Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 18 Aprili 2019

WAZIRI UMMY ATEMBELEWA NA BALOZI WA NORWAY JIJINI DODOMA








Na WAJMW-Dodoma

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Bi. Elisabeth Jacobsen katika ofisi za Wizara zilizopo jijini Dodoma.

Katika mazungumzo hayo yaliyolenga uboreshaji wa sekta ya afya nchini, Balozi Elisabeth amesema Serikali ya Norway itaendelea kusaidiana na Serikali ya Tanzania katika kuboresha sekta ya afya hasa katika kukabiliana na magonjwa ya Malaria, Kifua Kikuu, UKIMWI na ukosefu wa lishe bora.

Bi. Elisabeth amesema Serikali ya Norway itaendelea kuisaidia Tanzania katika sekta ya afya kupitia Shirika la GAVI ambalo linajihusisha na ununuaji na usambazaji wa chanjo kwa nchi wanachama wa shirika hilo.

Aidha, Balozi huyo amesema kupitia mfuko wa Global Fund utawezesha Serikali  kukabiliana na magonjwa ya Malaria, TB na UKIMWI na hivyo kuwezesha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zitakazofikia malengo ya maendeleo endelevu yaliyoanzishwa na Umoja Mataifa.

Kwa upande wake Waziri Ummy ameishukuru Serikali ya Norway kupitia Balozi huyo na Mifuko wa GAV, GF na GFF ambayo imesaidia kwa kiasi kikubwa kwa watoto kupata chanjo hadi kufikia asilimia 98 nchini. Pia Waziri huyo ameushukuru mfuko wa Global Fund kwa kusaidia kusambaza dawa za kufumbaza Virusi kwa UKIMWI(ARV) na kuwafikia watumiaji Milioni 1.1 mwaka 2018 kutoka watumiaji 965,000 mwaka 2017.

Lakini pia Waziri Ummy ameishukuru Global Fund kwa kuwezesha kuboresha huduma za upatikanaji wa huduma za mama na mtoto nchini na kuepusha vifo vinavyoweza kutokea kwa sababu ya uzazi .

Pamoja na hayo, Waziri Ummy amemuomba Balozi huyo kuisadia Serikali katika harakati za kuwawezesha wanawake kupambana na umasikini kwa kutoa mikopo kwenye vikundi vyao ili waweze kujihushisha na shughuli za maendeleo na kujikwamua kiuchumi.

Kwa upande wa lishe, Waziri Ummy amesema Serikali imeshaanza uhamasishaji wa Lishe Bora kupitia taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC) kwa kutoa elimu ya lishe kwa watoto walio chini ya miaka mitano ili kukabiliana na udumavu ambao kwa kiasi kikubwa umeathiri ukuaji wa watoto katika baadhi ya mikoa nchini.

0 on: "WAZIRI UMMY ATEMBELEWA NA BALOZI WA NORWAY JIJINI DODOMA"