Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 26 Novemba 2018

HOSPITALI YA KIBONG’OTO KUWA KITUO CHA TAFITI, TIBA NA MAFUNZO YA MAGONJWA AMBUKIZI


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akipata maelekezo namna wanavyopima wagonjwa wa kifua kikuu toka kwa Mganga Mfawidhi Hospitali Maalum ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto Dkt. Riziki Kisonga (kulia)

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (katikati) akikagua maabara katika Hospitali Maalum ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (wa kwanza kushoto) akikagua vyumba vya wagonjwa katika Hospitali Maalum ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua stoo ya dawa zilizopo katika Hospitali Maalum ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua ramani ya jengo la maabara litakalojengwa katika Hospitali Maalum ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo  kwa watumishi (hawapo pichani) wa Hospitali Maalum ya magonjwa ambukizi ya Kibong’oto.

Watumishi toka Hospitali Maalum ya Kibong’oto wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani)

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akitoa cheti kwa Dkt. Stellah Mpagama (kulia) mara baada ya kuzindua mpango wa Remodel. 

Na WAMJW - SIHA, KILIMANJARO

Serikali kuifanya Hospitali ya Kibong’oto kuwa kitovu cha utafiti, tiba na mafuzo ya magonja yakuambukiza na magonjwa yanayopatikana maeneo ya kazini.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipotembelea Hospitali hiyo ya magonjwa yakuambukiza iliyopo Wilaya ya Siha Mkoani Kilimanjaro jana Novemba 25, 2018.

“Nataka kuona hospitali hii inakuwa kitovu cha mafunzo katika ugonjwa huu wa kifua kikuu, magonjwa yanayopatikana maeneo ya kazi pamoja na magonjwa mengine yakuambukiza” alisema Dkt. Ndugulile

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa “Wapo watu wanaougua maeneo ya kazini na hufika hospitalini wakiwa katika hatua za mwisho kabisa za ugonjwa, hivyo kundi hilo nalo inabidi tulifikie kwa wakati”

Pia, Dkt. Ndugulime amesema kuwa takribani watu 150,000 huugua ugonjwa wa kifua kikuu kwa mwaka, huku idadi ya wagonjwa wanaopatiwa matibabu ikiwa ni 63,000 sawa na asilimia 42 huku tafiti zikionyesha kuwa mgonjwa mmoja wa kifua kikuu ndani ya mwaka mmoja anaweza kuwaambukiza watu 20 ugonjwa huo, hivyo kuwataka watendaji kuja na mkakati wa kutoka ofisini kwenda kuwatafuta wagonjwa wa Kifua Kikuu katika maeneo ya makazi.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile Dkt. Ndugulile, amezindua Mpango wa Remodel unaolenga kuongeza uwezo katika tafiti za tiba ili kuweza kudhibiti magonjwa yakuambukiza, kutoa mafunzo ya sayansi  kwa ngazi ya shahada ya uzamili na uzamiri pamoja na kuandaa miongozo ya namna ya kudhibiti magonjwa yakuambukiza  yaliyopo na ambayo hayategewi kutufikia.

Mpango huo unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya unawaunganisha madaktari wazalendo kutoka hapa nchini ukiongozwa na Dkt. Stellah Mpagama pamoja na madaktari wenza kutoka katika hospitali ya KCMC.

Dkt. Mpagama anasema kuwa wamekuja na mpango huo baada ya kubaini mataifa yaliyopo kusini wa jangwa la sahara yanakabiliwa na idadi kubwa ya magonjwa yakuambukiza  huku miongoni mwa magonjwa hayo kuwa ni Ebola, Homa ya manjano, Homa ya Bonde la Ufa pamoja na ugonjwa wa Kipindupindu.

Dkt. Mpagama amesema kuwa jamii nyingi za nchi za afrika zipo katika mazingira magumu ambayo hupelekea magonjwa yakuambukiza  kusambaa kimzunguko huku idadi ya madaktari waliopo ni ndogo.

“Takwimu toka shirika la afya duniani zinaonyesha katika nchi za afrika kuna daktari mmoja kwa wagonjwa 100,000. Kupitia mpango huu, tunaamini magonjwa haya yakuambukiza tunaenda kuyadhibiti” alisema Dkt Mpagama.

