Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 11 Julai 2019

DKT. NDUGULILE AONEKANA KUTORIDHISHWA NA UTAYARI WA MKOA WA KIGOMA KATIKA KUKABILIANA NA EBOLA

- Hakuna maoni

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akipimwa joto la mwili na mhudumu wa uwanja wa ndege mara baada ya kufika katika mkoa wa Kigoma ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake mkoani humo.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akioneshwa vifaa vya kujikinga na Ebola kutoka kwa mhudumu wa afya wa bandari ndogo ya Kibirizi Mkoani Kigoma wakati wa ziara yake mkoani humo kuangalia utayari wa mkoa katika kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akiwa na Mkuu wa Wilaya Samson Anga (kulia kwake) na viongozi wengine wakiwa wanatembelea maeneo mbalimbali katika Bandari ya Mkoa wa Kigoma mapema leo katika ziara yake ya kukagua utayari wa kukabiliana na Ebola mkoani humo.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile (Kulia) akitoa maelekezo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Paul Chaote jinsi ya kuweka vifaa na kupangiliana hema (Isolation centre) kwa ajili ya wagonjwa wa Ebola. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Samson Anga

Hema lilotengwa kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa Ebola katika bandari ndogo ya Kibirizi ikiyoko mkoani Kigoma.

Naibu Waziri Dkt. Faustine Ndugulile akikagua dawa na vifaa vinavyotumika katika kutibu mgonjwa wa Ebola, kulia ni Dkt. Praygod Swai wa Zahanati ya Bangwe iliyotengwa maalum kwa ajili ya kutibu wagonjwa wa Ebola akimuonesha vifaa hivyo. 

Na WAJMW-Kigoma

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile leo ametembelea baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Kigoma kuona utayari wa mkoa huo katika kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.

Dkt. Ndugulile ametembelea maeneo ya Bandari kuu ya Mkoa, Uwanja wa ndege, bandari ndogo ya Kibirizi na Zahanati ya Bangwe ambayo imetengwa maalumu kwa ajili ya kutoa matibabu kwa mtu atakayebainika kuwa na virusi vya Ebola.

Naibu Waziri ameonekana kutoridhishwa na utayari wa Mkoa katika kukabiliana na ugonjwa wa Ebola nchini huku akiitaka timu iliyoandaliwa chini ya Mkuu wa Wilaya Samson Anga na Mganga Mkuu wa Mkoa Paul Chaote kuendelea kutoa mafunzo kwa timu iliyoandaliwa jinsi ya kujikinga na kutoa huduma kwa mgonjwa atakayebainika.

“Hatuna mgonjwa wa Ebola ndani ya nchi, lakini kutokana na hali ya ugonjwa huu katika nchi jirani kuna umuhimu wa sisi kama nchi kuendelea kujipanga na kuhakikisha kwamba mifumo yetu yote imekaa vizuri kipindi mgonjwa atakapojitokeza, hivyo nakuomba Mkuu wa Wilaya na Mganga Mkuu wa mkoa kuendelea kusimamia hili”. Amesema Dkt. Ndugulile.

Mapungufu aliyobaini Dkt. Ndugulile ni pamoja na wahudumu kutozingatia kanuni walizofunzwa juu ya kujikinga na maambukizi pindi watakapokua wakihudumia mgonjwa, kutokua na vifaa vya kutosha kwa ajili ya wagonjwa wa Ebola kama vitanda kwenye vituo vya Isolation na watumishi kutokua na uelewa na utayari wa kutosha kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huu.

Dkt. Ndugulile yupo Mkoani Kigoma kwa ziara ya siku tatu ambapo pamoja na maeneo mengine atatembelea mpaka wa Manyovu ili kuona hali ya utayari ya mpaka huo kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa wa Ebola na kisha atatembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma. 


Mwisho

SERIKALI YATOA BILION 7 UJENZI WA JENGO LA WAZAZI HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akifuatilia ramani ya ujenzi wa mradi wa ujenzi wa ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongoza msafara wakati akifanya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongozana na Mkurugenzi  wa Hospitali  ya Rufaa ya Mkoa ya kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji wakati wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200.

Ujenzi wa mradi wa ghorofa sita wenye gharama ya shilingi Bilion 7, katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200 ukiendelea katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu pamoja na Mkurugenzi  wa Hospitali  ya Rufaa ya Mkoa ya kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji baada ya  ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya


SERIKALI YATOA BILION 7 UJENZI WA JENGO LA WAZAZI HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA.

Na WAMJW- MBEYA 

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya inajenga jengo la Wazazi lenye thamani ya shilingi Bilioni 7 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ya kuboresha huduma za Afya kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na nyanda za juu kusini.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya na ujenzi wa miradi katika Hospitali ya Rufaa ya kanda Mbeya. 

