Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 23 Novemba 2018

WAZIRI MKUU AWAAGIZA MAAFISA TAWALA KUSIMAMIA UJENZI WA VYOO BORA

- Hakuna maoni
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. kassim Majaliwa akifuatilia maelekezo katika banda la Hedhi salama  wakati wa mkutano wa Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri na Wadau wa Usafi nchini uliofanyika leo jijini Dodoma.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. kassim Majaliwa (wakwanza kulia) akiwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wakatikati) pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii Mhe. Peter Selukamba wakifuatilia kikundi cha ngoma cha Mpoto (hawapo kwenye picha) wakati wa mkutano wa Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri na Wadau wa Usafi nchini uliofanyika leo jijini Dodoma.



Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. kassim Majaliwa akimkabidhi Afisa Afya wa Mkoa wa Iringa zawadi ya Bodaboda wakati wa mkutano wa Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri na Wadau wa Usafi nchini uliofanyika leo jijini Dodoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. kassim Majaliwa akisikiliza maelezo kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu namna ya matumizi ya choo pindi walipopita katika mabanda ya maonesho, wakati wa mkutano wa Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri na Wadau wa Usafi nchini uliofanyika leo jijini Dodoma.


Makatibu Tawala wa Mikoa, Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri nchini wametakiwa  kusimamia vizuri kampeni ya ujenzi wa vyoo bora kwa kutimiza lengo la kila familia na jamii inakuwa na vyoo vya kisasa hadi kufikia Disemba 31 mwaka huu.

Hayo yamesemwa leo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakati akifunga mkutano wa maofisa afya wa Mikoa, Halmashauri na Wadau wa usafi Tanzania uliyofanyika jijini hapa.

Mhe. Majaliwa amesema kwamba ujenzi wa vyoo vya kisasa katika kila kaya utasaidia kupunguza uwezekano wa magonjwa ya milipuko ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutokuwa na vyoo bora.

“Nawataka mtumie mbinu yeyote ili kuwawezesha hawa Maofisa Afya katika kutoa elimu  kwa wananchi ili suala la ujenzi wa vyoo bora liweze kutekelezeka na hata kutimiza wajibu wao wa kila siku”. Alisema Waziri Mkuu.

Hata hivyo Waziri Mkuu aliwataka wananchi  kutunza mazingira kwa kufuata kanuni bora za afya ikiwa ni pamoja na matumizi ya vyoo bora na vya kisasa ambapo alisema kutumia kampeni hiyo imewezesha kupunguza idadi ya kaya zisizokuwa na vyoo kutoka asilimia 9.5 mwaka 2015 hadi asilimia 3.8 mwaka 2018.

“Serikali ya awamu ya tano inaendelea kusisitiza juu ya uhifadhi wa mazingira na nyinyi wataalamu wa afya mnaombwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa kuelimisha umma juu ya utunzaji wa mazingira ili kutekeleza dhana ya Tanzania ya viwanda kwa kutunza vyanzo vya maji na kutumia vyoo bora”. Alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Aidha, amewataka maafisa afya nchini kote kuhakikisha hakuna mfumo mbovu wa utililishaji maji kutoka viwandani na kutaka sheria ya utunzaji mazingira ya mwaka 2004 inatekelezwa ipasavyo ikiwa na kuhakikisha watumishi wa viwanda wanakua na mfumo wa utunzaji wa afya zao.

“Ninaagiza uwepo wa miundombinu ya ujenzi wa vyoo bora, sehemu ya kunawa mikono kwa maji safi na sabuni kwa taasisi zote za umma na binafsi, vituo vya afya, shule zote, vituo vya abiria na nyumba zote za ibada kabla ya Aprili 30 mwaka 2019.

Kuhusu tabia ya uchimbaji dawa wakati wa safari ambayo hivi sasa imeota mizizi, Waziri Kassim Majaliwa amesema kuwa hivi sasa serikali pamoja na watu binafsi wamejenga na kutoa huduma za vyoo katika vituo maalum, vituo vya kuuzia mafuta, hoteli pamoja na maeneo ya umbali mrefu hivyo kuwataka Maofisa Afya kuwachukulia hatua kali wale wote wanaogundulika wanachimba dawa sehemu ambazo siyo rasmi au zilizotengwa na hiyo itasaidia  kuondoa kero za uchafuzi wa mazingira kwa kuchimba dawa porini.

