Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 24 Julai 2019

BALOZI WA UFARANSA AFURAHISHWA NA HUDUMA ZA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI MUHIMBILI

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Mikrobiolojia na Immunolojia chuo cha  MUHAS Prof. Said Aboud, wakati alipofanya ziara katika chuo hicho ili kujionea maendeleo ya shughuli zakitafiti katika chuo hicho, Kulia kwa Waziri Ummy ni Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier na wamwisho ni  Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Andrea Pembe.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akiambatana na Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier na Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Andrea Pembe, wakwanza  kushoto ni Mtaalamu wa Mikrobiolojia na Immunolojia chuo cha  MUHAS Prof. Said Aboud.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akipokea maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Mikrobiolojia na Immunolojia chuo cha  MUHAS wwakati alipofanya ziara katika chuo hicho ili kujionea Maendeleo ya shughuli zakitafiti katika chuo hicho, Kulia kwake ni Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier.

Wataalamu mbali mbali wa masuala ya tafiti pamoja na Watumishi wa Sekta ya Afya, wakifuatilia hotuba kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara katika chuo cha MUHAS ili kujionea Maendeleo ya shughuli zakitafiti

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu pamoja na Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier na Wataalamu mbali mbali wa masuala ya tafiti pamoja na Watumishi wa Sekta ya Afya baada ya ziara ya kujionea Maendeleo ya shughuli zakitafiti katika chuo cha MUHAS.


BALOZI WA UFARANSA AFURAHISHWA NA HUDUMA ZA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI MUHIMBILI

NA WAJMW-DSM

Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Bw. Frederic Clavier amefurahishwa na huduma zinazotolewa katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi cha Muhimbili.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu mapema leo wakati wa kukagua na kufuatilia maendeleo ya ushirikiano kati ya nchi ya Ufaransa na Tanzania katika masuala ya utafiti mafunzo na utoaji wa huduma za Afya katika chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Muhimbili.

Kwa kiasi kikubwa Waziri Ummy pamoja na Balozi huyo wameridhishwa kwa kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Wataalamu katika chuo hicho ikiwemo utafiti, mafunzo na utoaji wa huduma za afya.

“Binafsi tumeridhishwa na kazi kubwa na nzuri zinazofanywa na wataalamu wetu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi cha Muhimbili, katika masuala ya utafiti tumeona kazi kubwa inayofanyika katika utafiti juu ya dawa za kuua wadudu”. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema hakuna sheria nzuri za udhibiti wa dawa hizi nchini hivyo Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Muhimbili na Serikali ya Ufaransa itaendelea kufanya utafiti na kuona jinsi gani itapunguza madhara ya utumiaji wa dawa za kuua wadudu kwa binadamu.

Pamoja na hayo, Waziri Ummy amefurahi kuona ushirikiano ambao Serikali ya Ufaransa inaendelea kuutoa katika huduma za watu wenye tatizo la Seli nundu “Sickle Cell".

“kwa Mujibu wa Tafiti tuna jumla ya watu 200,000 nchini ambao wana tatizo la seli nundu na watoto ambao wanazaliwa ni 11,000 kwahiyo tumejadiliana na Serikali ya Ufaransa kuona ni jinsi gani tunaweza kuboresha huduma za ugunduzi ili tuweze kuwatambua mapema watoto pale wanapozaliwa na tatizo hili na kuhakikisha huduma za matibabu zinapatikana ikiwepo dawa ya kupunguza maumivu inapatikana”. Amesema Waziri Ummy.

Kufuatia hatua hiyo Waziri Ummy amemuomba Balozi Frederic kushawishi makampuni makubwa ya  kutengeneza dawa kutoka Ufaransa yaweze kusaidia katika kuzalisha dawa ya kupunguza maumivu ya Seli nundu inapatikana kwa Watanzania wengi.

Mwisho

Jumatano, 17 Julai 2019

WAZIRI UMMY ATOA MIEZI 3 KUKAMILISHA MRADI WA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA GEITA.