Hospitali Maalum ya magonjwa yakuambukiza  Kibong’oto ilianzishwa mwaka 1925 na Dkt. Noman Davis (raia wa Uingereza) ikiwa ni kituo cha kutibu watu waliokuwa wanaugua ugonjwa wa Kifua Kikuu na mnamo mwaka 2006 Wizara ya Afya iliipa jukumu Hospitali hiyo kutibu ugonjwa sugu wa Kifua Kikuu hadi sasa hospitali hiyo inatoa huduma ya tiba na uchunguzi kwa wagonjwa wa nje na ndani wa Kifua Kikuu huku wastani wagonjwa 120 wa nje na 110 wa ndani hupatiwa huduma za matibabu kila siku.

Mwisho.

Ijumaa, 23 Novemba 2018

MATUKIO KATIKA PICHA, ZIARA YA DKT. NDUGULILE MKOANI KILIMANJARO.

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile jana Novemba 22, 2018 ameanza ziara yake ya kikazi kwa Mkoa wa Kilimanjaro.

Akiwa mkoani kilimanjaro jana alifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na kupokelewa na mwenyeji wake Bi.Anna Mghwira  Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ambapo alipata taarifa ya Mkoa huku sekta ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na kisha kuendelea na ziara yake katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi pamoja na Hospitali ya Rufaa na Kanda ya Kaskazini ya KCMC. yafuatayo ni matukio katika picha kama yalivyojiri.




Dkt, Ndugulile (kushoto) akisalimiana na mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bi. Anna Mghwira (kulia)
Dkt, Ndugulile (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Kippi Warioba kati kati ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bi. Anna  Mghwira


Dkt. Ngugulile (aliyesimama) akizungumza na waganga wakuu wa wilaya pamoja na wakurugenzi katika zoezi la ugawaji vyeti vya ubora kwa kwa Hospitali na Vituo vya afya vilivyopo Mkoani Kilimanjaro.



Dkt. Ndugulile (Kushoto) akitoa cheti cha ubora kwa Hospitali ya Mt. Joseph iliyotunukiwa hadhi ya nyota nne.



Dkt. Ndugulile (Kushoto) akitoa cheti cha ubora kwa Kituo cha afya cha Moshes kilichotunukiwa hadhi ya nyota nne.

Dkt. Ndugulile (Kushoto) akitoa zawadi ya ngao kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha Bw. Valerian Juwal kwa kuongoza Mkoani Kilimanjaro kuwa na Vituo bora vya afya.

Dkt. Ndugulile (kushoto) akiwa ameshika vipeperushi vya elimu ya afya kwa umma vilivyokuwa vimewekwa sehemu isiyo rasmi na kuuagiza uongozi wa Hospitali ya Mawenzi kuhakikisha ndani ya wiki moja vipeperushi hivyo vitolewe kwa wananchi kwa lengo la kuelimishwa, aliye kulia ni Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro- Mawenzi dkt. Japhet Boniphace.

Dkt. Ndugulile akikagua jokofu linalotunza dawa za Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro, Mawenzi.

Dkt. Ndugulile(kushoto) akikagua nyaraka za kitengo cha maabara ambapo amewaagiza watumishi wote hospitalini hapo kuandika rekodi muhimu zote za wagonjwa wakiwa hospitalini.

Ukaguzi ukiendelea....

Dkt Ndugulile (aliyesimama kulia) akizungumza na wananchi waliofika katika Hospitali ya Mawenzi kupata huduma za matibabu.

Dkt. Ndugulile akifurahi mara baada ya kukutana na Mzee franley Mnzava mwenye umri wa Miaka 98 aliyefika Hospitali ya Mawenzi kupata matibabu. Licha ya umri mkubwa alionao Mzee Mnzava bado yu mwenye nguvu na mcheshi muda wote ambapo amewasihi vijana kutunza miili yao ili kuishi miaka mingi.

Dkt, Ndugulile akikagua ramani ya jengo la kituo cmaalum cha uangalizi wa magonjwa ya mlipuko kinachojengwa pembeni ya Hospitali ya mawenzi kinachotarajiwa kukamilika mwezi Machi 2019.

Dkt. Ndugulile akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro.

Dkt. Ndugulile akipokelewa na mwenyeji wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini Dkt. Gileard Masenga.

Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akihojiana na Bw. Longini Mtalo, Mteknolojia kutoka kituo cha utengenezaji wa viungo bandia katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC  huku akiwa ameshika sampuli ya kiungo bandia kilichotengenezwa na kituo hicho.
wanafunzi wakiwa katika mafunzo ya vitendo kwenye Kituo cha utengenezaji wa viungo bandia katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini.


Mafuta Maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa ngozi yanayotengenezwa na Kituo cha Kilimanjaro Sunscreen Production Unit ndani ya Hospitali ya KCMC, mafuta haya huwaliwa walemavu wa ngozi dhidi ya jua kali linalodhuru ngozi ya miili yao.

Dkt. Ndugulile akizungumza jambo huku akiwa amebeba mafuta maalum kwa ajili ya wenye ulemavu wa ngozi yanayotumika kuwakinga dhidi ya jua kali.



WAZIRI MKUU AWAAGIZA MAAFISA TAWALA KUSIMAMIA UJENZI WA VYOO BORA

- Hakuna maoni
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. kassim Majaliwa akifuatilia maelekezo katika banda la Hedhi salama  wakati wa mkutano wa Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri na Wadau wa Usafi nchini uliofanyika leo jijini Dodoma.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. kassim Majaliwa (wakwanza kulia) akiwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wakatikati) pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii Mhe. Peter Selukamba wakifuatilia kikundi cha ngoma cha Mpoto (hawapo kwenye picha) wakati wa mkutano wa Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri na Wadau wa Usafi nchini uliofanyika leo jijini Dodoma.



Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. kassim Majaliwa akimkabidhi Afisa Afya wa Mkoa wa Iringa zawadi ya Bodaboda wakati wa mkutano wa Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri na Wadau wa Usafi nchini uliofanyika leo jijini Dodoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. kassim Majaliwa akisikiliza maelezo kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu namna ya matumizi ya choo pindi walipopita katika mabanda ya maonesho, wakati wa mkutano wa Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri na Wadau wa Usafi nchini uliofanyika leo jijini Dodoma.


Makatibu Tawala wa Mikoa, Wilaya pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri nchini wametakiwa  kusimamia vizuri kampeni ya ujenzi wa vyoo bora kwa kutimiza lengo la kila familia na jamii inakuwa na vyoo vya kisasa hadi kufikia Disemba 31 mwaka huu.

Hayo yamesemwa leo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakati akifunga mkutano wa maofisa afya wa Mikoa, Halmashauri na Wadau wa usafi Tanzania uliyofanyika jijini hapa.

Mhe. Majaliwa amesema kwamba ujenzi wa vyoo vya kisasa katika kila kaya utasaidia kupunguza uwezekano wa magonjwa ya milipuko ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutokuwa na vyoo bora.

“Nawataka mtumie mbinu yeyote ili kuwawezesha hawa Maofisa Afya katika kutoa elimu  kwa wananchi ili suala la ujenzi wa vyoo bora liweze kutekelezeka na hata kutimiza wajibu wao wa kila siku”. Alisema Waziri Mkuu.

Hata hivyo Waziri Mkuu aliwataka wananchi  kutunza mazingira kwa kufuata kanuni bora za afya ikiwa ni pamoja na matumizi ya vyoo bora na vya kisasa ambapo alisema kutumia kampeni hiyo imewezesha kupunguza idadi ya kaya zisizokuwa na vyoo kutoka asilimia 9.5 mwaka 2015 hadi asilimia 3.8 mwaka 2018.

“Serikali ya awamu ya tano inaendelea kusisitiza juu ya uhifadhi wa mazingira na nyinyi wataalamu wa afya mnaombwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa kuelimisha umma juu ya utunzaji wa mazingira ili kutekeleza dhana ya Tanzania ya viwanda kwa kutunza vyanzo vya maji na kutumia vyoo bora”. Alisema Waziri Mkuu Majaliwa.

Aidha, amewataka maafisa afya nchini kote kuhakikisha hakuna mfumo mbovu wa utililishaji maji kutoka viwandani na kutaka sheria ya utunzaji mazingira ya mwaka 2004 inatekelezwa ipasavyo ikiwa na kuhakikisha watumishi wa viwanda wanakua na mfumo wa utunzaji wa afya zao.