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema katika awamu ya pili ya kampeni ya taifa ya usafi wa mazingira ya mwaka 2016/2021 wizara yake imepanga kuhakikisha asilimia 75 ya kaya nchini zinakua na vyoo bora  na kwamba kuondoa kaya ambazo hazina vyoo kabisa.

Alisema kwa upande wa shule, lengo ni kujenga miundombinu ya usafi na huduma za maji kwenye shule za msingi 3,500 na 700 za sekondari.
”Na kwa upande wa vituo vya tiba tunapanga kufikia vituo 1,000 hivyo kwa bajeti ya mwaka 2018/2019  tumejenga vyoo vipatavyo 700”. Alisistitiza Waziri Ummy.

Katika mkutano huo ambao uliambatana na maadhimisho ya wiki ya usafi wa mazingira kitaifa ambapo kulitangazwa washindi wa mashindano ya usafi na  Halmashauri ya Njombe iliibuka mabingwa kwa miaka mitatu mfululizo katika kundi la halmashauri za miji, wilaya, vijiji, shule za msingi za vijijini pamoja na shule za sekondari za bweni za  serikali na binafsi.
-Mwisho-






DKT. NDUGULILE – “SEKTA YA AFYA NCHINI INAKUWA KWA KASI”

- Hakuna maoni

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akisoma nyaraka za matibabu za Bi. Mary Nyange (kulia) anayepatiwa huduma za matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akihojiana na Bw. Longini Mtalo, Mteknolojia kutoka kituo cha utengenezaji wa viungo bandia katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC  huku akiwa ameshika sampuli ya kiungo bandia kilichotengenezwa na kituo hicho.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akikagua benki ya damu zilizopo katika jokofu Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini ya KCMC

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akionyesha mafuta maalum kwa ajili ya kuwakinga wenye ulemavu wa ngozi dhidi ya miale ya jua yanayotengenezwa na  kitengo cha Kilimanjaro Sunscreen Production kilichopo Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini ya KCMC.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akihojiana na  Bw. Prosper Kaaya, Mteknolojia kutoka kituo cha utengenezaji wa viungo bandia katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC  huku akiwa ameshika kiungo bandia kilichotengenezwa na kituo hicho.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (aliyesimama) akisema jambo wakati wa kikao na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC (hawapo pichani) aliye upande kulia ni Mganga Mkuu Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Best Magoma upande wa kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskasini KCMC Dkt. Gileard Masenga.

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC wakisiliza jambo wakati wa kikao kazi na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani) aliyetembelea hospitali hiyo Novemba 22, 2018.


NA WAMJW- KILIMANJARO

“Sekta ya afya inakua kwa kasi huku huduma muhimu za afya kwa sasa zikiwa zinapatikana hapa hapa nchini”

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile alipokua akizungumza na watumishi wa Hospitali ya rufaa ya Kanda ya Kaskazini (KCMC) iliyopo katika Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro jana Novemba 22, 2018.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Sekta ya Afya imepewa kipaumbele cha hali ya juu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli katika kipindi cha miaka mitatu mageuzi makubwa ndani ya sekta ya afya yameanza kuonekana huku huduma za matibabu ya kibingwa yakiwa zikipatikana hapa hapa nchini.

“Tunasimama hapa kifua mbele tukiona mabadiliko katika hali ya upatikanaji wa dawa kuimarika zaidi, bajeti ya dawa imeongezeka toka Shilingi Bilioni 30 mpaka Shilingi Bilioni 270 yaani mara tisa zaidi ndani ya miaka mitatu” alisema Mhe.Naibu Waziri na kuendelea “Tumeboresha vituo vya afya takribani 300, huku Mkoa wa Kilimanjaro ukiwa na Vituo 8 vilivyoboreshwa vilivyogharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 3.5 na kwa mwaka huu 2018 Serikali imeanza kujenga Hospitali za Wilaya 67 nchini”

Aidha, Dkt. Ndugulile alisema kuwa Serikali imetenga Shilingi Bilioni 30 kwa ajili ya Hospitali mpya za Rufaa za Mikoa ili  ziweze kutoa huduma za kibingwa, kupunguza msongamano wa wagonjwa na ucheleweshwaji wa huduma katika Hospitali za rufaa za kanda.

