Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumamosi, 27 Julai 2019

MKAKATI WA KUZUIA MBU NA WADUDU DHURIFU NCHINI WAZINDULIWA LEO

- Hakuna maoni

Picha ya Juu ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu na Picha ya Chini ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo wakizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mkakati wa wa Kitaifa wa Upuliziaji wa dawa za kuua wadudu dhurifu wakiwemo Mbu ili kupunguza Magonjwa ya Malaria na Dengue pamoja na magonjwa Mengine. Uzinduzi huu umefanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar Es Salaam.


Baadhi wa Mabwana Afya kutoka Manispaa mbalimbali za jiji la Dar Es Salaam wakipita mbele ya mgeni rasmi Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kumuonesha zana zinazotumika katika kupuliza dawa za kuangamiza wadudu dhurifu katika hafla ya uzinduzi wa mkakati wa kupuliza dawa ili kutokomeza wadudu dhurifu.
Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mkakati wa wa Kitaifa wa Upuliziaji wa dawa za kuua wadudu dhurifu wakiwemo Mbu ili kupunguza Magonjwa ya Malaria na Dengue pamoja na magonjwa Mengine.

Baadhi ya mashine za kupulizia dawa za kuua mbu na wadudu dhurifu kwa binadamu zikiwa katika magari tayari kwa ajili ya ufunguzi wa mkakati wa taifa wa kudhibiti wadudu dhurifu. Uzinduzi huo ulifanywa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu mapema leo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wa pili kushoto) akizindua rasmi mkakati wa upuliziaji dawa kwa ajili ya kutokomeza wadudu dhurifu ikiwemo mbu. Wa pili kulia ni Waziri wa TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akiwa na Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo (katikati) mapema leo wakizindua mashine za kupuliza dawa ya kuua mbu na wadudu dhurifu zitakazosambazwa badae kwenye baadhi ya mikoa ikiwemo Tanga na Dar Es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu pamoja na Waziri wa TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo Jafo wakijaribu moja ya mashine za FOG maalumu kwa ajili ya upuliziaji wa dawa za kuua wadudu wadhurifu katika maeneo mbalimbali nchini.

Katibu tawala wa mkoa wa Dar Es Salaam Bw. Abubakar Kinenge (kushoto) akikabidhiwa moja ya mashine za kupuliza dawa za kuua wadudu dharifu na Waziri wa nchi ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo (Kulia) wakati wa  uzinduzi wa kitaifa wa mkakati wa kupuliza dawa za kuua wadudu dhurifu wakiwemo mbu na wengineo nchi nzima.

Picha ya Pamoja kati ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa OR-TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo wakiwa na Wakurugenzi na viongozi mbalimbali toka Wizara ya Afya na Serikali ya Mkoa wa Dar Es Salaam wakati wa uzinduzi wa mkakati wa taifa wa kutokomeza wadudu dhurifu uliofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar Es Salaam.
Na.WAMJW-DSM

Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi mahiri wa Mhe. Dkt.John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewekeza vya kutosha katika kudhibiti mbu anayesababisha  malaria hali ambayo imepelekea kupungua  kwa kiwango cha ugonjwa wa Malaria nchini.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati akizindua mkakati wa Taifa wa kudhibiti mbu na wadudu wadhurifu jijini hapa.

“Kiwango cha Malaria nchini kimepungua  kutoka asilimia 18.1 mwaka 2008 hadi asilimia 7.3 ya sasa. Hatahivyo, juhudi zinahitajika zaidi kutokomeza ugonjwa huu".Alisema Waziri Ummy Mwalimu

Aidha, alisema takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) linakadiria kuwa asilimia 17 ya magonjwa ya kuambukiza husambazwa na wadudu na kusababisha zaidi ya vifo millioni  moja kila mwaka." Kwa mfano, malaria peke yake inakadiriwa kusababisha vifo 400,000 kila mwaka na wengi wanaofariki ni watoto chini ya miaka 5"Aliongeza Waziri Ummy Mwalimu

Kwa upande wa ugonjwa wa homa ya Dengue Waziri huyo alisema   Mwaka huu ugonjwa wa Dengue umethibitishwa kuwepo hapa nchini hususani katika jiji la Dar es Salaam,Tanga na mikoa mingine. Kuanzia  Januari 2019 hadi kufikia tarehe 21 Julai 2019 jumla ya wagonjwa waliothibitishwa kuwa na homa ya dengue hapa nchini ni 6588 na vifo 6 .

