Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 5 Februari 2019

TUENDELEE KUSHIRIKIANA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati wa Hafla ndogo ya kuwaaga Balozi Dkt Mpoki Ulisubisya na Dkt. Dorothy Gwajima  waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile  akisisitiza jambo wakati wa Hafla ndogo ya kuwaaga Balozi Dkt Mpoki Ulisubisya na Dkt. Dorothy Gwajima waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu (kushoto) akiwa na Naibu wake Dkt. Faustine Ndugulile (kulia) wakifuatilia alichakuwa akiongea Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi (hayupo pichani) wakati wa hafla ndogo ya kuwaaga Dkt Mpoki Ulisubisya na Dkt. Dorothy Gwajima waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula wakati wa Hafla ndogo ya kuwaaga Dkt Mpoki Ulisubisya na Dkt. Dorothy Gwajima waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI Idara ya Afya Dkt Dorothy Gwajima.

Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya akiteta jambo na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi wakati wa Hafla ndogo ya kuwaaga  Dkt Mpoki Ulisubisya na Dkt. Dorothy Gwajima waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula, hafla ilofanyika katika ofisi za Wizara ya Afya jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakifuatilia maelekezo kutoka kwa Waziri Ummy  wakati wa Hafla ndogo ya kuwaaga Dkt Mpoki Ulisubisya na Dkt. Dorothy Gwajima waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula. Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi za Wizara ya Afya jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisaini Biblia Takatifu aliyopewa kama zawadi Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya  wakati wa Hafla ndogo ya kuwaaga Baozi Dkt Mpoki Ulisubisya Dkt. Dorothy Gwajima waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula, hafla ilofanyika katika ofisi za Wizara ya Afya jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto mhe.Ummy Mwalimu  akimkabidhi Zawadi Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya wakati wa Hafla ndogo ya kumuaga yeye na Dkt. Dorothy Gwajima waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto mhe.Ummy Mwalimu  akimkabidhi Zawadi Naibu Katibu Mkuu Idara ya Afya TAMISEMI Dkt. Dorothy Gwajima wakati wa Hafla ndogo ya kumuaga yeye na Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula.

Wakwanza kulia ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akifuatilia alichakuwa akiongea Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi wakati wa Hafla ndogo ya kuwaaga Balozi Dkt Mpoki Ulisubisya na Dkt. Dorothy Gwajima waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula (Wakatikati)  na (Wakwanza kishoto) ni Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI Idara ya Afya Dkt Dorothy Gwajima.

Mkurugenzi wa MSD ambae pia ni mwakilishi wa Wakurugenzi wa Taasisi zote za Wizara ya Afya Laurean Bwanakunu akitoa salamu za taasisi zote za Afya wakati wa Hafla ndogo ya kuwaaga Dkt Mpoki Ulisubisya na Dkt. Dorothy Gwajima waliohudumu Wizara ya Afya  kabla yakuteuliwa katika nafasi nyingine, na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula, hafla hiyo  imefanyika katika ofisi za Wizara ya Afya jijini Dodoma.


Na WAMJW - DOM
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo amewaongoza watumishi katika halfa fupi ya kumuaga rasmi aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Mpoki Ulisubisya ambae ameteuliwa kuwa Balozi, na aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Tiba Wizara ya Afya, ambaye amekuwa Naibu Katibu Mkuu Idara ya Afya TAMISEMI Dkt. Dorothy Gwajima na kuwakaribisha Watumishi wapya wakiongozwa na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Idara ya Afya TAMISEMI Dkt. Zainab Chaula ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Idara Kuu ya Afya na aliyekuwa Mganga Mkuu wa Dar es salaam ambaye kwa sasa ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara Tiba Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe

Katika hafla hiyo Waziri Ummy amewashukuru watumishi wote wakiongozwa na Dkt Mpoki Ulisubisya kwa ushirikiano waliouonesha katika kipindi chote walichofanya kazi Wizara ya Afya na kuwasihi kuendeleza uchapaji kazi ili kusukuma gurudumu la Maendeleo hususani maendeleo ya Sekta ya Afya.

Aidha, Waziri Ummy amewakaribisha Watumishi wote walioamia katika Wizara ya Afya, Waziri Ummy amesema kwamba licha ya mafanikio makubwa ambayo Sekta ya Afya imepiga, bado kuna changamoto nyingi ambazo zinapaswa kutatuliwa ikiwemo suala la uhaba wa watumishi, na upatikanaji wa Dawa na vifaa tiba.

Naye Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Fustine Ndugulile amewakumbusha Watumishi wa Sekta ya Afya juu ya uwajibikaji na kuwatoa hofu kuwa, kama Serikali milango yao ipo wazi muda wote, hivyo kwa yoyote mwenye wazo zuri la kujenga na kuipeleka mbele Sekta ya Afya asisite kuwaona.

Kwa upande wake, aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya amewashukuru Watumishi wote wa Sekta ya Afya wakiongozwa na Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu kwa ushirikiano waliomuonesha katika kipindi chote alichohudumu katika Wizara ya Afya, kisha kuahidi kuwa Balozi Mzuri huko atakoenda ili kuikuza Sekta ya Afya.

Naye, Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula amewakumbusha Watumishi wa Sekta ya Afya juu ya umoja na ushirikiano baina yao, huku akisisitiza kila mmoja ni lazima ahakikishe anatimiza wajibu wake ili kusukuma mbele Maendeleo ya Sekta ya Afya.

Kwa upande wake, aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Tiba Wizara ya Afya ambae sasa ni Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI Idara ya Afya Dkt Dorothy Gwajima ameahidi kuwa daraja zuri na imara baina ya Wizara ya Afya na TAMISEMI kutokana na kuzijua Wizara zote mbili kiundani na kuahidi kuendeleza mazuri yote yalioachwa na Dkt. Zainab Chaula.

Mwisho.


Jumatatu, 4 Februari 2019

WAUGUZI WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI KATIKA SEHEMU ZAO ZA KAZI


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa ameshika bango kuashiria uzinduzi wa Kampeni ya Kimataifa ya Uuguzi Sasa Kampeni inayolenga kuinua hadhi na muonekano wa kada ya uuguzi nchini.

Wadau wa Kampeni ya Uuguzi Sasa wakiwa wameinua mabango kuashiria kampeni hiyo kuzinduliwa rasmi.