“Ninaagiza uwepo wa miundombinu ya ujenzi wa vyoo bora, sehemu ya kunawa mikono kwa maji safi na sabuni kwa taasisi zote za umma na binafsi, vituo vya afya, shule zote, vituo vya abiria na nyumba zote za ibada kabla ya Aprili 30 mwaka 2019.

Kuhusu tabia ya uchimbaji dawa wakati wa safari ambayo hivi sasa imeota mizizi, Waziri Kassim Majaliwa amesema kuwa hivi sasa serikali pamoja na watu binafsi wamejenga na kutoa huduma za vyoo katika vituo maalum, vituo vya kuuzia mafuta, hoteli pamoja na maeneo ya umbali mrefu hivyo kuwataka Maofisa Afya kuwachukulia hatua kali wale wote wanaogundulika wanachimba dawa sehemu ambazo siyo rasmi au zilizotengwa na hiyo itasaidia  kuondoa kero za uchafuzi wa mazingira kwa kuchimba dawa porini.

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema katika awamu ya pili ya kampeni ya taifa ya usafi wa mazingira ya mwaka 2016/2021 wizara yake imepanga kuhakikisha asilimia 75 ya kaya nchini zinakua na vyoo bora  na kwamba kuondoa kaya ambazo hazina vyoo kabisa.

Alisema kwa upande wa shule, lengo ni kujenga miundombinu ya usafi na huduma za maji kwenye shule za msingi 3,500 na 700 za sekondari.
”Na kwa upande wa vituo vya tiba tunapanga kufikia vituo 1,000 hivyo kwa bajeti ya mwaka 2018/2019  tumejenga vyoo vipatavyo 700”. Alisistitiza Waziri Ummy.

Katika mkutano huo ambao uliambatana na maadhimisho ya wiki ya usafi wa mazingira kitaifa ambapo kulitangazwa washindi wa mashindano ya usafi na  Halmashauri ya Njombe iliibuka mabingwa kwa miaka mitatu mfululizo katika kundi la halmashauri za miji, wilaya, vijiji, shule za msingi za vijijini pamoja na shule za sekondari za bweni za  serikali na binafsi.
-Mwisho-






DKT. NDUGULILE – “SEKTA YA AFYA NCHINI INAKUWA KWA KASI”

- Hakuna maoni

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akisoma nyaraka za matibabu za Bi. Mary Nyange (kulia) anayepatiwa huduma za matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akihojiana na Bw. Longini Mtalo, Mteknolojia kutoka kituo cha utengenezaji wa viungo bandia katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC  huku akiwa ameshika sampuli ya kiungo bandia kilichotengenezwa na kituo hicho.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akikagua benki ya damu zilizopo katika jokofu Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini ya KCMC

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akionyesha mafuta maalum kwa ajili ya kuwakinga wenye ulemavu wa ngozi dhidi ya miale ya jua yanayotengenezwa na  kitengo cha Kilimanjaro Sunscreen Production kilichopo Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini ya KCMC.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akihojiana na  Bw. Prosper Kaaya, Mteknolojia kutoka kituo cha utengenezaji wa viungo bandia katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC  huku akiwa ameshika kiungo bandia kilichotengenezwa na kituo hicho.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (aliyesimama) akisema jambo wakati wa kikao na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC (hawapo pichani) aliye upande kulia ni Mganga Mkuu Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Best Magoma upande wa kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskasini KCMC Dkt. Gileard Masenga.

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC wakisiliza jambo wakati wa kikao kazi na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani) aliyetembelea hospitali hiyo Novemba 22, 2018.


NA WAMJW- KILIMANJARO

“Sekta ya afya inakua kwa kasi huku huduma muhimu za afya kwa sasa zikiwa zinapatikana hapa hapa nchini”

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile alipokua akizungumza na watumishi wa Hospitali ya rufaa ya Kanda ya Kaskazini (KCMC) iliyopo katika Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro jana Novemba 22, 2018.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Sekta ya Afya imepewa kipaumbele cha hali ya juu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli katika kipindi cha miaka mitatu mageuzi makubwa ndani ya sekta ya afya yameanza kuonekana huku huduma za matibabu ya kibingwa yakiwa zikipatikana hapa hapa nchini.