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wakatikati) akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel (Kulia kwa Waziri  Ummy) wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita,

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wapili kushoto) akipokea maelezo ya ujenzi kutoka kwa Mhandisi  kutoka Wizara ya Afya Eng. Mbuya (wakwanza kushoto) wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (watatu kushoto) akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel (wakwanza kushoto) pamoja na Mhandisi kutoka TBA (wapili kushoto) wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita,


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (aliyevaa kitambaa) akitoa maelekezo kwa Mhandisi  kutoka Wizara ya Afya Eng. MBuya wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita, Wakwanza kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel

Baadhi ya miradi ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita yenye thamani ya shilingi Bilion 2.5 inayotarajia kumalizika ndani ya miezi mitatu


WAZIRI UMMY ATOA MIEZI 3 KUKAMILISHA MRADI WA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA GEITA. 

Na WAMJW- GEITA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amefanya ziara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua miradi ya ujenzi wa Hospitali za Rufaa za mikoa nchini. 

Katika ziara hiyo Waziri Ummy amemwagiza Mkandarasi kutoka TBA Mkoa wa Geita kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha ndani ya miezi mitatu mradi huo unaisha ili huduma za Afya zianze kutolewa ifikapo Disemba 1, 2019.

"Nimemtaka Mkandarasi afanye kazi usiku na mchana ikiwezekana tukamilishe ujenzi huu hata mwezi wa kumi mwishoni, lengo langu nataka tarehe 1 mwezi Disemba 2019, tunaanza kutoa huduma hapa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita" alisema Waziri Ummy. 

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali imetoa kiasi cha shilingi Bilion 2.5 ili kukamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa Hospitali hiyo, ambayo itajenga jengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la Maabara, jengo la upasuaji pamoja na jengo la mionzi.

Hata hivyo, Waziri Ummy amesema kuwa licha ya kuwepo changamoto ya upungufu wa Watumishi katika Sekta ya Afya, Wizara ya Afya imepata kibali cha kuajiri Watumishi wengine kutoka Wizara ya Utumishi jambo litalosaidia kupunguza Uhaba wa Watumishi katika Sekta ya Afya. 

Waziri Ummy aliendelea, kwa kuwataka Wakurugenzi kujiongeza ili kupambana na uhaba wa Watumishi katika ngazi ya Mkoa, ikiwemo kuajiri baadhi ya Watumishi kupitia mapato ya ndani ili kupunguza changamoto ya uhaba wa Watumishi, huku akitoa Wito kwa vijana waliomaliza vyuo kujitolea katika Hospitali ili kuongeza uzoefu zaidi. 

Mbali na hayo, Waziri Ummy amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa kuendelea kujali Afya za Watanzania kwa kuboresha Sekta ya Afya ikiwemo kuboresha miundombinu ya Hospitali na kuhakikisha Dawa, vifaa na vifaa tiba vinapatikana.

Nae, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amemuomba Waziri Ummy kuanza kwa awamu ya pili ya ujenzi wa Hospitali hiyo ili kupata wodi ambazo zitatumika kulaza wagonjwa wataofika kupata huduma za Afya. 

"Uwepo wa wodi ndio utatoa taswira ya kuwa Hospitali hii kuwa ni Hospitali ya Mkoa, ili mtu akipata Rufaa aweze kulazwa na kuchukuliwa vipimo" alisema Mkuu wa Mkoa Mhandisi Robert Gabriel.

#tunaboreshaafya 

Mwisho.

Jumanne, 16 Julai 2019

SERIKALI YATOA BILION 5.7 UJENZI WA MAABARA NA JENGO LA UPASUAJI - SIMIYU

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongoza na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka na Watumishi wengine wa Serikali wakati alipofanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo  la upasuaji na jengo la naabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akifuatilia kwa makini ramani ya ujenzi  wa jengo la wazazi na jengo la upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu kutoka kwa Mhandisi kutoka Wizara ya Afya Bw. Mbuya (Wakulia kwa Waziri Ummy).  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka (wakwanza kulia) na Watumishi wengine wa Serikali wakati alipofanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo  la upasuaji na jengo la maabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongozana na Mhandisi Mbuya kutoka Wizara ya Afya wakishuka kwenye ngazi wakati akiendelea na ukaguzi wa mradi wa jengo la upasuaji na jengo la maabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akisaini kitabu cha wageni baada ya kumaliza ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la upasuaji na jengo la maabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu, Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Anthony Mtaka, akifuatiwa na Mhandisi kutoka Wizara ya Afya   Eng Mbuya.


Moja kati ya mradi wa ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji ikiwa na gharama ya shilingi Bilion 5.7 ikiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu



Na WAMJW- SIMIYU

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto yatoa kiasi cha shilingi Bilion 5.7 kwaajili ya ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji ikiwa ni awamu ya pili, baada yakuzinduliwa kwa awamu ya kwanza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli, Mwezi Agasti 2018.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.