Naibu Waziri huyo Aliendelea kusema  kuwa fedha hizo Shilingi Bilioni 30 zitaelekezwa katika maeneo makuu matano ambayo aliyataja kuwa ni kuhakikisha kila Hospitali ya Mkoa ina Kitengo cha dharura, chumba cha upasuaji, kitengo cha uangalizi wa wagonjwa mahututi pamoja na kitengo cha mama na mtoto.

"Hospitali hii inatakiwa kuhudumia wagonjwa waliopata rufaa toka hospitali za mikoa ya jirani waje huku kupatiwa huduma za matibabu na sio wagonjwa wa malaria na mafua alisema Dkt. Ndugulile.

Katika kuhakikisha huduma bora za afya zinatolewa kwenye hospitali za rufaa za mikoa, Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali imeweka maeneo muhimu katika mafunzo kwa watumishi wa kada ya afya huku akitaja watumishi wenye kuhitajika zaidi kwa sasa kuwa ni madaktari wa magonjwa ya ndani, watoto, wakina mama, upasuaji, mifupa pamoja na madaktari wa usingizi.

Kuhusu upatikanaji wa huduma za kibingwa, Dkt.Ndugulile alisema  mafanikio  kuona huduma hizo zikiwa zinapatikana hapa nchini tofauti na zamani  “Tunafanya upandikizaji wa figo pamoja na upandikizaji wa vifaa vya usikivu kwa wa watoto huduma ambazo zilikuwa ni za kufikirika ndani ya miaka mitatu sasa zinapatikana hapa nchini” alisema Dkt. Ndugulile.

Awali akitoa taarifa yake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC Dkt. Gileard Masenga aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Hospitali hiyo "Licha ya kumilikiwa na Taasisi ya kidini lakini Serikali imeendelea kutupatia wataalam, misamaha ya kodi za malighali zinazoingizwa nchini ambazo hutumika kutengeneza mafuta ya kuwakinga wenye ulemavu wa ngozi dhidi ya jua.

Aidha, Dkt.Masenga alisema hospitali yake imetengewa  Shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya dawa za Saratani huku fedha kiasi cha Shilingi Milioni 250 tayari  zimeshapelekwa Bohari ya dawa kwa ajili ya ununuzi wa dawa hizo.

 Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto yupo Mkoani hapa kwa ziara  ya kikazi  inayolenga kukagua shughuli za huduma ya Afya,Maendeleo ya Jamii pamoja na kuongea na watumishi wa sekta  hizo.

MWISHO.

Jumatano, 21 Novemba 2018

DKT. MPOKI AKEMEA TABIA YA ABIRIA NA MADEREVA KUCHIMBA DAWA MAENEO YASIYOHUSIKA

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya akitoa neno mbele ya Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri pamoja na Wadau wa Mazingira leo katika Ukumbi wa CCM jijini Dodoma.




Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya akikagua maonesho ya vyoo baada ya kufungua kikao cha Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri pamoja na Wadau wa Mazingira leo jijini Dodoma. 
Picha ya Pamoja ikiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya katika baada ya kikao cha  Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri pamoja na Wadau wa Mazingira kilichofanyika leo jijini Dodoma.
NA WAJMW-DODOMA

Madereva wa mabasi yaendayo mikoani na abiria wametakiwa kuacha tabia ya kujisaidia “Kuchimba dawa” katika maeneo yasiyo rasmi ili kutunza na kuepuka uharibifu wa mazingira unaoweza kujitokeza ikiwa ni pamoja kusababisha magonjwa ya milipuko.

Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati akifungua mkutano unaojumuisha Maafisa Afya kutoka mikoa na Halmashauri mbalimbali nchini pamoja na wadau wa mazingira, katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Dkt. Mpoki amekemea tabia hiyo hatarishi kwa ustawi wa mazingira huku akiwataka maafisa Afya na wadau wa mazingira nchini kusimamia afua zilizowekwa zinaendelea kutekelezwa ili kulinda mazingira ambayo yanatuzunguka.

