Ijumaa, 23 Novemba 2018
DKT. NDUGULILE – “SEKTA YA AFYA NCHINI INAKUWA KWA KASI”
Ijumaa, Novemba 23, 2018
-
Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na
Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akisoma nyaraka za matibabu za
Bi. Mary Nyange (kulia) anayepatiwa huduma za matibabu katika Hospitali ya
Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akihojiana na Bw. Longini Mtalo, Mteknolojia kutoka kituo cha utengenezaji wa viungo bandia katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC huku akiwa ameshika sampuli ya kiungo bandia kilichotengenezwa na kituo hicho.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na
Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akikagua benki ya damu zilizopo katika
jokofu Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini ya KCMC
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na
Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akionyesha mafuta maalum kwa
ajili ya kuwakinga wenye ulemavu wa ngozi dhidi ya miale ya jua
yanayotengenezwa na kitengo cha Kilimanjaro Sunscreen Production kilichopo Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini ya KCMC.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akihojiana na Bw. Prosper Kaaya, Mteknolojia kutoka kituo cha utengenezaji wa viungo bandia katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC huku akiwa ameshika kiungo bandia kilichotengenezwa na kituo hicho.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na
Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (aliyesimama) akisema jambo wakati wa kikao
na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC (hawapo pichani) aliye upande kulia ni Mganga Mkuu Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Best Magoma upande wa kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskasini KCMC Dkt. Gileard Masenga.
Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC
wakisiliza jambo wakati wa kikao kazi na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani)
aliyetembelea hospitali hiyo Novemba 22, 2018.
NA WAMJW- KILIMANJARO
“Sekta ya afya inakua kwa kasi huku huduma muhimu za afya kwa sasa zikiwa zinapatikana hapa hapa nchini”
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile alipokua akizungumza na watumishi wa Hospitali ya rufaa ya Kanda ya Kaskazini (KCMC) iliyopo katika Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro jana Novemba 22, 2018.
Dkt. Ndugulile amesema kuwa Sekta ya Afya imepewa kipaumbele cha hali ya juu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli katika kipindi cha miaka mitatu mageuzi makubwa ndani ya sekta ya afya yameanza kuonekana huku huduma za matibabu ya kibingwa yakiwa zikipatikana hapa hapa nchini.
“Tunasimama hapa kifua mbele tukiona mabadiliko katika hali ya upatikanaji wa dawa kuimarika zaidi, bajeti ya dawa imeongezeka toka Shilingi Bilioni 30 mpaka Shilingi Bilioni 270 yaani mara tisa zaidi ndani ya miaka mitatu” alisema Mhe.Naibu Waziri na kuendelea “Tumeboresha vituo vya afya takribani 300, huku Mkoa wa Kilimanjaro ukiwa na Vituo 8 vilivyoboreshwa vilivyogharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 3.5 na kwa mwaka huu 2018 Serikali imeanza kujenga Hospitali za Wilaya 67 nchini”
Aidha, Dkt. Ndugulile alisema kuwa Serikali imetenga Shilingi Bilioni 30 kwa ajili ya Hospitali mpya za Rufaa za Mikoa ili ziweze kutoa huduma za kibingwa, kupunguza msongamano wa wagonjwa na ucheleweshwaji wa huduma katika Hospitali za rufaa za kanda.
Naibu Waziri huyo Aliendelea kusema kuwa fedha hizo Shilingi Bilioni 30 zitaelekezwa katika maeneo makuu matano ambayo aliyataja kuwa ni kuhakikisha kila Hospitali ya Mkoa ina Kitengo cha dharura, chumba cha upasuaji, kitengo cha uangalizi wa wagonjwa mahututi pamoja na kitengo cha mama na mtoto.
"Hospitali hii inatakiwa kuhudumia wagonjwa waliopata rufaa toka hospitali za mikoa ya jirani waje huku kupatiwa huduma za matibabu na sio wagonjwa wa malaria na mafua alisema Dkt. Ndugulile.
