwa Wananchi/Wakulima kutumia Bima ya Afya (UshirikaAfya) katika Mkoa wa Lindi, Wilaya ya Nachingwea.

Waziri Ummy amesema kuwa yeyote katika katika Sekta ya Afya atakaekutwa anajihusisha na vitendo vyovyote vya Rushwa atachukuliwa hatua kali ikiwemo kufutiwa leseni yake ya kutoa huduma za afya popote nchini. 

“Masuala yakuchukua Rushwa tuachane nayo, na kama tukikukuta hatutakuwa na msalia mtume na wewe, hatuwezi kukubali, kama umeamua kujitolea kuwahudumia Wagonjwa, wahudumie wagonjwa, suala la rushwa hatutalifumbia macho” Alisema Waziri Ummy

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy alikutana na Viongozi wa vikundi muhimu vya Ushirika vya Wakulima (AMCOS) lengo likiwa ni kuwahamasisha ili wajue umuhimu wa kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya kisha wakawahamasishe Wakulima wengine katika maeneo yao.

Waziri Ummy alisema kuwa katika kila Watanzania 100, Watanzania 67 wanapata huduma za afya kwa kulipa papo kwa papo jambo ambalo linawaumiza Wakulima wengi kutokana na matibabu kuwa gharama kubwa bila kutumia Bima ya Afya.

“Wananchi wanatakiwa kuchangia huduma za Afya, kila Watanzania 100,  Watanzania 67 wanalipa fedha hapo hapo, maana yake wanaolipa malipo ya papo kwa hapo wanatumia fedha nyingi zaidi kuliko wanaolipa kwa kutumia Bima ya Afya” Alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa, Serikali kupititia mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, wameanzisha utaratibu mpya wa Bima ya Afya kwaajili ya Wakulima (Ushirika Afya), lengo ni kuona namna ya kuwakwamua Watanzania kupata huduma za matibabu bila ya kikwazo cha fedha 

“Katika kuona ni jinsi gani tunaweza kuwakwamua Watanzania kupata huduma za afya bila kikwazo chochote cha fedha, Serikali kupitia mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, tumeanzisha utaratibu mpya wa bima ya afya kwaajili ya wakulima (Ushirika Afya)” alisema Waziri Ummy.

MWISHO.

0 on: "WAZIRI UMMY AWAASA WATOA HUDUMA ZA AFYA KUZINGATIA MAADILI NA WELEDI WA TAALUMA YAO"