Waziri Ummy amesema kuwa, uwekezaji huu umeweka alama kubwa kwa Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt.John Pombe Magufuli kwa kuwasogezea huduma bora zakibingwa kwa Wananchi wa Simiyu jambo litalosaidia kuondoa usumbufu katika kutafuta huduma hizo.

"Kipekee kabisa nimshukuru Mhe. Rais katika mwaka huu 2018/2019 ameipatia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu kiasi cha shilingi Bilion 5.7 kwaajili ya ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji lakini pia litakuwa na huduma za mionzi" alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy ameongeza kuwa Serikali tayari umeshapata kiasi cha shilingi Bilion 2.2 kwaajili ya ujenzi wa jengo la mama na mtoto ili huduma za kulaza Wagonjwa zianze kutolewa katika Hospitali hiyo.

"Tuna pesa nyingine kiasi cha shilingi Bilion 2.2 ukiacha zile Bilion 5.7 tutaanza kujenga jengo la mama na mtoto ili sasa tuanze kulaza wagonjwa, kwasababu ukiangalia wagonjwa wengi ni Wanawake na Watoto, lakini hili kingine la wodi nyingine nalibeba pia" alisema Waziri Ummy.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amewaagiza Watumishi wa Sekta ya Afya kuzingatia maadili na weledi wa kazi zao ikiwemo matumizi mazuri ya lugha kwa wagonjwa pindi wakiwa kupata huduma za Afya.

"Niinawataka tena Wauguzi kuzingatia maadili na weledi wa kazi zao ,ikiwemo kutumia lugha nzuri, lugha yenye busara na lugha yenye upendo kwa wagonjwa, asili ya muuguzi ni upendo na heshima na kumthamini mtu ambae unampa huduma " amesema Waziri Ummy.

Hata hivyo, Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa Serikali haitokuwa na msamaha na Mtumishi yeyote ambae atabainika ametoa lugha chafu kwa wagonjwa ikiwemo kujihusisha na masuala ya Rushwa kwa kuwachukulia hatua kali ikiwemo kufuta reseni zao.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwa changamoto kubwa ambayo itakuwepo katika ujenzi wa Hospitali hiyo ni uwepo wa wodi, hivyo amemwomba Waziri Ummy kuharakisha ujenzi wa wodi ili huduma zianze mara moja.

"Wakati wote tunapokuwa tunakuja changamoto kubwa ilikuwa ni wodi, na hata wagonjwa wanaokuja wanaulizia kuhusu wodi za kulala wagonjwa " amesema Mhe. Mtaka.

#tunaboreshaafya


Mwisho .

RAIS MAGUFULI AMWAGIZA WAZIRI UMMY KUFUATILIA MALIPO YOTE YA SERIKALI KWA WAGONJWA WA NJE YA NCHI

- Hakuna maoni
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuonesha ishara ya uzinduzi rasmi wa miradi 7 yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando. Kulia kwake ni Baba Askofu Mhashamu Askofu Renatus Nkwande huku kushoto kwake ni Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu akifuatiwa na Waziri wa Nishati Medard Kalemani na mwisho ni Naibu  Waziri wa Ardhi Mhe. Angelina Mabula

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimpa mkono Baba Askofu Mhashamu Askofu Renatus Nkwande baada ya kuzindua mradi wa NHIF ikiwa ni moja kati ya miradi 7 iliyozinduliwa yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akieleza jambo wakati wa uzinduzi rasmi wa miradi 7 yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitoa taarifa ya Wizara ya utekelezaji mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (hayupo kwenye picha) wakati wa uzinduzi rasmi wa miradi 7 yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando.

Baadhi ya viongozi wa Serikali wakifuatilia Maelekezo kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (hayupo kwenye picha) wakati wa uzinduzi rasmi wa miradi 7 yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando.

Wananchi waliojitokeza kumsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wwakati wa uzinduzi wa miradi 7 yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando.


Na WAMJW-MWANZA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli amemwagiza Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kufuatilia malipo yote ya Wagonjwa wanoenda kutibiwa nje ya nchi ili kubaini ubadilifu unaofanywa na baadhi ya watu wasiowaaminifu.

