Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 20 Agosti 2018

WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII WANAHITAJIKA NCHINI

- Hakuna maoni
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na wadau wa sekta ya afya wakati akifungua kikao cha wahudumu wa afya ngazi ya jamii hii leo jijini Dodoma

Mkurugenzi wa huduma za Kinga Wizara ya Afya, Dkt. Leonard Subi akifuatilia kwa makini Maelekezo ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya hayupo pichani katika kikao kilichoshirikisha wadau wa afya na wahudumu wa afya ngazi ya jamii kinachofanyika jijini Dodoma.

Wadau wa afya kutoka mikoa mbalimbali nchini wakisikiliza kwa makini mjadala unaoendelea katika kikao kilichoshirikisha wadau wa afya na wahudumu wa afya ngazi ya jamii kinachofanyika jijini Dodoma.

Katibu mkuu wizara ya afya, Maendeleo ya jamii, jinsia wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa afya katika ufunguzi wa kikao kinachoshirikisha wadau wa afya nchini na wahudumu wa afya ngazi ya jamii.


Wadau wa afya kutoka mikoa mbalimbali nchini wakijadili kwa makundi mada mbalimbali  katika kikao kilichoshirikisha wadau wa afya na wahudumu wa afya ngazi ya jamii kinachofanyika jijini Dodoma.

NA WAMJW-DODOMA 

Wahudumu wa afya ngazi ya jamii wanahitajika nchini ili waweze kusaidia kutoa elimu kwa wananchi ili kuweza waweze kutafuta huduma za afya kwenye vituo vya kutolea huduma za afya mahali popote.
Hayo yamesemwa leo na katibu Mkuu Wiraya ya Afya,maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Mpoki Ulisubisya wakati kikao cha wadau cha kujadili taarifa ya uchambuzi yakinifu  kwa ajili ya kuhuisha mtaala wa watoa huduma  ya afya ngazi ya jamii kinachofanyika jijini hapa.
Dkt.Mpoki alisema Serikali inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya sekta ya afya yenye lengo la kuboresha huduma za afya na kuimarifa afya za wananchi.
Aidha,alisema wahudumu wa afya ngazi ya jamii  wana nguvu  kwani wana mchango mkubwa mkubwa kwani ni makomandoo ambao wanaweza kutoa elimu kwa jamii na hivyo kusaidia kuzuia magonjwa yanayosababisha vifo vitokanavyo na uzazi.
Alisema takwimu zinaonesha kuwa vifo vitokanavyo na uzazi kati ya akina mama 100,000  ni vifo 556 hutokea  hivyo kuwapo wa hudumu wa afya gazi ya jamii wanaweza kupunguza hali hiyo.
“ Katika kufikia malengo ya Tanzania ya uchumi wa kati na  viwanda, wahudumu wa afya ngazi ya jamii wanatakiwa kutumika kuwaibua akina mama ambao hawapeleki watoto wao kupata chanjo, na matumizi sahihi ya matumizi ya vyandarua ili kuepuka ugonjwa wa Malaria nah ii imeonekana  pia katika nchi za afrika kam Ethiophia,Rwanda na zingine
Hata hivyo Dkt.Mpoki aliwataka wadau  kuunga mkono  jitihada hizi za serikali na hivyo kubainisha maeneo ambayo watasaidia
Naye Mkurugenzi wa Mafunzo na Wataalam wa Rasiliamali watu Dkt.Otilia Gowele alisema kwa sasa wanapitia upya  mtaala wa mafunzo kwa wa hudumu wa afya ngazi  ili kuendana na hali halisi ya sasa na mahiaji katika sekta ya afya.
“tuekutana ili kupokea na kujadili maoni ya wadau kwa kuzingatia tathimini ya kina iliyofanywa katika kuuhisha mtaala wa mafunzo ya wahudumu wa afya ngazi ya jamii na kuangalia changamoto ili kuendana na mahitaji halisi na kukidhi soko la ajira katika hopsitali za umma na binafsi,” alisema.
Alisema tangu kuanza kutumika kwa mataala wa mafunzo ya watoa huduma wa afya ngazi ya jamii mwaka 2015 na kutumika kwenye vyuo 78 hapa nchini, tayari wataoa huduma wapatao 9,000 wamehitimu.
.
 


