Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 21 Machi 2019

HOSPITALI ZA MIKOA ZATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU ILI KUWEZA KUJIENDESHA

- Hakuna maoni
Kaimu Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii ambae pia ni Mbunge wa Biharamulo  Mhe. Oscar Mukasa akiteta jambo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati kamati hiyo ilipotembelea hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula akijibu hbaadhi ya hoja za Wabunge wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii wakati kamati hiyo ilipotembelea hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Mbunge wa Nzega mjini Hussein Bashe akisisitiza jambo wakati wa kikao cha kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii pindi ilipotembelea hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akijibu hoja mbele ya Wabunge wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii pindi kamati hiyo hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Kaimu Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii ambae pia ni Mbunge wa Biharamulo  Mhe. Oscar Mukasa (Watatu kushoto) akiongozana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (wapili kushoto) pamoja na Wabunge wengine kutoka kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii pindi kamati hiyo hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akieleza kuhusiana na unyanyasaji wa kijinsia, pindi alipotembelea wodi ya wagonjwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala wakati kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii pindi ilipotembelea hospitali hiyo kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Kaimu Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii ambae pia ni Mbunge wa Biharamulo  Mhe. Oscar Mukasa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula na Wabunge wengine kutoka kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii pindi kamati hiyo hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.


HOSPITALI ZA MIKOA ZATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU ILI KUWEZA KUJIENDESHA

Na WAMJW - DSM

Matumizi ya fedha za ndani katika Hospitali za umma yanaweza  kutumika katika kutatua uhaba wa watumishi katika ngazi zote na kuacha tabia ya kuisubiri Serikali kufanya kila kitu.

Hayo yamesemwa leo na Kaimu Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Huduma ya Maendeleo ya Jamii ambae pia ni Mbunge wa Biharamulo  Mhe. Oscar Mukasa wakati kamati hiyo ilipotembelea hospitali ya rufaa ya mkoa ya Mwananyamala katika kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Aidha,Mhe.Mukasa ameziasa Hospitali hizo kuwa wabunifu ili ziweze  kujiendesha katika kutoa huduma bora  kwa wananchi. 

"Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya ni moja ya maeneo ambayo nimewahi kushuhudia matumizi bora ya fedha za ndani katika kutatua ikama ya watumishi hata ngazi ya Madaktari na Wauguzi " alisema Mhe. Oscar Mukasa.

Akijibu hoja za baadhi ya Wabunge Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha vituo vya Afya na kujenga Hospitali za Wilaya ili kupunguza msongamano katika Hospitali za Rufaa za mikoa.

"Serikali kwa kushirikiana na mamlaka nyingine tumeamua kuboresha vituo vya Afya ili kupunguza mzigo mkubwa kwa Hospitali za Rufaa, na katika Wilaya ya Kinondoni kuna vituo vya afya viwili vinavyojengwa" alisema Dkt Ndugulile 

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa Serikali inatambua kuwa zaidi ya 60% ya watu wanaoenda kupata huduma za Afya ni watu wa misamaha, hivyo kupoteza zaidi ya Bilioni mbili kwa mwezi na hiyo ni kutoka Julai 2018 mpaka mwezi Februari 2019, hali inayorudisha nyuma shughuli za utoaji huduma bora za Afya. 

Aidha,  Dkt Ndugulile amesema kuwa Serikali ipo katika hatua ya  kuhakikisha kila mwananchi anakuwa na Bima ya Afya, ikiwa ni moja ya njia ya kuondokana na tatizo la misamaha kwa matibabu kwa wananchi. 

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula ameahidi kuendelea kuboresha Sera na miongozo ya Sekta ya Afya ili hali ya utoaji wa huduma bora kwa wananchi iwe ya kuridhisha na stahili kwa wananchi. 

Mwisho.