Wauguzi wakisikiliza kwa umakini yanayoendela kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Uuguzi Sasa

Picha ya wadau wa kampeni ya uuguzi sasa waliojitokeza kwenue uzinduzi wa kampeni hiyo inayokenga kuinua hadhi na muonekano wa kada ya uuguzi nchini.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akimpongeza Mwalimu Mstaafu wa Kada ya Uuguzi  Mwl. justina Venant (kulia) kwa kumpatia cheti cha utumishi ulitukuka wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Uuguzi Sasa.

Picha ya pamoja ya Viongozi na Watendaji wa Serikali pamoja na wadau wa Sekta ya Afya wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Uuguzi Sasa.


Na WAMJW - Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amewataka wauguzi kutimiza wajibu wao na kutoa huduma bora wakati wa kazi kulingana na miongozo na maadili ya kazi ya uuguzi na ukunga.

Waziri Ummy ametoa agizo hilo leo Jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Kimataifa ya Uuguzi Sasa inayolenga kuinua hadhi na muonekano wa kada ya Uuguzi.

“Nataka kuona wauguzi wanafanya kazi kwa kuzingatia miongozo na maadili ya taaluma ya kada ya uuguzi na kuwa na heshima na utu kwa wagonjwa” alisema Waziri Ummy na kuendela “Nimefurahi kuona kwenye kampeni hii mmejipanga kuondoa changamoto zilizopo”

Aidha Waziri Ummy amewataka viongozi kuwatambua wauguzi ambao wamekuwa hawana kauli nzuri na kuwachukulia hatua ili kuondokana na vitendo vya wauguzi kutoa kauli za kebehi kwa wateja na kuwaasa wauguzi kuacha lugha za kebehi na zisizowafurahisha wateja kwani kufanya hivyo kuwachafua taswira ya wauguzi nchini.

Licha ya changamoto zilizopo Waziri Ummy hakusita kutoa pongezi kwa wauguzi ambao wamekuwa na mchango mkubwa katika utoaji wa huduma za afya nchini. “Napenda kuwapongeza wauguzi wote kwa kazi mnayofanya, Kazi ya wauguzi wanne inafanywa na muuguzi mmoja, Kazi ya wakunga watano, inafanywa na mkunga mmoja” alisema Waziri Ummy.

Naye Rais wa Chama cha Wauguzi nchini Tanzania (TANNA) Bw. Paul Magesa amekiri kuwepo kwa baadhi ya wauguzi wasio na maadili katika kazi amabo wamekuwa wakitoa kauli mbaya kwa wagonjwa huku akiahidi kuwa kupitia chama anachoongoza changamoto hizo zitatatuliwa ndani ya muda mfupi.

Aidha Bw. Magesa alitumia nafasi hiyo kuipongeza Serikali kwa kuongeza bajeti ya dawa nchini ambapo sasa dhana ya wauguzi kuwa ndio wezi wa dawa inaanza kufutika katika jamii.

“Hapo awali tulionekana sisi wauguzi ndio wezi wa dawa, tunaotumia vibaya dawa lakini ukweli ni kwamba dawa hazikuwepo, kitendo cha Serikali kuongeza bajeti ya dawa kimetusafisha sisi wauguzi” alisema Bw. Paul Magesa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Bw. Gustav Moyo amesema kuwa Kampeni ya Uuguzi Sasa imekuja wakati mwafaka kuja kutatua changamoto zilizopo muda mrefu ambazo zimekuwa zikikwamisha utendaji kazi wa wauguzi nchini.

Bw. Gustav amesema kuwa Uuguzi sasa ni kampeni ya kimataifa inayokusudia kuongeza hadhi na muonekano wa kada ya uuguzi nchini ambayo inalenga kuwawezesha wauguzi na wakunga kufikia na kumudu malengo ya afya ya karne ya 21 pamoja na changamoto zake.

CHANJO YA MLANGO WA KIZAZI HAIHUSIANI NA UZAZI WA MPANGO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akisisitiza jambo leo wakati akiongea na Waandishi wa Habari katika siku ya Saratani Duniani, iliyofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari Bunge jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mkurugenzi wa Ubora kutoka Wizara ya Afya Dkt. Mohammed Mohammed ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Afya.

Mkurugenzi wa Ubora ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mohammed Mohammed akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe leo katika  tamko la siku ya Saratani Duniani lililofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari Bunge jijini Dodoma.

Waandishi wa Habari wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu  wakati akitoa tamko la siku ya Saratani Duniani, leo jijini Dodoma


 Waandishi wa Habari wakifuatilia tamko la Saratani lililosomwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo katika Ukumbi wa Idara ya habari Bungeni jijini Dodoma.

CHANJO YA MLANGO WA KIZAZI HAIHUSIANI NA UZAZI WA MPANGO.

Na WAMJW - DOM

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu amewatoa hofu Wananchi kwa kusisitiza kuwa chanjo ya kuwakinga wasichana na Saratani ya Mlango wa kizazi haihusiani na uzazi wa mpango wala kumzuia msichana kuja kupata uja uzito baadae.

Ameyasema hayo leo wakati akiongea na Waandishi wa Habari katika siku ya Saratani Duniani, iliyofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari Bunge jijini Dodoma, huku kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa ni "NITAFANYA JITIHADA ZOTE KUPUNGUZA JANGA LA SARATANI DUNIANI".

Waziri Ummy amesema kuwa Chanjo ya Mlango wa kizazi ni salama na imethibitishwa na Shirima la Afya Duniani kwaajili yakuwakinga Wasichana dhidi ya maambulizi ya Saratani ya Mlango wa kizazi.

" Chanjo ya kuwakinga wasichana na saratani ya mlango wa kizazi haihusiani na uzazi wa mpango, ni chanjo ambayo imethibitishwa na Shirika la Afya Duniani kwaajili yakuwakinga wasichana dhidi ya maambukizi ya Saratani ya mlango wa Kizazi" Alisema Waziri Ummy

Waziri Ummy amesema kuwa katika kila wagonjwa wa Saratani 100, takribani wagonjwa 31 ni wanawake wa Saratani ya Mlango wa kizazi, hivyo amewahasa wazazi na walezi nchini kuhakikisha wasichana wanaostahili kupata chanjo hii, wanaipata bila vikwazo vyovyote ili kutokomeza kabisa Saratani hii nchini.