“Kuna watu wengine nimeshawahi kuwaona kwenye basi wanatupa taka ovyo na mabasi mengine yanasimama porini ili abiria wajisaidie, hii tabia siyo nzuri na inatakiwa ikemewe kwa nguvu zote, Dkt. Subi na wenzake wanakuja na mpango mkakati  wa kuondoa kabisa dhana ya watu kusimama kujisaidia porini, sisi tunatakiwa kuwa msitari wa mbele kupiga marufuku mabasi  kusafiri bila kuchafua mazingira”.

Dkt. Mpoki amesema ni aibu kubwa kwa taifa kuona watu hawafuati kanuni za usafi huku akiwataka Maafisa Afya kuhakikisha wanafanya kazi kwa nguvu ili ionekane kuwa kero kwa watu wengine na watakaobainika kuchafua mazingira wachukuliwe hatua za kinidhamu na kisheria.

Aidha, Dkt. Mpoki ameongeza kuwa jamii inatakiwa kuzingatia matumizi ya vyoo bora na kunawa mikono mara baada ya kujisaidia ili kuepuka magonjwa ya milipuko yanayoweza kusababishwa na tabia ya uchafu ikiwa ni pamoja na kuacha tabia ya kujisaidia ovyo porini ili kaulimbiu ya “Nyumba ni Choo” iweze kutekelezwa ipasavyo kwa kujenga vyoo vya kisasa katika maeneo mbalimbali ili huduma ipatikane mahala pote.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi amesema takwimu zinaonesha kaya zilizokua na vyoo bora mwaka 2012 zilikua asilimia 19.5 lakini hivi sasa nchi nzima kaya zenye vyoo bora ni asilimia 51.4.

Dkt. Subi amesema kutokana na takwimu hiyo inaonesha kuna mafanikio katika uhamasishaji kwa jamii kutumia vyoo bora na kuacha kutumia vyoo ambavyo havina viwango na salama kwa matumizi, na badala yake serikali inaendelea kutoa elimu na kusisitiza jamii kutumia vyoo bora ili kuepuka magonjwa yanayoweza kuzuilika ikiwemo kipindupindu, magonjwa ya tumbo na kuhara.

Pamoja na hayo, maafisa Afya wametakiwa kuongeza nguvu katika kutoa elimu kwa umma, kuhamasisha usafi wa mazingira na kufukia maeneo ya mazalia ya vimelea vya ugonjwa wa Malaria ili kutokomeza ugonjwa huo ambao umekua hatari kwa jamii hasa kwa wanawake wajawazito na watoto.

Mkutano huo unaojumuisha Maafisa wa Afya nchi nzima una lengo la kutoa elimu na kubadilishana uzoefu wa kufanya kazi lakini msisitizo mkubwa ikiwa ni utunzaji wa mazingira na kuzingatia kanuni bora za afya pamoja na usafi wa mazingira na usafi na afya ya binadamu. 

Alhamisi, 15 Novemba 2018

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYOJIRI KWENYE MKUTANO MKUU WA MWAKA WA KUJADILI MASUALA MBALIMBALI YA AFYA JIJINI DODOMA




Wadau na wataalam mbalimbali wa afya wakiangalia na kujadili utekelezaji wa vipaumbele vya matamko ya Kisera yaliyoidhinishwa kwa mwaka wa fedha 2017/18 pamoja na utekelezaji wa vikundi kazi 11 vya Kitaalam katika kutekeleza mpango mkakati wa nne kwa mwaka wa fedha 2017/2018

SERIKALI YAJIPANGA KUTOKOMEZA MAAMBUKIZI YA VVU KWA WATOTO WACHANGA.

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na wadau mbalimbali wa maendeleo na sekta ya afya hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma.

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akikata utepe kuashiria kuzindua chapisho la uchambuzi  wa masuala ya lishe wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma, wa pili kushoto ni Naibu Waziri OFisi ya Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara .

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akionesha moja ya chapisho la uchambuzi  wa masuala ya lishe wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma, wa pili kushoto ni Naibu Waziri OFisi ya Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara .

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akifuatilia mada iliyokuwa inawasilishwa na moja ya wawasilishaji hayupo pichani  wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma, wa pili kulia ni Naibu Waziri OFisi ya Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara .

Baadhi ya  wadau mbalimbali wa maendeleo na sekta ya afya wakifuatilia kwa makini hotuba ya Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma.