Jumanne, 19 Machi 2019

TANZANIA YATOA MSAADA KWA MSUMBIJI, ZIMBABWE NA MALAWI

- Hakuna maoni
Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Kimataifa Prof. Palamagamba Kabudi akimkabidhi boksi la dawa Balozi wa Malawi nchini Tanzania Mhe. Glad Chembe Munthali (Wakwanza kushoto), Watatu kushoto ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula wakati wakikabidhi msaada wa vyakula na madawa kwa nchi za Msumbiji, Malawi na Zimbabwe zilizopata janga la mafuriko. Tukio limefanyika leo katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (Wakwanza kulia) akionesha maboksi ya Dawa zinazotaraji kupelekwa katika nchi za Msumbiji, Malawi na Zimbabwe zilizopata janga la mafuriko.

Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Kimataifa Prof. Palamagamba Kabudi akiongozana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakiwa ndani ya ndege itayotumika kubeba dawa vyakula kwaajili ya msaada kwa nchi za Msumbiji, Malawi na Zimbabwe zilizopata janga la mafuriko.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wa kulia) akiongozana na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt Zainab Chaula baada yakujionea dawa zilizoingizwa ndani ya ndege yakijeshi itayopeleka misaada hiyo.


Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Kimataifa Prof. Palamagamba Kabudi (Wakwanza kushoto)  akiongozana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wapili kutoka kushoto)  wakati wakikabidhi msaada wa vyakula na madawa kwa nchi za Msumbiji, Malawi na Zimbabwe zilizopata janga la mafuriko. Tukio limefanyika leo katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es salaam.





Shughuli yakupakia Dawa na Vyakula katika ndege ikiwa tayari kuelekea katika nchi zilizopata majanga ya mafuriko (Zimbabwe,Malawi na Msumbiji).


TANZANIA YATOA MSAADA KWA MSUMBIJI, ZIMBABWE NA MALAWI 

Na WAMJW - DSM

Nchi ya Tanzania kupitia Rais wake Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli imedhihirisha ule msemo wa "undugu ni kufaana na si kufanana" baada kujitolea  msaada wa vyakula na madawa ili kuwasaidia wananchi walioathirika na mafuriko  ikiwa ni sehemu ya kudumisha umoja na ushirikiano baina ya nchi hizi.

Hayo yamejiri leo baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Prof. Palamagamba Kabudi kwa kushirikiana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kutoa msaada wa vyakula na madawa kwa nchi za Msumbiji na Malawi baada yakupata janga la mafuriko.

"Hawa ni ndugu zetu, jirani zetu,  tupo pamoja katika jumuia ya Maendeleo ya kusini mwa Afrika (SADC), kwahiyo Tanzania imeona ni vyema katika undugu wetu, umoja wetu na ujirani wetu tuweze kuwapelekea nchi hizi msaada wa madawa na chakula ikiwa ni sehemu ya kuwapa pole kwa maafa haya" alisema Prof.  Kabudi. 

Prof. Kabudi amesema kuwa Kimbunga hicho cha Idai kimepelekea mafuriko ambayo yameleta maafa makubwa sana, huku nchi ya Msumbiji jumla ya watu 221 wamepoteza maisha,  huku watu 88 kutoka Beira, watu 68 Manika, watu 51 Zambezi, na watu 19 kutoka Tete, huku zaidi ya watu 1000 hawana mahali pa kuishi.

Prof. Kabudi aliendelea kusema kuwa,  kwa upande wa Zimbabwe watu 98 kutoka mji wa Manipaland wamefariki,  huku watu 122 wakiwa wamefariki katika nchi ya Malawi, huku wengine wakiachwa katika hali ngumu. 

Aidha, Prof. Kabudi amewaasa Wafanya biashara na wananchi wengine walioguswa na maafa haya wasisite kutoa msaada kwa nchi jirani ambazo zimepata majanga Hayo kadiri ya uwezo wao.

Pia,  Prof. Kabudi aliendelea kuyaasa mashirika, makampuni na watu binafsi ambao wameguswa na hali ambayo imezikuta nchi za Msumbiji, Malawi na Zimbabwe waweze kuchanga na kuvikabidhisha vitu hivyo katika Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Afya ili viweze kupelekwa mahala husika. 

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa Wizara ya Afya imeandaa tani 24, ambazo ni sawa na tani (8) kwa kila nchi ambazo zitasaidia wananchi waliopata janga hilo kukabiliana dhidi magonjwa.