Waziri Ummy amesema kuwa Serikali imedhamiria kuboresha upatikanaji wa huduma za Afya nchini ikiwemo huduma za kibingwa ili kuondoa usumbufu kwa Wananchi wanaohitaji huduma hizo kwa kusafiri umbali mrefu i jambo linalopelekea gharama kubwa na usumbufu kwa wananchi. 

"Tunajenga jengo la wazazi na watoto wachanga la ghorofa sita, ambalo litakuwa na jumla ya vitanda 200, vyumba vitatu  vya upasuaji kwa ajili ya wanawake wajawazito ,vyumba sita kwa ajili ya uangalizi maalum (ICU) kwa wanawake wajawazito, pia vyumba  maalum vinne kwa ajili ya vitoto vichanga (NICU)" alisema Waziri Ummy. 

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amemwagiza Mkandarasi wa majengo hayo kuhakikisha wanaharakisha ujenzi wa majengo hayo ili wananchi waanze kupata huduma mapema jambo litalosaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto  nchini. 

Aidha, Waziri Ummy ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na nyanda za juu kusini kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya ili kurahisisha gharama za matibabu.

"Nitoe Wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na nyanda za juu kusini ili waweze kufurahia huduma nzuri lazima wajiunge na huduma za Bima ya Afya, Kuna NHIF Toto Afya kadi kwa mtu yoyote mwenye umri wa chini ya miaka 18 ni shilingi 50,400 huduma mwaka mzima ndani ya Mbeya na Tanzania kwa ujumla" alisema Mhe. Ummy Mwalimu 

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amesema kuwa katika kila wanawake 100, wanawake 85 wanajifungua bila matatizo yoyote, huku akisisitiza kukamilika kwa ujenzi huu kutasaidia kukokoa wanawake 15 waliobaki kutokana na huduma Bora zakibingwa zitakuwa zikitolewa.

Naye, Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kukubali kutenga fedha ili kujenga jengo la ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200 jambo litalosaidia kutatua changamoto ya ufinyu wa nafasi.

"Tunapenda kutoa shukurani za dhati kwa Serikali ya awamu ya tano, kwa kukubali kutenga fedha kupitia Wizara unayoiongoza ili kuweza kujenga jengo la ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta, ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200." Alisema Waziri Ummy 

Mwisho.

SERIKALI YASHUSHA NEEMA KWA WANANJOMBE

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka wakiongea na Wazee waliofika kupata huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe wakati alipofanya uzinduzi wa huduma  za Afya katika Hospitali hiyo.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitoa maelekezo kwa uongozi wa Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe  wakati alipotenbelea kukagua chumba cha kuhifadhia Dawa katika Hospitali hiyo, wakatikati (mwenye Koti jeupe) ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt. Kyambile.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikagua kadi inayoonesha kiasi cha dawa kilichopo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe pindi alipofanya ziara ya kuzindua Huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akieleza juu ya umuhimu wa kuwepo kwa mabango yanayohamasisha haki ya mgonjwa kupata  huduma  za Afya zilozo Bora wakati wa  uzinduzi wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, kushoto kwake (mwenye Koti jeupe) ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt. Kyambile.



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimjulia hali moja kati ya wagonjwa waliofika kupata matibabu kwa mara ya kwanza katika Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, ni baada ya kufanya  uzinduzi wa  huduma za Afya katika Hospitali hiyo, Kulia kwake (mwenye Koti jeupe) ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt. Kyambile.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka wakati wa uzinduzi wa Huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akipanda mti wa matunda (mpalachichi) ikiwa ni ishara ya kuhifadhi mazingira, shughuli iliyofanyika baada ya uzinduzi wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka akipanda mti wa matunda (mpalachichi) ikiwa ni ishara ya kuhifadhi mazingira, shughuli iliyofanyika baada ya uzinduzi wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ulioongozwa na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikabidhi ramani ya ujenzi wa majengo mengine mapya saba  kwa Mkandarasi, shughuli iliyofuata baada ya uzinduzi  wa huduma katika Hospitali hiyo ya Rufaa  ya Mkoa wa Njombe.

Moja kati ya vyumba vya Wagonjwa kilicho na vitanda pamoja na mashine zakutambua hali ya Mgonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, iliyoanza kutoa huduma rasmi Julai 10, baada ya Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kufanya uzinduzi huo

Wananchi waliojitokeza kushuhudia uzinduzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ulioongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliyeambatana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka (Hawapo kwenye picha)

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliyeambatana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka baada ya uzinduzi  wa huduma katika Hospitali hiyo ya Rufaa  ya Mkoa wa Njombe.



Na WAMJW-NJOMBE

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imeshusha neema kwa Wananchi wa Mkoa wa Njombe kwa kutoa kiasi cha shilingi Bilion 7.6 kwaajili ya ujenzi wa awamu ya pili ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ili kuboresha huduma kwa Wananchi.