Rais Magufuli ameagiza hilo leo wakati akizindua miradi Saba ya huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya Ziwa Bugando yenye thamani ya shilingi Bilion15, jambo litalosaidia kurahisisha upatikanaji wa huduma bora kwa ukaribu pamoja na kuokoa kiasi cha fedha miongoni mwa wanaohitaji huduma. 

"Na kwasababu Waziri wa Afya yupo hapa, akafuatilie malipo yote ambayo tunatakiwa kulipa, kule nje , akikuta kunamalipo yakulipa mtu ambae hakuwa mgonjwa aliyejihifadhi huko, akazilipe mwenyewe " alisema Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 

Rais Magufuli amesema kuwa baadhiya Watendaji waliona kupeleka Wagonjwa nje ya nchi kwaajili ya matibabu ni fursa yakujipatia kipato, jambo lililokuwa linapelekea hasara kubwa kwa nchi ya Tanzania kutokana na malipo kwa baadhiya watu wasiostaholi.

" Hata kupeleka kwa wagonjwa nje kwa Watanzania ilikuwa ni dili, ilikuwa ni fursa kwa Watendaji, wapo watu waliokuwa wanapewa vibali kwenda kutibiwa India lakini anaumwa mafia, ilikusudi apate safari na msindikizaji, bill zote zinaletwa kwa Serikali " alisema Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 

Dkt. Magufuli aliendelea kusema kuwa ni lazima tujenge nidhamu katika nchi, huku akisisitiza kuwa Serikali haijakataza kupeleka wagonjwa nje ya nchi, huku akisisitiza kuwa wagonjwa wanaostahili kupelekwa kwa matibabu nje ya nchi ni wale walioshindikana ndani ya nchi.

Aidha, Waziri Ummy ameagiza kuboresha uzalishaji wa oksijeni ili kuhakikisha zinazalishwa kwa wingi jambo litalosaidia kuokoa kiwango kikubwa cha mapato kinachopotea kwa kuagiza nje ya nchi, pia itasaidia kuongeza ajira kwa wananchi wa Tanzania. 

"Ninawaomba ndugu zangu, tengenezeni oksijeni nyingi, panueni uzalishaji ili Wizara ya Afya iagize hapa hapa Bugando ili vijana wanaomaliza famasi hapa hapa Bugando wapate ajira hapa yakutengeneza Oksijeni " alisema Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 

Nae, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu amesema kuwa hadi kufikia juni 30, 2019 Serikali ina jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya vya umma 5756 (71%),Taasisi za Dini 923 (11%) na vituo vya watu binafsi ni 1440 (18%). 

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa, pia Serikali, ina Jumla ya Vituo vya Afya vya Mashirika ya Dini ikiwemo Hospitali Teule za Wilaya vipatavyo 43, ambazo zinapata ruzuku (OC) kiasi cha shilingi 30,704,000/= kwa mwezi na mishahara kiasi cha Tshs.1.8 bilioni kwa mwezi kwa ajili ya watumishi 2600. 

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali imepunguza malalamiko ya upatikanaji wa dawa kwa Wananchi na katika hospitali ya rufaa ya Bugando hii ni kufuatia ongezeko la bajeti ya dawa hadi kufikia Tshs.270 bilioni, huku Serikali ikitoa kiasi cha Tshs. milioni 100 kila mwezi kwa ajili ya kununulia dawa, huku Mwaka 2015/16 walikuwa wanapata Tshs.534 milioni na Mwaka 2018/19 wanapata Tshs.1.5 bilioni.

Naye, Mkurugenzi wa Hospitali ya kanda ya Bugando Prof. Abel Makubi akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, amesema  kwa  kipindi cha miaka minne wamefanikiwa kuboresha huduma za afya na kukamilisha miradi saba ambayo ni  kitengo cha  saratani, mahututi, upasuaji, oksijeni na viwanda vidogo ambavyo vitakuwa vinazalisha dawa kwa ajili ya wagonjwa.

Ameongeza kuwa asilimia 70 ya wagonjwa wa saratani ambao walikuwa wanakwenda katika Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam walikuwa wanatoka Kanda ya Ziwa, hivyo imewapunguzia gharama na usumbufu wa kusafiri kutafuta huduma hiyo.