Mbali na hayo,  Waziri Ummy amesema kuwa kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Mawaziri wa Afya kutoka nchi za Zimbabwe na Malawi dawa kubwa zinazohitajika ni dawa za kuzuia maambukizi ya bakteria (antibiotics) na dawa kwa ajili ya magonjwa ya matumbo, (ORS) na dripu.

"tumeweka takribani aina tano za dawa za kuzuia maambukizi ya bakteria, tumeweka dawa kwa ajili ya magonjwa ya matumbo, Kama vile kuhara (ORS), tumeweka dawa kwa  ajili ya kutibu kwa kutumia maji (dripu), pia mashuka, magodoro, vyandarua, blanket na dawa za maumivu " alisema Waziri Ummy. 

Hata hivyo,  Waziri Ummy amesema kuwa kila nchi itapata tani  saba (7) za mchele kwa ajili ya Msumbiji na Zimbabwe na Malawi watapata tani 200 za mahindi ambayo yatatoka katika mkoa wa Mbeya ambayo upo karibu na nchi hiyo. 

Kwa upande wa Balozi wa Malawi nchini Tanzania Mhe. Glad Chembe Munthali ameishukuru nchi ya Tanzania kwa upendo na msaada waliouonesha kwa Malawi na kuahidi kufikisha salam hizo za upendo kwa rais wa Malawi huku akisisitiza kuwa Serikali ya Tanzania na ya Malawi zitaendelea kuwa marafiki milele. 

Mwisho

Jumamosi, 16 Machi 2019

WAGONJWA WATANO WAPANDIKIZWA FIGO BENJAMIN MKAPA

- Hakuna maoni
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiwa na Daktari Bingwa wa magonjwa ya Figo kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Charles Shija

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (Wakwanza kushoto) akiwa katika kikao na Madaktari bingwa kutoka shirika la Tokushukai kutoka nchi ya Japan baada yakufanikisha upandikizaji wa figo kwa kushirikiana na Madaktari kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma.

Kikao cha Madaktari bingwa kutoka shirika la Tokushukai kutoka nchi ya Japan na kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa, kilichoongozwa na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile baada yakufanikisha upandikizaji wa figo katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto akiwa na Madaktari bingwa kutoka shirika la Tokushukai kutoka nchi ya Japan na Wataalamu kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma baada yakujionea upandikizaji wa figo wenye mafanikio.

Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma


WAGONJWA WATANO WAPANDIKIZWA FIGO BENJAMIN MKAPA

Na WAMJW - DOM

Hospitali ya  Benjamin Mkapa imefanikiwa kupandikiza Figo jumla ya Wagonjwa saba tangu ilipoanza kufanya huduma hiyo kwa kushirikiana na Madaktari kutoka shirika la afya la Tokushukai lilopo nchi ya Japan.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto   wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za kibingwa za magonjwa ya Figo katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma.

Dkt.  Ndugulile amesema kuwa Idadi ya wagonjwa waliokwishapandikizwa figo hapa nchini ni 43, ambapo 38 wamepatiwa huduma hiyo kwenye hospitali ya Taifa Muhimbili na wagonjwa watano(5) hospitali ya Benjamin Mkapa

"Hivi navyoongea tayari mgonjwa mmoja amekwishapandikizwa figo na ameshatoka salama, yupo anaendelea kuangaliwa, lakini wana mpango wa kuwafanyia wengine wawili tutapokuwa tumekamilisha hili tutakuwa na wagonjwa saba ambao wamefanyiwa hospitali hii" alisema Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile aliendelea kusema kuwa, Serikali imelenga kuhakikisha kwamba inawajengea uwezo Wataalamu wa ndani kufanya upasuaji  wa kibingwa ili waweze kuwahudumia Watanzania bila msaada kutoka Wataalamu wa nje.