TAARIFA KWA UMMA

- Hakuna maoni
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VYETI VYA WAHITIMU WA KADA ZA AFYA

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inapenda kuwajulisha kuwa imepokea vyeti vya wahitimu kutoka Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).Vyeti hivyo ni kwa wahitimu waliofanya mitihani  2016, mwezi Septemba na Oktoba 2017 kwa Mafunzo ya Astashada na Stashahada ya Uuguzi na Ukunga, Mafunzo ya Astashahda ya Wahudumu wa Afya ya Jamii na Mafunzo ya Sayansi Shirikishi za Afya (Utabibu, Wateknolojia wa Maabara, Famasia, Sayansi ya Afya ya Mazingira, Utunzaji kumbukumbu za Afya, Mazoezi ya viungo ,Utabibu wa Meno na Wateknolojia Macho).
Wizara inawajulisha wahitimu wa mafunzo hayo kuwasiliana na Wakuu wa Vyuo kuanzia tarehe 20/08/2018 ili kuweza kupewa utaratibu wa kwenda kuchukua vyeti vyao kwenye vyuo walivyopatia mafunzo hayo.
Imetolewa na,
KATIBU MKUU (AFYA)
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
20 Agosti, 2018.

Ijumaa, 17 Agosti 2018

PICHA MBALI MBALI ZA MATUKIO YA KUFUNGA KWA MKUTANO WA WAGANGA WAKUU WA MIKOA NA HALMASHAURI.

- Hakuna maoni
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na Waganga wakuu wa Mikoa na Halmashauri wakati wa kufunga mkutano wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri hawapo pichani ,kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa OR-TAMISEMI Dkt. Zainabu Chaula .
 
 Mkurugenzi wa Utawala na Rasirimali watu kutoka Wizara ya Afya Deodata Makani akiongea na Waganga wakuu wa Mikoa na Halmashauri wakati wa kufunga mkutano wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri  hawapo pichani uliofanyika jijini Dodoma.

Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri wakifuatilia kwa makini maada mbalimbali zilizokuwa zinatolewa na wawasilishaji mbalimbali hawapo pichani wakati wa kufunga mkutano wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri uliofanyika jijini Dodoma.

DKT. SUBI AWAHASA WANAWAKE KUWAI KLINIKI PINDI WANAPOHISI WANAUJAUZITO.

- Hakuna maoni
Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na  Watoto Dkt.Leonard Subi

Na.WAMJW - Dodoma

Akina Mama wajawazito wametakiwa  kuwahi kliniki mara wanapohisi wana ujauzito na kufuata ushauri wa wataamu wa afya  ili kuwakinga watoto wanaotarajia kujifungua dhidi ya maabukizi ya Virus vya UKIMWI
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na  Watoto Dkt.Leonard Subi mjini Dodoma hivyo kuwataka wananchi kuchukua hatua katika kujikinga na maradhi mbalimbali ikiwemo Virusi Vya Ukimwa (VVU).
Amesema Utafiti uliofanywa mwaka 2010 maambukizi ya Virus yalikua  asilimia 26  kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto huku utafiti uliofanywa mwaka  2016/2017 unaonesha kuwa maambukizi haya yamepungua na kufikia asilimia 7.6 ambapo Serikali imesema inatarajia maambukizi haya yapungue mpaka asilimia 2 ifikapo 2020-2021.
“Ni  muhimu kwa wajawazito kuhudhuria kliniki na kupima VVU hii itasaidia kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, malezi na makuzi  mzuri ya Mtoto yanategemea wazazi wote wawili yaani baba na mama wazazi wote wanaaswa kushirikiana hasa katika kupima afya afya ili mtoto atakaezaliwa asiwe na maambukizi ya VVU”Alisema Dkt.Subi. 
Aliongeza kuwa  moja ya changamoto inayokwamisha mpango huu ni  wanaume kukumbatia mila na destuli za kutoandamana na wenzi wao kliniki wakati wa kipindi cha ujauzito,
“hivyo familia au makabila ambayo bado yanaona kwamba mwanaume kumsindikiza mwenzi wake kliniki ni kujishushia hadhi waachane nazo”.
Aidha, Dkt.Subi amewataka vijana kuchukua hatua za kwenda katika vituo vya afya kupata elimu ya uzazi na kupima afya zao maana wao ndio mama au baba wanaotarajiwa,mimba za utotoni ni hatari kwa afya zao na kama kuna tatizo lolote wafike katika vituo vya afya ili kupata msaada wa kitalaamu.
Alisisitiza kuwa vituo vya kutolea huduma za afya vyote nchini hivi sasa vinatoa huduma ya elimu bure kuhusiana na afya ya uzazi na endapo mama mjamzito atagundulika ana maambukizi ya VVU ataanzishiwa dawa ambazo zitamkinga mtoto asizaliwe na maambukizi ya  Virus vya UKIMWI.


