Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 12 Desemba 2017

MADEREVA WAANZA KUTII SHERIA ZA BARABARANI BILA SHURUTI

- Hakuna maoni
Kamanda wa Kikosi Cha Usalama Barabarani Nchini SACP Fortunatus Musilimu aliyesimama akiongea na wadau mbalimbali wa usalama barabarani  hawapo pichani wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma.

Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Bi. Mary Kessy akiongea na wadau mbalimbali wa usalama barabarani  hawapo pichani wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma.

ASP Deus Sokoni wa kwanza kulia akiongea na wadau mbalimbali wa usalama barabarani  hawapo pichani wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma, wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Wizara ya Mambo ya Ndani  Bi. Marlin Komba  anayefuata ni Kamanda wa Kikosi Cha Usalama Barabarani Nchini SACP Fortunatus Musilimu.

Katibu Mkuu wa Shirikishi wa vyama vya Walemu nchini Bw. Felicina Mkude aliyesimama akiongea na baadhi ya wadau mbalimbali wa usalama barabarani  hawapo pichani wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma.

Baadhi  ya wadau mbalimbali wa usalama barabarani  wakimsikiliza kwa makini Kamanda wa Kikosi Cha Usalama Barabarani Nchini SACP Fortunatus Musilimu hayupo pichani  wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma.



Kamanda wa Kikosi Cha Usalama Barabarani Nchini SACP Fortunatus Musilimu katikati ya waliokaa akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa usalama barabarani  wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma.



Na.WAMJW-Dodoma     
Madereva nchini wamepongezwa   kwa kuanza kubadilika na kutii sheria bila shuruti katika kukabiliana na ajali za barabarani na hivyo kupungua kwa ajali pamoja na vifo vitokanavyo na ajali kwa uendeshaji unaofuata taratibu na sheria za barabarani.
Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kikosi cha Barabarani Tanzania  Fortunatus Musilimu -Kamishana Msaidizi Mwandamizi wa Polisi(SACP) wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa kupokea maoni ya sheria kuhusu ajali za barabarani  unaojumlisha mashirika yasiyo ya Kiserikali.
Kamanda Musilimu alisema tatizo la ajali barabarani bado ni kubwa kwani watu wengi wanafariki na kujeruhiwa kutokana na ajali barabarani.
”sisi sote  ni wahanga wa usalama barabarani hivyo hatuna budi  wadau wote kushirikiana katika kukabiliana na suala hili  na kila mmoja anayo nafasi ya kuchangia ili usalama wa barabarani uimarike  na kuboreka zaidi”Alisema.
Alisema hivi sasa watu wengi wameanza kubadilika hususani madereva wengi ambapo kuna wakati inabidi jeshi la polisi kutumia nguvu nyingi ili kuweza kuepuka ajali zinazoweza kuepukika na nguvu hizi zimetumika kwa nia nzuri ili watanzania kuwa salama wanapotumia vyombo vya moto.
Akitolea mfano kwa hali ya usalama barabarani kwa siku ya jana (juzi) nchi nzima kulikua na ajali nne ambazo zimesababisha vifi viwili na majeruhi nne,hivyo ni hatua nzuri na hata hivyo aliwataka wadau hao kuhakikisha wanatoa maoni mazuri ambayo yatasaidia kupata sheria ambayo haitamkandamiza mwananchi na ambayo itakua salama na kupunguza ajali za barabarani nchini na kuwa na sheria inayotekelezeka kwa kupunguza ajali kwa asilimia 50.