Katika kuhakikisha huduma bora za afya zinatolewa kwenye hospitali za rufaa za mikoa, Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali imeweka maeneo muhimu katika mafunzo kwa watumishi wa kada ya afya huku akitaja watumishi wenye kuhitajika zaidi kwa sasa kuwa ni madaktari wa magonjwa ya ndani, watoto, wakina mama, upasuaji, mifupa pamoja na madaktari wa usingizi.
Kuhusu upatikanaji wa huduma za kibingwa, Dkt.Ndugulile alisema mafanikio kuona huduma hizo zikiwa zinapatikana hapa nchini tofauti na zamani “Tunafanya upandikizaji wa figo pamoja na upandikizaji wa vifaa vya usikivu kwa wa watoto huduma ambazo zilikuwa ni za kufikirika ndani ya miaka mitatu sasa zinapatikana hapa nchini” alisema Dkt. Ndugulile.
Awali akitoa taarifa yake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC Dkt. Gileard Masenga aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Hospitali hiyo "Licha ya kumilikiwa na Taasisi ya kidini lakini Serikali imeendelea kutupatia wataalam, misamaha ya kodi za malighali zinazoingizwa nchini ambazo hutumika kutengeneza mafuta ya kuwakinga wenye ulemavu wa ngozi dhidi ya jua.
Aidha, Dkt.Masenga alisema hospitali yake imetengewa Shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya dawa za Saratani huku fedha kiasi cha Shilingi Milioni 250 tayari zimeshapelekwa Bohari ya dawa kwa ajili ya ununuzi wa dawa hizo.
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto yupo Mkoani hapa kwa ziara ya kikazi inayolenga kukagua shughuli za huduma ya Afya,Maendeleo ya Jamii pamoja na kuongea na watumishi wa sekta hizo.
MWISHO.
Jumatano, 21 Novemba 2018

DKT. MPOKI AKEMEA TABIA YA ABIRIA NA MADEREVA KUCHIMBA DAWA MAENEO YASIYOHUSIKA
Jumatano, Novemba 21, 2018
-
Hakuna maoni
![]() |
| Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya akitoa neno mbele ya Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri pamoja na Wadau wa Mazingira leo katika Ukumbi wa CCM jijini Dodoma. |
![]() |
![]() |
| Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya akikagua maonesho ya vyoo baada ya kufungua kikao cha Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri pamoja na Wadau wa Mazingira leo jijini Dodoma. |
Alhamisi, 15 Novemba 2018
SERIKALI YAJIPANGA KUTOKOMEZA MAAMBUKIZI YA VVU KWA WATOTO WACHANGA.
Alhamisi, Novemba 15, 2018
-
Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee
na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema serikali ina mpango madhubuti wa
kuhakikisha wamama wajawazito hawawaambukizi watoto walio tumboni Virusi vya
Ukimwi na kipindi wanapozaliwa.
Waziri Ummy amesema hayo leo wakati wa uzinduzi wa
machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya maendeleo ya jamii ikiwa ni
pamoja na masuala ya lishe, uliofanyika katika ukumbi wa Hazini, Jijini Dodoma.
Waziri Ummy amesema hadi hivi sasa asilimia 99 ya
wajawazito wenye maambukizi ya VVU wanapewa huduma za kumkinga mtoto asipate
maambukizi hayo huku la serikali ifikapo mwaka 2020 ni kuhakikisha hakuna mtoto atakayezaliwa na maambukizi ya VVU.
“Sasa hivi asilimia 99 ya wanawake wajawazito wote
wenye maambukizi ya VVU tumewaingiza
katika mpango wa dawa, na hiyo asilimia moja bado hatujawafikia ila kwa nguvu
na msukumo tuliouweka juzi wa kuwasainisha Wakuu wa Mikoa kwenda kufuatilia
masuala ya afya ya mama na mtoto, tunaamini hakuna mtoto yeyote Tanzania
atakayezaliwa na maambukizi ya UKIMWI”. Amesema Waziri Ummy.
Katika Uzinduzi huo, Waziri Ummy ameipongeza
Wizara ya Fedha na Mipango kupitia kwa Waziri wake Mhe. Dkt. Philipo
Mpango inavyojikita katika mipango ya
kuendeleza wanawake na watoto kwa kutoa huduma bora za afya, elimu, maji na
masuala ya maendeleo ya jamii kwa ujumla.
Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na
Shirika la Watoto Duniani (UNICEF) imefanya uchambuzi wa bajeti katika sekta
mtambuka ya jamii, hususani katika elimu, afya, Virusi vya Ukimwi, maji, usafi
wa mazingira na lishe kwa lengo la kuboresha upangaji na utekelezwaji wa
masuala ya mama na mtoto.
Pamoja na hayo, uzinduzi wa machapisho hayo
umelenga kupunguza tatizo la lishe linalosababisha udumavu kwa watoto walio
katika umri mdogo. Ambapo katika ripoti iliyotolewa katika mkutano wa IMF na
Benki ya dunia uliofanyika nchini Indonesia mwezi Oktoba mwaka 2018, inaonesha
Tanzania inashika nafasi ya 128 kati ya nchi 157 duniani katika kipimo cha
ubora wa nguvukazi katika uwekezaji wa
rasilimali watu hususani katika sekta ya afya na elimu ya lishe.
Kufuatia hali hiyo, Tanzania inaonekana kuwa na
matatizo ya udumavu, elimu ya lishe na afya kwa watoto wenye umri mdogo ambapo
serikali inafanya kazi kubwa ya kuhakikisha elimu ya lishe inawafikia wazazi na
jamii kwa ujumla ili kupambana na tatizo la udumavu. Na kufikia mwaka 2015
tatizo la udumavu limeshuka kutoka asilimia 34 kutoka asilimia 42 mwaka 2010.
Alisema Waziri huyo.
Tatizo la lishe limeonekana kupungua nchini huku
viashiria vya tatizo hilo vikipungua ambavyo ni uzito pungufu umeshuka kutoka
asilimia 16 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 14 mwaka 2015/16, pamoja na
ukondefu wa mwili kuendelea kubakia chini ya asilimia 5 kwa mwaka 2015/16.
Jumatano, 14 Novemba 2018
TANZANIA INATOA HUDUMA ZA CHANJO KWA ASILIMIA 98.
Jumatano, Novemba 14, 2018
-
Hakuna maoni
NA WAMJW- DODOMA
TANZANIA ni miongoni mwa nchi zinazofanya vizuri katika kutoa huduma za chanjo kwa magonjwa yanayohitaji huduma hiyo kwa asilimia 98 Afrika Mashariki.
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wa ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa kujadili masuala mbalimbali ya afya uliofanyika jijini Dodoma.
"Tanzania tumepiga hatua katika kutoa huduma za chanjo kwa asilimia 98 ambapo tumetanguliwa na wenzetu wa Rwanda kwa asilimia 99 ila tunaamini mpaka kufikia mwakani tutakua mbele zaidi" alisema Dkt. Ulisubisya.
Aidha, Dkt. Ulisubisya amesema kuwa mpaka hivi sasa Tanzania inatoa chanjo ya Surua na Rubella kwa asilimia 78 ambapo bado lengo halijatimia.
Dkt. Ulisubisya amesema kuwa mpaka sasa Serikali kupitia Wizara ya Afya imefanikiwa kutibu wagonjwa wa Kifua Kikuu kwa asilimia 99 kwa wote waliogundulika wana vimelea vya ugonjwa huo.
Dkt. Ulisubisya amesema kuwa pia katika mkutano huo wanajadili na kutoka na mikakati mbalimbali ya kuibua maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi nchini ili kuweza kufikia lengo la 90 90 90 .
Mbali na hayo Dkt. Ulisubisya amesema kuwa licha ya changamoto zilizopo katika jamii kutekeleza afua za kupambana na ugonjwa wa Malaria katika mkutano huo watahakikisha wanatoka na afua za kufikia malengo ya kutokomeza ugonjwa huo nchini.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI Dkt. Zainabu Chaula amesema kuwa mpaka hivi sasa Serikali imepata fedha ya kukarabati vituo 350 na kuweka vifaa na vifaa tiba kwa ajili ya matibabu ya kibingwa ya huduma za mama na mtoto.