"lengo na kusudio ni kuhakikisha kwamba tunajenga uwezo wa ndani wa kuweza kufanya upasuaji huu" Alisema Dkt. Ndugulile

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali imeokoa zaidi ya kiasi cha shilingi bilioni 4.2 ambacho kingetumika katika matibabu ya wagonjwa 80 mpaka 100 ambao wangepelekwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

“Wagonjwa waliokwishapandikizwa figo hapa nchini ni 42, kama tungewapeleka  wagonjwa nje ya nchi ingegharimu serikali kiasi cha shilingi bilioni 4.2 kwa idadi hiyo ya wagonjwa.  80 mpaka 100, wakati huduma hii hapa nchini inagharimu kiasi cha shilingi milioni 21 kwa kila mgonjwa.” alisema Dkt. Ndugulile

Aidha, Dkt. Ndugulile amewashukuru Wataalamu kutoka shirika la Tokushukai kutoka nchi ya Japan kwa kujitoa na kuja kuwajengea uwezo Wataalamu wa ndani hali iliyosaidia kupunguza kiasi kikubwa cha fedha ambacho hutumika kwa ajili ya matibabu kwa wagonjwa wanaoenda kutibiwa nje.

"Kwa niaba ya Serikali ya Tanzania nimepita kuwashukuru na kuwapongeza,  kwa sababu badala ya kutusaidia sisi samaki, wenzetu wa Japan wameamua kutupatia sisi mishipi na kutufundisha jinsi ya kujua naamini ujuzi huu utatusaidia sana " alisema Dkt. Ndugulile.

Mwisho.

WATUMISHI TUISHI KWA UPENDO

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akisisitiza jambo wakati akiongea na Watumishi wa Sekta ya Afya, katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula akiongea na Watumishi wa Sekta ya Afya (Hawapo kwenye picha) wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma 

Naibu Katibu Mkuu TUGHE Taifa Eng. Amani Msuya akiwasilisha hoja za Wafanyakazi mbele ya Mgeni rasmi wa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula

Meza Kuu ikiongozwa na Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile (Watatu kutoka kushoto) wakati wakiimba wimbo wa kuhamasisha umoja na mshikamano wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi wa Sekta ya Afya ambao pia ni Wanachama wa TUGHE Taifa wakishikana mikono huku wakiimba wimbo wa kuhamasisha umoja na mshikamano, wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma.


Baadhi ya Watumishi wa Sekta ya Afya ambao pia ni Wanachama wa TUGHE wakifuatilia maelekezo kutoka kwa Mgeni rasmi ambae ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile(Hayupo kwenye picha) wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni mgeni rasmi wa Mkutano huo Dkt Faustine Ndugulile akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma

Picha ya pamoja ikiongozwa na Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula wakiwa na baadhi ya Wajumbe wa TUGHE Taifa akati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi kujadili bajeti ya Wizara ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Mipango Jijini Dodoma.


WATUMISHI TUISHI KWA UPENDO

Na WAMJW – Dodoma.
Watumishi watakiwa kudumisha upendo, umoja na mshikamano katika mahala pa kazi na kufanya kazi kwa bidii ili kutoa huduma iliyo bora.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile alipokuwa akizungumza na watumishi wa Sekta ya afya wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi lililofanyika jijini hapa

Dkt. Ndugulile amesema anaamini kuwa Wizara ya Afya itafika mbali zaidi ikiwa watumishi watafanya kazi kwa bidii kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma na kuheshimiana bila kujali utofauti wa vyeo baina ya watumishi.

“Kila mmoja amuheshimu mwenzake kwa sababu ana mchango katika haya yote tunayoyafanya na tunategemeana sana kwenye kazi zetu za kila siku” amesema Dkt. Ndugulile.

Aidha, Dkt. Ndugulile amewataka watumishi kuziheshimu nafasi za uongozi walizonazo sasa kwa kuzienzi na kuhakikisha wanafanya kazi ili kuthibitisha kuwa kweli wanastahili kuwa kwenye nafasi hizo.

“Bado kuna watumishi wengine hawajajitafakari katika nafasi zao, lugha tunazozitoa, kutojituma, tuache kufanya kazi kwa mazoea” alisema Dkt. Ndugulile.