Hayo yamejiri leo wakati wa zoezi la Uzinduzi wa huduma za Afya na lililoongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe iliyofunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Katika uzinduzi huo, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma za Afya katika Mkoa wa Njombe ikiwemo kujenga jengo la wazazi la ghorofa tatu, jengo la maabara, jengo la wagonjwa mahututi na jengo la upasuaji gorofa mbili, wodi za wagonjwa gorofa tatu, nyumba za Watumishi tano, pamoja na kichomea taka.

" Tunajenga jengo la wazazi la ghorofa tatu, tunajenga jengo la jengo la maabara, tunajenga jengo la wagonjwa mahututi na jengo la upasuaji gorofa mbili, tunajenga wodi za wagonjwa gorofa tatu, tunajenga jengo la kufulia, tunajenga kichomea taka na tunajenga nyumba za watumishi tano" alisema Waziri Ummy.

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amemwagiza Mkandarasi wa Hospitali hiyo kuhakikisha anakamilisha ujenzi wa majengo hayo hayo ndani ya miezi kumi ili wananchi wa Mkoa wa Njombe waanze kufaidika na huduma za Afya katika Hospitali hiyo, huku akiwatoa hofu wananchi kuwa pesa zote zipo tayari.

Mbali na hayo, Waziri Ummy mewaasa Wananchi kupambana dhidi ya magonjwa yasiyo yakuambukiza kama Kisukari, shinikizo la damu, Saratani na magonjwa ya Moyo kwa kubadilisha mtindo wa maisha ikiwamo ulaji mlo sahihi , kuacha uvutaji wa sigara na tumbaku, kuacha unywaji wa pombe kupita kiasi pamoja na kutofanya mazoezi mara kwa mara.

Aidha, Waziri Ummy ametoa with kwa vijana kujiepusha na mambo ambayo yatapelekea kipata maambukizi ya VVU, huku akiweka wazi kuwa maambukizi mapya ya VVU ni 82,000 kila mwaka nchini Tanzania, huku katika kila watu 100, watu 40 ni vijana wenye umri kati ya 15 hadi 24 umri ambao ni nguvu kazi ya taifa.

"Tunatambua kwamba kuna maambukizi makubwa ya virusi vya Ukimwi Mkoani Njombe,lazima tuzingatie kanuni za kujikinga na maambukizi ya VVU, kujizuia kufanya mapenzi kwa vijana hasa kwa wasichana ambao muda wao haijafika, pili kuwa mwaminifu kwa mwenza wako au mpenzi wako na tatu kutumia kinga" alisema Waziri Ummy

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka amewatoa hofu wananchi wa Mkoa wa Njombe kwa kuweka wazi kuwa huduma za Afya katika Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe haitoathiri utoaji huduma katika Hospitali ya Kibena iliyokuwa Hospitali ya Mkoa, ambayo kwa sasa imerudishwa chini ya Halmashauri ya Mji wa Njombe.

"Na mimi ntahakikisha wale Watumishi ambao tilikubaliana waje kwenye Hospitali hii, waje na nguo zao , vifaa vyote waviache Kibena na huduma ya Kibena iendelee, na kazi ya Hospitali hii Mhe. Ummy Mwalimu na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wataweka vifaa vyote vitakavyohitajika na huduma zitaendelea" alisema Mhe. Olesendeka

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Mhe. Edwirn Mwanzinga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kupitia Wizara ya Afya kwa kuongeza bajeti ya dawa na vifaa tiba jambo linalosaidia kuokoa kwa kiasi kikubwa maisha ya Wananjombe.

Mwisho.

Jumatano, 10 Julai 2019

ASILIMIA 90 YA WAGONJWA WA MOYO WANATIBIWA TANZANIA

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi kizimia moto kilichotolewa na kampuni ya SUKOS KOVA Foundation kwa kushirikiana na kampuni ya One Extreme Solution leo katika ukumbi wa taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Jumla ya vizimia moto 12 vya kisasa vimefungwa katika maeneo mbalimbali ya taasisi hiyo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile akizungumza na mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa moyo wa kufungua kifua katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa ziara yake kutembelea taasisi hiyo pamoja na kupokea vizimia moto vilivyotolewa na kampuni ya SUKOS KOVA Foundation kwa kushirikiana na kampuni ya One Extreme Solution leo Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile akizungumza na mtoto aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kupatiwa matibabu ya moyo Asha Luhomo wakati wa ziara yake kutembelea taasisi hiyo pamoja na kupokea vizimia moto vilivyotolewa na kampuni ya SUKOS KOVA Foundation kwa kushirikiana na kampuni ya One Extreme Solution leo Jijini Dar es Salaam

Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi na Mkurugenzi wa Kampuni ya SUKOS KOVA Foundation Suleiman Kova akimkabidhi Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndungulile moja kati ya vizimia moto 12 vilivyotolewa na kampuni yake kwa kushirikiana na kampuni ya One Extreme Solution kwa ajili ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo katika ukumbi wa Taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Prof. Mohamed Janabi

Na.WAMJW,Dsm

Asilimia tisini ya wagonjwa wanaokabiliwa na matatizo ya moyo waliokuwa wanatibiwa nje ya nchi, hivi sasa wanatibiwa ndani ya nchi kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya kikwete (JKCI).
Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile, alipofanya ziara kwenye hospitali hiyo ambapo alitembelea  jengo la watoto lililofanyiwa ukarabati hivi karibuni.

