Jumatano, 21 Februari 2018
Jumanne, 20 Februari 2018
Alhamisi, 15 Februari 2018
Jumatano, 14 Februari 2018
SERIKALI YAENDELEA KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI KWA KUONGEZA VITUO VYA AFYA NCHINI.
Jumatano, Februari 14, 2018
-
Hakuna maoni
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akiweka jiwe la Msingi katika
ufunguzi wa jengo la mama na mtoto lililopo katika Hospitali ya Amana, mapema
leo jijini Dar es salaam, katikati ni Naibu waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akimjulia hali moja ya mama aliyekuwa
akiuguliwa na mtoto wake, akifanya hivyo baada ya kuzindua jengo la mama na
mtoto lililopo katika Hospitali ya Amana, kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam Mhe. Poul Makonda.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakisalimiana na Mbunge wa Ilala Mhe.
Azan Zungu wakati wa Uzinduzi wa jengo la mama na mtoto lililopo katika
Hospitali ya Amana, wa pili ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Poul Makonda
na wa mwisho ni Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Dkt. Faustine Ndugulile.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa mama aliyekuwa akiuguliwa na mtoto
wake, akifanya hivyo baada ya kuzindua jengo la mama na mtoto lililopo katika
Hospitali ya Amana, kulia kwake ni Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile.
Picha ya pamoja ikiongozwa na
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, kulia
kwake ni Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt.
Faustine Ndugulile na kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Poul
Makonda.
Na WAMJW. DSM
SERIKALI yaendelea kuongeza
vituo vya Afya nchini ikiwa ni moja ya jitihada za Serikali za kuboresha Huduma
za afya nchini jambo litakalo saidia kupunguza msongamano wa wagonjwa katika
Hospitali za Wilaya na Mkoa kwa kuwa huduma zote zitakuwa zimeishia kwenye
ngazi ya Kata.
Hayo yamebainishwa na Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakati wa ufunguzi
wa jengo la mama na mtoto lililopo katika Hospitali ya Amana, mapema leo jijini
Dar es salaam.
“Kumekuwa na ongezeko kubwa
la vituo vya Afya nchini kutoka vituo vya Afya 6321 kwa mwaka 2010 hadi vituo
vya Afya 7680 kwa mwaka 2016, na kazi ya nyongeza inaendelea, kwaiyo
tunaamini vituo hivi vitaweza kupunguza
msongamano katika hospitali za Wilaya, pamoja na Hospitali za Mkoa”, alisema
Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Mhe. Waziri Mkuu alisema
kwamba Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
ametenga kiasi cha Zaidi ya Bilioni 100 ikiwa ni fedha za kuboresha Vituo vya
Afya nchini ili kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi katika maeneo yote
nchini.
“Tumeanza kuboresha Vituo vya
Afya kwa kujenga Wodi yakinamama wanaojifungua, thieta, wodi za magonjwa yakawaida,
maabara, tunaongeza na nyumba za watumishi, ili kila kituo cha Afya kiwe na
miundombinu hiyo ili utoaji huduma uwe rahisi” alisema Mh. Waziri Mkuu Kassim
Majaliwa.
Mhe. Waziri Mkuu aliendele
kusema kwamba Serikali imetumia Zaidi ya Bilioni 161 katika kuendelea kuboresha
Huduma za Mama na Mtoto kwa lengo la kuokoa Maisha ya mama na mtoto jambo
ambalo ni moja kati ya changamoto kubwa nchini.
Aidha Mhe. Waziri Mkuu alisema
kwamba Serikali imeendelea kuboresha Huduma za Afya kwa kutenga kiasi cha shilingi
Bilioni 129 kwaajili ya vifaa vya kuwezesha kundesha shughuli za upasuaji
katika kila kituo cha Afya ambacho kinaboreshwa.
Wakati akitoa taarifa ya Afya
ya Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Poul Makonda alisema
kwamba wakina mama 126,164 walipata nafasi ya kujifungua katika vituo vya Afya,
huku wakinamama 202 ambao ni sawa na Asilimia 0.5 walilazimika kujifungua kwa
wakunga, na Asilimia 1.5 zaidi ya akinamama 1976 walijifungua njiani wakielekea
kupata huduma, idadi inayoonekana kuwa kubwa sana katika Mkoa wa Dar Es salaam.