NA WAMJW-DODOMA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema serikali ina mpango madhubuti wa kuhakikisha wamama wajawazito hawawaambukizi watoto walio tumboni Virusi vya Ukimwi na kipindi wanapozaliwa.

Waziri Ummy amesema hayo leo wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya maendeleo ya jamii ikiwa ni pamoja na masuala ya lishe, uliofanyika katika ukumbi wa Hazini, Jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema hadi hivi sasa asilimia 99 ya wajawazito wenye maambukizi ya VVU wanapewa huduma za kumkinga mtoto asipate maambukizi hayo huku la serikali ifikapo mwaka 2020 ni kuhakikisha  hakuna mtoto atakayezaliwa na maambukizi ya VVU.

“Sasa hivi asilimia 99 ya wanawake wajawazito wote wenye maambukizi  ya VVU tumewaingiza katika mpango wa dawa, na hiyo asilimia moja bado hatujawafikia ila kwa nguvu na msukumo tuliouweka juzi wa kuwasainisha Wakuu wa Mikoa kwenda kufuatilia masuala ya afya ya mama na mtoto, tunaamini hakuna mtoto yeyote Tanzania atakayezaliwa na maambukizi ya UKIMWI”. Amesema Waziri Ummy.

Katika Uzinduzi huo, Waziri Ummy ameipongeza Wizara ya Fedha na Mipango kupitia kwa Waziri wake Mhe. Dkt. Philipo Mpango  inavyojikita katika mipango ya kuendeleza wanawake na watoto kwa kutoa huduma bora za afya, elimu, maji na masuala ya maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na Shirika la Watoto Duniani (UNICEF) imefanya uchambuzi wa bajeti katika sekta mtambuka ya jamii, hususani katika elimu, afya, Virusi vya Ukimwi, maji, usafi wa mazingira na lishe kwa lengo la kuboresha upangaji na utekelezwaji wa masuala ya mama na mtoto.

Pamoja na hayo, uzinduzi wa machapisho hayo umelenga kupunguza tatizo la lishe linalosababisha udumavu kwa watoto walio katika umri mdogo. Ambapo katika ripoti iliyotolewa katika mkutano wa IMF na Benki ya dunia uliofanyika nchini Indonesia mwezi Oktoba mwaka 2018, inaonesha Tanzania inashika nafasi ya 128 kati ya nchi 157 duniani katika kipimo cha ubora wa nguvukazi  katika uwekezaji wa rasilimali watu hususani katika sekta ya afya na elimu ya lishe.

Kufuatia hali hiyo, Tanzania inaonekana kuwa na matatizo ya udumavu, elimu ya lishe na afya kwa watoto wenye umri mdogo ambapo serikali inafanya kazi kubwa ya kuhakikisha elimu ya lishe inawafikia wazazi na jamii kwa ujumla ili kupambana na tatizo la udumavu. Na kufikia mwaka 2015 tatizo la udumavu limeshuka kutoka asilimia 34 kutoka asilimia 42 mwaka 2010. Alisema Waziri huyo.

Tatizo la lishe limeonekana kupungua nchini huku viashiria vya tatizo hilo vikipungua ambavyo ni uzito pungufu umeshuka kutoka asilimia 16 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 14 mwaka 2015/16, pamoja na ukondefu wa mwili kuendelea kubakia chini ya asilimia 5 kwa mwaka 2015/16.


TANGAZO LA KUITWA KAZINI

ORODHA YA MAJINA IMEAMBATANISHWA HAPA CHINI





Jumatano, 14 Novemba 2018

TANZANIA INATOA HUDUMA ZA CHANJO KWA ASILIMIA 98.

Katibu Mkuu Wizara ya afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto  (Idara Kuu ya afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na baadhi ya wataalam na wadau wa afya hawapo pichani wakati wa mkutano wa mwaka wa kujadili mafanikio na chanagamoto za sera ya afya uliofanyika leo jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto  (Idara Kuu ya afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya wa kwanza kulia akifuatilia kwa makini mada iliyokuwa ikiwasilishwa na mmoja wa wawasilishaji mada hayupo pichani mkutano wa mwaka wa kujadili mafanikio na chanagamoto za sera ya afya uliofanyika leo jijini Dodoma.

