![]() |
|
Wadau wa afya kutoka mikoa mbalimbali nchini
wakisikiliza kwa makini mjadala unaoendelea katika kikao kilichoshirikisha
wadau wa afya na wahudumu wa afya ngazi ya jamii kinachofanyika jijini Dodoma.
|
Jumatatu, 20 Agosti 2018

WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII WANAHITAJIKA NCHINI
Jumatatu, Agosti 20, 2018
-
Hakuna maoni

TAARIFA KWA UMMA
Jumatatu, Agosti 20, 2018
-
Hakuna maoni
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VYETI VYA WAHITIMU WA KADA ZA AFYA
Wizara
ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inapenda
kuwajulisha kuwa imepokea vyeti vya wahitimu kutoka Baraza la Taifa la
Elimu ya Ufundi (NACTE).Vyeti hivyo ni kwa wahitimu waliofanya mitihani 2016, mwezi Septemba na Oktoba 2017 kwa Mafunzo ya Astashada na Stashahada ya
Uuguzi na Ukunga, Mafunzo ya Astashahda ya Wahudumu wa Afya ya Jamii na
Mafunzo ya Sayansi Shirikishi za Afya (Utabibu, Wateknolojia wa Maabara,
Famasia, Sayansi ya Afya ya Mazingira, Utunzaji kumbukumbu za Afya,
Mazoezi ya viungo ,Utabibu wa Meno na Wateknolojia Macho).
Wizara
inawajulisha wahitimu wa mafunzo hayo kuwasiliana na Wakuu wa Vyuo
kuanzia tarehe 20/08/2018 ili kuweza kupewa utaratibu wa kwenda kuchukua
vyeti vyao kwenye vyuo walivyopatia mafunzo hayo.
Imetolewa na,
KATIBU MKUU (AFYA)
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
20 Agosti, 2018.
Ijumaa, 17 Agosti 2018

PICHA MBALI MBALI ZA MATUKIO YA KUFUNGA KWA MKUTANO WA WAGANGA WAKUU WA MIKOA NA HALMASHAURI.
Ijumaa, Agosti 17, 2018
-
Hakuna maoni
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,
Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na
Waganga wakuu wa Mikoa na Halmashauri wakati wa kufunga mkutano wa
Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri hawapo pichani ,kulia ni Naibu
Katibu Mkuu wa OR-TAMISEMI Dkt. Zainabu Chaula .
Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri wakifuatilia kwa makini maada
mbalimbali zilizokuwa zinatolewa na wawasilishaji mbalimbali hawapo
pichani wakati wa kufunga mkutano wa Waganga Wakuu wa Mikoa na
Halmashauri uliofanyika jijini Dodoma.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)