Idadi ya 2016 inaonesha Zaidi
ya akina mama 85 walikuwa wanapoteza Maisha kati ya kina mama 100,000 waliokuwa
wanajifungua lakini kwa sasa tangu maboresho yafanyike ni akina mama 57 kati ya
akina mama 100,000 wanaojifungua ndio hupoteza Maisha, huku mikakati thabiti
yakupunguza vifo hivyo ikiendelea kuwekwa.
Mhe. Makonda aliendelea
kusema kwamba zaidi ya watoto ambao wanafanikiwa kuwa hai na kuwa salamakatika
kujifungua ni Zaidi ya watoto 126,712, na watoto 131 huzaliwa wakiwa tayari
wameshakufa, idadi hii ikilinganishwa .
Pia Mhe. Makonda alimshukuru
AMSONS GROUP ambayo imetoa mchango mkubwa katika ujenzi wa Jengo hilo la Mama
na Mtoto lililopo katika Hospitali ya Amana huku akiwataka Wadau wengine kuiga
mfano huo katika dhana ya kusukuma gurudumu la maendeleo katika jamii zetu.
Nae Naibu
waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine
Ndugulile alisema kuwa Serikali ya awamu ya tano tangu iingie madarakani imeongeza
Bajeti ya Dawa kutoka Bilioni 30 mpaka sasa ni Bilioni 270 likiwa ni ongezeko
la Zaidi ya mara 9, huku Wastani wa upatikanaji wa dawa ukiwa Zaidi ya asilimia
80.
“Serikali wakati inaingia
madarakani Bajeti ya dawa ilikuwa ni Bilioni 30, mwaka unaofuata ikafikia
Bilioni 200, na hivi tunavyoongea Bajeti ya Dawa ni Bilioni 270, likiwa ni
ongezeko la mara 9, kama msaidizi wako nasimama kifua mbele na kusema ya kwamba
hatuna uhaba wa Dawa muhimu”, alisema Dkt. Ndugulile.
Jumatatu, 12 Februari 2018

TANZANIA INATUMIA DAWA ZILIZO SALAMA KWA UHAKIKA MKUBWA
Jumatatu, Februari 12, 2018
-
Hakuna maoni
![]() |
| Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kuifungua mkutano huo. |
![]() |
| Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Faustine Ndugulile akifuatilia mada (mwasilishaji hayupo pichani) katika mkutano huo. |
![]() |
| Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bi.Agnes Kijo akiongea kwenye ufunguzi wa mkutano wa wa Mamlaka za Kudhibiti Chakula na Dawa Barani Afrik. |

TUMEKOSOGEZA KARIBU
Jumatatu, Februari 12, 2018
-
Hakuna maoni
Wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia wazee na watoto.
Inayo
furaha kubwa kuwakaribisha wananchi wote ndani na nje ya nchi
kutembelea katika mitandao yake ya kijamii ili kupata taarifa mbalimbali
za kiafya. Aidha tunakaribisha maoni na ushauri mbalimbali kuhusu sekta
ya afya. "Jenga taifa lenye afya bora kwa uchumi imara"
#AFYA_YANGU_MTAJI_WANGU
Jumatano, 7 Februari 2018

SERIKALI YAAZIMIA KUKUSANYA TAKWIMU ZA AFYA KIELEKTRONIKI NCHI NZIMA.
Jumatano, Februari 07, 2018
-
Hakuna maoni
SERIKALI imeazimia kukusanya na kutumia takwimu kwa
njia ya kielektroniki nchi nzima ili kuweza kumudu na kutoa huduma za afya kwa
ubora zaidi nchini.
Hayo yamezungumzwa na Katibu Mkuu Wizara ya afya Dkt.
Mpoki Ulisubisya wakati wa kutia Sahihi ya makubaliano ya kuanzisha mfumo wa
ukusanyaji takwimu za afya utakaotekelezwa na Wizara ya afya,Wadau wa
Maendeleo,Asasi za Kiraia na Shirika la Afya Duniani (WHO) uliofanyika leo
jijini Dar es salaam.
“Takwimu ni muhimu sana amabazo zitazomuwezesha mtoa
huduma kujua mgonjwa historia yake ya ugonjwa
na matibabu aliyopewa awali,kuwapa Uwezo utumishi kujua tunahitaji
rasilimali watu kwa kiasi gani katika
kituo cha Afya” alisema Dkt. Ulisubsya.
