Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Kumbukumbu la Blogu

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 2 Septemba 2019

HABARI PICHA: WATAALAM WA MAWASILIANO WAJIDHATITI KUTANGAZA MAFANIKIO YA SEKTA YA AFYA NCHINI.

Na Englibert Kayombo, WAMJW - Mwanza

Habari Picha

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu AFYA) Bw. Gerard Chami akisema jambo kwa Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano kutoka Wizara ya Afya na Taasisi zake katika Kikao kazi Jijini Mwanza kupanga mkakati wa mawalisiano wa mafanikio ya Sekta ya Afya.

"Ni lazima tufanye kazi kwa umoja na ushirikiano kuhakikisha kwamba tunatangaza vyema mafanikio ya Sekta ya Afya nchini" Bi. Anjela Mziray Meneja Mawasiliano Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)

"Mikakati yote ya kuboresha Sekta ya Afya imewekwa kwenye Ilani ya Chama Tawala (Chama Cha Mapinduzi CCM), ni vyema kuielewa vizuri ili kujua dira ya Serikali ya Awamu ya Tano kwenye Sekta ya Afya nchini" Bw. Aminiel Aligaesha Mkuu wa Kitengo cha Habari na Uhusiano Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Afisa Mawasiliano kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC) Bw. Hamza Mwangomale akiteta jambo na Afisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Tawi la Mloganzila Bi. Neema Mwangomo (kushoto) kwenye kikao kazi cha  Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano kutoka Wizara ya Afya na Taasisi zake Jijini Mwanza.

Afisa Habari na Uhusiano kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa Bw. Karimu Meshack (wa katikati) akisema jambo wakati wa kikao kazi cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano kutoka Wizara ya Afya na Taasisi zake Jijini Mwanza.

Afisa Uhusiano kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Bi. Grace Michael akirejea kusoma Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kufahamu zaidi malengo ya Chama Tawala kwenye Sekta ya Afya nchini.
_________________________________________________________________________________

Picha Mbalimbali za Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano kutoka Wizara ya Afya na Taasisi zake wakiwa kwenye kikao kazi Jijini Mwanza wakijadili mpango kazi wa utekelezaji wa mkakati wa mawasiliano ya Sekta ya Afya katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli.












0 on: "HABARI PICHA: WATAALAM WA MAWASILIANO WAJIDHATITI KUTANGAZA MAFANIKIO YA SEKTA YA AFYA NCHINI."