“Serikali ya awamu ya tano inapenda kulinda maisha ya watanzania,serikali inatengeneza uchumi wa kati  na viwanda kwa kuboresha miundombinu ikiwemo barabasha hivyo jukumu letu kushirikiana na serikali kuilinda  miundombinu yote inayotengenezwa”
Aidha,Kamanda Musilimu aliwataka wananchi waondoe dhana kwamba ajali zinatokana na mapenzi ya Mungu, “Hii siyo kweli ila matatizo yote ya ajali ni sisi wenyewe tunasababisha kutokana na mwendo kasi na kutotii sheria za barabarani".
Alitaja takwimu za ajali barabarani kwa Tanzania kwa mwezi Julai hadi Septemba mwaka 2016 ilikua 639,vifo 923 na majeruhi 2,469 na kwa mwaka 2017 kuanzia Julai hadi Septemba ajali za barabarani zilikuwa 1,376,vifo 655 pamoja na majeruhi 1,469.
Naye  Mwakilishi toka shirika la Afya Dunia  Mery Kessy alisema zaidi ya asilimia 90 za ajali zinazotokea katika nchi zinazoendelea ingawa ni asilimia 10 tu nchi hizo  zinamiliki vyombo vya moto na hiyo ni kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo miundombinu,mazingira pamoja na tabia.
Alisema wahanga wakubwa wanaopata ajali na vifo ni  vijana kati ya miaka miaka 15 mpaka 29 kwani umri huu wanakuwa kwenye hatari kubwa ya kusababisha ajali na hivyo ajali hizo kuchukua zaidi ya asilimia 3 za pato la Taifa kwani serikali inaingia gharama kubwa kutibu majeruhi katika sekta ya afya.


Jumatatu, 11 Desemba 2017

MH. UMMY(MB) AWEKA HISTORIA KATIKA ZIARA YA ZAHANATI YA MHANDU KATA YA CHELA WILAYANI MSALALA.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akimsalimia  mgonjwa aliyekuwa anasubiri huduma katika Zahanati ya Segese wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa  malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.

Baadhi ya Wanakijiji wa Kijiji cha Segese wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu hayupo pichani wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa  malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikagua choo cha Zahanati ya Mhandu wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa  malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi , aliyevaa suti nyeusi ni Mkuu wa Wilaya ya Kahama Bw. Fadhil Mkuru.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akisisitiza jambo kuhusu upatikanaji wa dawa katika  Zahanati ya Mhandu wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa  malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.

 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akifurahia jambo na baadhi ya  wazee wa kijiji cha Segese wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa  malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akimkabidhi kitambulisho cha matibabu bila ya malipo mmoja wa wazee wa kijiji cha Segese Bibi. Shija Petro (60) kulia  wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa  malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi, Bibi huyo aliwawakilisha wazee 413 waliopata vitambulisho hivyo katika Halmashauri ya Msalala ambapo lengo  ni kuwafikia wazee742 kufikia Machi 2018.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati  akiangalia  friji la kuhifadhia chanjo kwa  ajili ya watoto  katika Zahanati ya Segese wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa  malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akipata maelekezo juu ya upatikanaji wa dawa kutoka kwa mtoa huduma kushoto  katika Zahanati ya Segese wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama leo ili kuangalia utekelezaji wa mpango wa  malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi.



Na WAMJW-MSALALA

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto aweka historia kwa kutembelea Zahanati ya Mhandu kata  ya Chela Wilayani Msalala ambapo tangu Uhuru wa Tanzania kijiji hicho hakijawahi kutembekewa na Kiongozi wa Kitaifa.

Waziri Ummy Mwalimu yupo ziara ya kikazi Wilayani Msalala kujionea Utekelezaji wa  Mpango wa Malipo kwa Ufanisi(RBF) ambapo ulianza Januari 2016 kwa Mkoa wa  Shinyanga

RBFni Mpango wa malipo wa ufanisi kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya ngazi ya msingi ambapo vituo vinapewa maeneo ya utekelezaji na kupimwa kuona kama wamekidhi na kufikiwa malengo hivyo kituo huhakikiwa na hatimaye kutolewa fedha kulingana na matokeo ya idadi za huduma zilizotolewa na ubora kulingana na miongozo ya utoaji wa huduma za Afya.

Fedha zinazopatikana zinafanya maboresho ya vituo ikiwemo miundombinu ya kituo,madawa na vifaa tiba

Waziri Ummy Mwalimu ameipongeza halmashauri ya wilaya hiyo kwa kufanya vizuri katika kutekeleza Mpango huo hata hivyo aliwataka watendaji kufanya uhakiki na kujiridhisha kwamba huduma za Afya zitolewazo zinakidhi viwango kulingana na miongozo ya Afya ndipo malipo yatolewe

Alisema Mpango huo unahakikisha huduma ya Afya ya msingi zinatolewa bila vikwazo,"nimekuja kufuatilia utekelezaji kwakweli nimefurahi kwani mnatekeleza na mmeboresha huduma zenu"

Aidha,alisema kabla ya utekelezaji wa Mpango huo kuanza mwaka 2015 hali ya miundombinu ilikua mibovu,hakukuwa na dawa,hivyo kupitia Mpango huo Serikali hupeleka fedha ambazo zinasaidia kuimarisha mifumo ya vituo vya Afya,kuongeza huduma za huduma,kuchochea jamii kutumia vituo vya Afya hususan wanawake wajawazito pamoja na kutoa motisha kwa wahudumu na watumishi wa Afya katika vituo vya kutolea huduma.