Alitaja mikoa hiyo ni Mkoa wa Dar es Salaam umeongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi ( 6,170 na vifo 4), Tanga (316 na kifo kimoja), Pwani ( 57), Morogoro (22), Lindi (8), Arusha (5), Dodoma (3 na kifo kimoja), Kagera (2), Singida (2),Ruvuma (2) na Kilimanjaro.

Hata hivyo Waziri Ummy alisema kutokana na kuendelea kujitokeza kwa magonjwa yaenezwayo na wadudu na,kusababisha madhara kwenye jamii,wizara yake imeandaa mkakati huo wa kudhibiti mbu na wadudu wengine wadhurifu wa mwaka 2019-2024 ikiwa na lengo la kuhakikisha wanadhibiti mbu na wadudu wengine wadhurifu kwa njia ya utengamano na kuhakikisha jamii inashiriki kikamilifu.

Katika kuimarisha udhibiti huo wizara imeagiza zenye uwezo mkubwa wa kupulizia zipatazo 8 na zinapelekwa katika mkoa wa Dar es Salaam,Tanga na Dodoma.

Kwa upande wake Waziri wa nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo amemshukuru Waziri Ummy kwa kuzindua mkakati huo huku akionesha nia ya dhati ya kuendeleza mkakati huo katika Mikoa yote nchini huku akiwataka Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuhakikisha wanatenga bajeti ya kununua mashine ili kuweza kufikia malengo ya kutokomeza kabisa Malaria, Dengue na magonjwa mengine yanayosababishwa na wadudu dhurifu.

MWISHO

Ijumaa, 26 Julai 2019

KAMBI YA UPASUAJI NA MATIBABU YA MOYO YAZINDULIWA TAASISI YA JAKAYA KIKWETE

- Hakuna maoni

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akipokea zawadi kutoka kwa mgeni wake Naibu Waziri wa Afya wa Jamhuri ya Watu wa China wakati walipozindua Kambi ya matibabu na upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Jakaya Kikwete Jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na Naibu Waziri wa Afya wa China Bw. Li Bin (waliosimama) wakishuhudia kusainiwa kwa makubaliano ya kambi ya upasuaji na matibabu ya moyo katika Taasisi ya Jakaya Kikwete yatayoratibiwa kwa ushirikiano wa madaktari wa JKCI na wa jimbo la Shadong nchini China. Kushoto anayesaini ni Prof. Mohamed Janabi na kulia ni mwakilishi kutoka Shadong.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea katika uzinduzi wa kambi ya matibabu na upasuaji wa moyo katika Taasisi ya Jakaya Kikwete Jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (Kulia) akiwa na Naibu Waziri wa Afya wa China Bw. Li Bin wakifuatilia maelezo ya daktari (hayupo pichani) wakati walipotembelea chumba cha uangalizi maalumu kwa wagonjwa wa moyo kilichopo taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete jijini Dar Es Salaam.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akisalimiwa na mtoto aliyelazwa katika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete wakati alipotembelea baadhi ya wodi ili kuona hali ya huduma za matibabu zinazotolewa kwenye taasisi hiyo kabla ya uzinduzi wa kambi ya matibabu na upasuaji wa moyo mapema leo.

Picha ya Pamoja ya Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu, Naibu Waziri wa Afya wa China Bw. Li Bin, Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Prof. Mohamed Janabi, Mwenyekiti wa Bodi ya JKCI Prof. William Mahalu wakiwa na Wataalamu wa upasuaji na matibabu ya moyo kutoka jimbo la Shadong la nchini China.