“Tunasimama hapa kifua mbele tukiona mabadiliko katika hali ya upatikanaji wa dawa kuimarika zaidi, bajeti ya dawa imeongezeka toka Shilingi Bilioni 30 mpaka Shilingi Bilioni 270 yaani mara tisa zaidi ndani ya miaka mitatu” alisema Mhe.Naibu Waziri na kuendelea “Tumeboresha vituo vya afya takribani 300, huku Mkoa wa Kilimanjaro ukiwa na Vituo 8 vilivyoboreshwa vilivyogharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 3.5 na kwa mwaka huu 2018 Serikali imeanza kujenga Hospitali za Wilaya 67 nchini”

Aidha, Dkt. Ndugulile alisema kuwa Serikali imetenga Shilingi Bilioni 30 kwa ajili ya Hospitali mpya za Rufaa za Mikoa ili  ziweze kutoa huduma za kibingwa, kupunguza msongamano wa wagonjwa na ucheleweshwaji wa huduma katika Hospitali za rufaa za kanda.

Naibu Waziri huyo Aliendelea kusema  kuwa fedha hizo Shilingi Bilioni 30 zitaelekezwa katika maeneo makuu matano ambayo aliyataja kuwa ni kuhakikisha kila Hospitali ya Mkoa ina Kitengo cha dharura, chumba cha upasuaji, kitengo cha uangalizi wa wagonjwa mahututi pamoja na kitengo cha mama na mtoto.

"Hospitali hii inatakiwa kuhudumia wagonjwa waliopata rufaa toka hospitali za mikoa ya jirani waje huku kupatiwa huduma za matibabu na sio wagonjwa wa malaria na mafua alisema Dkt. Ndugulile.

Katika kuhakikisha huduma bora za afya zinatolewa kwenye hospitali za rufaa za mikoa, Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali imeweka maeneo muhimu katika mafunzo kwa watumishi wa kada ya afya huku akitaja watumishi wenye kuhitajika zaidi kwa sasa kuwa ni madaktari wa magonjwa ya ndani, watoto, wakina mama, upasuaji, mifupa pamoja na madaktari wa usingizi.

Kuhusu upatikanaji wa huduma za kibingwa, Dkt.Ndugulile alisema  mafanikio  kuona huduma hizo zikiwa zinapatikana hapa nchini tofauti na zamani  “Tunafanya upandikizaji wa figo pamoja na upandikizaji wa vifaa vya usikivu kwa wa watoto huduma ambazo zilikuwa ni za kufikirika ndani ya miaka mitatu sasa zinapatikana hapa nchini” alisema Dkt. Ndugulile.

Awali akitoa taarifa yake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC Dkt. Gileard Masenga aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Hospitali hiyo "Licha ya kumilikiwa na Taasisi ya kidini lakini Serikali imeendelea kutupatia wataalam, misamaha ya kodi za malighali zinazoingizwa nchini ambazo hutumika kutengeneza mafuta ya kuwakinga wenye ulemavu wa ngozi dhidi ya jua.

Aidha, Dkt.Masenga alisema hospitali yake imetengewa  Shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya dawa za Saratani huku fedha kiasi cha Shilingi Milioni 250 tayari  zimeshapelekwa Bohari ya dawa kwa ajili ya ununuzi wa dawa hizo.

 Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto yupo Mkoani hapa kwa ziara  ya kikazi  inayolenga kukagua shughuli za huduma ya Afya,Maendeleo ya Jamii pamoja na kuongea na watumishi wa sekta  hizo.

MWISHO.

Jumatano, 21 Novemba 2018

DKT. MPOKI AKEMEA TABIA YA ABIRIA NA MADEREVA KUCHIMBA DAWA MAENEO YASIYOHUSIKA

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya akitoa neno mbele ya Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri pamoja na Wadau wa Mazingira leo katika Ukumbi wa CCM jijini Dodoma.




Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya akikagua maonesho ya vyoo baada ya kufungua kikao cha Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri pamoja na Wadau wa Mazingira leo jijini Dodoma. 
Picha ya Pamoja ikiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya katika baada ya kikao cha  Maafisa Afya wa Mkoa, Halmashauri pamoja na Wadau wa Mazingira kilichofanyika leo jijini Dodoma.
NA WAJMW-DODOMA

Madereva wa mabasi yaendayo mikoani na abiria wametakiwa kuacha tabia ya kujisaidia “Kuchimba dawa” katika maeneo yasiyo rasmi ili kutunza na kuepuka uharibifu wa mazingira unaoweza kujitokeza ikiwa ni pamoja kusababisha magonjwa ya milipuko.

Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati akifungua mkutano unaojumuisha Maafisa Afya kutoka mikoa na Halmashauri mbalimbali nchini pamoja na wadau wa mazingira, katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Dkt. Mpoki amekemea tabia hiyo hatarishi kwa ustawi wa mazingira huku akiwataka maafisa Afya na wadau wa mazingira nchini kusimamia afua zilizowekwa zinaendelea kutekelezwa ili kulinda mazingira ambayo yanatuzunguka.

“Kuna watu wengine nimeshawahi kuwaona kwenye basi wanatupa taka ovyo na mabasi mengine yanasimama porini ili abiria wajisaidie, hii tabia siyo nzuri na inatakiwa ikemewe kwa nguvu zote, Dkt. Subi na wenzake wanakuja na mpango mkakati  wa kuondoa kabisa dhana ya watu kusimama kujisaidia porini, sisi tunatakiwa kuwa msitari wa mbele kupiga marufuku mabasi  kusafiri bila kuchafua mazingira”.

Dkt. Mpoki amesema ni aibu kubwa kwa taifa kuona watu hawafuati kanuni za usafi huku akiwataka Maafisa Afya kuhakikisha wanafanya kazi kwa nguvu ili ionekane kuwa kero kwa watu wengine na watakaobainika kuchafua mazingira wachukuliwe hatua za kinidhamu na kisheria.

Aidha, Dkt. Mpoki ameongeza kuwa jamii inatakiwa kuzingatia matumizi ya vyoo bora na kunawa mikono mara baada ya kujisaidia ili kuepuka magonjwa ya milipuko yanayoweza kusababishwa na tabia ya uchafu ikiwa ni pamoja na kuacha tabia ya kujisaidia ovyo porini ili kaulimbiu ya “Nyumba ni Choo” iweze kutekelezwa ipasavyo kwa kujenga vyoo vya kisasa katika maeneo mbalimbali ili huduma ipatikane mahala pote.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi amesema takwimu zinaonesha kaya zilizokua na vyoo bora mwaka 2012 zilikua asilimia 19.5 lakini hivi sasa nchi nzima kaya zenye vyoo bora ni asilimia 51.4.

Dkt. Subi amesema kutokana na takwimu hiyo inaonesha kuna mafanikio katika uhamasishaji kwa jamii kutumia vyoo bora na kuacha kutumia vyoo ambavyo havina viwango na salama kwa matumizi, na badala yake serikali inaendelea kutoa elimu na kusisitiza jamii kutumia vyoo bora ili kuepuka magonjwa yanayoweza kuzuilika ikiwemo kipindupindu, magonjwa ya tumbo na kuhara.

Pamoja na hayo, maafisa Afya wametakiwa kuongeza nguvu katika kutoa elimu kwa umma, kuhamasisha usafi wa mazingira na kufukia maeneo ya mazalia ya vimelea vya ugonjwa wa Malaria ili kutokomeza ugonjwa huo ambao umekua hatari kwa jamii hasa kwa wanawake wajawazito na watoto.

Mkutano huo unaojumuisha Maafisa wa Afya nchi nzima una lengo la kutoa elimu na kubadilishana uzoefu wa kufanya kazi lakini msisitizo mkubwa ikiwa ni utunzaji wa mazingira na kuzingatia kanuni bora za afya pamoja na usafi wa mazingira na usafi na afya ya binadamu. 

Alhamisi, 15 Novemba 2018

MATUKIO KATIKA PICHA YALIYOJIRI KWENYE MKUTANO MKUU WA MWAKA WA KUJADILI MASUALA MBALIMBALI YA AFYA JIJINI DODOMA




Wadau na wataalam mbalimbali wa afya wakiangalia na kujadili utekelezaji wa vipaumbele vya matamko ya Kisera yaliyoidhinishwa kwa mwaka wa fedha 2017/18 pamoja na utekelezaji wa vikundi kazi 11 vya Kitaalam katika kutekeleza mpango mkakati wa nne kwa mwaka wa fedha 2017/2018

SERIKALI YAJIPANGA KUTOKOMEZA MAAMBUKIZI YA VVU KWA WATOTO WACHANGA.