"Katika kila wagonjwa wa Saratani 100, Wagonjwa takribani 31 ni wanawake wa Saratani hii ya Mlango wa kizazi, kwahiyo hatuna haja ya kuiogopa chanjo hii kwasababu ndio itayowakinga watoto wetu na maambukizi ya Saratani ya mlango wa kizazi" alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa  kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Tafiti za Saratani (IARC), zinaonyesha kwamba kwa Tanzania kunatokea mgonjwa 1 wa Saratani kwa kila watu 1000, hivyo Tanzania inakua na wagonjwa wapya wa Saratani 55,000 kwa mwaka na takribani wagonjwa 28,610 hufariki kwa mwaka, ambapo ni vifo asilimia 52 ya wagonjwa wapya. 

Aliendelea kusema kuwa Taarifa kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road zinaonesha kwamba kumekuwa na ongezeko la wagonjwa wa Saratani mwaka hadi mwaka, huku akisema kuwa Mwaka 2015  wagonjwa wapya 5,764, huku mwaka 2016  wagonjwa wapya 6,338, na mwaka 2017  wagonjwa wapya 7,091, pia mwaka 2018 wagonjwa wapya 7,649.

Kwa upande mwingine Waziri Ummy amedai kuwa Serikali imeanzisha huduma kwenye vituo 624 vilivyopo katika Halmashauri mbalimbali nchini ambapo jumla ya wanawake 375,522 walifanyiwa uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi na saratani ya matiti mnamo mwaka 2017, ukilinganisha na wanawake 416,841 waliofanyiwa uchunguzi huo mwaka 2018. Kati ya hao, wanawake 16,147 waligundulika kuwa na mabadiliko ya awali mwaka 2017, na wanawake 18,341 mwaka 2018.

Jumanne, 29 Januari 2019

IDADI YA WANANCHI WALIOJIUNGA NA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA (NHIF)

- Hakuna maoni

HALI YA HUDUMA ZA AFYA  NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018

7. Idadi ya Wananchi waliojiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)

#Hadi kufikia Desemba mwaka 2018, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ulikuwa na jumla ya wanachama wachangiaji 899,654 na ikihudumia jumla ya wanufaika 4,219,192 sawa na asilimia 8 ya Watanzania wote.

#Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) unahudumia wanufaika 13,506,330 sawa na asilimia 25 ya Watanzania wote ukilinganisha na asilimia 24 kwa kipindi kama hicho mwaka 2017.

# Kwa ujumla wake NHIF na CHF inahudumia wanufaika 17,725,522 sawa na asilimia 33 ya watanzania wote. 

Imetolewa na;
Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto
29/01/2019

TAMKO LA MHE. UMMY MWALIMU (MB) KATIKA KUADHIMISHA SIKU YA UKOMA DUNIANI

- Hakuna maoni

TAMKO LA MHE. UMMY MWALIMU (MB) WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO KATIKA KUADHIMISHA SIKU YA UKOMA DUNIANI TAREHE 27/01/2019
KIGAMBONI, DAR ES SALAAM

Ndugu wanahabari,
Siku ya Ukoma Duniani huadhimishwa ulimwenguni kote kila Jumapili ya mwisho ya mwezi Januari. Kwa mwaka huu, siku hii itaadhimishwa tarehe 27 Januari, 2019. 

Lengo kuu la maadhimisho haya ni kukumbusha umma wa watanzania juu ya ugonjwa huu. Ni dhahiri kuwa ugonjwa wa Ukoma umekuwa ukiogopwa sana katika jamii yetu toka enzi na enzi hasa kutokana na ukweli kwamba unasababisha ulemavu wa kudumu mwilini na kufanya waathirika kuwa tegemezi na kutothaminiwa.

Sanjali na madhimisho haya, hapa Tanzania tunaadhimisha miaka 60 ya uwepo wa Shirika la Ujerumani linaloshughulikia masuala ya Kifua kikuu na Ukoma (GLRA). Shirika hili limekuwa mstari wa mbele katika kuisaidia serikali kuhakikisha Ukoma unatokomezwa kwa kufadhili shughuli mbali mbali ikiwa ni pamoja na kutoa vyombo vya usafiri kwa waratibu wa Kifua kikuu na Ukoma nchi nzima.



Ndugu wanahabari,
Siku ya Ukoma Duniani inatupa fursa ya kutathmini mwelekeo wa jitihada zetu nchini na zile za kimataifa katika kupambana na ugonjwa huu. Kauli mbiu katika maadhimisho ya mwaka huu ni “TUTOKOMEZE UBAGUZI, UNYANYAPAA NA CHUKI DHIDI YA WAATHIRIKA WA UKOMA”. Ni kweli kuwa waathirika wengi wa Ukoma wananyanyapaliwa na kubaguliwa katika maeneo mengi, takriban asilimia 50 ya wagonjwa wa Ukoma hupatwa na sonona na huishi maisha ya huzuni na wasi wasi mkubwa. Haya yote husababishwa na mtazamo hasi wa jamii dhidi ya waathirika wa ugonjwa wa Ukoma. Mtazamo huu hasi ndio kikwazo kikubwa katika vita ya kutokomeza Ukoma duniani na hapa nchini. 

Serikali, wadau na wananchi wote wanahimizwa kuungana na kuongeza nguvu katika kupinga matukio vyote vya ubaguzi na unyanyapaa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha hakuna sheria kandamizi kwa watu walioathirika na ugonjwa wa Ukoma. Kwa kufanya kazi pamoja na kupinga kwa nguvu zote vitendo hivi itatusaidia kupiga hatua mbele kuelekea kutokomeza Ukoma.

Ndugu wanahabari,
Pamoja na kwamba nchi yetu ilifikia viwango vya utokomezaji wa Ukoma kitaifa mnamo mwaka 2006 kwa kiwango cha chini ya mgonjwa 1 kati ya watu 10,000, Ukoma bado unaendelea kuwa tatizo la kiafya miongoni mwa jamii nchini kwetu. Kwa mujibu wa takwimu za Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua kikuu na Ukoma (NTLP) za mwaka 2017, jumla ya wagonjwa wapya 1,933 waligunduliwa na hivyo kufanya kiwango cha ugunduzi kuwa watu 4 kwa kila watu 100,000. Takwimu hizi zinaifanya Tanzania kuendelea kuwa miongoni mwa nchi 22 zenye wagonjwa wengi wa Ukoma duniani nchi nyingien ni pamoja na India, Indonesia, Brazil, Ethiopia, Msumbiji, Nigeria na DRC Kongo. Hivi sasa bado kuna mikoa kumi ambayo inagundua wagonjwa wapya wa Ukoma wengi zaidi kila mwaka na kuchangia karibia 80% ya wagonjwa wote. Mikoa hiyo ni pamoja na: Lindi, Rukwa, Mtwara, Morogoro, Pwani; Tanga, Geita, Dodoma, Tabora na Kigoma. 