Jumatatu, 13 Agosti 2018

WAZIRI UMMY AMSHUKURU BALOZI WA CANADA NCHINI TANZANIA KWA KUBORESHA SEKTA YA ÁFYA.

- Hakuna maoni

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiagana na Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles mapema leo katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam baada ya mazungumzo juu ya Maboresho katika Sekta ya Afya.

Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles (Wapili kushoto) akimweleza jambo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu mapema leo wakati alipotembelea katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es salaam. Wakwanza kushoto ni ofisa wa Ubalozi wa Canada Susan Steffen.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimsikiliza kwa makini Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles (Hayupo kwenye picha)

Picha ya Pamoja ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles baada ya kikao cha kumuaga Balozi huyo kilichofanyika mapema leo katika Ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam.

WAZIRI UMMY AMSHUKURU BALOZI WA CANADA NCHINI TANZANIA KWA KUBORESHA SEKTA YA ÁFYA. 

Na WAMJW - DSM 

Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu ameishukuru Serikali ya Canada kupitia Balozi wake nchini Tanzania kwa ushirikiano walioonesha katika kuboresha sekta ya Áfya hususani katika Kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Ameyasema hayo mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Áfya jijini Dar es salaam wakati akiagana na Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Ian Myles anayetarajia kuondoka hivi karibuni hapa nchini.

Nae Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe Ian Myles  ameishukuru Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Áfya kwa kuendelea kutatua changamoto za sekta ya Áfya nchini.

Ijumaa, 10 Agosti 2018

TAMKO KUHUSU UGONJWA WA EBOLA ULIOTOKEA KATIKA NCHI JIRANI YA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO

- Hakuna maoni
TAMKO KUHUSU UGONJWA WA EBOLA ULIOTOKEA KATIKA NCHI JIRANI YA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO

Utangulizi
Ndugu wanahabari, 
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea kutoa taarifa kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Nchi hiyo ya DRC imetangaza tena kuwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola mnamo tarehe 1 mwezi Agosti, 2018, ambapo jumla ya wagonjwa 26 na vifo 10 vilitolewa taarifa na wagonjwa 4 kati yao walithibitishwa kimaabara kuwa na ugonjwa wa Ebola. Wagonjwa hawa wametokea katika vijiji/Maeneo ya Mangina ikiwa ni kama km 30 tu magharibi mwa mji wa Beni kwenye jimbo la Kivu Kaskazini linalopakana na nchi ya Uganda ikiwa ni kama km 100 tu, na pia likiwa karibu sana na nchi ya Rwanda. 
Huu ni mlipuko wa 10 wa ugonjwa wa Ebola kutokea nchini DRC, na umetokea wiki moja baada ya nchi hiyo kutangaza kuisha kwa mlipuko mwingine uliotokea mwezi Mei mwaka huu ambao ulikuwa katika jimbo la Equator, Magharibi mwa DRC, umbali wa zaidi ya km 2,000 kutoka eneo la huu mlipuko mpya uliotokea.
Ndugu wanahabari,
HADI SASA HAPA NCHINI TANZANIA HAKUNA MGONJWA YOYOTE ALIYEHISIWA AU KUTHIBITISHWA KUWA NA VIRUSI VYA EBOLA. Hata hivyo, kugunduliwa kwa ugonjwa huu kwenye jimbo la Kivu Kaskazini linalopakana na nchi za Uganda na Rwanda ni jambo la kutuweka kwenye wasi wasi kwani eneo hili liko karibu sana na nchi yetu kuliko eneo lingine lolote ambako ugonjwa huu umeshawahi kutokea kwenye nchi ya DRC. Hivyo nchi yetu ipo hatarini kuambukizwa ugonjwa huu kutokana na ukaribu na muingiliano wa watu, hasa kuhusiana na wasafiri wanaotoka na kuingia hapa nchini. 
Kwa sababu hizi, watanzania hatuna budi kuchukua tahadhari ya hali ya juu ili kujikinga na kudhibiti na ugonjwa wa Ebola.  Hivyo Wizara inapenda kutoa tahadhari ya ugonjwa huu kwa wananchi wote katika Mikoa yote ya Tanzania, lakini hasa ile inayopakana na nchi jirani za DRC, Uganda na Rwanda. Mikoa hiyo ni pamoja na Mwanza, Kagera, Kigoma, Katavi, Rukwa na Songwe. Aidha tahadhari na hatua stahiki zichukuliwe katika maeneo yote ya mipakani ambapo abiria wanaingia nchini kutoka nchi jirani.

Ugonjwa wa Ebola
Ugonjwa wa Ebola husababishwa na virusi vya Ebola ambavyo huambukiza kwa njia zifuatazo; 
Kugusa Damu au majimaji kutoka kwa mtu aliyeambukizwa ugonjwa huo, 
Kugusa maiti ya mtu aliyekufa kwa ugonjwa huo, 
Kugusa wanyama (Mizoga na wanyama wazima) walioambukizwa kama vile Sokwe na Swala wa msituni. 
Dalili za Ugonjwa
Dalili za Ugonjwa huanza kuonekana kwa mtu aliyeambukizwa baada ya siku 2 hadi 21 tangu kupata maambukizi. Dalili hizo ni pamoja na;
Homa kali ya ghafla, 
Kulegea kwa mwili,
Maumivu ya misuli, 
Kuumwa kichwa na vidonda kooni. 
Mara nyingi dalili hizo hufuatiwa na kutapika, kuharisha, vipele vya ngozi na pia figo na Ini kushindwa kufanya kazi. 
Kwa baadhi ya wagonjwa kutokwa na damu ndani na nje ya mwili. 


Namna ya Kujikinga na ugonjwa wa Ebola:
Ugonjwa wa Ebola unaweza kuzuilika. Njia kuu za kujikinga na ugonjwa huu ni:-
Kuepuka kugusa au kuingiwa na mate, damu, mkojo, jasho, kinyesi, machozi na majimaji mengine yanayotoka mwilini mwa mgonjwa mwenye dalili za ugonjwa  wa Ebola
Kuepuka kushughulikia maiti ya mtu aliyefariki akiwa na dalili za Ebola; badala yake watoe taarifa kwa uongozi wa kituo cha huduma za Afya kwa ushauri.
Kuepuka kula nyama za Wanyama wa porini kama sokwe, swala na popo na pia kugusa mizoga ya Wanyama hao
Kuepuke mila na desturi  zinazoweza kuchelewesha kupata huduma muhimu na kuzidi kueneza ugonjwa wa Ebola.
Kuzingatia usafi wa mwili
Kutoa taarifa mapema kwa viongozi wa Serikali na wa huduma za Afya katika ngazi zote pale anapotokea mtu mwenye  dalili za Ebola.
Kuwahi katika vituo vya huduma za Afya pale mtu anapoona dalili za ugonjwa huu.




Hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa na Wizara kufuatia kupatikana kwa taarifa ya Ugonjwa huu huko DRC 
Kufuatia kuwepo kwa taarifa hizi tangu mwezi Mei 2018, hatua zifuatazo zinaendelea/zimechukuliwa na Wizara ili kujiandaa kukabiliana na mlipuko huo:
Kufanya tathmini ya utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola nchini (Operational readiness assessment) kwa nchi nzima kwa kushirikiana na WHO na kuainisha mapungufu ambayo yanapaswa kufanyiwa kazi. Mapungufu hayo yanaendelea kuyafanyiwa kazi ili kujenga uwezo na utayari katika nchi yetu.
Tumetengeneza mpango mkakati wa kujiandaa na kupambana na mlipuko wa Ebola endapo utatokea nchini (Costed Ebola Contingency Plan). Mpango huu umeandaliwa kwa kushirikiana na WHO. Mpango umeainisha maeneo ya kujenga uwezo kwa wakati huu wa kujiandaa, pamoja na hatua za kuchukua endapo ugonjwa utaingia ikiwa ni pamoja na gharama zake.
Tumefanya mafunzo ya Timu za dharura (Rapid Response Teams) ngazi ya Taifa na katika Mikoa ya Dar es Salaam, Songwe, Rukwa, Katavi, Kigoma na Kagera
Tumeimarisha ufuatiliaji wa wasafiri mipakani (travellers entry screening) kwa kutumia vifaa vya kupima joto la mwili (thermo scanners) na fomu maalum za wasafiri
Wizara imepokea vifaa vya kukabiliana na Ebola kutoka WHO vikiwemo; Thermo scanners, Vifaa Kinga, au PPE, kama vile gloves, body bags, vifaa vya ufungashaji wa sampuli nk. Vifaa hivyo vimeanza kusambazwa mikoani kupitia MSD
Uelimishaji wa umma umefanyika na unaendelea kufanyika kwa kupitia vyombo vya habari vya kitaifa na kijamii, na mitandao ya kijamii. Vile vile vipeperushi na mabango vinaendelea kuandaliwa
Vikao vya uratibu vimefanyika katika ngazi ya taifa na mikoa ambayo ipo katika hatari zaidi. Pia ufuatiliaji wa karibu unaendelea kupitia Kituo cha ufuatiliaji wa magonjwa ya dharura cha Wizara (Public Health Emergency Operation Centre is on High Alert) 
Wataalam kutoka ngazi ya Taifa kwa sasa wako katika mikoa ya Kigoma Katavi Rukwa Kagera Kilimanjaro Mwanza Songwe na Mbeya kufanya tathmini ya utayari katika ngazi ya mikoa na Wilaya (Readiness Assessment)
Maandalizi yanaendelea kwa ajili ya kutekeleza kazi nyingine kama ifuatavyo:
Kufanya mafunzo katika mikoa iliyo salia ikiwemo Mwanza, Kilimanjaro na Mbeya ambayo imesalia katika ile mikoa nane iliyo katika hatari zaidi
Mafunzo ya waandishi wa habari 30 (media orientation)
Zoezi la udhibiti wa matukio ya dharura (simulation exercise) katika ngazi ya Taifa
Mafunzo kwa wasfirishaji wa sampuli kwenda katika maabara

Hitimisho
Nawaomba Wakuu wa Mikoa na Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri wote nchini kuchukua Tahadhari na kuendelea kuelimisha wananchi wote juu ya ugonjwa huu na kuwataka kutokuwa na hofu ila kuendelea kuchukua tahadhari za kujikinga na ugonjwa huu kwani mpaka sasa hakuna mtu aliyethibitishwa kuugua ugonjwa huu hapa nchini. 

Aidha Wizara itaendelea kushirikiana na sekta mbalimbali katika kuimarisha ufuatiliaji na kuendelea kutekeleza mikakati ya kudhibiti ili ugonjwa huu usiingie nchini. Vilevile Wizara itaendelea kutoa taarifa pamoja na Elimu kwa Jamii kadri itakavyohitajika. 
Imetolewa na 

Ummy A. Mwalimu (Mb)
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, 
Jinsia, Wazee na Watoto
10/08/2018

IDADI YA WANAWAKE WANAOTUMIA HUDUMA ZA ZA UZAZI WA MPANGO ZAONGEZEKA NCHINI.