Awali akizungumza na wajumbe wa mkutano, Mwenyekiti wa Baraza hilo ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Zainab Chaula amesisitiza watumishi kufanya kazi kwa umoja na kujitolea ili wote kwa pamoja kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Katika Mkutano huo wajumbe walipitia na kujadili masuala kadha wa kadha kuhusiana na Wizara ya Afya ikiwemo bajeti ya Wizara, mabadiliko ya sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii, Sera ya Afya, Bima ya Afya pamoja na masuala ya utendaji ndani na nje ya Wizara.

Mwisho




Ijumaa, 15 Machi 2019

SERIKALI YAOKOA BILION 4.2 KWENYE MATIBABU YA UGONJWA WA FIGO

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo wakati akitoa tamko la Siku ya Figo Duniani, lililotolewa leo katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na Waandishi wa Habari (Hawapo kwenye picha) wakati akitoa tamko la Siku ya Figo Duniani, lililotolewa leo katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma. Wakwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe na wamwisho ni Mwenyekiti wa Chama cha Magonjwa ya Figo nchini Dkt. Kisanga




Waandishi wa Habari waliojitokeza kumsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akitoa tamko la Siku ya Figo Duniani, lililotolewa leo katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma.



SERIKALI YAOKOA BILION 3.4 KWENYE MATIBABU YA UGONJWA WA FIGO

Na WAMJW-DOM.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Serikali imefanukiwa kuokoa kiasi cha Shilingi Bilion 4.2 ambacho kingetumika katika matibabu kwa Wagonjwa wa Figo nje ya Nchi.

Dkt. Ndugulile ameyasema hayo leo Machi 14 wakati akiongea na Waandishi wa Habari katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma ikiwa ni Siku ya Figo Duniani ambayo inaongozwa na kauli mbiu ya Afya ya figo kwa kila mmoja kila.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali imeokoa kiasi cha shilingi bilioni 4.2 ambacho kingetumika katika matibabu ya wagonjwa 80 mpaka 100 ambao wangepelekwa nje ya nchi kwaajili ya matibabu.

“Wagonjwa waliokwishapandikizwa figo hapa nchini ni 42, kama tungewapeleka  wagonjwa nje ya nchi ingegharimu serikali kiasi cha shilingi bilioni 4.2 kwa idadi hiyo ya wagonjwa.  80 mpaka 100, wakati huduma hii hapa nchini inagharimu kiasi cha shilingingi milioni 21 kwa kila mgonjwa.” Alisema Dkt. Ndugulile

Aidha, Dkt, Ndugulile amesema kuwa miongoni mwa sababu zinazochangia magonjwa ya figo ni pamoja na uzito wa kupindukia (obesity), matumizi makubwa ya sigara, unywaji wa pombe, uvutaji wa sigara,kutokufanya mazoezi na kunywa madawa kiholela hasa dawa za kupunguza maumivu.

Aliendelea kusema kuwa, magonjwa ya kisukari na shinikizo la damu ni magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha matatizo ya figo, magonjwa haya yakitambuliwa mapema yanaweza kudhibitiwa kwa matibabu na kuepusha madhara kwenye figo.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile amesema kuwa Kufikia Desemba mwaka 2018, jumla ya vituo 28 vyenye jumla ya wagonjwa 1050 vilikuwa vikitoa huduma ya usafishaji damu katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Arusha, Kilimanjaro na Dodoma.

Alhamisi, 14 Machi 2019

TAMKO LA NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, DKT. FAUSTINE NDUGULILE (MB) KWENYE MAADHIMISHO YA WIKI YA KUONGEZA UELEWA KUHUSU UGONJWA WA SHINIKIZO LA MACHO “GLAUCOMA”

- Hakuna maoni

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (MB)

 

TAMKO LA NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, DKT. FAUSTINE NDUGULILE (MB) KWENYE MAADHIMISHO YA WIKI YA KUONGEZA UELEWA KUHUSU UGONJWA WA SHINIKIZO LA MACHO “GLAUCOMA”