Naye Mwakilishi wa watoa huduma za Afya binafsi Dkt. Josephine Balati amesema kuwa mpaka sasa zaidi ya vituo vya afya binafsi 190 vimeweza kuingia mkataba na Serikali katika kutoa huduma za afya nchini .
"Katika vituo binafsi vya afya 190 vilivyoingia mkataba na Serikali vituo 84 ni vya mashirika ya dini na 106 ni vya watu binafsi" alisema Dkt. Balati .
Mkutano huo wa kila mwaka unaokutanisha wataalam na wadau mbalimbali wa afya una lengo la kupitia changamoto na mafanikio sera ya afya inayotumika katika kuboresha afya za Watanzania.
Jumanne, 13 Novemba 2018

DKT. MPOKI AELEZA UCHOVU NI SABABU ZA AJALI ZA BARABARANI
Jumanne, Novemba 13, 2018
-
Hakuna maoni
![]() |
| Mkurugenzi wa idara ya dharura hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dkt.Juma Mfinanga akipokea kitabu hicho cha mafunzo kutoka kwa Katibu Mkuu Dkt.Mpoki Mara baada ya kukizindua |
![]() |
| Picha ya Pamoja ya watumishi toka wizara ya Afya, hospitali, Shirika la msalaba Mwekundu, Chuo kikuu MUHAS Pamoja na majeshi ambao kwa Pamoja watatekeleza mpango huo nchini. |
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa moja ya sababu za ajali barabarani, ni uchovu wa madereva.
Dkt. Mpoki ameyasema leo Novemba 13,2018 wakati wa kufungua mafunzo ya watoa huduma za tiba, uokoaji na usafirishaji wa majeruhi wa ajali na wagonjwa wenye dharura mbalimbali nje ya Hospitali nchini.
Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo, Dkt. Mpoki amelitaka jeshi la Polisi nchini kuangalia namna ya kuweka utaratibu wa madereva kubadilishana kwani suala la uchovu linachangia kwa kiasi kikubwa ajali za barabarani.
Aidha,akitolea mfano suala la uchovu, dereva kutoka Mwanza au Bukoba kwenda Dar es Salaam, basi ashuke Singida ili aingie dereva mwingine kumalizia safari na hiyo itasaidia kuepusha ajali.
“Tumemuomba Mkuu wa Jeshi la Polisi atusaidie kama mchango wa Polisi katika kupunguza ajali kwa kuhakikisha kwamba wanaweka utaratibu wa madereva wanaendesha kwa muda maalum. Kuliko ilivyo sasa madereva wanaweza kuendesha siku nzima, Hivyo wanakuwa wachovu na kuchangia kwa kiasi kikubwa sana ajali mbalimbali barabarani” amesema Dkt. Mpoki.
Hata hivyo ameeleza kuwa, mpango huo ni hatua ya kwanza ambayo Serikali imewekeza kuingilia kati pale watu wanapokuwa wameumia, ambapo huko nyuma maisha ya watu wengi yalikuwa yakipotea kwa sababu vifaa vilikuwa vinachelewa sana kufika mahali tukio na hivyo kushirikiana na Benki ya dunia kwa kutenga kiasi cha shilingi Bilioni 8 kwa ajili ya uwekezaji na shilingi bilioni 2.5 kwa ajili ya kuendesha shughuli za kila siku za wataalam.
“Katika fani ya tiba, Tunazungumzia saa ya kwanza ni saa muhimu sana kusaidia mtu aliyepata changamoto ya ajali. Hawa watakuwa chachu ya kusaidia kati ya wale waliopata mafunzo.” Amesema Dkt. Mpoki
Dkt. Mpoki ameongeza kuwa katika afua hiyo,itakuwa na vituo maalum vyenye miundombinu ya kutoa huduma hizo ambapo awamu ya kwanza itaanzia Dar e Salaam hadi Ruaha Mbuyuni na kwa kila kituo kutakuwa na gari la kubebea wagonjwa, vifaa vya zima moto na kuweka utaratibu wa kusafirisha majeruhi kwa kushirikiana majeshi yakiwemo la Jeshi la Wananchi (JWTZ), Polisi, Zimamoto pamoja na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROAD).
