Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 22 Agosti 2019

CHUPA 51819 ZAIDI ZA DAMU SALAMA ZAKUSANYWA KWA MWAKA 2018/2019

Meneja Mpango wa Taifa wa Damu Salama Dkt.Magdalena Lyimo akiwasilisha mada ya hali ya upatikanaji damu kwenye kikao cha Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri unaoendelea jijini Dodoma

Wadau wa sekta ya afya ambao ni wastaafu Dkt.Deo Mtasiwa ambaye alikua ni Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI  na Bi.Jane Ndyetabula ambaye alikua kamishna wa ustawi wa jamii wakifuatilia uwasilishaji wa mada wakati wa kikao kazi hicho.

Mmoja wa washiriki wa kikao kazi hicho akiuliza swali


CHUPA 51819 ZAIDI ZA DAMU SALAMA ZAKUSANYWA KWA MWAKA 2018/2019

Na. Catherine Sungura,WAMJW-Dodoma

 Mpango wa damu salama umefanikiwa kukusanya chupa  51819 sawa  na asilimia ishirini zaidi ya malengo waliyojiwekea kwa mwaka 2018/2019.

Hayo yameelezwa leo na meneja mpango wa taifa wa damu salama Dkt. Magdalena Lyimo wakati akiwasilisha mada ya upatikanaji wa damu kwenye kikao kazi cha waganga wakuu wa mikoa na halmashauri  kinachoendelea jijini hapa.

Dkt. Lyimo amesema kwamba kwa mwaka 2018/2019
wizara ya afya kupitia mpango huo uliweka malengo ya kukusanya kiasi cha chupa 309376 nchi nzima ikilinganishwa na chupa 257557 zilizokusanywa mwaka 2017/2018.

Hata hivyo Dkt. Lyimo alisema kuwa wameweza kukusanya chupa 309,376 sawa na,asilimia sitini ya mahitaji ya nchi kulingana na idadi ya wananchi waliopo “tumeweza kufanikiwa kuvuka lengo la kukusanya chupa za damu zaidi na hii ni kutokana na uelewa mkubwa wa wananchi wa kuelewa umuhimu wa kuchangia damu katika kuokoa maisha hususani akina mama wajawazito na wahitaji wengine wa damu".Alisema.

Aidha, Dkt. Lyimo alitaja makundi ya wachangia damu kuwa wanawake  ni asilimia 14 pekee huku idadi ya wanaume ikiwa ni asilimia 86 hapa nchini.

Hata hivyo alisema hali ya maambukizi  ya magonjwa kwa damu zinazobainika katika ukusanyaji huo  ameeleza kuwa ugonjwa wa homa ya Ini ndio inayoongoza kwa asilimia 5.9 ikifuatiwa HIV kwa asilimia 2.8.

Dkt. Lyimo amewashukuru wananchi  wanaoendelea kuchangia damu ikiwemo vijana watumishi wa umma, taasisi na mashirika mbalimbali  kwa moyo wa kutekeleza zoezi hilo ili kufikia malengo yanayotarajiwa.

0 on: "CHUPA 51819 ZAIDI ZA DAMU SALAMA ZAKUSANYWA KWA MWAKA 2018/2019"