SERIKALI YAAZIMIA KUKUSANYA TAKWIMU ZA AFYA KIELEKTRONIKI NCHI NZIMA.
Jumatano, Februari 07, 2018
-
Hakuna maoni
Katibu Mkuu wa Wizara ya
Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akitoa
taarifa mbele ya Wadau wa Sekta ya Afya wakati wa Kikao cha kusaini makubaliano
ya Mfumo wa Ukusanyaji wa takwimu takwimu wa kielektroniki kilichofanyika
mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam.
Wadau wa Sekta ya Afya
wakifuatilia kwa makini taarifa ya mgeni
rasmi (Hayupo kwenye picha) ambae ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo
ya Jamii, jinsia, Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wa Kikao cha
kusaini makubaliano ya Mfumo wa Ukusanyaji wa takwimu takwimu wa kielektroniki.
Mwinyekiti wa DPG HEALTH Mhe.
Norzin Grigoleit-Dagyab akitutubia mbele ya Wadau wa Sekta ya Afya na Watumishi
wa Serikali wa Idara kuu ya Afya wakati wa Kikao cha kusaini makubaliano ya
Mfumo wa Ukusanyaji wa takwimu takwimu wa kielektroniki jijini Dar es Salaam.
Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya na wa mwisho kulia ni Mwakilishi kutoka WHO Dkt.
Matthieu Kamwa.
Picha ya Pamoja ikiongozwa na
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt.
Mpoki Ulisubisya akiwa na Wadau mbali mbali wa Sekta ya Afya katika Kikao cha
kusaini makubaliano ya Mfumo wa Ukusanyaji wa takwimu wa kielektroniki kilichofanyika
mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es Salaam.
Picha ya Pamoja ya Viongozi
wa Sekta ya Afya wakiwa wameshika mikataba iliyosainiwa ya makubaliano ya Mfumo
wa Ukusanyaji wa takwimu wa kielektroniki ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara
ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya.
Na WAMJW-DAR ES SALAAM.
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya,Maendeleo ya
jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imeazimia kukusanya na kutumia takwimu kwa
njia ya kielektroniki nchi nzima ili kuweza kumudu na kutoa huduma za afya kwa
ubora zaidi nchini.
Hayo yamezungumzwa na Katibu Mkuu Wizara ya afya Dkt.
Mpoki Ulisubisya wakati wa kutia Sahihi ya makubaliano ya kuanzisha mfumo wa
ukusanyaji takwimu za afya utakaotekelezwa na Wizara ya afya,Wadau wa
Maendeleo,Asasi za Kiraia na Shirika la Afya Duniani (WHO) uliofanyika leo
jijini Dar es salaam.
“Takwimu ni muhimu sana amabazo zitazomuwezesha mtoa
huduma kujua mgonjwa historia yake ya ugonjwa
na matibabu aliyopewa awali,kuwapa Uwezo utumishi kujua tunahitaji
rasilimali watu kwa kiasi gani katika
kituo cha Afya” alisema Dkt. Ulisubsya.
Aidha, Dkt. Ulisubisya amesema kuwa kwa kuanzia zoezi hilo
litaanza kwenye mikoa ya Tanga,Kilimanjaro na Manyara hatimaye kufikia nchi
nzima mpaka kufika 2020 ili kuweza kuwa
na takwimu za afya.
Dkt. Ulisubisya amesema kuwa mfumo wa kujaza takwimu
kwenye makaratasi umepitwa na wakati kwani kadri makaratasi ya takwimu
yanapokuwa mengi na makosa ya utoaji huduma unaweza kutokea kwani mpaka uanze kutafuta takwimu zilizopita
inachukua muda mrefu tofauti na kuhifadhi takwimu kielektroniki.
Mbali na hayo Dkt. Ulisubisya amesema kuwa mpaka hivi sasa
hali ya utoaji wa chanjo imefikia asilimia 97 na lengo letu ni kufikia asilimia
100 kupitia mfumo huu wa kukusanya takwimu kwa njia ya kielektroniki.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani
(WHO) Dkt. Matthieu Kamwa amesema kuwa wapo
tayari kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Afya
katika kutekeleza hilo ili kuweza kuboresha mifumo ya afya nchini.