Dkt.Ndugulile alisema Serikali inaendelea kufanya maboresho ya sekta ya afya kuanzia huduma za msingi hadi za kibingwa kwa kuwezesha vituo zaidi ya 352 kutoa huduma za upasuaji wa dharura wa kumtoa mtoto tumboni.

Alisema hivi sasa ujenzi wa hospitali 67 za wilaya unaendelea katika maeneo mbalimbali nchini na kwamba tangu Uhuru kumekuwako na hospitali 70 za Wilaya pekee, hivyo idadi itaongezeka.
“Nawapongeza sana JKCI kwa maboresho makubwa mliyofanya katika jengo ya watoto ni ya kiwango kikubwa sana, hongereni sana, hivyo hatutarajii hospitali kama hii iwe inatibu magonjwa madogo madogo ambayo yanaweza kutibiwa kwenye hospitali za rufaa za wilaya au mikoa,” alisema.
Aliongeza kusema kuwa, katika miaka minne ya uongozi, serikali imeweza kupiga hatua kubwa kwani ikiwamo kupunguza idadi ya wagonjwa wengi walikua wanatibiwa nje ya nchi.

“Kwa hatua hii, tumeweza kupunguza gharama za matibabu nje ya nchi tulikuwa tunaweza kuhudumia watu wachache lakini kwa kuwa yanapatikana ndani wananufaika watu wengi, kwa gharama ile ile nje ya nchi angetibiwa mtu mmoja, ndani wanatibiwa watu wapatao watatu,” alibainisha.

Alisema mafanikio hayo ni matokeo ya hatua za kuwajengea uwezo kwa kuwapatia mafunzo madaktari wa ndani (wazalendo) ambapo sasa wanaweza kufanya upasuaji mkubwa wao wenyewe.
“Hivyo, Serikali itaendelea kuwapatia mafunzo wataalam wa afya na kuwapatia vibali kwenda kujifunza ama kusoma nje ya nchi ili kuleta mapinduzi makubwa katika sekta ya afya nchini na kuweza kuwatibia wananchi.

Aidha, katika ziara hiyo Dkt. Ndugulile alipokea vifaa vya kuzima moto vipatavyo kumi na mbili vya hospitali hiyo kutoka kampuni ya SUKOS Kova Foundation inayomilikiwa na Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi, Suleiman Kova, kwa kushirikiana na kampuni ya One Extreme Solution ya hapa nchini.

Dkt. Ndugulile alisema Watanzania wengi wanafariki wakati wa uokoaji kwani watu wengi hawana elimu ya uokoaji kwani zipo kanuni zinazotumika wakati wa  kumuokoa mtu anayepata ajali.
MWISHO

Jumatatu, 8 Julai 2019

TANZANIA IMEFANIKIWA KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA VIKOPE

- Hakuna maoni
Mratibu wa Taifa wa Mpango wa Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele Dkt. Upendo Mwingira akifungua mafunzo ya Kimataifa ya uchukuaji wa Takwimu za  ugonjwa wa Vikope(Trakoma) yanayofanyika jijini Arusha

Wataalam wa Macho kutoka mataifa mbalimbali wakisikiliza hotuba ya ufunguzi wa mafunzo hayo

Picha ya pamoja ya washiriki wa mafunzo hayo kutoka Wizara ya afya,wadau mbalimbali wa macho nchini pamoja na nchi mbalimbali Duniani zikiwemo Afrika Mashariki,Magharibi na Kati


Na.WAMJW,Arusha

Tanzania imeweza kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa Trakoma kutoka wilaya 71 hadi
sita ambazo zitaendelea na umezaji kingatiba

Hayo yamesemwa leo na Mratibu wa Taifa wa Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele kutoka Wizara ya Afya Dkt.Upendo Mwingira wakati wa mafunzo ya Kimataifa ya uchukuaji wa takwimu za ugonjwa wa vikope(Trakoma) yanayofanyika jijini hapa.

Dkt.Mwingira amesema kuwa kama nchi inajivunia kwa mafanikio makubwa kwani hivi sasa wilaya 65 hazihitaji tena kingatiba kulingana na vigezo vilivyowekwa na Shirika la Afya Duniani (WHO).

