Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 7 Machi 2019

DUP NA MATOKEO BORA YA SEKTA YA AFYA NCHINI


DUP NA MATOKEO BORA YA SEKTA YA AFYA NCHINI

#Serikali yaTanzania imejiwekea mkakati wa Kitaifa wa kuboresha matumizi ya takwimu za afya, utakaosaidia kuboresha utoaji wa huduma katika Sekta ya Afya,  ambao unaitwa 'Data Use Partnership' #DUP

# Mpango huu unalenga kujenga utamaduni wa ukusanyaji na matumizi ya takwimu katika sekta ya afya.

# Uwepo wa Mifumo mingi iliyopo katika sekta ya afya unapelekea mifumo hiyo kushindwa kuwasiliana (visiwa vya taarifa).

#Mpango huu umeanzishwa ili kuboresha mfumo mzima wa taarifa na takwimu, hali itakayosaidia kuimarisha utoaji huduma katika Sekta ya Afya.
                
# Mpango wa kuboresha matumizi ya takwimu utasaidia kutatua changamoto mbalimbali katika Sekta ya Afya mfano Magonjwa ya Mlipuko, kutambua vituo vyenye utendaji  unaoridhisha na usioridhisha

#Mpango wa kuboresha matumizi ya takwimu za afya Tanzania hauishii kuhamasisha mfumo wa Afya wa kidijitali tu, pia Unajenga uwezo wa kutumia takwimu hizo.

#Sekta ya afya lazima iingize utamaduni wa matumizi ya taarifa ili kuimarisha utawala na sera.

#Matumizi sahihi na ya mara kwa mara ya takwimu yatapelekea maamuzi sahihi, mifumo kuboreshwa na matokeo mazuri katika sekta

# Takwimu sahihi zinazopatikana kwa wakati zinawawezesha wahudumu wa afya kufanya maamuzi sahihi pale wanapotoa huduma za Afya katika vituo vyao.

# Mpango wa kuboresha matumizi ya takwimu za afya unafanya kazi kuakikisha kila mmoja kuanzia watumishi wa serikali, wahudumu na wateja wa afya wanaweza kufanya maamuzi sahihi ya afya.

0 on: "DUP NA MATOKEO BORA YA SEKTA YA AFYA NCHINI"