- Hakuna maoni
Waziri wa Maendeleo kutoka nchi ya Uingereza Mhe.  Penny Mordaunt (katikati) akimsalimia mtoto mchanga aliyebebwa na baba yake katika jengo la Kliniki ya Baba, Mama Na Mtoto. Kulia ni Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.





Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisoma mbao ya matangazo katika Zahanati ya Tabata jijini Dar es salaam pindi alipofika kupokea ugeni wa Waziri wa Maendeleo kutoka nchi ya Uingereza.

Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitoa Elimu juu ya umuhimu wa kukata Bima ya Áfya kwa mtoto (Toto Afya Card) kwa mmoja kati ya wazazi  waliofika katika Zahanati ya Tabata kupata huduma za matibabu ya mtoto.

Mshauri wa masuala Ya Afya kutoka ubalozi wa Uingereza DKt. Gloria Ngaiza (wapili Kushoto) akimtafasiria Waziri wa Maendeleo kutoka nchi ya Uingereza Mhe. Penny Mordaunt kilichokuwa kikisemwa na Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Tabata (Wakwanza Kushoto).Wa mwisho Kulia ni Waziri wa Áfya Mhe. Ummy Mwalimu.
IDADI YA WANAWAKE WANAOTUMIA HUDUMA ZA ZA UZAZI WA MPANGO ZAONGEZEKA NCHINI 

Na WAMJW - DSM

SERIKALI kupitia Wizara ya Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,  Wazee na Watoto imesema kuwa idadi ya wanawake wanaotumia huduma za Afya za Kisasa za uzazi wa mpango zimeongezeka nchini mpaka kufikia Asilimia 32.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Áfya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu leo wakati alipoupokea ugeni  wa Waziri wa Maendeleo kutoka nchini Uingereza katika Zahanati ya Tabata jijini Dar es salaam ukiwa na lengo la kutatua changamoto za Sekta ya Áfya hususani katika huduma za Afya ya mama na mtoto.

"Kupitia Msaada wao tumeweza kuongeza idadi ya wanawake wanaotumia huduma za Kisasa za uzazi wa mpango, hatupo vizuri,  tupo Asilimia 32, tumeweka lengo itapofika 2020 tufikie Asilimia 45 ya wanawake walioolewa wanatumia njia hizi" Alisema Waziri Ummy Mwalimu. 

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa, bado kuna changamoto ya vifo vitokanavyo na uzazi nchini, takribani wanawake 556,000 katika kila vizazi hai laki moja wanafariki na kwa mujibu wa Wataalam uzazi wa mpango utaweza kuchangia Mpaka Asilimia 30 katika Kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi. 

Pia Waziri Ummy alisema kuwa Serikali ya Tanzania imechukua hatua kwa kutenga fedha za ndani katika kupambana na changamoto za sekta ya Áfya ikiwemo kuajiri watumishi wa sekta ya Áfya jambo linalosaidia Kupunguza changamoto hizo za vifo vya akina mama wajawazito na mtoto wachanga. 

"Sisi kama Serikali tumejiongeza, tumechukua hatua na kutenga rasilimali fedha za ndani ikiwemo kuajili watoa huduma za afya, kuhakikisha Kwamba tunatatua changoamoto hiyo " alisema Waziri Ummy.

Hata hivyo Waziri Ummy aliishukuru Serikali ya Uingereza kupitia kwa Waziri wa Maendeleo Mhe. Penny Mordaunt kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuboresha huduma za afya hasa katika huduma za mama na mtoto. 

Kwa upande wake Waziri wa Maendeleo kutoka Uingereza Mhe. Penny Mordaunt ameshukuru Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Áfya kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuhudumia wananchi wa Tanzania na kuahidi kupeleka salamu za Tanzania nchini Uingereza.