Mkurugenzi  Msaidizi wa Tathimini na Ufuatiliaji  Wizara ya Afya Tumainieli Macha akiwasilisha mada kwa wataalam na wadau wa afya  wakati wa mkutano wa mwaka wa kujadili mafanikio na chanagamoto za sera ya afya uliofanyika leo jijini Dodoma.

Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Sarah Maongezi  akiongea na baadhi ya wataalam na wadau wa afya hawapo pichani wakati wa mkutano wa mwaka wa kujadili mafanikio na chanagamoto za sera ya afya uliofanyika leo jijini Dodoma.

Baadhi ya wadau na wataalam wa afya nchini wakimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto  (Idara Kuu ya afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya hayupo pichani wakati wa mkutano wa mwaka wa kujadili mafanikio na chanagamoto za sera ya afya uliofanyika leo jijini Dodoma.


NA WAMJW- DODOMA 

TANZANIA ni miongoni mwa nchi zinazofanya vizuri katika kutoa huduma za chanjo kwa magonjwa yanayohitaji huduma hiyo kwa asilimia 98 Afrika Mashariki. 

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wa ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa kujadili masuala mbalimbali ya afya uliofanyika jijini Dodoma. 

"Tanzania tumepiga hatua katika kutoa huduma za chanjo kwa asilimia 98 ambapo tumetanguliwa na wenzetu wa Rwanda kwa asilimia 99 ila tunaamini mpaka kufikia mwakani tutakua mbele zaidi" alisema Dkt. Ulisubisya. 

Aidha, Dkt. Ulisubisya amesema kuwa mpaka hivi sasa Tanzania inatoa chanjo  ya Surua na Rubella kwa asilimia 78 ambapo bado lengo halijatimia. 

Dkt. Ulisubisya amesema kuwa mpaka sasa Serikali kupitia Wizara ya Afya imefanikiwa kutibu wagonjwa wa Kifua Kikuu kwa asilimia 99 kwa wote waliogundulika wana vimelea vya ugonjwa huo. 

Dkt. Ulisubisya amesema kuwa pia katika mkutano huo wanajadili na kutoka na mikakati mbalimbali ya kuibua  maambukizi mapya ya  Virusi vya Ukimwi nchini ili kuweza kufikia lengo la 90 90 90 . 

Mbali na hayo Dkt. Ulisubisya amesema kuwa licha ya changamoto zilizopo katika jamii kutekeleza afua za kupambana na ugonjwa wa Malaria katika mkutano huo watahakikisha wanatoka na afua za kufikia malengo ya kutokomeza ugonjwa huo nchini. 

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI  Dkt.  Zainabu Chaula amesema kuwa mpaka hivi sasa Serikali imepata fedha ya kukarabati vituo 350 na kuweka vifaa na vifaa tiba kwa ajili ya matibabu ya kibingwa ya huduma za mama na mtoto. 

Naye Mwakilishi wa watoa huduma za Afya binafsi Dkt.  Josephine Balati amesema kuwa mpaka sasa zaidi ya vituo vya afya binafsi 190 vimeweza kuingia mkataba na Serikali katika kutoa huduma za afya nchini . 

"Katika vituo binafsi vya afya 190 vilivyoingia mkataba na Serikali vituo 84 ni vya mashirika ya dini na 106 ni vya watu binafsi" alisema Dkt. Balati . 

Mkutano huo wa kila mwaka  unaokutanisha wataalam na wadau mbalimbali wa afya una lengo la kupitia changamoto na mafanikio  sera ya afya inayotumika katika kuboresha afya za Watanzania. 


TAARIFA KWA UMMA - TAMKO LA WIZARA KUHUSU SIKU YA KISUKARI DUNIANI TAREHE 14 NOVEMBA, 2018.






Jumanne, 13 Novemba 2018

DKT. MPOKI AELEZA UCHOVU NI SABABU ZA AJALI ZA BARABARANI

- Hakuna maoni
Katibu Mkuu Dkt. Mpoki Ulisubisya akizindua kitabu cha mafunzo ya watoa huduma za tiba, uokoaji na usafirishaji wa majeruhi  Wa ajali na wagonjwa wenye dharura mbalimbali nje  ya hospitali nchini Tanzania.