Na WAMJW-DSM

Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Jamhuri ya watu wa China imezindua kambi ya huduma za hali ya juu za upasuaji na matibabu ya moyo kwa wananchi wenye matatizo hayo.

Kambi hiyo imezinduliwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kwa kushirikiana na Naibu Waziri wa Afya wa Jamhuri ya watu wa China Bw. Li Bin ili kutoa huduma za matibabu ya moyo pamoja na upasuaji lengo likiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa rufaa za wagonjwa kwenda nje ya nchi kufuata huduma hizi.

“Kupitia kambi hii  Watanzania watapata huduma za hali ya juu za upasuaji na matibabu ya moyo, itatusaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa rufaa za wagonjwa nje ya nchi kwa ajili ya huduma hizi, pia kambi itatoa mafunzo ya juu katika ujuzi wa kisasa kwenye upasuaji na Tiba ya moyo kwa wataalamu wetu kwa kushirikiana na madaktari kutoka jimbo la Shadong”. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema tatizo la magonjwa yasiyoambukizwa Tanzania na duniani kote limeongezeka kwa kasi ambapo takwimu za sasa kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) inaonesha ukubwa wa tatizo hili kuwa takribani watu Milioni 17 hupoteza maisha kila mwaka ikiwa ni sawa na asilimia 60 ya vifo vyote huku akiongeza kuwa vifo hivyo asilimia kubwa vinatokea katika nchi zinazoendelea kama Tanzania.

Aidha, Waziri Ummy ameongeza kuwa sababu kuu ya maradhi ya moyo nchini kama zilivyo nchi nyingine za kiafrika ni homa ya Rumatiki (Rheumatic Fever). Hivyo inakisiwa kuna watoto kuanzia umri wa mwaka 1-15 kati ya watoto 1000 wa shule waliobalehe wana ugonjwa huu.

Waziri Ummy ametaja sababu nyingine ya magonjwa ya moyo kuwa ni ya kurithi au kuzaliwa nayo kwa asilimia 0.35, ikimaanisha kuwa kuna takribani watoto 5000 wanaozaliwa na magonjwa ya moyo ya kurithi na karibu asilimia 50 wanahitaji upasuaji ili kurekebisha kasoro zilizopo katika mioyo yao kwa mwaka.

Hata hivyo, Waziri Ummy ameishukuru Serikali ya China katika kupunguza mzigo wa maradhi haya nchini kufuatia kuanzishwa kwa Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete na sasa timu bora ya madaktari wa moyo kutoka jimbo la Shadong imekuja kutoa huduma katika kambi ya upasuaji na matibabu ya moyo inayoendelea katika taasisi hiyo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya wa China Bw. Li Bin amesema Serikali ya China itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuimarisha huduma za sekta ya afya nchini ikiwa ni kuenzi ushirikiano ulioanzishwa na waasisi wa mataifa hayo. Serikali ya China imesaidia kujenga Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kupitia Rais wa zamani wa nchi hiyo Mh. Hu Jintao na jiwe la msingi liliwekwa mwezi Machi mwaka 2010 na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete.

MWISHO

Alhamisi, 25 Julai 2019

SERIKALI YA CHINA NA TANZANIA KUENDELEZA USHIRIKIANO KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA.

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) pamoja na Naibu Waziri wa Afya kutoka China Mhe. Lin Bin wakiwa wameshikilia dawa ambazo hutengenezwa nchini China mapema leo wakiwa Ikwiriri-Rufiji Mkoani Pwani kuzindua Mradi wa Ushirikiano baina na China na Tanzania katika Kupambana na Ugonjwa wa Malaria Wilayani Rufiji.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akiangalia kinga za ugonjwa wa malaria pamoja na Naibu Waziri wa Afya kutoka China Mhe. Lin Bin leo Ikwiriri-Rufiji Mkoa wa Pwani kabla ya uzinduzi wa mradi wa  ushirikiano wa pamoja kati ya China na Tanzania kupambana na ugonjwa wa malaria Wilayani Rufiji.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akipima ugonjwa wa Malaria leo Ikwiriir Wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani alipoenda kuzindua Mradi wa Ushirikiano wa pamoja baina ya Tanzania na China wa kupambana na ugonjwa wa malaria Wilayani Rufiji