"Mpango huu tunataka wanawake wajawazito waje vituoni ndani ya miezi mitatu ya mwanzo na serikali tunaleta shilingi 8290,na mjamzito akihudhuria kliniki angalau Mara NNE wakati wa ujauzito tunaleta shilingi 6210 kwenye zahanati" alisema Waziri Ummy

Alitaja kiasi cha shilingi 20,700 serikali inatoa kwa mjamzito akienda kujifungua kwenye Zahanati hivyo alitoa ari kwa wanawake wajawazito wilayani Msalala kuacha kwenda kujifungua kwa wakunga wa jadi kwani Serikali ya awamu ya tano imeboresha huduma za Afya nchini ikiwemo hali ya  upatikanaji wa dawa ambapo Msalala kwa mwaka wa fedha 2017/2018 wametengewa shilingi milioni 417 tofauti na ile ya mwaka 2015/2016 ya shilingi milioni 108.

DKT. NDUGULILE AMPA MAAGIZO DMO MPWAPWA.

Naibu Waziri akimuuliza maswali mmoja kati ya wauguzi anayehusika na stoo hiyo ya dawa kwenye kituo cha afya kibakwe.

Dkt.Ndugulie akiongea na baadhi ya wakazi wa Kibakwe waliofika kituoni hapo kuwajulia hali wagonjwa wao.Dkt.Ndugulile aliwasisitiza wakazi hao kusimamia matumizi ya fedha na dawa kwani kituo hicho kimetengewa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha upasuaji wa dharura,nyumba za watumishi pamoja na ununuzi wa vifaa tiba kituoni hapo.

 Dkt.Ndugulile akiongea na watumishi wa kituo cha afya Kibakwe nje ya kituo hicho

Dkt.Faustine Ndugulile Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto akikagua fomu ya orodha ya dawa iliyofanywa na kituo hicho kwa mnunuzi wa nje na ile ya MSD kwenye stoo ya dawa ya kituo cha afya cha kibakwe.


Picha ya pamoja ya Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto pamoja na watumishi wa kituo cha afya Kibakwe wilayani Mpwapwa.