Mkurugenzi wa idara ya dharura hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dkt.Juma Mfinanga akipokea  kitabu hicho  cha mafunzo  kutoka kwa Katibu Mkuu  Dkt.Mpoki  Mara baada ya kukizindua

Picha ya Pamoja ya watumishi toka wizara ya Afya, hospitali, Shirika la msalaba Mwekundu, Chuo kikuu MUHAS  Pamoja na majeshi ambao kwa Pamoja watatekeleza mpango huo  nchini.


KATIBU Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa moja ya sababu za ajali barabarani, ni uchovu wa madereva.

Dkt. Mpoki ameyasema leo Novemba 13,2018 wakati wa kufungua mafunzo ya watoa huduma za tiba, uokoaji na usafirishaji wa majeruhi wa ajali na wagonjwa wenye dharura mbalimbali nje ya Hospitali nchini.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo, Dkt. Mpoki amelitaka jeshi la Polisi nchini kuangalia namna ya kuweka utaratibu wa madereva kubadilishana kwani suala la uchovu linachangia kwa kiasi kikubwa ajali za barabarani.

Aidha,akitolea mfano suala la uchovu, dereva kutoka Mwanza au Bukoba kwenda Dar es Salaam, basi ashuke Singida ili aingie dereva mwingine kumalizia safari na hiyo itasaidia kuepusha ajali.

“Tumemuomba Mkuu wa Jeshi la Polisi atusaidie kama mchango wa Polisi katika kupunguza ajali kwa kuhakikisha kwamba wanaweka utaratibu wa madereva wanaendesha kwa muda maalum. Kuliko ilivyo sasa madereva wanaweza kuendesha siku nzima, Hivyo wanakuwa wachovu na kuchangia kwa kiasi kikubwa sana ajali mbalimbali barabarani” amesema Dkt. Mpoki.

Hata hivyo ameeleza kuwa, mpango huo ni hatua ya kwanza ambayo Serikali imewekeza kuingilia kati pale watu wanapokuwa wameumia, ambapo huko nyuma maisha ya watu wengi yalikuwa yakipotea kwa sababu vifaa vilikuwa vinachelewa sana kufika mahali tukio na hivyo kushirikiana na Benki ya dunia kwa kutenga kiasi cha shilingi Bilioni 8 kwa ajili ya uwekezaji na shilingi bilioni 2.5 kwa ajili ya kuendesha shughuli za kila siku za wataalam.

“Katika fani ya tiba, Tunazungumzia saa ya kwanza ni saa muhimu sana kusaidia mtu aliyepata changamoto ya ajali. Hawa watakuwa chachu ya kusaidia kati ya wale waliopata mafunzo.” Amesema Dkt. Mpoki

Dkt. Mpoki ameongeza kuwa katika afua hiyo,itakuwa na vituo maalum   vyenye miundombinu ya kutoa huduma hizo ambapo awamu ya kwanza itaanzia Dar e Salaam hadi Ruaha Mbuyuni na kwa kila kituo kutakuwa na gari la kubebea wagonjwa, vifaa vya zima moto na kuweka utaratibu wa kusafirisha majeruhi kwa kushirikiana  majeshi yakiwemo la Jeshi la Wananchi (JWTZ), Polisi, Zimamoto pamoja na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROAD).

Kwa upande wake Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma (MUHAS), Profesa Appolenary Kamuhabwa  amesema mafunzo hayo ni muhimu sana kwani  kutakuwa na mfumo thabiti wa kuwahudumia wagonjwa wa dharura watokanao na ajali na  ni hatua muhimu  kwani bila afya bora, wananchi hawawezi kutumikia nchi hususani  ajenda ya Serikali ya  viwanda.

Profesa Kamuhabwa amesema katika mpanguo huo, utakuwa na vituo mbalimbali vya Afya vitakavyokuwa vikitoa huduma za dharura ikiwemo: Vituo vya Afya vya Kimara (Dar es Salaam), Tumbi,  Chalinze (Pwani), Mikese, St, Kizito, Doma-Mikumi (Morogoro) na Ruaha Mbuyuni (Iringa).