#tunaboreshaafya

Jumapili, 14 Julai 2019

ZIARA YA MAFUNZO 5S-KAIZEN KWA WAGENI KUTOKA WIZARA YA AFYA NA WATUMISHI YA BANGLADESH

- Hakuna maoni
Muuguzi Mkuu - Hospital ya Rufaa ya Mkoa- Amana,Beauty Mwambebule akitoa maelezo kwa wageni kutoka nchi ya  Bangladesh namna mfumo wa KAIZEN  unavyofanya kazi katika Hospital hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Mratibu wa Hospitali za Rufaa za Mikoa kutoka Wizara ya Afya -Idara ya Tiba -Kitengo cha Uratibu wa Hospitali za Rufaa za Mikoa,Dkt. Angelina Clarisa Sijaona (kushoto) akiwa na wageni kutoka nchi ya Bangladesh akiwaonesha mambo mbalimbali yanayo tumika kwenye  mfumo wa KAIZEN  katika Hospital Amana  jijini Dar es Salaam.

Wangeni kutoka Bangladesh wakiwa katika Hospital ya Amana iliyopo Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam

Picha ya pamoja ya maofisa kutoka wizara ya afya,hospitali ya rufaa ya mkoa Amana pamoja na wageni kutoka Bangladesh baada ya kutembelea hospitali ya Amana

Na.WAMJW,Dsm
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mradi wa Kuimarisha Hospitali za Rufaa za Mikoa (RRHMP) katika kuendelea kuziwezesha Hospitali za Rufaa za Mikoa  ilipanga kukaribisha wageni kutoka katika nchi mbalimbali za Afrika ili kubadilishana uwezo katika utekelezaji wa 5S-KAIZEN katika kuboresha utoaji wa huduma za afya nchini.

Kulingana na mpango kazi wa mwaka huu, Mradi ukishirikiana na Wizara ya Afya ulitarajia kupokea wageni kutoka Wizara ya Afya na watumishi wa sekta hiyo kutoka nchini Ghana  (7) na Bangladesh (7) kwa ajili ya ziara ya mafunzo ya Falsafa ya 5S-KAIZEN-TQM pamoja na wawakilishi wa JICA wawili kutoka kila nchi.  Pamoja na hao, tulitegemea kupokea watumishi wa Afya 14 kutoka nchi za kiafrika zikiwemo Uganda, Kenya, Malawi, Liberia, Siera Leoni, Sudan, Zambia, Zimbabwe na Benin.

Tayari wageni wote hawa waliishafika na kupata mafunzo kutoka haya.

Wiki hii, tumewapokea wageni kutoka Katika Wizara ya Afya na watumishi 7 wa sekta na wawakilishi wawili wa JICA-Bangladesh. Wageni hawa watakuwepo hapa nchini kwa wiki moja  Katika kipindi hicho watapata mafunzo ya KAIZEN na leo wametembelea Hospitali za Rufaa ya Mkoa Amana na kesho wanategemewa kutembelea Hospitali za Taifa Muhimbili.

Lengo la ziara hii ni kubadilishana uzoefu katika utekelezaji wa 5S-KAIZEN-TQM katika hospitali zetu kwa ajili ya kujifunza na kuiga mazuri ya kujifunza watakaporejea nchini kwao. Aidha, Timu zetu zinategemewa kupata nafasi ya kupata uzoefu kutoka kwa nchi zinazotutembelea.

Falsafa ya 5S-KAIZEN-TQM hii inalenga kuboresha mazingira ya kutoa huduma za afya  na kukidhi mahitaji ya wateja wetu, wale wa ndani na wa nje.

Kwa ujumla wake, falsafa ya 5S-KAIZEN-TQM hii inarahisha kazi, inahakikisha usalama kwa wateja wa ndani na nje na inapunguza upotevu wa rasilimali, napunguza makosa na inapunguza gharama za uendeshaji.

Kwa Hospitali za Rufaa za Mikoa ambayo wanaitimia falsafa hii wameweza kufanya vizuri katika kutoa huduma bora, kuongeza katika mapato na wafanyakazi kufurahia mazingira yao ya kazi.

Ni falsafa inayoweza kutumika katika maeneo mbalimbali pamoja na viwandani.