Aidha, bado zipo wilaya 20 ambazo kiwango cha ukubwa wa tatizo la Ukoma lipo juu sana na bado hazijafikia lengo la utokomezaji, nazo ni Liwale,  Lindi vijijini, Nachingwea, Ruangwa, Nanyumbu, Masasi mjini,  Pangani, Mkinga, Korogwe,  Mvomero, Kilombero, Morogoro vijijini, Ulanga, Shinyanga manispaa,  Mafia, Rufiji, Kilwa, Chato, Nkasi,  na Mpanda. 

Ndugu wanahabari,  
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Wizara ya TAMISEMI inatekeleza shughuli mbali mbali katika kuhakikisha Ukoma unatokomezwa  kabisa. Shughuli hizo ni pamoja na : 
Kuhakikisha dawa za kutibu Ukoma zinaendelea kupatikana wakati wote na bila malipo yoyote, 
Kuendesha kampeni za uibuaji wa wagonjwa wapya ngazi ya jamii kwa kuwashirikisha watoa huduma ngazi ya jamii ( Leprosy Elimination Campaigns) hasa katika wilaya zenye kiwango kikubwa cha wagonjwa wa Ukoma,
Kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu dalili za Ukoma na upatikanaji wa huduma kwa kutumia vifaa vya habari, Elimu na mawasiliano kama vile vipeperushi, mabango na mikanda ya video, 
Utekelezaji wa shughuli za kuzuia ulemavu unaotokana na Ukoma ikiwemo kutathmini wagonjwa wenye vidonda, kufanya upasuaji maalum, huduma za kitaalam za macho na utoaji wa viungo bandia pamoja na viatu maalum.

Ndugu wanahabari,
Pamoja na hatua zinazochukuliwa na serikali na mafanikio zipo changamoto kubwa mbili ambazo ni jamii kuendelea kushikilia imani potofu juu ya Ukoma kuwa ni ugonjwa wa kurithi au kulogwa; na wagonjwa kuchelewa kujitokeza kupata matibabu hadi wanapopata ulemavu. Ukoma ni ugonjwa wa kuambukizwa unaosababishwa na vimelea vinavyoshambulia mishipa ya fahamu na huambukizwa kwa njia ya hewa pekee.

Nitoe rai kwa jamii, wazazi na walezi kuwa sote tujenge tabia ya kuchunguza miili yetu na ya watoto wetu. Endapo utaona mojawapo ya dalili za Ukoma ambazo ni baka au mabaka mwilini yenye rangi ya shaba na hayana hisia, vijinudu kwenye ngozi au mishipa ya fahamu kuvimba. Dalili nyingine ni ganzi kwenye mikono na miguu. Unashauriwa kwenda kwenye kituo cha tiba kilicho karibu nawe kwa uchunguzi bila kuchelewa. Hii itawawezesha wataalam wa afya kuchunguza na kubainisha kama mgonjwa ana Ukoma ili apate tiba sahihi mapema na hivyo kuzuia maambukizi na ulemavu wa kudumu unaoweza kuzuilika.

Ugonjwa wa Ukoma unatibika. Mgonjwa aliyeanza tiba hawezi kuambukiza mtu mwingine na hivyo hakuna sababu ya kumtenga na anaweza kuendelea na shughuli za kawaida za maisha.

Tiba ya Ukoma inapatikana nchini kote na hutolewa bila malipo kwa wagonjwa wote.
Nirudie tena kuwa, pale tunapoona mabadiliko yoyote yanajitokeza kwemye miili yetu twende mapema katika vituo vyetu vya huduma kuchunguzwa ili tupate matibabu stahili. 

Ndugu wanahabari,
Aidha, napenda kuwashukuru watoa huduma katika vituo vya huduma za afya kote nchini kwa juhudi wanazofanya kila siku kuhakikisha ugonjwa huu si tatizo la kiafya tena nchini. Pia wanahabari kwa kuendelea kuendelea kuelimisha jamii kuhusu magonjwa mbalimbali.

Pia nachukua nafasi hii kwa niaba ya serikali ya awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuyashukuru mashirika mbali mbali ya ndani na nje yanayounga mkono juhudi zetu za kutokomeza Ukoma nchini kama vile Norvatis Foundation ya Uswisi, Germany Leprosy and Tuberculosis Relief Association (GLRA) ya Ujerumani, Nippon Foundation chini ya  Sasakawa Memorial Health Initiative ya Japani na Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa michango yao ya hali na mali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukoma hapa nchini Tanzania. 
“TUTOKOMEZE UBAGUZI, UNYANYAPAA NA CHUKI DHIDI YA WAATHIRIKA WA UKOMA”.


Asanteni kwa kunisikiliza!



Jumatatu, 28 Januari 2019

6. HALI YA HUDUMA ZA AFYA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018



HALI YA HUDUMA Za AFYA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2018

6.Vituo vya kutolea huduma za afya nchini

#Hadi kufikia Desemba 2018, jumla ya vituo vya kutolea huduma za Afya vilifikia 7,768 kutoka vituo 7,435 mwaka 2017 sawa na ongezeko la vituo 333 kwa mwaka.

#Katika vituo hivyo Serikali ilikuwa inamiliki asilimia 71 ya vituo vya kutolea huduma.

# Mashirika ya dini asilimia 12, Taasisi za Serikali (Parastatal) asilimia 3 na vituo binafsi asilimia 15.

#Wakati ambapo hospitali zilikuwa asilimia 3, Vituo vya afya asilimia 11 na Zahanati asilimia 86.