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) pamoja na Naibu Waziri wa Afya China wakisalimia mtoto katika Kituo cha Afya Ikwiriri- Rufiji Mkoa wa Pwani leo kabla ya kuzindua Mradi wa Ushirikiano baina ya Tanzania na China wa kupambana na ugonjwa wa malaria Wilayani Rufiji.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akipokea hundi kutoka Taasisi ya Fosun Pharma ya china kwa ajili ya dawa za malaria katika Wilaya ya Rufiji.
Picha ya pamoja Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wa kati kati mstari wa chini)  akiwa na Naibu Waziri wa Afya China Mhe. Lin Bin aliyeongozana na wataalam wake kutoka China pamoja na wataalam na wadau wa  sekta ya afya nchini


Na WAMJW - Rufiji, Pwani.

Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China imeahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya Malaria ili kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi salama isiyo ya maambukizi ya Ugonjwa huo.

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya kutoka Uchina Mhe. Lin Bin alipotembelea Ikwiriri, Rufiji Mkoa wa Pwani katika mradi wa ushirikiano wa pamoja baina ya China na Tanzania katika kudhibiti ugonjwa wa malaria huku akiongozana na mwenyeji wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu.

“China kuwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa kimatafa tutaendelea kushirikiana kwa pamoja katika kusaidia Tanzania inafikia malengo ya kutokomeza ugonjwa wa malaria” amesema Mhe. Lin Bin na kuendelea kusema Ugonjwa wa malaria unatibika na kuzuilika

Waziri Lin Bin amesema kuwa ushirikiano baina ya Tanzania na China umeleta manufaa katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria kwa kupunguza kiwango cha maambukizi ya ugonjwa huo Wilayani Rufiji kutoka asilimia 25 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 4.9 mwaka 2019.

“Kwa muda wa miaka 60 tumekuwa tukipambana dhidi ya ugonjwa wa malaria ambao umeathiri zaidi ya watu milioni 30, na tangia mwaka 2017 hakuna taarifa zilizolipotiwa kuhusu ugonjwa wa malaria nchini China” amesema Mhe. Lin Bin huku akiipongeza Tanzania kwa mikakati mizuri yenye lengo la kuhakikisha inatokomeza ugonjwa wa malaria.

Kwa upande wake Waziri wa Afya Tanzania, Mhe. Ummy Mwalimu ameishuruku Serikali ya China inayoongozwa na Rais Xi Jinping kwa kuendeleza ushirikiano wa enzi uliopo wa baina ya nchi hizo.

Waziri Ummy amesema kuwa ugonjwa wa malaria bado ni tatizo kubwa sana nchini Tanzania, huku takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zikionyesha kuwa asilimia 55 ya vifo vitokanavyo na malaria vinatoka katika nchini saba za Bara la Afrika ikiwemo Tanzania.

“Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli tumechukua hatu ambali mbali kwa kushirikiana na wadau wakiwemo China kupambana na malaria na yapo mafanikio makubwa ambayo tumeyapata” Amesema Waziri Ummy Mwalimu na kuendelea “Tumeweza kupunguza kiwango cha maambukizi ya malaria kutoka asilimia 14.7 mwaka 2015 hadi 7.3 mwaka 2018”

Amesema kuwa wagonjwa wapya wa malaria wamepungua kwa asilimia 26 kutoka watu 161 katika kila watu 1000 mwaka 2014 hadi kufikia 119 katika kila watu 1000 mwaka 2018 huku vifo vitokanavyo na malaria vimepungua kwa asilimia 55, kutoka vifo 20 katika watu 1000 mwaka 2014 hadi kufikia vifo 9 kati ya watu 1000 mwaka 2018.