Alhamisi, 11 Julai 2019

DKT. NDUGULILE AONEKANA KUTORIDHISHWA NA UTAYARI WA MKOA WA KIGOMA KATIKA KUKABILIANA NA EBOLA

- Hakuna maoni

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akipimwa joto la mwili na mhudumu wa uwanja wa ndege mara baada ya kufika katika mkoa wa Kigoma ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake mkoani humo.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akioneshwa vifaa vya kujikinga na Ebola kutoka kwa mhudumu wa afya wa bandari ndogo ya Kibirizi Mkoani Kigoma wakati wa ziara yake mkoani humo kuangalia utayari wa mkoa katika kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile akiwa na Mkuu wa Wilaya Samson Anga (kulia kwake) na viongozi wengine wakiwa wanatembelea maeneo mbalimbali katika Bandari ya Mkoa wa Kigoma mapema leo katika ziara yake ya kukagua utayari wa kukabiliana na Ebola mkoani humo.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile (Kulia) akitoa maelekezo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Paul Chaote jinsi ya kuweka vifaa na kupangiliana hema (Isolation centre) kwa ajili ya wagonjwa wa Ebola. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Samson Anga

Hema lilotengwa kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa Ebola katika bandari ndogo ya Kibirizi ikiyoko mkoani Kigoma.

Naibu Waziri Dkt. Faustine Ndugulile akikagua dawa na vifaa vinavyotumika katika kutibu mgonjwa wa Ebola, kulia ni Dkt. Praygod Swai wa Zahanati ya Bangwe iliyotengwa maalum kwa ajili ya kutibu wagonjwa wa Ebola akimuonesha vifaa hivyo. 

Na WAJMW-Kigoma

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile leo ametembelea baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Kigoma kuona utayari wa mkoa huo katika kukabiliana na ugonjwa wa Ebola.

Dkt. Ndugulile ametembelea maeneo ya Bandari kuu ya Mkoa, Uwanja wa ndege, bandari ndogo ya Kibirizi na Zahanati ya Bangwe ambayo imetengwa maalumu kwa ajili ya kutoa matibabu kwa mtu atakayebainika kuwa na virusi vya Ebola.

Naibu Waziri ameonekana kutoridhishwa na utayari wa Mkoa katika kukabiliana na ugonjwa wa Ebola nchini huku akiitaka timu iliyoandaliwa chini ya Mkuu wa Wilaya Samson Anga na Mganga Mkuu wa Mkoa Paul Chaote kuendelea kutoa mafunzo kwa timu iliyoandaliwa jinsi ya kujikinga na kutoa huduma kwa mgonjwa atakayebainika.

“Hatuna mgonjwa wa Ebola ndani ya nchi, lakini kutokana na hali ya ugonjwa huu katika nchi jirani kuna umuhimu wa sisi kama nchi kuendelea kujipanga na kuhakikisha kwamba mifumo yetu yote imekaa vizuri kipindi mgonjwa atakapojitokeza, hivyo nakuomba Mkuu wa Wilaya na Mganga Mkuu wa mkoa kuendelea kusimamia hili”. Amesema Dkt. Ndugulile.

Mapungufu aliyobaini Dkt. Ndugulile ni pamoja na wahudumu kutozingatia kanuni walizofunzwa juu ya kujikinga na maambukizi pindi watakapokua wakihudumia mgonjwa, kutokua na vifaa vya kutosha kwa ajili ya wagonjwa wa Ebola kama vitanda kwenye vituo vya Isolation na watumishi kutokua na uelewa na utayari wa kutosha kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huu.

Dkt. Ndugulile yupo Mkoani Kigoma kwa ziara ya siku tatu ambapo pamoja na maeneo mengine atatembelea mpaka wa Manyovu ili kuona hali ya utayari ya mpaka huo kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa wa Ebola na kisha atatembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma. 


Mwisho

SERIKALI YATOA BILION 7 UJENZI WA JENGO LA WAZAZI HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akifuatilia ramani ya ujenzi wa mradi wa ujenzi wa ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongoza msafara wakati akifanya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongozana na Mkurugenzi  wa Hospitali  ya Rufaa ya Mkoa ya kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji wakati wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200.

Ujenzi wa mradi wa ghorofa sita wenye gharama ya shilingi Bilion 7, katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200 ukiendelea katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu pamoja na Mkurugenzi  wa Hospitali  ya Rufaa ya Mkoa ya kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji baada ya  ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta Jijini Mbeya


SERIKALI YATOA BILION 7 UJENZI WA JENGO LA WAZAZI HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA.

Na WAMJW- MBEYA 

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya inajenga jengo la Wazazi lenye thamani ya shilingi Bilioni 7 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ya kuboresha huduma za Afya kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na nyanda za juu kusini.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya na ujenzi wa miradi katika Hospitali ya Rufaa ya kanda Mbeya. 