Imetolewa na ;
Wizara ya Afya,Maendeleonya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto
28/01/2019

Dkt Ndugulile - “UGONJWA WA UKOMA HAUNA UHUSIANO NA IMANI ZA KISHIRIKINA”

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akitoa kingatiba kwa mtoto aliyekuwa akiishi na mgonjwa wa ukoma. Kingtiba hiyo itamlinda dhidi ya ugonjwa wa ukoma imezinduliwa na Dkt. Ndugulile katika maadhimisho ya siku ya Ukoma Duniani yaliyofanyika Wilayani Mvomero, Morogoro.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kulia) akisalimiana na wazee waliopata msaaada wa viatu vya kutembelea toka Taasisi ya GLRA inayowasaidai watu wenye ugonjwa wa ukoma nchini.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kulia)akisalimiana na Mzee Anthony Martin (kushoto) wakati alipotembelea makazi ya wasiojiweza ya Chazi, Katika Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akisalimiana na Rais wa Taasisi ya GLRA bw. Patric Meisen kutoka Ujerumani inayowahudumia waathrika wa ukoma nchini.

Picha ya pamoja, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulike (wa nne kutoka kushoto, walioketi) akiwa na wadau wa Sekta ya Afya nchini.

Na WAMJW -Mvomero, Morogoro.

“Ugonjwa wa ukoma hausababishwi na imani za kishirika bali ni vimelea vya magonjwa ambavyo huingia ndani ya mwili na kusababisha ukoma”

Hiyo ni kauli ya Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipokuwa akizungumza na waathirika wa ugonjwa wa ukoma pamoja na wananchi katika maadhimisho ya siku ya Ukoma Duniani, wilayani Mvomero, katika Mkoa waMorogoro.

 Dkt. Ndugulile amewaasa wananchi kuachana na imani za kishirikina  kwa kuamini kuwa ya kwamba ugonjwa huo unahusika moja kwa moja na imani hizo za giza.

“Dhana ya kwamba ugonjwa huu ni wa kurogwa siyo kweli, ugonjwa wa ukoma hausababishwi na mtu kulogwa wala kutupiwa jini bali ni vimelea ambavyo huingia mwilini na kusababisha ugonjwa wa ukoma, ni watu kama mimi na wewe” anasema Dkt Ndugulile.

Aidha Dkt Ndugulile ametumia nafasi hiyo kuwaelimisha wananchi kuwa ugonjwa wa ukoma unatibika na kusema kuwa dawa za kutibu ugonjwa huo zipo na kuwaondolea hofu ya kuwa ugonjwa huo kutotibika. Hata hivyo Dkt. Ndugulile ametoa rai kwa wananchi wote kujitokeza mapema katika vituo vya kutolea huduma za afya kupata huduma za matibabu pindi wanapohisi kuwa na dalili za ugonjwa wa ukoma.

“Mtu yeyote ambaye anaanza kuona mabadiliko kwenye ngozi yake, anapata mabaka ambayo hayaelewi au kupoteza hisia pindi unapojigusa ni muda wa kwenda hospitalini kufanya uchunguzi na kama utagundulika kuwa na vimelea vya ugonjwa wa ukoma utapewa matibabu” alisisitiza Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile amewataka wananchi kuwa mabalozi wa kuwaelimisha watu wengine juu ya dalili na athari za ugonjwa wa ukoma. “Niwaombe ndugu wananchi tuendelee kutoa elimu kuhusiana na ugonjwa huu ni ugonjwa ambao tunaweza tukauzuia na tusiwe na athari kwenye jamii na tusingependa kuona kwenye zama hizi watu wanapata athari za kudumu na wanapoteza viungo, hisia katika sehemu za miili yao au kuharibika ngozi kwa sababu ya kutopata matibabu mapema” alifafanua Dkt Ndugulile.

Naibu Waziri huyo wa Afya amesema kuwa Serikali ipo katika hatua nzuri za kutokomeza ugonjwa wa ukoma nchini licha ya changamoto ambazo zipo katika baadhi ya maeneo sugu ambayo ugonjwa huo umeonekana kuwa ni tatizo. “Takwimu zinaonyesha kuwa takribani watu 1993 huugua ugonjwa wa ukoma kila mwaka huku mikoa ya Lindi, Rukwa, Mtwara, Pwani, Tanga, Geita, Dodoma, Tabora, Kigoma na Mkoa wa Morogoro ikiwa na idadi kubwa ya wagonjwa” alisema Dkt. Ndugulile.

Sasa hivi tumepiga hatua kubwa, tunajua jinsi gani ugonjwa unaambukizwa, na namna ya kuutibu pamoja na kujikinga dhidi ya maambukizi mapya, naamini kwa mikakati iliyopo tunaweza kuutokomeza ugonjwa huu.

Akizungumiza mikakati iliyopo Dkt Ndugulile amesema kuwa pamoja na elimu ambayo wamekuwa wakiitoa, Serikali imehamishia nguvu kwenda kwenye jamii moja kwa moja kuwabaini wagonjwa wa ukoma. “Hatusubiri watu watufate, tumewekeza nguvu nyingi kwenye jamii na kuwafikia huko huko maeneo wanayoishi” alisema Dkt Ndugulile.

Kwa upande mwingine, Dkt Ndugulile amezindua Mpango wa Kingatiba ya Ugonjwa wa Ukoma mahususi kwa wale ambao wamekuwa wakiishi na wagonjwa wa ukoma ili waweze kujikinga kutopata ugonjwa huo na kutoa rai kwa wananchi wote ambao wamekuwa wakiishi na wagonjwa wa ukoma kujitokeza katika vituo vya huduma za afya kumeza dawa hizo za kujikinga na ukoma.

“Mtu mwenye ukoma na ambaye amekunywa dawa za kingatiba hawezi kusambaza ugonjwa huu na tunaweza kuishi na kushirikiana naye kufanya shughuli mbalimbali kimaendeleo” alisema Dkt Ndugulile na kuwaasa wananchi kuacha tabia za kuwanyanyapaa wenye ukoma.

Dkt Ndugulile ameipongeza taasisi ya GLRA kutoka Ujerumani inayojihusisha na kuwatunza watu wenye ukoma kwa kuwaanzishia miradi ya ujasiriamali na kuwaunganisha wahanga wa ugonjwa huo na jamii pamoja na kuwapongeza pia wagonjwa wa ukoma kujishughulisha na shughuli za uzalishaji kipato kuliko kuwa omba omba barabarani.