Na WAMJW-DODOMA
NAIBU Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amemuagiza Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa  Dkt. Said Mawjji kuandaa maoteo ya mahitaji ya dawa mapema na kupeleka Bohari kuu ya Dawa (MSD) kwa ajili ya upatikanaji huo na sio kununua dawa kiholela.
Hayo ameyasema wakati wa ziara yake kwa ajili ya kuangalia miundo mbinu pamoja na upatikanaji wa dawa na huduma za afya zitolewazo katika wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma aliyoifanya jana.
“Katika milioni 57 ya kununua dawa laki saba tu ndo imeenda MSD zilizobaki zimeenda kwa mshitiri mwingine ambapo ni uagizaji dawa kiholela kwani mmeshindwa kufuata taratibu za uagizaji dawa wakati dawa hizo zinapatikana MSD” alisema Dkt. Ndugulile.
Aidha Dkt. Ndugulile alimuagiza Dkt. Mawjji kuhakikisha upanikaji wa dawa zote muhimu zinapatikana kwa asilimia 80 katika vituo vya afya wilayani hapo kama ilivyofikiwa na MSD katika kusambaza dawa hapa nchini ili kuondokana na tatizo la uhaba wa dawa ambapo ni kipaumbele cha Serikali kwa uapande wa sekta ya afya nchini.
Dkt. Ndugulile alimuagiza DMO wa Mpwapwa mpaka kufikia Desemba 13 mwaka huu awe tayari amewasilisha nyaraka za uagizaji dawa zote kuanzia Julai 2017mpaka Septemba mwaka huu ili kujiridhisha na utaratibu wao wa uagizaji dawa.
Mbali na hayo Dkt. Ndugulile amemuagiza DMO huyo kujitahidi kuongeaa baadhi ya watumishi katika kituo cha afya cha Kibakwe kilichopo katika tarafa ya Kibakwe Wilayani Mpwapwa kwani wanahitajika watumishi akiwemo mtaalam wa maabara na mfamasia wa kituo ili kuleta ufanisi katika huduma za afya kituoni hapo.
Aidha Dkt. Ndugulile ameumbia uongozi wakituo cha afya Kibakwe na pamoja na wanakijiji kuwa Serikali imetenga milioni 500 kwa ajili ya ujenzi na  ukarabati wa jengo la upasuaji wa dharura kwa akina mama wajawazito,nyumba za watumishi pamoja na ununuzi wa  vifaa tiba ili kuokoa maisha ya akina mama wanapopata uzazi tata wakati wa kujifungua
Katika kituo hicho cha afya Kibakwe Naibu Waziri huyo alikutana na changamoto ya tofauti ya dawa kwenye fomu za kuagiza dawa MSD na zile za kununua dawa hizo kwa mshitiri wa nje hali iliyomlazimu Dkt.Ndugulile kuanza kuhakikia fomu moja kwa dawa moja hadi nyingine na kugundua ubadilishaji wa aina za dawa zilizoagizwa MSD na baadae kwa mnunuzi wa nje.
Hata hivyo Dkt.Ndugulile aliwakanya watumishi wa stoo ya dawa ya kituo hicho kuacha kufanya mchezo huo wa kubadilisha mahitaji ya dawa pale wanapokosa MSD na kiruhusiwa kununua nje kwani Serikali ya awamu ya tano imejipanga na kuhakikisha upatikanaji wa dawa katika vituo vya afya kote nchi ni zaidi ya asilimia 80 na hivyo kuwataka wakazi wa Kibakwe kusimamia kwa makini matumizi ya dawa kituoni hapo.

Jumamosi, 9 Desemba 2017

DKT. NDUGULILE AFANYA ZIARA KATIKA CHUO CHA AFYA NA MAZINGIRA WILAYANI MPWAPWA.

Naibu Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile wa kwanza kulia akimjulia hali mgonjwa aliyelazwa katika kituo cha afya cha kibakwe wakati wa ziara yake katika Kijiji hiko  wilani Mpwapwa mkoani Dodoma.


Naibu Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile katikati aliyevaa shati la bluu akiongea na baadhi ya wananchi na watumishi wa afya wa kituo cha afya cha Kibakwe kuhusu changamoto na maendeleo ya sekta ya afya katika Kijiji hicho wakati wa ziara yake wilani Mpwapwa mkoani Dodoma.

Naibu Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua dawa zilizopo kwenye stoo ya dawa ya Kituo cha afya cha  Kibakwe  wakati wa ziara yake katika Kijiji hiko  wilani Mpwapwa mkoani Dodoma.

Naibu Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile wa kwanza kulia akiwajulia hali wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma wakati wa ziara  yake leo wilayani humo.

Naibu Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile wa pili kushoto akiongea na baadhi ya watumishi wa Chuo Cha Afya na Mazingira Mpwapwa alipotembelea chuo hiko wakati wa ziara yake wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma, wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Chuo hiko Bw. Rogasian Tarimo.

Naibu Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile mbele aliyevaa shati la bluu akisikiliza changamoto kutoka kwa  badhi ya wanafunzi wa mwaka wa pili fani ya udaktari katika Chuo Cha Afya na Mazingira Mpwapwa alipotembelea chuo hiko wakati wa ziara yake wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa ziara yake katika Chuo Cha Afya na Mazingira  wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma.

HOSPITALI YA SARATANI YA OCEAN ROAD YATOA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA SARATANI KWA WATU WENYE ALBINO

 





Hospitali ya Saratani ya Ocean Road imefanikisha kutoa huduma za uchunguzi wa Saratani kwa watu wenye albino.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa huduma za jamii hospitali ya Saratani ya Ocean Road Dkt. Cyrpian katika ziara yake Mkoani Simiyu.