"Lengo la WHO hadi ifikapo mwaka 2020 tuwe tumeweza kutokomeza ugonjwa wa Trakoma kama tatizo la kijamii,kwamba hatutaki maambukizi mapya"Alisisitiza Dkt.Mwingira.

Aidha,alisema mwaka 2010 katika tathimini Tanzania kulikua na makadirio ya wagonjwa wa vikope  takribani 160,000,lakini kutokana na jitihada za Wizara ya Afya  hadi Julai 2018 inakadiriwa wagonjwa hao wamepungua mpaka kufikia 17,000.

Hata hivyo Dkt.Mwingira alisema zoezi la kusawazisha vikope hapa nchini linaendelea zaidi ya mikoa kumi sasa hivi katika halmashauri zenye maambukizi.

Mafunzo haya yanahusisha wataalam wa macho kutoka mataifa mbalimbali Duniani na kwa nchi za Afrika yanahudhuriwa na nchi za afrika Mashariki,Magharibi na Kati.

Ijumaa, 5 Julai 2019

DKT. NDUGULILE ATAKA UONGOZI BORA NA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA ILI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA NCHINI.

- Hakuna maoni

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na Waganga Wafawidhi wa Hospitali za Rufaa za Mikoa wakati akifunga Kikao kazi kilichofanyika kwa siku tano na kupitisha maazimio ya kuimarisha huduma Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa tiba toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Grace Maghembe akiongea wakati wa kilele cha kikao kazi cha Waganga Wafawidhi kilichofanyika Jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimkabidhi cheti cha pongezi kwa uongozi bora na usimamizi kwa Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi Dkt. Yustina Tizeba wakati akifunga kikao cha waganga wafawidhi kilichofanyika Jijini Dodoma.


Picha mbalimbali zikimuonesha Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikabidhi vyeti kwa Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Amana Dkt. Meshack Shimwela wakati akifunga kikao cha waganga wafawidhi kilichofanyika Jijini Dodoma. Hospitali ya Rufaa ya Amana imeongoza na kupata vyeti vitatu ikiwa ni pamoja na kuongoza kupunguza vifo vya mama na mtoto, uongozi bora na mikakati endelevu ya kukusanya mapato.


Picha za pamoja za Viongozi wa Wizara ya Afya wakiongozwa na Naibu Waziri Dkt. Faustine Ndugulile, Katibu Mkuu Dkt. Zainab Chaula na Wakurugenzi wa Idara Mbalimbali wakati wa kufunga kikao cha Waganga Wafawidhi kilichofanyika katika ukumbu wa Mwalimu Nyerere Chuo cha Mipango Jijini Dodoma.

Na WAJMW-DOM

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewataka Waganga wafawidhi kutekeleza maazimio waliyopitisha katika kikao kazi kilichofanyika kwa siku tano Jijini Dodoma.

Dkt. Ndugulile amesema hayo wakati akifunga kikao hicho kilichohusisha Waganga Wafawidhi, Makatibu Tawala wa Halmashauri na Manispaa pamoja na wataalamu mbalimbali wa sekta ya afya nchini waliohudhuria kikao hicho.

“Ninatambua kuwa katika kikao hiki tumepitia mwongozo wa uendeshaji wa Hospitali za Rufaa za Mikoa na kuweka mipango na mikakati endelevu kwa timu za uendeshaji wa Hospitali hizi, ninaomba sana muende mkatekeleze ili kuimarisha Hospitali zetu za Rufaa za Mikoa. Amesema Dkt. Ndugulile.

Katika kikao hicho Waganga Wafawidhi wameweka maazimio ambayo yataratibiwa katika Hospitali zote za Rufaa za Mikoa nchini ikiwa ni pamoja na kuimarisha mifumo ya kukusanya mapato na kuondoa mianya ya upotevu wa mapato, kuimarisha na kuendelea kuzijengea uwezo timu za uendeshaji za Hospitali za rufaa za Mikoa katika kusimamia rasilimali watu, fedha, miundombinu n.k. Kuweka mikakati endelevu ya kupunguza vifo vya mama na mtoto, kila Hospitali kuandaa mkakati wa kununua vifaa na vifaa tiba vitakavyowezesha huduma za kibingwa kutolewa wakati wote, pamoja na kila Hospitali kuja na ubunifu/mikakati ya kukabiliana na upungufu wa watumishi katika maeneo yao kwa kushirikiana na wadau wa mikoa yao.

Aidha, Dkt. Ndugulile ametoa maagizo kwa Waganga Wafawidhi kutekeleza mambo muhimu katika maeneo yao ya kazi ikiwa ni pamoja na kuwa na mfumo wa uongozi na utawala, upatikanaji wa watumishi wenye sifa stahiki katika kada zote, uimarishaji wa miundombinu kwa ajili ya huduma zilizokusudiwa, upatikanaji wa vifaa na vifaa tiba na vitendanishi pamoja na uimarishaji wa matumizi ya teknolojia, taarifa za afya na mawasiliano.