Kwa upande wake Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma (MUHAS), Profesa Appolenary Kamuhabwa amesema mafunzo hayo ni muhimu sana kwani kutakuwa na mfumo thabiti wa kuwahudumia wagonjwa wa dharura watokanao na ajali na ni hatua muhimu kwani bila afya bora, wananchi hawawezi kutumikia nchi hususani ajenda ya Serikali ya viwanda.
Profesa Kamuhabwa amesema katika mpanguo huo, utakuwa na vituo mbalimbali vya Afya vitakavyokuwa vikitoa huduma za dharura ikiwemo: Vituo vya Afya vya Kimara (Dar es Salaam), Tumbi, Chalinze (Pwani), Mikese, St, Kizito, Doma-Mikumi (Morogoro) na Ruaha Mbuyuni (Iringa).
Jumanne, 6 Novemba 2018

Jumanne, Novemba 06, 2018
-
Hakuna maoni
![]() |
| Baadhi ya Wakuu wa Mikoa wakifurahia Mambo wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo |
![]() |
| Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ahadi ya makubaliano ya uwajibikaji katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wachanga. |
MAMA SAMIA AWASAINISHA WAKUU WA MIKOA AHADI YA MAKUBALIANO YA UWAJIBIKAJI WAKUPUNGUZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI.
NA WAMJ-DODOMA
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasainisha Wakuu wa mikoa yote nchini AHADI ya makubaliano ya uwajibikaji katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo cha Watoto wachanga nchini.
Hayo yamefanyika leo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kitaifa inayolenga kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi nchini inayojulikana kwa jina la "JIONGEZE TUWAVUSHW SALAMA " jijini Dodoma.
"Leo nawasainisha makubaliano haya wakuu wa mikoa mkaifanyie kazi na kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga ntahitaji taarifa ya viashiria vya afya ya uzazi kila baada ya miezi 6 katika ofisi yangu", alisema Mhe. Samia.
Aidha,Mhe. Samia amesema kuwa mbali na wakuu wa mikoa kuwasilisha taarifa hizo kwake pia kila baada ya miezi 3 wawasilishe Wizara ya Afya ili kuzifanyia kazi taarifa hizo na kutatua changamoto za vifo vitokanavyo na uzazi.
Kwa mujibu wa Mhe. Samia amesema kuwa mbali na vikwazo vingine vinavyosababisha vifo vitokanavyo na uzazi tunatakiwa kuzingatia lishe bora wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua.
Mbali na hayo Mhe. Samia Suluhu amesema kuwa mapambano haya zidi ya vifo vitokanavyo na uzazi ni la kila mtu kuanzia, Viongozi wa Serikali, Jamii nzima inaotuzunguka, watumishi wa sekta ya afya, wanahabari pamoja na viongozi wa dini.
Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa takwimu ya mwaka 2017 za Wizara ya Afya zinaonesha kuwa wanawake milioni 2. 2 kila mwaka wanapata ujauzito na asilimia 85 hujifungua bila ya shida na asilimia 15 sawa na laki 3. 3 hupata matatizo mbalimbali yatokanayo na uzazi.
"Kuna sababu mbalimbali zinazochangia vifo vitokanavyo na uzazi ikiwa kutokwa na damu nyingi kabla na baada ya kujifungua, asilimia 28, kifafa cha mimba asilimia 17, uchungu pingamizi asilimia 11, uambukizo asilimia 11 na mengineyo asilimia 11" alisema Waziri Ummy.
Aidha,Waziri Ummy amesema kuwa wajawazito wanatakiwa kuhudhuria kliniki kwani ni asilimia 60 ndio wanaohudhuria kliniki angalau mara nne .
Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binirith Mahenge amesema kuwa mkoa wake umepiga hatua katika ujenzi wa vituo vya afya mpaka kufikia 21 ndani ya miaka 3.
"Licha ya ujenzi huo pia Serikali imeongeza bajeti ya dawa kwa upande wa mkoa wa Dodoma kutoka milioni 900 mpaka kufikia bilioni 4 kwa mwaka wa fedha 2018" alisema Dkt. Mahenge.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)