Waziri Ummy amesema kuwa Serikali imedhamiria kuboresha upatikanaji wa huduma za Afya nchini ikiwemo huduma za kibingwa ili kuondoa usumbufu kwa Wananchi wanaohitaji huduma hizo kwa kusafiri umbali mrefu i jambo linalopelekea gharama kubwa na usumbufu kwa wananchi. 

"Tunajenga jengo la wazazi na watoto wachanga la ghorofa sita, ambalo litakuwa na jumla ya vitanda 200, vyumba vitatu  vya upasuaji kwa ajili ya wanawake wajawazito ,vyumba sita kwa ajili ya uangalizi maalum (ICU) kwa wanawake wajawazito, pia vyumba  maalum vinne kwa ajili ya vitoto vichanga (NICU)" alisema Waziri Ummy. 

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amemwagiza Mkandarasi wa majengo hayo kuhakikisha wanaharakisha ujenzi wa majengo hayo ili wananchi waanze kupata huduma mapema jambo litalosaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto  nchini. 

Aidha, Waziri Ummy ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na nyanda za juu kusini kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya ili kurahisisha gharama za matibabu.

"Nitoe Wito kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na nyanda za juu kusini ili waweze kufurahia huduma nzuri lazima wajiunge na huduma za Bima ya Afya, Kuna NHIF Toto Afya kadi kwa mtu yoyote mwenye umri wa chini ya miaka 18 ni shilingi 50,400 huduma mwaka mzima ndani ya Mbeya na Tanzania kwa ujumla" alisema Mhe. Ummy Mwalimu 

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amesema kuwa katika kila wanawake 100, wanawake 85 wanajifungua bila matatizo yoyote, huku akisisitiza kukamilika kwa ujenzi huu kutasaidia kukokoa wanawake 15 waliobaki kutokana na huduma Bora zakibingwa zitakuwa zikitolewa.

Naye, Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kukubali kutenga fedha ili kujenga jengo la ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200 jambo litalosaidia kutatua changamoto ya ufinyu wa nafasi.

"Tunapenda kutoa shukurani za dhati kwa Serikali ya awamu ya tano, kwa kukubali kutenga fedha kupitia Wizara unayoiongoza ili kuweza kujenga jengo la ghorofa sita katika kitengo cha wazazi Meta, ambalo litakuwa na uwezo wa vitanda 200." Alisema Waziri Ummy 

Mwisho.

SERIKALI YASHUSHA NEEMA KWA WANANJOMBE

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka wakiongea na Wazee waliofika kupata huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe wakati alipofanya uzinduzi wa huduma  za Afya katika Hospitali hiyo.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitoa maelekezo kwa uongozi wa Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe  wakati alipotenbelea kukagua chumba cha kuhifadhia Dawa katika Hospitali hiyo, wakatikati (mwenye Koti jeupe) ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt. Kyambile.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikagua kadi inayoonesha kiasi cha dawa kilichopo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe pindi alipofanya ziara ya kuzindua Huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akieleza juu ya umuhimu wa kuwepo kwa mabango yanayohamasisha haki ya mgonjwa kupata  huduma  za Afya zilozo Bora wakati wa  uzinduzi wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, kushoto kwake (mwenye Koti jeupe) ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt. Kyambile.



Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimjulia hali moja kati ya wagonjwa waliofika kupata matibabu kwa mara ya kwanza katika Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, ni baada ya kufanya  uzinduzi wa  huduma za Afya katika Hospitali hiyo, Kulia kwake (mwenye Koti jeupe) ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe Dkt. Kyambile.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka wakati wa uzinduzi wa Huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akipanda mti wa matunda (mpalachichi) ikiwa ni ishara ya kuhifadhi mazingira, shughuli iliyofanyika baada ya uzinduzi wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka akipanda mti wa matunda (mpalachichi) ikiwa ni ishara ya kuhifadhi mazingira, shughuli iliyofanyika baada ya uzinduzi wa huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ulioongozwa na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikabidhi ramani ya ujenzi wa majengo mengine mapya saba  kwa Mkandarasi, shughuli iliyofuata baada ya uzinduzi  wa huduma katika Hospitali hiyo ya Rufaa  ya Mkoa wa Njombe.