“Unajua Takwimu ni utajiri hasa katika kutekeleza shughuli
za kutoa huduma za afya kwa wananchi hivypo hatuna budi kuunga mkono juhudu za
Serikali ya Tanzania katika kufanikisha hili jambo kwani litaturahisishia hata
sisi katika kutoa miongozo ya afya” alisema Dkt. Kamwa.
Jumanne, 6 Februari 2018

TIBA MTANDAO KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA NCHINI
Jumanne, Februari 06, 2018
-
Hakuna maoni
Na WAMJWW. Dom
Serikali
imejipanga kutumia tiba mtandao kuboresha huduma za afya nchini kwenye
hospitali zote za ngazi ya taifa, rufaa na wilaya ili kuwawezesha
wagonjwa waishio sehemu mbali mbali nchini kupata huduma za afya kwa
wakati na kwa ufanisi.
Hayo
yameelezwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati akifungua
kongamano la ubunifu na utekelezaji wa huduma za tiba mtandao Tanzania
lililofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa jengo la LAPF, Dodoma.
Dkt.
Ulisubisya amesema kuwa lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha
watendaji wakuu wa hospitali za taifa nchini, madaktari bingwa wa sekta
ya Afya, wakuu wa taasisi zinazoshughulika na sekta ya Afya, Wizara ya
TAMISEMI, Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano; taasisi nyingine za Serikali;
sekta binafsi na wabia wa maendeleo ili kujadiliana na kuwa na uelewa
wa pamoja wa kufanikisha utekelezaji wa huduma za tiba mtandao ili
kuboresha huduma za afya nchini.
Amesema
kuwa tiba mtandao itawezesha na kuongeza ufanisi katika kufanya
uchunguzi, utoaji wa tiba na madawa kwa wagonjwa wanaosumbuliwa na
magonjwa mbalimbali yasiyoambukiza na yanayotokana na ajali za
barabarani.
“Hadi hivi sasa ni asilimia 37 tu ya wagonjwa wa kifua kikuu
ndio wanaotambulika na kupatiwa huduma na Wizara ya Afya katika
hospitali mbalimbali nchini. Hivyo, tiba mtandao itawezesha upatikanaji
wa wagonjwa na ufikishaji wa huduma kwao kwa wagonjwa wengine asilimia
63”, alifafanua Dkt. Ulisubisya.
Aliongeza
kuwa tiba mtandao itapunguza gharama za wagonjwa na wanaowahudumia
kusafiri kufuata madaktari. Aidha, amewataka wakuu hao wa taasisi
kuwaruhusu wataalamu wao, wa Wizara ya TAMISEMI na wa Wizara ya Afya,
kushiriki mafunzo ya tiba mtandao ili kuongeza ufanisi wao katika
kuhudumia wagonjwa.
Amewataka
wataalamu wa afya na wakuu wa taasisi zinazohusika na masuala ya afya
kununua vifaa tiba vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
vyenye viwango na ubora unaohitajika ili kuwezesha tiba mtandao na
manunuzi hayo yazingatie na kufuata ununuzi wa pamoja wa huduma na
bidhaa za Serikali.
Vifaa vya kisasa vya TEHAMA vinavyohusika na tiba
mtandao vitawawezesha wataalamu kufanya uchunguzi kwa mgonjwa, kupata
majibu ya uhakika na kumpatia mgonjwa tiba inayostahili na ya uhakika.
Aidha, amemuelekeza Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote
(UCSAF), Eng. Ulanga, ambao ndio waanadaji na waratibu wa kongamano
hilo, kushirikiana na TTCL kuhakikisha kuwa tiba mtandao inapatikana
katika hospitali zote za rufaa na hospitali ambazo zina changamoto ya
kijiografia ya kufikika kwa urahisi.
Ijumaa, 2 Februari 2018

DKT MPOKI ASEMA WATOA HUDUMA ZA USINGIZI WANAHITAJIKA ZAIDI NCHINI.
Ijumaa, Februari 02, 2018
-
Hakuna maoni
Watumishi wa wa afya wa kutoa huduma za usingizi wanahitajika zaidi nchini ili kuweza kutoa huduma hiyo kwa wingi na ukaribu zaidi mara zinapohitajika kwa wagonjwa wanaohitaji upasuaji kwa usalama katika hospitali zetu
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)