Pamoja na hayo Naibu Waziri amewapongeza Waganga Wafawidhi kwa kushiriki kikao hicho na kuwataka kwenda kutekeleza maazimio waliyopitisha ili kuboresha Hospitali za Rufaa za Mikoa katika maeneo tofauti yaliyokusudiwa ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Kabla ya kufunga kikao Dkt. Ndugulile alitoa vyeti vya ubora wa huduma na pongezi, ambapo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Katavi Dkt. Yustina Tizeba alipata cheti cha pongezi kwa muongozo wa maono, uongozi bora na usimamizi huku Hospitali ya Rufaa ya Amana ikipata vyeti vitatu vya ubora ikiwa ni pamoja na kuongoza katika kupunguza vifo vya mama na mtoto, uongozi bora na mikakati endelevu ya kukusanya mapato na kuwepo kwa vifaa na vifaa tiba vinavyotumika katika huduma za kibingwa.

MWISHO

MAKATIBU TAWALA WAOMBWA KUENDELEA KUZISIMAMIA HOSPITSLI ZA RUFAA.

- Hakuna maoni

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula akisema jambo kwa wajumbe wa kikao cha Viongozi wa Hospitali za Rufaa za Mikoa kilichofanyika jana Jijini Dodoma.

Mwakilishi wa Makatibu Tawala Mikoa Bi. Zena Said, Katibu Tawala Mkoa wa Tanga akisema jambo katika kikao kazi cha Viongozi wa Hospitali za Rufaa za Mikoa kilichoandaliwa na Wizara ya Afya na kufanyika katika ukumbi wa mikutano Chuo cha Mipango Dodoma.

Makatibu Tawala Mikoa nchini Tanzania wakisikiliza mada zinazowasilishwa katika Kikao Kazi na Viongozi wa Hospitali za Rufaa za Mikoa.


Na WAMJW - Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula amewataka Makatibu Tawala nchini kuendelea kuzisimamia Hospitali za rufaa za mikoa ambazo kwa sasa zinasimamiwa na Wizara ya Afya.

Dkt. Chaula amesema hayo alipokutana na Makatibu Tawala kutoka Mikoa ya Tanzania Bara katika Kikao Kazi cha Viongozi wa Hospitali za Rufaa za Mikoa kinachoendela kufanyika katika ukumbi wa Chuo cha mipango Jijini Dodoma.

“Licha ya Hospitali hizi kuhamishiwa usimamizi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)  lakini bado zipo kwenye maeneo yenu, tunawategemea nyie Makatibu Tawala kuzisimamia hospitali hizi.” Amesema Dkt Chaula.

Dkt. Chaula amesema kuwa ni dhahiri lengo lilikuwa ni jema tuu kutoka kwa Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli, kwamba Hospitali zisimamiwe na Wizara ya Afya ili ziweze kuwa na mahusiano ya moja kwa moja na Wizara ya Afya ambayo ndiyo Wizara mama inayotunga Sera na Miongozo pamoja na kusimamia Wadau.

Naye Mwakilishi wa Makatibu Tawala wa Mikoa katika kikao hicho Bi. Zena Said amempongeza Katibu Mkuu Wizara ya Afya kwa kuandaa kikao hicho cha kihistoria ambacho hakijawahi kufanyika kabla.

“Hili ni jambo la busara, pamoja na kwamba hizi Hospitali zimeondolewa kwenye mamlaka za Tawala za Mikoa lakini bado kuna mambo mengi ambayo bado tunayafanya kwa niaba ya Wizara” amesema Bi. Zena na kuendelea “Sisi kama viongozi tupo mikoani hatuwezi kukaa kuangalia mambo yakiharibika tukisema hizi Hospitali sio za kwetu”

Bi. Zena Said amesema kuwa Bado wanawajibika kwa njia moja au nyingine kuzisimamia kwa ajili ya kuleta ustawi kwa wananchi.

Kikao hicho cha kihistoria kinafanyika kwa mara ya kwanza tangu kuhamishiwa kwa usimamizi wa  Hospitali za Rufaa za Mikoa tarehe 25, Novemba 2017 ambacho kitakuwa endelevu kila mwaka huku kikiwakutanisha viongozi wa hospitali, Waganga wakuu wa Mikoa pamoja na watendaji na wadau wa Sekta ya Afya nchini.