Awali akitoa salamu zake Rais wa Taasisi ya GLRA Bw. Patric Meisen amesema kuwa anafuraha kuona Tanzania na Ujerumani zikiwa na mahusiano mazuri na kuahidi kuendelea kuwasaida waathirika wa ugonjwa ukoma nchini.

“Tumekuwa tukifanya kazi na wataalam wa afya katika kuwatunza waathirika waugonjwa wa ukoma, hatujaishia hapo tuu, tumewasaidia waathirika wa ugonjwa huu kwa kuwapatia mitaji itakayowasaidia kujiongezea kipato ambacho kitawasaidia” alisema Bw. Meisen.

Siku ya Ukoma Duniani huadhimishiwa kila jumapili ya mwisho wa mwezi Januari, ambapo kwa mwaka huu 2019, maadhimisho hayo kitaifa yamefanyika Wilayani Mvomero, Mkoa wa Morogoro yakiwahusisha wadau mbalimbali wa Sekta ya afya huku kauli mbiu ikiwa ni “Tutokomeze Ubaguzi, Unyanyapaa na Chuki dhidi ya Waathirika wa Ukoma”

Mwisho

UKOMA HAUNA UHUSIANO NA IMANI ZA KISHIRIKINA - SERIKALI

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akitoa kingatiba kwa mtoto aliyekuwa akiishi na mgonjwa wa ukoma. Kingtiba hiyo itamlinda dhidi ya ugonjwa wa ukoma imezinduliwa na Dkt. Ndugulile katika maadhimisho ya siku ya Ukoma Duniani yaliyofanyika Wilayani Mvomero, Morogoro.

Baadhi ya Wanafunzi waliofika kusikiliza ujumbe kuhusu Ugonjwa wa Ukoma na kupata Kingatiba ya kuzuia ugonjwa huo ilikuwa ikitolewa katika viwanja vya kijiji cha Chazi, vilivyopo Wilaya ya Mvomero Mkoa wa Morogoro.

Wazee waliopata msaaada wa viatu vya kutembelea toka Taasisi ya GLRA inayowasaidai watu wenye ugonjwa wa ukoma nchini, wakifuatilia kwa makini, ujumbe kutoka kwa mgeni rasmi  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katika siku ya Ukoma Duniani.

Wakina mama wa Kijiji cha Chazi, Mvomero , Mkoa wa Morogoro wakifuatilia kwa makini, ujumbe kutoka kwa mgeni rasmi  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katika siku ya Ukoma Duniani.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (Wapili kushoto) akifuatilia kwa makini risala kutoka kwa Mwakilishi wa Wazee wenye ulemavu wanaoishi na Ukoma katika kijiji cha Chazi, Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kulia)akisalimiana na Mzee Anthony Martin (kushoto) wakati alipotembelea makazi ya wasiojiweza ya Chazi, Katika Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akishika kito cha Mtumbwi katika moja kati ya banda la maonesho katika kijiji cha Chazi, Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro

Picha ya pamoja, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulike (wa nne kutoka kushoto, walioketi) akiwa na wadau wa Sekta ya Afya nchini.



UKOMA HAUNA UHUSIANO NA IMANI ZA KISHIRIKINA - SERIKALI

Na WAMJW -Mvomero, Morogoro.

“Ugonjwa wa ukoma hausababishwi na imani za kishirika bali ni vimelea vya magonjwa ambavyo huingia ndani ya mwili na kusababisha ukoma”

Hiyo ni kauli ya Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipokuwa akizungumza na waathirika wa ugonjwa wa ukoma pamoja na wananchi katika maadhimisho ya siku ya Ukoma Duniani, wilayani Mvomero, katika Mkoa waMorogoro.

 Dkt. Ndugulile amewaasa wananchi kuachana na imani za kishirikina  kwa kuamini kuwa ya kwamba ugonjwa huo unahusika moja kwa moja na imani hizo za giza.

“Dhana ya kwamba ugonjwa huu ni wa kurogwa siyo kweli, ugonjwa wa ukoma hausababishwi na mtu kulogwa wala kutupiwa jini bali ni vimelea ambavyo huingia mwilini na kusababisha ugonjwa wa ukoma, ni watu kama mimi na wewe” anasema Dkt Ndugulile.

Aidha Dkt Ndugulile ametumia nafasi hiyo kuwaelimisha wananchi kuwa ugonjwa wa ukoma unatibika na kusema kuwa dawa za kutibu ugonjwa huo zipo na kuwaondolea hofu ya kuwa ugonjwa huo kutotibika. Hata hivyo Dkt. Ndugulile ametoa rai kwa wananchi wote kujitokeza mapema katika vituo vya kutolea huduma za afya kupata huduma za matibabu pindi wanapohisi kuwa na dalili za ugonjwa wa ukoma.

“Mtu yeyote ambaye anaanza kuona mabadiliko kwenye ngozi yake, anapata mabaka ambayo hayaelewi au kupoteza hisia pindi unapojigusa ni muda wa kwenda hospitalini kufanya uchunguzi na kama utagundulika kuwa na vimelea vya ugonjwa wa ukoma utapewa matibabu” alisisitiza Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile amewataka wananchi kuwa mabalozi wa kuwaelimisha watu wengine juu ya dalili na athari za ugonjwa wa ukoma. “Niwaombe ndugu wananchi tuendelee kutoa elimu kuhusiana na ugonjwa huu ni ugonjwa ambao tunaweza tukauzuia na tusiwe na athari kwenye jamii na tusingependa kuona kwenye zama hizi watu wanapata athari za kudumu na wanapoteza viungo, hisia katika sehemu za miili yao au kuharibika ngozi kwa sababu ya kutopata matibabu mapema” alifafanua Dkt Ndugulile.

Naibu Waziri huyo wa Afya amesema kuwa Serikali ipo katika hatua nzuri za kutokomeza ugonjwa wa ukoma nchini licha ya changamoto ambazo zipo katika baadhi ya maeneo sugu ambayo ugonjwa huo umeonekana kuwa ni tatizo. “Takwimu zinaonyesha kuwa takribani watu 1993 huugua ugonjwa wa ukoma kila mwaka huku mikoa ya Lindi, Rukwa, Mtwara, Pwani, Tanga, Geita, Dodoma, Tabora, Kigoma na Mkoa wa Morogoro ikiwa na idadi kubwa ya wagonjwa” alisema Dkt. Ndugulile.