Jumanne, 6 Novemba 2018

- Hakuna maoni
Makamu wa Rais Mama  Samia Suluhu  Hassan wakibadilishana mawazo  na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee  na Watoto  Mhe.Ummy Mwalimu tayari kwa UzinduZi wa Kampeni ya Tuwajushe  Salama kwenye  ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma leo

Makamu wa Rais akipitia  Ratiba  ya uzinduzi  wa Kampeni hiyo na MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge.Kampeni hiyo ina  lengo la kuhamasisha viongozi wa Serikali,Dini,Mashirika  yasiyo  ya kiserikali,wadau wa  Maendeleo na datos huduma za afya kuchangia katika juhudi za  kitaifa za kupunguza  vifo vitokanavyo  na uzazi  na watoto  wachanga


Baadhi ya Wakuu wa Mikoa wakifurahia Mambo wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimuelezea Makamu wa Rais vinavyoonesha ubora na mapungufu ya utoaji wa huduma za afya ya uzazi kwa mama na mtoto wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Jiongeze, Tuwavushe Salama.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizindua rasmi kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama yenye lengo la kuhamasisha viongozi wa Serikali, Dini, Mashirika yasiyo ya kiserikali, Wadau wa Maendeleo, Watoa huduma za afya, Familia na jamii kwa ujumla ili kuchangia katika juhudi za taifa za kupunguza vifo vinyotokana na uzazi na vifo vya watoto wachanga.

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ahadi ya makubaliano ya uwajibikaji katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wachanga.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe wa kitabu cha muongozo wa pili wa kuzuia maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati uzinduzi huo.



MAMA SAMIA  AWASAINISHA WAKUU WA MIKOA AHADI YA MAKUBALIANO YA UWAJIBIKAJI WAKUPUNGUZA  VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI. 

NA WAMJ-DODOMA

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasainisha Wakuu wa mikoa yote nchini AHADI ya makubaliano ya uwajibikaji katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo cha Watoto wachanga nchini. 

Hayo yamefanyika leo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kitaifa inayolenga kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi nchini inayojulikana kwa jina la "JIONGEZE TUWAVUSHW SALAMA "  jijini Dodoma. 

"Leo nawasainisha makubaliano haya wakuu wa mikoa mkaifanyie kazi na kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga ntahitaji taarifa ya viashiria vya afya ya uzazi kila baada ya miezi 6 katika ofisi yangu", alisema Mhe. Samia. 

Aidha,Mhe. Samia amesema kuwa mbali na wakuu wa mikoa kuwasilisha taarifa hizo  kwake pia  kila baada ya miezi 3 wawasilishe Wizara ya Afya ili kuzifanyia kazi taarifa hizo na kutatua changamoto za vifo vitokanavyo na uzazi. 

Kwa mujibu wa Mhe. Samia amesema kuwa mbali na vikwazo vingine vinavyosababisha vifo vitokanavyo na uzazi tunatakiwa kuzingatia lishe bora wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua. 

Mbali na hayo Mhe. Samia Suluhu amesema kuwa mapambano haya zidi ya vifo vitokanavyo na uzazi ni la kila mtu kuanzia, Viongozi wa Serikali,  Jamii nzima inaotuzunguka, watumishi wa sekta ya afya, wanahabari pamoja na viongozi wa dini. 

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa takwimu ya mwaka  2017 za Wizara ya Afya zinaonesha kuwa wanawake milioni 2. 2 kila mwaka wanapata ujauzito na asilimia 85 hujifungua bila ya shida na asilimia 15 sawa na laki 3. 3 hupata matatizo mbalimbali yatokanayo na uzazi. 

"Kuna sababu mbalimbali zinazochangia vifo vitokanavyo na uzazi ikiwa kutokwa na damu nyingi kabla na baada ya kujifungua, asilimia 28, kifafa cha mimba asilimia 17, uchungu pingamizi asilimia 11, uambukizo asilimia 11 na mengineyo asilimia 11" alisema Waziri Ummy. 

Aidha,Waziri Ummy amesema kuwa wajawazito wanatakiwa kuhudhuria kliniki kwani ni asilimia 60 ndio wanaohudhuria kliniki angalau mara nne . 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binirith Mahenge amesema kuwa mkoa wake umepiga hatua katika ujenzi wa vituo vya afya mpaka kufikia 21 ndani ya miaka 3. 

"Licha ya ujenzi huo pia Serikali imeongeza bajeti ya dawa kwa upande wa mkoa wa Dodoma kutoka milioni 900 mpaka kufikia bilioni 4 kwa mwaka wa fedha 2018" alisema Dkt. Mahenge.