Mwisho

Alhamisi, 4 Julai 2019

TANZANIA BILA DENGUE INAWEZEKANA

- Hakuna maoni
Timu ya Wahamasishaji wa masuala ya Afya, kutoka Manispaa ya Kinondoni wakichanganya dawa, ikiwa ni moja kati ya maandalizi ya kuanza zoezi la upuliziaji wa viuadudu katika maeneo yenye mazalia ya mbu wa Dengue.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu (aliyevaa buti) akiongoza zoezi la upuliziaji wa viuadudu katika Manispaa ya Kinondoni

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akieleza jambo mbele ya viongozi wa Manispaa wakati wa zoezi la upuliziaji wa viuadudu katika Manispaa ya Kinondoni. Wakatikati ni Mbunge wa Kinondoni kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Maulid Mtulia.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu (aliyevaa buti) wakielekea katika eneo lenye mazalia ya  mbu wanaosababisha homa ya Dengue, zoezi limefanyika katika eneo la Msisili Manispaa ya Kinondoni.

Moja kati ya eneo la mazalia ya mbu wanaosababisha ugonjwa wa homa ya Dengue, ililopo eneo la Msisili Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.


TANZANIA BILA DENGUE INAWEZEKANA

Na WAMJW-DSM

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. @ummymwalimu leo ametembelea katika Manispaa ya Kinondoni ikiwa ni muendelezo wa ziara yake kukagua utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa kwa Mikoa/Halmashauri ya kupambana dhidi ya ugonjwa wa Dengue.

Katika ziara hiyo Waziri @ummymwalimu ameridhishwa kwa kiasi kikubwa na jitihada zinazochukuliwa na Manispaa ya Kinondoni za kupambana na Ugonjwa wa Homa ya Dengue hali iliyochangia kupungua kwa Idadi ya Wagonjwa kutoka Wagonjwa 604 Mwezi Mei hadi kufikia Wagonjwa 450 Mwezi Juni. 

“ Nafurahi kuona kwamba idadi ya Wagonjwa wa homa ya Dengue katika Wilaya ya Kinondoni, Mwezi Mei kulikuwa na Wagonjwa ambao wamepima na kuthibitishwa 604, lakini mwezi wa tano Wagonjwa wamepungua hadi 450” Alisema Waziri Ummy

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa, takwimu za Kitaifa za Wizara ya Afya, mwezi Mei tulikuwa na idadi ya Wagonjwa wa homa ya Dengue 3170, na wamepungua Mwezi wa Sita hadi kufikia Wagonjwa 1446, hali inayotoa matumaini katika kuimaliza vita hii ya homa ya Dengue.

Aidha, Waziri Ummy amewapongeza Watendaji wa Sekta ya Afya katika Manispaa ya Kinondoni kwa hatua wanazoendelea kuchukua, ikiwemo kununua Viuadudu vya kuangamiza mazalia ya mbu na kununua mashine mpya za kupuliza dawa (motorised sprayers), katika maeneo yenye mazalia ya mbu.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amesisitiza juu ya ushiriki wa Wananchi katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa homa ya Dengue, huku akieleza kuwa mapambano dhidi ya mbu wa Dengue yatasaidia kupunguza magonjwa mengine kama Malaria, Matende, Chikungunya, Zika, Homa ya Manjano.

“Ushiriki wa Wananchi ni muhimu sana katika kupambana na ugonjwa wa Dengue, tukipambana na Dengue, kwa upande mwingine tunakuwa tunapambana na ugonjwa wa Malaria, Matende, Chikungunya, Zika, Homa ya Manjano, kwhiyo ni lazima tuhakikishe kila mtu anashiriki katika kupambana dhidi ya mbu.” Alisema Waziri Ummy.

Kwa upande wake Mbunge wa Kinondoni kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Maulid Mtulia amekazia kwa kuwahasa Wananchi juu ya ushiriki katika vita hii dhidi ya ugonjwa wa Dengue na kusisitiza kuwa Serikali haiwezi kushinda vita hii bila ushirikiano wa Wananchi.

Nae, Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamin Sitta amesema kuwa Jumla ya shilingi Milion 132 kwaajili ya zoezi lakutokomeza homa ya Dengue, 90 zimetumika kwaajili ya zoezi zima la upuliziaji wa viuadudu katika mazalia ya mbu, huku 42 kwaajili ya kununua Mashine za kubwa ya upuliziaji wa dawa hizo.

“Tumetumia gharama ya takribani Milion 90 kwaajili ya upuliziaji katika kila kata na tupo mbioni kuongeza Milioni 42 kwajili ya mashine kubwa yenye uwezo wa kusambaza mara moja kwa kata 10, kwahiyo kwa ujumla tutakuwa tumetumia takribani Milion 132 kwaajili ya zoezi la kuhakikisha tunatokomeza ugonjwa wa Dengue.” Alisema Mhe. Benjami Sitta.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni Dkt.  Festo amesisitiza kuwa Huduma za vipimo vya homa ya Dengu zinapatikana katika vituo vya Serikali vya Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala na Hospitali ya Lugalo bila malipo na vituo binafsi bei elekezi isizidi shilingi 50,000/

“Huduma hizi za vipimo zinapatikana kwenye vituo vyetu, na katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala na Hospitali ya Lugalo bila malipo, lakini katika vituo binafsi, bei elekezi isizidi 50,000/ kwa kipimo cha Dengue” alisema Dkt. Festo

Pia, amewaasa Wananchi kuwahi katika vituo vya Afya, pindi waonapo dalili za ugonjwa wa homa ya Dengue na kuachana na mawazo potofu ya matibabu ya Dengue kama majani ya mpapai kwani yanawezapelekea kupata matatizo mengine yakiafya.

