Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 8 Aprili 2019

WATOA HUDUMA ZA TIBA ASILI WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA IMANI ZA KISHIRIKINA KATIKA HUDUMA ZAO










Picha mbalimbali zikionesha Maafisa kutoka Baraza la  Tiba Asili na Tiba Mbadala wakiongozwa na Msajili Dkt. Ruth Suza wakitoa elimu kwa Waganga wa Tiba Asili na Tiba Mbadala katika Mikoa ya Kagera, Geita na Mwanza.


WATOA HUDUMA ZA TIBA ASILI WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA IMANI ZA KISHIRIKINA KATIKA HUDUMA ZAO

Na WAMJW-MWANZA

Watoa huduma za tiba asili na tiba mbadala wametakiwa kutojihusisha na imani za kishirikina ikiwa ni pamoja na uchawi katika kutoa huduma kwa wananchi wanaohitaji huduma hizo.

Hayo yamesemwa na Msajili kutoka Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala Dkt. Ruth Suza wakati akiongea na Waganga wa tiba asili na tiba mbadala wa mikoa ya Mwanza, Kagera na Geita waliojitokeza katika kikao kazi kilichohusisha wataalam kutoka Baraza hilo lililo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Dkt. Ruth amesema kuna baadhi ya Watoa huduma wa tiba za asili wanaojihusisha na mambo ya kishirikina ikiwa ni pamoja na kupiga ramli chonganishi, kuhitaji viungo vya binadamu kwa ajili ya kutengeneza dawa na kuwa na nyara za serikali ambazo kiuhalisia hazitakiwi katika matibabu hayo.

“Ninawataka waganga wote kutojihusisha na tiba za kishirikina zinazoenda sambamba na uchawi, kupiga ramli chonganishi na kutumia nyara ambazo hazina vibali kama mikia na ngozi za wanyama wa porini. Endapo mganga yeyote akikutwa na kasoro hizi baraza halitasita kumfutia usajili mhusika na atashitakiwa kwa mujibu wa sheria zilizowekwa na Serikali”. Amesema Dkt. Ruth.

Aidha, Dkt. Ruth amewataka waganga hao kufuata taratibu zilizowekwa na Serikali ikiwa ni pamoja na kupata vibali vya vitendea kazi vyao hasa nyara za Serikali zinazotokana na wanyama, nyoka, ndege na wadudu wa porini, ambapo vibali hivyo vinatolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii.

Dkt. Ruth pia amewataka waganga hao kutunza siri za wagonjwa wanaowatibu ikiwa ni haki ya msingi ya mgonjwa kama hospitali zinavyofanya. Vile vile Dkt. Ruth amewataka waganga wa jadi kuwapeleka Hospitalini haraka wagonjwa walioshindwa kupata ahueni kwa dawa za jadi ili kupunguza vifo vinavyoweza kuepukika.

Kwa upande wao Waganga wa mkoa hiyo wametoa kero zao ikiwa ni pamoja na  kukamatwa mara kwa mara na vyombo vya usalama wanapokua katika kazi zao, dawa zao kutosajiliwa kwa wakati na kupata leseni kutoka Baraza. Hivyo kulitaka baraza hilo kuhakikisha Serikali inawatambua kwa kuwapa vibali na kusajili dawa zao ambazo kwa kiasi kikubwa zimekua tegemeo kwa wananchi wengi wenye matatizo mbalimbali.

Baraza la tiba asili na tiba mbadala limeendelea kufanya zoezi la ukaguzi nchi nzima kwa ajili ya kuangalia usajili na vibali kwa waganga wanaotoa huduma. Ambapo zoezi hili limeanzia mkoa wa Dar Es Salaam, Kagera, Geita na Mwanza na kufuatiwa na mikoa mingine.


0 on: "WATOA HUDUMA ZA TIBA ASILI WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA IMANI ZA KISHIRIKINA KATIKA HUDUMA ZAO"