TAREHE 10-16 MARCH 2019
Ndugu wananchi,
Maadhimisho ya wiki ya elimu juu ya ugonjwa wa Shinikizo la Macho huadhimishwa duniani kote ikiwa ni Mpango ulioanzishwa na Chama cha Wagonjwa wa Shinikizo la Macho na Chama cha Wataalamu wa Afya wa Shinikizo la Macho kwa lengo kuu la kuongeza uelewa na kujenga ufahamu wa wananchi juu ya ugonjwa huu hatari wa Shinikizo la Macho, ujulikanao kwa kitaalam “Glaucoma” au Presha ya Macho, katika azma nzima ya kuzuia ulemavu wa kutokuona.  Tanzania, inaungana na nchi nyingine duniani kuadhimisha wiki hii muhimu kwa Afya ya Macho.
Maadhimisho haya yaliyoungwa mkono na wadau wa Afya ya Macho duniani, kwa mwaka huu, yanafanyika wiki ya tarehe 11 mpaka 17 mwezi wa Machi.
Ndugu wananchi,
Asilimia 2.8 ya watu wote wenye upungufu wa kutokuona vizuri, sawa na watu milioni 7 duniani wana Ugonjwa wa Shinikizo la Macho, kati yao, milioni 4.5 hawaoni kabisa.
Shinikizo la Macho ni kati ya vyanzo vinayoongoza kwa idadi ya watu wasioona duniani. Kwa Afrika, ugonjwa wa Shinikizo la Macho unachangia asilimia 15 ya watu wasioona. Ugonjwa wa Shinikizo la macho unaathiri zaidi watu wenye umri kuanzia miaka 40. Kwa Tanzania, inakadiriwa kuwa asilimia 4.2 ya watu wenye umri zaidi ya miaka 40 wana ugonjwa huu, sawa na watu 440,000. Kwa bahati mbaya, 70-90% ya watu wenye ugonjwa huu hawajijui iwapo wanao ugonjwa huu. Hii inatokana na watu kutokuwa na tabia ya kuchunguzwa Afya ya Macho kama inavyoshauriwa na wataalamu. Kwa kuwa ugonjwa huu huleta ulemavu wa kutokuona katika umri mdogo, Taifa hupoteza nguvu kazi.
Kwa mwaka 2018, ni watu 18,000 tu waliohudhuria kwenye vituo vyetu vya tiba wakiwa na tatizo la Shinikizo la Macho kulingana na vituo vilivyowasilisha taarifa zao. Idadi hii ni ndogo ikilinganishwa na watu walio kwenye hatari ya kuwa na ugonjwa huu ambao wapo kwenye jamii yetu na hawajagunduliwa.
Ndugu wananchi,
Ugonjwa huu wa Shinikizo la Macho ni moja kati ya kundi la Magonjwa ya Macho yanayoshambuliwa mshipa wa fahamu unaopeleka mawasiliano ya uoni kwenye ubongo (Neva ya Optiki) ili kuweza kutafsiri kile unachokiona. Ugonjwa huu husababisha upofu kwa taratibu sana kwa siku hadi siku bila dalili yoyote katika hatua ya awali na hivyo umepewa jina la Mwizi wa kimya kimya wa uwezo wa Macho kuona. Ili kugungua iwapo mtu ana ugonjwa huu, kuna umuhimu sana wa kupima macho angalau mara moja kila mwaka haswa kwa makundi yaliyo hatarini hata kama mtu haoni tatizo lolote kwenye macho.