Sasa hivi tumepiga hatua kubwa, tunajua jinsi gani ugonjwa unaambukizwa, na namna ya kuutibu pamoja na kujikinga dhidi ya maambukizi mapya, naamini kwa mikakati iliyopo tunaweza kuutokomeza ugonjwa huu.

Akizungumiza mikakati iliyopo Dkt Ndugulile amesema kuwa pamoja na elimu ambayo wamekuwa wakiitoa, Serikali imehamishia nguvu kwenda kwenye jamii moja kwa moja kuwabaini wagonjwa wa ukoma. “Hatusubiri watu watufate, tumewekeza nguvu nyingi kwenye jamii na kuwafikia huko huko maeneo wanayoishi” alisema Dkt Ndugulile.

Kwa upande mwingine, Dkt Ndugulile amezindua Mpango wa Kingatiba ya Ugonjwa wa Ukoma mahususi kwa wale ambao wamekuwa wakiishi na wagonjwa wa ukoma ili waweze kujikinga kutopata ugonjwa huo na kutoa rai kwa wananchi wote ambao wamekuwa wakiishi na wagonjwa wa ukoma kujitokeza katika vituo vya huduma za afya kumeza dawa hizo za kujikinga na ukoma.

“Mtu mwenye ukoma na ambaye amekunywa dawa za kingatiba hawezi kusambaza ugonjwa huu na tunaweza kuishi na kushirikiana naye kufanya shughuli mbalimbali kimaendeleo” alisema Dkt Ndugulile na kuwaasa wananchi kuacha tabia za kuwanyanyapaa wenye ukoma.

Dkt Ndugulile ameipongeza taasisi ya GLRA kutoka Ujerumani inayojihusisha na kuwatunza watu wenye ukoma kwa kuwaanzishia miradi ya ujasiriamali na kuwaunganisha wahanga wa ugonjwa huo na jamii pamoja na kuwapongeza pia wagonjwa wa ukoma kujishughulisha na shughuli za uzalishaji kipato kuliko kuwa omba omba barabarani.

Awali akitoa salamu zake Rais wa Taasisi ya GLRA Bw. Patric Meisen amesema kuwa anafuraha kuona Tanzania na Ujerumani zikiwa na mahusiano mazuri na kuahidi kuendelea kuwasaida waathirika wa ugonjwa ukoma nchini.

“Tumekuwa tukifanya kazi na wataalam wa afya katika kuwatunza waathirika waugonjwa wa ukoma, hatujaishia hapo tuu, tumewasaidia waathirika wa ugonjwa huu kwa kuwapatia mitaji itakayowasaidia kujiongezea kipato ambacho kitawasaidia” alisema Bw. Meisen.

Siku ya Ukoma Duniani huadhimishiwa kila jumapili ya mwisho wa mwezi Januari, ambapo kwa mwaka huu 2019, maadhimisho hayo kitaifa yamefanyika Wilayani Mvomero, Mkoa wa Morogoro yakiwahusisha wadau mbalimbali wa Sekta ya afya huku kauli mbiu ikiwa ni *“Tutokomeze Ubaguzi, Unyanyapaa na Chuki dhidi ya Waathirika wa Ukoma”*

Mwisho

Jumapili, 27 Januari 2019

UKOMA SI UGONJWA WAKURITHI AU KUROGWA



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisalimiana na Wazee ambao Waathirika wa ugonjwa wa Ukoma katika Kambi ya Wazee Nunge, Kigamboni Jijini Dar es salaam.

Na WAMJW - DSM

Jana nilitembelea Makazi ya Wazee Nunge, Kigamboni jijini Dar es salaam, ambapo pia nimepeana mikono na waathirika wa Ukoma ikiwa ni ishara ya kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu yetu ya maadhimisho ya Siku ya Ukoma 2019 ni Tutokomeze Ubaguzi, Unyanyapaa na Chuki dhidi ya Waathirika wa Ukoma.
Katika maadhimisho haya ninapenda kuwakumbusha watanzania kuwa, ukoma bado ni tatizo katika nchi yetu. Kwa mujibu wa Takwimu za 2017, jumla ya wagonjwa wapya 1,933 waligundulika kuwa na ukoma na hivyo kufanya kiwango cha ukoma kuwa watu 4 kwa kila watu 100,000. Takwimu hizi zinaifanya Tanzania kuendelea kuwa  miongoni mwa nchi 22 zenye wagonjwa wengi wa ukoma duniani. Nchi nyingine ni India, Indonesia, Brazil, Ethiopia, Msumbiji, Nigeria na DRC Congo.

Aidha kuna mikoa 10 ambayo hugundua wagonjwa wapya wengi zaidi. Mikoa hii ni Lindi, Mtwara, Pwani, Morogoro, Tanga, Dodoma, Geita, Kigoma, Rukwa na Tabora. Aidha zipo Wilaya 20 zenye kiwango kikubwa cha wagonjwa wapya wa Ukoma ambazo ni; Liwale, Lindi Vijijini, Nachingwea, Ruangwa, Nanyumbu, Masasi Mjini, Pangani, Mkinga, Korogwe, Mvomero, Kilombero, Morogoro Vijijini, Ulanga, Shinyanga Manispaa, Chato, Mafia, Rufiji, Kilwa, Nkasi na Mpanda.

Serikali kwa kushirikiana na wadau tutaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha ukoma unatokomezwa nchini. Hivyo nitoe wito wangu kwa jamii, wazazi na walezi kujenga tabia ya kuchunguza miili yetu na ya watoto wetu. Endapo utaona mojawapo ya dalili za ukoma ni muhimu kwenda kituo cha Tiba kwa uchunguzi bila kuchelewa. Dalili za Ukoma ni baka au mabaka mwilini yenye rangi ya shaba na hayana hisia, vijinundu kwenye ngozi au mishipa ya fahamu kuvimba, ganzi kwenye mikono au miguu.

Ugonjwa wa ukoma unatibika. Mgonjwa aliyeanza tiba hawezi kuambukiza mtu mwingine hivyo hakuna sababu ya kumtenga. Tiba ya Ukoma inapatikana nchini kote na hutolewa bila malipo kwa wagonjwa wote.
Aidha, ninaitaka jamii kuachana na imani potofu kuwa ukoma ni ugonjwa wa kurithi au kulongwa. Ukoma ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na vimelea vinavyoshambulia mishipa ya fahamu na huambukizwa kwa njia ya hewa pekee! Aidha ninawataka wagonjwa wa ukoma kuacha kuchelewa kujitokeza kupata matibabu hadi wanapopata ulemavu.