“Serikali ya Tanzania itaendela kuchukua hatua kwa kushirikiana na wadau wetu wakiwemo Serikali ya China kuhakikisha tunapunguza kiwango cha maambukizi ya maralia hadi kufikia asilimia 1 ifikapo mwaka 2020” alisema Waziri Ummy Mwalimu.

MWISHO.

Jumatano, 24 Julai 2019

BALOZI WA UFARANSA AFURAHISHWA NA HUDUMA ZA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI MUHIMBILI

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Mikrobiolojia na Immunolojia chuo cha  MUHAS Prof. Said Aboud, wakati alipofanya ziara katika chuo hicho ili kujionea maendeleo ya shughuli zakitafiti katika chuo hicho, Kulia kwa Waziri Ummy ni Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier na wamwisho ni  Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Andrea Pembe.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akiambatana na Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier na Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Andrea Pembe, wakwanza  kushoto ni Mtaalamu wa Mikrobiolojia na Immunolojia chuo cha  MUHAS Prof. Said Aboud.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akipokea maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Mikrobiolojia na Immunolojia chuo cha  MUHAS wwakati alipofanya ziara katika chuo hicho ili kujionea Maendeleo ya shughuli zakitafiti katika chuo hicho, Kulia kwake ni Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier.

Wataalamu mbali mbali wa masuala ya tafiti pamoja na Watumishi wa Sekta ya Afya, wakifuatilia hotuba kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara katika chuo cha MUHAS ili kujionea Maendeleo ya shughuli zakitafiti

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu pamoja na Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier na Wataalamu mbali mbali wa masuala ya tafiti pamoja na Watumishi wa Sekta ya Afya baada ya ziara ya kujionea Maendeleo ya shughuli zakitafiti katika chuo cha MUHAS.


BALOZI WA UFARANSA AFURAHISHWA NA HUDUMA ZA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI MUHIMBILI

NA WAJMW-DSM

Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Bw. Frederic Clavier amefurahishwa na huduma zinazotolewa katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi cha Muhimbili.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu mapema leo wakati wa kukagua na kufuatilia maendeleo ya ushirikiano kati ya nchi ya Ufaransa na Tanzania katika masuala ya utafiti mafunzo na utoaji wa huduma za Afya katika chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Muhimbili.

Kwa kiasi kikubwa Waziri Ummy pamoja na Balozi huyo wameridhishwa kwa kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Wataalamu katika chuo hicho ikiwemo utafiti, mafunzo na utoaji wa huduma za afya.

“Binafsi tumeridhishwa na kazi kubwa na nzuri zinazofanywa na wataalamu wetu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi cha Muhimbili, katika masuala ya utafiti tumeona kazi kubwa inayofanyika katika utafiti juu ya dawa za kuua wadudu”. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema hakuna sheria nzuri za udhibiti wa dawa hizi nchini hivyo Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Muhimbili na Serikali ya Ufaransa itaendelea kufanya utafiti na kuona jinsi gani itapunguza madhara ya utumiaji wa dawa za kuua wadudu kwa binadamu.

Pamoja na hayo, Waziri Ummy amefurahi kuona ushirikiano ambao Serikali ya Ufaransa inaendelea kuutoa katika huduma za watu wenye tatizo la Seli nundu “Sickle Cell".

“kwa Mujibu wa Tafiti tuna jumla ya watu 200,000 nchini ambao wana tatizo la seli nundu na watoto ambao wanazaliwa ni 11,000 kwahiyo tumejadiliana na Serikali ya Ufaransa kuona ni jinsi gani tunaweza kuboresha huduma za ugunduzi ili tuweze kuwatambua mapema watoto pale wanapozaliwa na tatizo hili na kuhakikisha huduma za matibabu zinapatikana ikiwepo dawa ya kupunguza maumivu inapatikana”. Amesema Waziri Ummy.