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na wadau mbalimbali wa maendeleo na sekta ya afya hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma.

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akikata utepe kuashiria kuzindua chapisho la uchambuzi  wa masuala ya lishe wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma, wa pili kushoto ni Naibu Waziri OFisi ya Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara .

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kulia akionesha moja ya chapisho la uchambuzi  wa masuala ya lishe wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma, wa pili kushoto ni Naibu Waziri OFisi ya Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara .

Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akifuatilia mada iliyokuwa inawasilishwa na moja ya wawasilishaji hayupo pichani  wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma, wa pili kulia ni Naibu Waziri OFisi ya Waziri TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara .

Baadhi ya  wadau mbalimbali wa maendeleo na sekta ya afya wakifuatilia kwa makini hotuba ya Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii pamoja na masuala ya lishe leo jijini Dodoma.


NA WAMJW-DODOMA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema serikali ina mpango madhubuti wa kuhakikisha wamama wajawazito hawawaambukizi watoto walio tumboni Virusi vya Ukimwi na kipindi wanapozaliwa.

Waziri Ummy amesema hayo leo wakati wa uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya maendeleo ya jamii ikiwa ni pamoja na masuala ya lishe, uliofanyika katika ukumbi wa Hazini, Jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema hadi hivi sasa asilimia 99 ya wajawazito wenye maambukizi ya VVU wanapewa huduma za kumkinga mtoto asipate maambukizi hayo huku la serikali ifikapo mwaka 2020 ni kuhakikisha  hakuna mtoto atakayezaliwa na maambukizi ya VVU.

“Sasa hivi asilimia 99 ya wanawake wajawazito wote wenye maambukizi  ya VVU tumewaingiza katika mpango wa dawa, na hiyo asilimia moja bado hatujawafikia ila kwa nguvu na msukumo tuliouweka juzi wa kuwasainisha Wakuu wa Mikoa kwenda kufuatilia masuala ya afya ya mama na mtoto, tunaamini hakuna mtoto yeyote Tanzania atakayezaliwa na maambukizi ya UKIMWI”. Amesema Waziri Ummy.

Katika Uzinduzi huo, Waziri Ummy ameipongeza Wizara ya Fedha na Mipango kupitia kwa Waziri wake Mhe. Dkt. Philipo Mpango  inavyojikita katika mipango ya kuendeleza wanawake na watoto kwa kutoa huduma bora za afya, elimu, maji na masuala ya maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na Shirika la Watoto Duniani (UNICEF) imefanya uchambuzi wa bajeti katika sekta mtambuka ya jamii, hususani katika elimu, afya, Virusi vya Ukimwi, maji, usafi wa mazingira na lishe kwa lengo la kuboresha upangaji na utekelezwaji wa masuala ya mama na mtoto.

Pamoja na hayo, uzinduzi wa machapisho hayo umelenga kupunguza tatizo la lishe linalosababisha udumavu kwa watoto walio katika umri mdogo. Ambapo katika ripoti iliyotolewa katika mkutano wa IMF na Benki ya dunia uliofanyika nchini Indonesia mwezi Oktoba mwaka 2018, inaonesha Tanzania inashika nafasi ya 128 kati ya nchi 157 duniani katika kipimo cha ubora wa nguvukazi  katika uwekezaji wa rasilimali watu hususani katika sekta ya afya na elimu ya lishe.

Kufuatia hali hiyo, Tanzania inaonekana kuwa na matatizo ya udumavu, elimu ya lishe na afya kwa watoto wenye umri mdogo ambapo serikali inafanya kazi kubwa ya kuhakikisha elimu ya lishe inawafikia wazazi na jamii kwa ujumla ili kupambana na tatizo la udumavu. Na kufikia mwaka 2015 tatizo la udumavu limeshuka kutoka asilimia 34 kutoka asilimia 42 mwaka 2010. Alisema Waziri huyo.

Tatizo la lishe limeonekana kupungua nchini huku viashiria vya tatizo hilo vikipungua ambavyo ni uzito pungufu umeshuka kutoka asilimia 16 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 14 mwaka 2015/16, pamoja na ukondefu wa mwili kuendelea kubakia chini ya asilimia 5 kwa mwaka 2015/16.


TANGAZO LA KUITWA KAZINI

ORODHA YA MAJINA IMEAMBATANISHWA HAPA CHINI