Ndugu wananchi,
Maadhimisho ya Wiki ya Shinikizo la Macho kwa mwaka 2019 yamebeba kauli mbiu isemayo:
OKOA UONI WA MACHO YAKO
Sambamba na kauli mbiu hii, ujumbe mahususi kwa jamii na wadau wa huduma za macho na afya kwa ujumla ni:
“TAA YA KIJANI, NENDA KAPIME IWAPO UNA SHINIKIZO LA MACHO!
Kauli mbiu hii inatuhimiza wana jamii kwenda kwenye Vituo vya Tiba kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi iwapo una tatizo la Shinikizo la Macho. Kila mwana jamii anapaswa kupimwa Afya ya Macho yake angalao mara moja kwa mwaka.
Ndugu wananchi,
Aina ya Shinikizo la Macho linalopatikana zaidi kwa Waafrika ikiwemo Tanzania huwa na tabia zifuatazo; haina dalili kama maumivu katika hatua za mwanzo za ugonjwa, huwapata zaidi watu wenye umri wa miaka 40 na kuendelea, huambatana na tatizo la kutokuona mbali (myopia) na kuna uwezekano wa hadi asilimia 20 kuwepo katika familia. Ugonjwa huu husababisha upofu katika muda mfupi kutokana na kuanza kujitokeza katika umri mdogo na wagonjwa huwa na viwango vya juu sana vya presha ya maji ya macho.  Pamoja na kuwa ugonjwa huu mara nyingi hujitokeza kuanzia umri wa miaka 40, watu wengi zaidi hudhurika kadri umri wa kuishi unapokuwa mkubwa.
Ndugu wananchi,
Matibabu ya ugonjwa huu wa Shinikizo la Macho yanapatikana hapa nchini katika vituo vyetu vya tiba vyenye wataalamu wa Macho. Kuna Tiba ya dawa za kushusha Presha ya jicho lakini pia tiba kwa njia ya Upasuaji kwa wale ambao tiba ya dawa haitashusha presha kufikia kiwango cha presha kilicho salama. Iwapo Ugonjwa wa Shinikizo la Macho utagundulika mapema kabla ya mtu amepoteza uwezo wa kuona, tiba ya mapema itawezesha kuzuia hali ya upofu kwa asilimia kubwa.
Ndugu wananchi,
Serikali kwa kushirikiana na wadau inaendelea kuboresha miundombinu pamoja na kuongeza wataalamu wa afya ya macho, Vifaa na Vifaa Tiba ili kusogeza huduma za uchunguzi na Tiba kwa Matatizo ya Macho ikiwemo Shinikizo la Macho karibu zaidi na wananchi. Aidha, kwa kupitia Mwongozo wa Tiba na Orodha ya Dawa Muhimu, Serikali itasimamia na kuhakikisha hali ya upatikanaji wa Dawa za Macho katika vituo vyetu vya tiba inazidi kuimarika.

Ndugu wananchi,
Kama sehemu ya Maadhimisho ya Juma hili, kutakuwa na shughuli za Elimu ya Afya ya Macho pamoja na upimaji wa Afya ya Macho kwenye hospitali mbalimbali hapa nchini kwa wiki nzima ya kuanzia tarehe 10 hadi 16 Machi kwa wale wote watakaojitokeza kwenye kliniki za macho. Iwapo wewe au mmoja kwenye familia yako ana umri wa miaka 40 na kuendelea au kuna ndugu mwenye tatizo hili, mnahimizwa kufika katika hospitali iliyo karibu na wewe ili uweze kupimwa presha ya macho na vipimo vingine vya kuchunguza hali ya mshipa fahamu wa ndani ya jicho.  Aidha, pamoja na elimu kwa wagonjwa wote watakaojitokeza kwenye kliniki za macho, elimu kuhusu Shinikizo la Macho itaendelea kutolewa kupitia vyombo mbalimbali vya kuelimisha jamii.

Ndugu wananchi,
Napenda kutumia fursa hii kutoa wito kwa kila mmoja wetu kutumua Maadhimisho haya kwa kupima Macho. Ikumbukwe uwezo wa kuona uliopotea kutokana na Shinikizo la Macho hauwezi kurejeshwa tena hata baada ya tiba. Lengo kuu la matibabu ni kuzuia uharibifu usiendelee kutokea kwa kupunguza presha ya macho tu. Hivyo kupima mapema ni bora zaidi kuliko kusubiri ugundulike wakati madhara ya ugonjwa yameshajitokeza. Endapo utashindwa kupima kwa kipindi cha Juma hili la Maadhimisho, unaaswa kufika kwa ajili ya huduma ya upimaji katika hospitali zetu zote hapa nchini mara upatapo fursa hiyo.

“Tushirikiane kutokomeza ulemavu wa kutokuona”


ASANTENI KWA KUNISIKILIZA