Kufuatia hatua hiyo Waziri Ummy amemuomba Balozi Frederic kushawishi makampuni makubwa ya  kutengeneza dawa kutoka Ufaransa yaweze kusaidia katika kuzalisha dawa ya kupunguza maumivu ya Seli nundu inapatikana kwa Watanzania wengi.

Mwisho

Jumatano, 17 Julai 2019

WAZIRI UMMY ATOA MIEZI 3 KUKAMILISHA MRADI WA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA GEITA.

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wakatikati) akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel (Kulia kwa Waziri  Ummy) wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita,

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wapili kushoto) akipokea maelezo ya ujenzi kutoka kwa Mhandisi  kutoka Wizara ya Afya Eng. Mbuya (wakwanza kushoto) wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (watatu kushoto) akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel (wakwanza kushoto) pamoja na Mhandisi kutoka TBA (wapili kushoto) wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita,


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (aliyevaa kitambaa) akitoa maelekezo kwa Mhandisi  kutoka Wizara ya Afya Eng. MBuya wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita, Wakwanza kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel

Baadhi ya miradi ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita yenye thamani ya shilingi Bilion 2.5 inayotarajia kumalizika ndani ya miezi mitatu


WAZIRI UMMY ATOA MIEZI 3 KUKAMILISHA MRADI WA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA GEITA. 

Na WAMJW- GEITA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amefanya ziara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua miradi ya ujenzi wa Hospitali za Rufaa za mikoa nchini. 

Katika ziara hiyo Waziri Ummy amemwagiza Mkandarasi kutoka TBA Mkoa wa Geita kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha ndani ya miezi mitatu mradi huo unaisha ili huduma za Afya zianze kutolewa ifikapo Disemba 1, 2019.

"Nimemtaka Mkandarasi afanye kazi usiku na mchana ikiwezekana tukamilishe ujenzi huu hata mwezi wa kumi mwishoni, lengo langu nataka tarehe 1 mwezi Disemba 2019, tunaanza kutoa huduma hapa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita" alisema Waziri Ummy. 

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali imetoa kiasi cha shilingi Bilion 2.5 ili kukamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa Hospitali hiyo, ambayo itajenga jengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la Maabara, jengo la upasuaji pamoja na jengo la mionzi.

Hata hivyo, Waziri Ummy amesema kuwa licha ya kuwepo changamoto ya upungufu wa Watumishi katika Sekta ya Afya, Wizara ya Afya imepata kibali cha kuajiri Watumishi wengine kutoka Wizara ya Utumishi jambo litalosaidia kupunguza Uhaba wa Watumishi katika Sekta ya Afya. 

Waziri Ummy aliendelea, kwa kuwataka Wakurugenzi kujiongeza ili kupambana na uhaba wa Watumishi katika ngazi ya Mkoa, ikiwemo kuajiri baadhi ya Watumishi kupitia mapato ya ndani ili kupunguza changamoto ya uhaba wa Watumishi, huku akitoa Wito kwa vijana waliomaliza vyuo kujitolea katika Hospitali ili kuongeza uzoefu zaidi. 

Mbali na hayo, Waziri Ummy amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa kuendelea kujali Afya za Watanzania kwa kuboresha Sekta ya Afya ikiwemo kuboresha miundombinu ya Hospitali na kuhakikisha Dawa, vifaa na vifaa tiba vinapatikana.

Nae, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amemuomba Waziri Ummy kuanza kwa awamu ya pili ya ujenzi wa Hospitali hiyo ili kupata wodi ambazo zitatumika kulaza wagonjwa wataofika kupata huduma za Afya. 

"Uwepo wa wodi ndio utatoa taswira ya kuwa Hospitali hii kuwa ni Hospitali ya Mkoa, ili mtu akipata Rufaa aweze kulazwa na kuchukuliwa vipimo" alisema Mkuu wa Mkoa Mhandisi Robert Gabriel.

#tunaboreshaafya 

Mwisho.