Dkt. Cyrpian alibainisha kuwa Uchunguzi huo umefanywa kwa kushirikiana na Taasisi ya Albino nchini huku likijumuisha kuwafundisha wataalamu wa Afya na kuanzisha Kliniki za kutoa huduma  hizi.

“tumefanyia uchunguzi albino 16 Kati ya hao 2 wana saratani, watu 12 wenye dalili za awali za saratani tumewatibu papo hapo kwa tiba baridi huku wawili wakiwa vizuri” alisema Dkt. Dkt. Cyrpian.

Dkt. Cyrpian alibainisha kuwa zoezi hili limeanza tangu Desemba 3 mpaka Desemba 9 Wilayani Misungwi liliwalenga wanafunzi 65 kutoka shule ya msingi Misungwi Mitindo huku wanafunzi 50 wakipewa mafuta ya albino yakujikinga na jua. Wanafunzi 2 walikuwa na dalili za aratani ya ngozi na walitibiwa kwa tiba baridi (cryotherapy) na 13 walikuwa hawana shida.

Dkt. Cyrpian alikiri kuwafundisha madaktari katika hospitali ya wilaya  ya Misungwi, hospital ya shinyanga na Simiyu.

Ijumaa, 8 Desemba 2017

WATANZANIA WATAKIWA KUZINGATIA MATUMIZI YA VYOO BORA

- Hakuna maoni

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan akisisitiza jambo mbele ya wadau na wakazi wa Chang’ombe Mkoa wa Dodoma katika Uzinduzi wa kampeni ya Usichukulie Poa Nyumba ni Choo iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Chang’ombe.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akimkabidhi zawadi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa usafi wa mazingira na vyoo bora kutoka halmashauri mbali mbali nchini Tanzania.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakipiga makofi ishara ya kupongeza uzuri na usafi wa moja ya mfano wa choo bora.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan wapili kutoka kushoto wakiwa mbele ya choo bora, tukio lililifanyika katika viwanja vya shule ya msingi Chang’ombe Mkoani Dodoma. Wakwanza ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu, watatu ni Elizabeth Arthur na wa mwisho ni Waziri wa TAMISEMI Suleiman Jaffo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan wapili kutoka kushoto akiwapungia mkono wakazi wa Chang'ombe na wadau wa masuala ya mazingira na usafi wa vyoo. akwanza ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu, watatu ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Mahenge.

Timu ya viongozi wa serikali ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakiwa tayari kumpokea mgeni rasmi Makamu wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan.

Mratibu wa Kampeni ya kitaifa ya Usafi na Mazingira kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Anyitike Mwakitalima akitoa maelezo mbele ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akimuelekeza jambo Waziri wa TAMISEMI Suleiman Jaffo wakiwa katika banda la maonesho la Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Meneja Mpango wa Simavi Thea Bongertman, wa kwanza ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu.

Kikundi cha Burudani kutoka eneo la Chang’ombe Mkoani Dodoma, kikionesha manjonjo mbele ya mgeni rasmi Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wa Serikali.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha akipokea zawadi ya Usafi bora ya gari kutoka kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiwa na Naibu wa Wizara hiyo Mh. Faustine Ndugulile wakimkabidhi zawadi ya Usafi bora Mwakilishi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bi Eveline Kibenya.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiwa na Naibu wa Wizara hiyo Mh. Faustine Ndugulile na Elizabeth Arthur katika bango la kampeni ya “Usichukulie Poa Nyumba ni Choo”

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiwa na Naibu wa Wizara hiyo Mh. Faustine Ndugulile wakiwa pamoja na Washindi Usafi na vyoo bora kutoka Halmashauri mbali mbali nchini.

NA WAMJW-DODOMA.

WATANZANIA  wanapaswa kuzingatia mambo  ya msingi hususani matumizi ya vyoo bora  ili kuepuka magonjwa  ya kuambukiza na mlipuko kwa ajili ya kujenga Tanzania ya Viwanda pasipokuwa na adui mkubwa wa maradhi nchini.

Hayo yamesemwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya kampeni ya taifa ya mazingira uliyofanyika mkoani leo Mkoani Dodoma.

“Watanzania tunapaswa kuzingatia mambo ya msingi ikiwemo kutumia vyoo bora ,kunawa mikono kwa maji safi yanayotiririka na sabuni pamoja na kuchemsha maji ya kunywa ili kuepuka magonjwa mlipuko nchini” alisema Mhe. Samia.