“Nirudie tena kusisitiza pale tunapoona mabadiliko yoyote yanajitokeza kwenye miili yetu twende mapema ktk vituo vya Tiba kuchunguzwa ili tupate matibabu” Nimalizie kwa kuwashukuru watoa huduma katika vituo vya afya kote nchini kwa juhudi kubwa wanazofanya kila siku kuhakikisha ugonjwa wa ukoma unatokomezwa nchini. 
Ninawashukuru wanahabari kwa kuendelea kuelimisha jamii kuhusu magonjwa mbalimbali ikiwemo ukoma. Pia, ninayashukuru mashirika mbalimbali ya ndani na nje ya nchi yanayounga mkono juhudi zetu za kutokomeza ukoma nchini.

“Tutokomeze Ubaguzi, Unyanyapaa na Chuki dhidi ya Waathirika wa Ukoma”.

Ummy Mwalimu, Mb
WAMJW
27 Jan. 2019.

TAASISI ZA DINI NI WADAU WAKUBWA WA SEKTA YA AFYA NCHINI

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile(mwenye shati jeupe) akikata utepe wakati wa uzinduzi wa Zahanati ya St. Mary's Mivumoni wilayani Pangani, Tanga. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Pangani Bi. Zainab Abdallah Issa, aliye kulia ni Mhashamu Baba Askofu Anthony Banzi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile (kushoto) akipokea pongezi toka kwa Mhashamu Baba Askofu Athony Banzi wa Jimbo Katoliki Tanga (kulia) mara baada ya kuzindua Zahanati ya St. Mary's Mivumoni iliyopo katika Wilaya ya Pangani Mkoani Tanga

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akipokea baraka toka kwa Mhashamu Baba Askofu Banzi wakati wa misa ya kubariki Zahanati ya St. Mary's Mivumoni iliyoko Wilayani Pangani, Tanga.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akikagua vifaa katika Zahanati ya St. Mary's Mivumoni iliyoko WIlayani Pangani, Tanga mara  baada ya kuizindua.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa WIlaya ya Pangani Bi. Zainab Abdallah Issa (kulia) mara baada ya kuwasili wilayani humo tayari kwa ziara ya kikazi.

NA WAMJW - Pangani, TANGA.

Pamoja na juhudi zinazofanywa na Serikali kuboresha sekta ya afya nchini, Taasisi za Dini bado ni wadau wakubwa wanaotegemewa na Serikali kuboresha Sekta hiyo kutokana na uwekezaji mkubwa wa miundombinu pamoja na utoaji wa  huduma ya afya nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipokuwa akizindua Zahanati ya St. Mary Mivumoni, inayomilikiwa na Masista wa Mtakatifu Francis wa Capuchin katika Kata ya Bushiri, Wilayani Pangani, Mkoa wa Tanga.

Dkt Ndugulile amesema kuwa Taasisi za Dini zina mchango mkubwa kwa maendeleo ya wananchi, kutokana na huduma za kijamii kama vile elimu na afya ambazo zimekuwa zikitolewa na madhebeu ya dini mbalimbali nchini na kusema kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha ushirikiano uliopo unaleta manufaa kwa wananchi.

Akitaja takwimu za idadi ya vituo vya kutolea huduma za afya nchini, Dkt Ndugulile amesema kuwa “Takwimu zinaonyesha kuwa katika Sekta ya Afya, makanisa yana zahanati zaidi ya 791, vituo vya afya 160 pamoja na hospitali 116” na kuendelea “huu ni mchango mkubwa sana ambao haupaswi kupuuzwa bali kuenziwa na sisi tunashukuru sana” alisikika akisema Dkt. Ndugulile.

Aidha baada ya ukaguzi wa jengo hilo la zahanati, Dkt Ndugulile amefurahishwa kuona zahanati hiyo ina vifaa vya kisasa ambavyo vinaifanya kituo hicho kuvuka sifa za kuwa zahanati kutaka mchakato wa kuipandisha kuwa kituo cha afya huku uongozi wa zahanati hiyo ukiombwa kushughulikia suala la kuboresha miundombinu ya majengo ili kupata wodi za kulaza wagonjwa.

“Zahanati mliyojenga ni kubwa, nzuri na ina nafasi, tutakuwa hatujatenda haki kama tutaiacha ikiwa katika ngazi ya zahanati, tuweke malengo ya kuifanya kuwa kituo cha afya unaanza ili huduma nyingi za matibabu ziwe zinapatikana katika eneo hili” Alisema Dkt Ndugulile.

Kwa upande wake Mhashamu Baba Askofu Anthony Banzi wa Jimbo Katoliki Tanga amesema kuwa ni jambo la faraja kuona Taasisi za Dini zikishirikiana na Serikali katika kutoa huduma kwa jamii.

“Tunaishukuru sana Serikali kwa kutoa nafasi kwa mashirika ya dini kuweza kushirikiana na Serikali katika kutoa huduma kwa jamii zikiwemo elimu, afya pamoja na huduma nyingine” alisema Mhashamu Baba Askofu Anthony Banzi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Pangani Bi zainab Abdallah Issa amesema kuwa uwepo wa zahanati hiyo itawasaidia wakazi wa mivumoni na Tarafa ya Madanga kwa ujumla kupata huduma za afya karibu na maeneo yao tofauti na awali ambapo walikuwa wanatumia muda mwingi kusafiri umbali mrefu kufata huduma za afya.

Kwa upande mwingine Dkt Ndugulile ametumia jukwaa hilo kuzungumzia mikakati iliyopo katika kuboresha sekta ya afya kwa upande wa bima ya afya ambapo amesema kuwa Serikali iko mbioni kuboresha mifumo ya bima ya afya itakayoiwezesha mwananchi mmoja na mwenza pamoja na wategemzi wanne kupata huduma za afya kwa gharama za shilingi 30,000, fedha ambayo itawaweza kupata huduma za matibabu kuanzia ngazi ya zahanati hadi hospitali ya Mkoa na kutoa rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kukata bima ya afya pindi utaratibu huo utakapo anza  rasmi.