Moja kati ya vyumba vya Wagonjwa kilicho na vitanda pamoja na mashine zakutambua hali ya Mgonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, iliyoanza kutoa huduma rasmi Julai 10, baada ya Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kufanya uzinduzi huo

Wananchi waliojitokeza kushuhudia uzinduzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ulioongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliyeambatana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka (Hawapo kwenye picha)

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliyeambatana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka baada ya uzinduzi  wa huduma katika Hospitali hiyo ya Rufaa  ya Mkoa wa Njombe.



Na WAMJW-NJOMBE

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imeshusha neema kwa Wananchi wa Mkoa wa Njombe kwa kutoa kiasi cha shilingi Bilion 7.6 kwaajili ya ujenzi wa awamu ya pili ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ili kuboresha huduma kwa Wananchi.

Hayo yamejiri leo wakati wa zoezi la Uzinduzi wa huduma za Afya na lililoongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe iliyofunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Katika uzinduzi huo, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha huduma za Afya katika Mkoa wa Njombe ikiwemo kujenga jengo la wazazi la ghorofa tatu, jengo la maabara, jengo la wagonjwa mahututi na jengo la upasuaji gorofa mbili, wodi za wagonjwa gorofa tatu, nyumba za Watumishi tano, pamoja na kichomea taka.

" Tunajenga jengo la wazazi la ghorofa tatu, tunajenga jengo la jengo la maabara, tunajenga jengo la wagonjwa mahututi na jengo la upasuaji gorofa mbili, tunajenga wodi za wagonjwa gorofa tatu, tunajenga jengo la kufulia, tunajenga kichomea taka na tunajenga nyumba za watumishi tano" alisema Waziri Ummy.

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amemwagiza Mkandarasi wa Hospitali hiyo kuhakikisha anakamilisha ujenzi wa majengo hayo hayo ndani ya miezi kumi ili wananchi wa Mkoa wa Njombe waanze kufaidika na huduma za Afya katika Hospitali hiyo, huku akiwatoa hofu wananchi kuwa pesa zote zipo tayari.

Mbali na hayo, Waziri Ummy mewaasa Wananchi kupambana dhidi ya magonjwa yasiyo yakuambukiza kama Kisukari, shinikizo la damu, Saratani na magonjwa ya Moyo kwa kubadilisha mtindo wa maisha ikiwamo ulaji mlo sahihi , kuacha uvutaji wa sigara na tumbaku, kuacha unywaji wa pombe kupita kiasi pamoja na kutofanya mazoezi mara kwa mara.

Aidha, Waziri Ummy ametoa with kwa vijana kujiepusha na mambo ambayo yatapelekea kipata maambukizi ya VVU, huku akiweka wazi kuwa maambukizi mapya ya VVU ni 82,000 kila mwaka nchini Tanzania, huku katika kila watu 100, watu 40 ni vijana wenye umri kati ya 15 hadi 24 umri ambao ni nguvu kazi ya taifa.

"Tunatambua kwamba kuna maambukizi makubwa ya virusi vya Ukimwi Mkoani Njombe,lazima tuzingatie kanuni za kujikinga na maambukizi ya VVU, kujizuia kufanya mapenzi kwa vijana hasa kwa wasichana ambao muda wao haijafika, pili kuwa mwaminifu kwa mwenza wako au mpenzi wako na tatu kutumia kinga" alisema Waziri Ummy

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka amewatoa hofu wananchi wa Mkoa wa Njombe kwa kuweka wazi kuwa huduma za Afya katika Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe haitoathiri utoaji huduma katika Hospitali ya Kibena iliyokuwa Hospitali ya Mkoa, ambayo kwa sasa imerudishwa chini ya Halmashauri ya Mji wa Njombe.

"Na mimi ntahakikisha wale Watumishi ambao tilikubaliana waje kwenye Hospitali hii, waje na nguo zao , vifaa vyote waviache Kibena na huduma ya Kibena iendelee, na kazi ya Hospitali hii Mhe. Ummy Mwalimu na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wataweka vifaa vyote vitakavyohitajika na huduma zitaendelea" alisema Mhe. Olesendeka

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Mhe. Edwirn Mwanzinga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kupitia Wizara ya Afya kwa kuongeza bajeti ya dawa na vifaa tiba jambo linalosaidia kuokoa kwa kiasi kikubwa maisha ya Wananjombe.

Mwisho.