Aidha Mhe. Samia amesema kuwa watanzania tunatakiwa kuwa kipaumbele kwenye usafi wa mazingira kwa tumepoteza kiasi cha shilingi bilioni 440 kutokana na hali duni ya usafi wa hasa ukosefu wa huduma ya vyoo bora.

Kwa mujibu wa Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu  Hassan amesema kuwa takwimu zinaonyesha watu wapatao elfu thelathini huugua magonjwa ya kuhara kila mwaka na baadhi yao hupoteza maisha hivyo tunatakiwa kuzingatia usafi wa mazingira  ili kuepuka idadi ya wastani wa watu 83 kwa siku.

“Taifa hatuna kuwekeza nguvu na rasilimali zetu katika suala la usafi wa mazingira ikiwemo matumizi ya maji safi na vyoo bora ili kufikia malengo yetu ya kitaifa pampja nay ale ya kidunia” alisema Mhe. Samia Suluhu.

Mbali na hayo  Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa endapo watoto wataendlea kuishi kwenye  mazingira machafu ni hatarishi kwani kuna uwezekano wa kuwa na watoto waliodumaa kimwili na kiakili.

Kwa upande wake Waziri wa afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Me. Ummy Mwalimu amesema kuwa Tanzania inaendelea kupambana na ugonjwa wa kipindupindu ambao ulirejea tena mwaka 2015 baada ya kupotea takribani miaka minne.

“ Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameonesha kusikitishwa kwake kutokana na uwepo wa kipindupindu nchini hivyo watanzania hatuna budi kuwa wasafi wa mazingira ili kuepuka mlipuko wa ugonjwa huo” alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amewataka watanzania kupambana na adui wa afya kwa kutunza mazingira na kuepuka vishiria vya magonjwa mbalimbali  kuliko kulalamika ukosefu wa dawa kwani kinga ni bora kuliko tiba.

Kwa upande Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Bw. Suleiman Jaffo amesema kuwa kupitia ofisi yake atahakikisha anasimamia na kuwaagiza watendaji wake  wa ngazi zote kusimamia  usafi wa mazingira kama alivyoagizwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Kampeni iliyozinduliwa leo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  jijini Dodoma ni ya awamu ya pili ya usafi wa mazingira ambayo imebeba ujumbe usemao “USICHUKULIE POA NYUMBA NI CHOO” imeenda sambamba na ugawaji wa zawadi na vyeti kwa waliofanya vizuri kwenye usafi wa mazingira ambapo Halmashauri ya Mji wa Njombe umeibuka kidedea na kupata zawadi ya Trekta.

Jumatano, 6 Desemba 2017

WAZIRI UMMY ATAKA UTARATIBU WA UONGOZI KWENYE VITUO VYA AFYA UFATWE


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Viongozi na Wananchi wa Wilaya ya Chamwino wakati alipotembelea kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika Wilaya hiyo.


Mkuu wa Wilaya ya Chamwino  Mh. Vumilia Nyamonga akiongea na wananchi wake (hawapo kwenye picha) juu ya Usafi wa mazingira na matumizi ya choo, katika ziara ya Waziri wa Afya katika Wilaya hiyo mjini Dodoma, kushoto ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu na kulia kwake ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. James Charles.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. James Charles akijibu hoja ya mwananchi wa Kijiji cha Humekwa mbele ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (hayupo kwenye picha) kuhusu upatikanaji wa kadi za matibabu ya wazee wilayani hapo.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiteta jambo na Elizabeth Arthur wakati alipotembelea kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika Wilaya hiyo.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiongea na mkazi wa Kijiji cha Humekwa Wilaya ya Chamwino Bi Cesilliah Isaya aliyefanikiwa kujenga choo chenye ubora kwa gharama ndogo ya shiringi 55,000 tu.

 Kikundi cha ngoma kutoka Kijiji cha Humekwa kikitoa Burudani mbele ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara ya kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika Wilaya hiyo ya Chamwino Mkoani Dodoma.