Mwisho.

Jumatano, 3 Julai 2019

DKT. NDUGULILE AISIFU HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI KWA KUFANIKISHA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akitoa maelekeozo kwa Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma wakati alipofanya ziara ya kutembelea ujenzi wa Hospitali ya Mpya ya Wilaya hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya Bi. Mwanahamisi Mkunda, Mkurugenzi wa Halmashauri Dkt. Fatuma Mganga na kulia ni Mbunge viti maalum wa Dodoma Bi. Felista Bula, mbunge wa jimbo la Bahi Omary Badwel na Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt. Philipina Philipo.

Naibu Waziri Dkt. Faustine Ndugulile akimuangalia fundi mwana mama aliyekua anapaka rangi katika majengo ya Hospitali Mpya ya Wilaya ya Bahi wakati alipofanya ziara ya kutembelea Hospitali hiyo mapema leo.
Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulie akielekeza jambo kwa viongozi wa wilaya wakati alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa Hospitali mpya ya wilaya ya Bahi mapema leo. 



Baadhi ya majengo ya Hospitali mpya ya Wilaya ya BAHI.

Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndugulile akihesabu mabati ya ujenzi wa Zahanati ya kijiji cha Chonde Wilayani Bahi wakati alipofanya ziara ya kutembelea maendeleo ya ujenzi wa zahanati hiyo leo.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na wananchi wa kijiji cha Chonde waliofika katika mkutano ambao ulitanguliwa na ziara ya ukaguzi wa zahanati ya kijiji hicho.

NA WAMJW-BAHI

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameusifu uongozi wa Wilaya ya Bahi kwa kutekeleza ujenzi wa Hospitali mpya ya Wilaya hiyo ukiwa umekamilika kwa asilimia zaidi ya 90.

Dkt. Ndugulile amesema hayo mapema leo baada ya kutembelea ujenzi wa Hospitali hiyo ambao umefikia hatua za mwisho na kuridhishwa na hatua iliyofikia hadi sasa huku akiusifu uongozi wa Halmashauri chini ya Mkuu wa Wilaya Bi. Mwanahamisi Mkunda kwa kuonesha ushirikiano mkubwa katika kutekeleza majukumu yao.

“Napenda kuwapongeza sana kwa kazi nzuri na ushirikiano mnaoonesha katika kutekeleza mradi huu, ninaamini majengo haya yakikamilika tutaanza kutoa huduma kwa sababu OPD tunayo, jengo la upasuaji, Maabara, jengo la Radiolojia na pia huduma ya Mama na Mtoto tunaweza kuanza nazo”. Amesema Dkt. Ndugulile.

Baada ya kutembelea majengo mbalimbali ya Hospitali hiyo Dkt. Ndugulile ameonesha kuridhishwa na ujenzi huo na kutoa maelekezo kwa uongozi wa Wilaya kuhakikisha huduma zinaanza kutolewa haraka iwezekanavyo ili kusogeza huduma za matibabu karibu na wananchi wa eneo hilo.

Aidha, Dkt. Ndugulile ametembelea ujenzi wa Zahanati ya kijiji cha Chonde Wilayani Bahi na kushangazwa na kasi ndogo ya ujenzi ambao ulianza toka mwaka 2007 lakini haujakamilika mpaka leo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya uhaba wa fedha.

Dkt. Ndugulile ameonyesha kutoridhishwa na gharama za ujenzi ambao unagharimu Shilingi Milioni 90 mpaka kukamilika. Kufuatia hatua hiyo ameagiza ujenzi wa zahanati hiyo kutumia utaratibu wa Force Account na kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Dkt. Fatuma Mganga kuleta wataalamu kwa ajili ya kuhakiki gharama za vifaa vinavyohitajika.

Pamoja na hayo Naibu Waziri huyo ameahidi kutoa mifuko 50 ya Saruji ili kuchangia gharama za ujenzi huku akitoa miezi mitatu ya ukamilishaji wa ujenzi huo. Kufuatia hatua hiyo Mkuu wa Wilaya ya Bahi Bi. Mwanahamisi Mkunda amemuahidi Naibu Waziri kukamilika kwa ujenzi wa zahanati ndani ya muda uliowekwa na amechangia mifuko 10 ya saruji huku Mbunge wa Viti Maalum wa Dodoma Bi. Felista Bula akichangia Mifuko 20 ili kuchochea kasi ya ujenzi na huduma zianze kutolewa ifikapo Septemba mwaka 2019.

MWISHO