 Wanafunzi wa Shule ya Msingi na Wakazi wa Kijiji cha Humekwa waliojumuika katika kuunga mkono ziara ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (hayupo kwenye picha) ili kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika Wilaya hiyo ya Chamwino Mkoani Dodoma.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akifuatilia kwa ukaribu ratiba  katika kituo kidogo cha Afya Kijiji cha Humekwa wakati wa ziara yake katika Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akikagua moja ya choo wakati alipofanya ziara katika Kijiji cha Humekwa Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma ili kuhamasisha usafi wa mazingira na choo.

 Mwanakijiji wa Kijiji cha Humekwa Bi Evaline Gidore akisoma risala mbele ya mgeni rasmi Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (hayupo kwenye picha) wakati alipofanya ziara ya kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika kijiji hicho mapema leo.

 Diwani wa kata ya Aneti Mh. Peter Chidawali akitoa mapendekezo mbele ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu (hayupo kwenye picha) kuhusu maboresho katika huduma za Afya kijijini hapo.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. James Charles wakati wa ziara ya kujionea Usafi wa mazingira na matumizi ya Choo katika Wilaya hiyo, wa katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Chamwino  Mh. Vumilia Nyamonga.


Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiongoza  ziara katika kijiji cha Humekwa Wilaya ya Chamwino mapema leo Mkoani Dodoma.






NA WAMJW-DODOMA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imedhamiria kuhakikisha kuwa kila Kituo cha Afya au Zahanati yoyote inaongozwa na kusimamiwa na mganga na sio mhudumu wa afya au nesi kama inavyofanyika kwenye baadhi ya vituo vya afya .

Hayo yamesemwa na Waziri wa afya ,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu wakati wa ukaguzi wa usafi wa mazingira  leo Mkoani Dodoma Wilaya ya Chamwino kata ya aneti Kijiji cha humekwa  kuelekea uzinduzi  wa awamu ya pili ya kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira iliyobeba ujumbe wa nipo tayari  ambapo Makamuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajia kuwa mgeni rasmi.

"Hatua ya kuimarisha  upatikanaji wa dawa, upatikanaji wa vifaa na vifaa tiba hususani vya dharura na upasuaji sanjari na kuweka mazingira safi ya upatikanaji wa maji na vyoo safi na salama ili kupunguza magonjwa na vifo vitokanavyo na kutokuwepo kwa huduma bora za  maji na afya kwa wakati ndiyo lengo letu" alisema Waziri Ummy.


 Aidha Waziri Ummy amesema kuwa kabla ya Serikali ya Mhe. Rais John Pombe Magufuli haijaingia madarakani bajeti ya dawa ya wilaya ya chamwino ilikuwa milioni 113 lakini mwaka jana bajeti ya dawa  ilikuwa milioni 436 ambapo katika mwaka wa pili wametengewa milioni 505 hali inayoonesha jitihada za dhati za serikali ya awamu ya tano kuboresha hali ya  afya ya wananchi hususani waliokuwa Vijijini.

Mbali na hayo Waziri Ummy amewataka wananchi wa kijiji cha Humekwa kukata kadi ya matibabu za CHF kwani zinarahisha upatikanaji wa huduma za afya kwa urahisi na kupunguza gharama .

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa wananchi ambao wana ugonjwa kifua kikuu hawana  budi kuwahi hospitali na vituo vya kutolea huduma za afya kwa ajili ya kupata dawa ili kuokoa maisha yao kwani dawa hizo hazilipiwi gharama yoyote.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Aneti  Peter Chidawali ameiomba Serikali kuwasaidia Wananchi wa Humekwa katika hatua iliyofikiwa kwenye ujenzi wa jengo la upasuaji ambalo wananchi wanajitolea michango yao kujenga ili likamilike kwa matumizi yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake Msomarisala wa Kijiji cha Homekwe Evaline Gidore amebainisha kuwa kampeni ya usafi wa mazingira na ujenzi  wa vyoo bora imeasaidia kupunguza idadi ya wagonjwa walioathiriwa na magonjwa  yatokanayo na uchafuzi wa mazingira .

"Kampeni hii imechangia kuepuka magonjwa hatari kama vile kuhara damu, typhoid na minyoo kutoka wagonjwa138 mwezi  disemba 2015 hadi kufikia wagonjwa 26 Novemba Mwaka huu kwa vile tumejitahidi kuzingatia usafi wa mazingira na matumizi ya vyoo bora"Alisema Bi Eveline.