Jumanne, 16 Julai 2019

SERIKALI YATOA BILION 5.7 UJENZI WA MAABARA NA JENGO LA UPASUAJI - SIMIYU

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongoza na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka na Watumishi wengine wa Serikali wakati alipofanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo  la upasuaji na jengo la naabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akifuatilia kwa makini ramani ya ujenzi  wa jengo la wazazi na jengo la upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu kutoka kwa Mhandisi kutoka Wizara ya Afya Bw. Mbuya (Wakulia kwa Waziri Ummy).  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka (wakwanza kulia) na Watumishi wengine wa Serikali wakati alipofanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo  la upasuaji na jengo la maabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongozana na Mhandisi Mbuya kutoka Wizara ya Afya wakishuka kwenye ngazi wakati akiendelea na ukaguzi wa mradi wa jengo la upasuaji na jengo la maabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akisaini kitabu cha wageni baada ya kumaliza ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la upasuaji na jengo la maabara katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu, Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Anthony Mtaka, akifuatiwa na Mhandisi kutoka Wizara ya Afya   Eng Mbuya.


Moja kati ya mradi wa ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji ikiwa na gharama ya shilingi Bilion 5.7 ikiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu



Na WAMJW- SIMIYU

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto yatoa kiasi cha shilingi Bilion 5.7 kwaajili ya ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji ikiwa ni awamu ya pili, baada yakuzinduliwa kwa awamu ya kwanza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli, Mwezi Agasti 2018.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu.

Waziri Ummy amesema kuwa, uwekezaji huu umeweka alama kubwa kwa Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt.John Pombe Magufuli kwa kuwasogezea huduma bora zakibingwa kwa Wananchi wa Simiyu jambo litalosaidia kuondoa usumbufu katika kutafuta huduma hizo.

"Kipekee kabisa nimshukuru Mhe. Rais katika mwaka huu 2018/2019 ameipatia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu kiasi cha shilingi Bilion 5.7 kwaajili ya ujenzi wa jengo la maabara na jengo la upasuaji lakini pia litakuwa na huduma za mionzi" alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy ameongeza kuwa Serikali tayari umeshapata kiasi cha shilingi Bilion 2.2 kwaajili ya ujenzi wa jengo la mama na mtoto ili huduma za kulaza Wagonjwa zianze kutolewa katika Hospitali hiyo.

"Tuna pesa nyingine kiasi cha shilingi Bilion 2.2 ukiacha zile Bilion 5.7 tutaanza kujenga jengo la mama na mtoto ili sasa tuanze kulaza wagonjwa, kwasababu ukiangalia wagonjwa wengi ni Wanawake na Watoto, lakini hili kingine la wodi nyingine nalibeba pia" alisema Waziri Ummy.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amewaagiza Watumishi wa Sekta ya Afya kuzingatia maadili na weledi wa kazi zao ikiwemo matumizi mazuri ya lugha kwa wagonjwa pindi wakiwa kupata huduma za Afya.

"Niinawataka tena Wauguzi kuzingatia maadili na weledi wa kazi zao ,ikiwemo kutumia lugha nzuri, lugha yenye busara na lugha yenye upendo kwa wagonjwa, asili ya muuguzi ni upendo na heshima na kumthamini mtu ambae unampa huduma " amesema Waziri Ummy.

Hata hivyo, Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa Serikali haitokuwa na msamaha na Mtumishi yeyote ambae atabainika ametoa lugha chafu kwa wagonjwa ikiwemo kujihusisha na masuala ya Rushwa kwa kuwachukulia hatua kali ikiwemo kufuta reseni zao.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwa changamoto kubwa ambayo itakuwepo katika ujenzi wa Hospitali hiyo ni uwepo wa wodi, hivyo amemwomba Waziri Ummy kuharakisha ujenzi wa wodi ili huduma zianze mara moja.

"Wakati wote tunapokuwa tunakuja changamoto kubwa ilikuwa ni wodi, na hata wagonjwa wanaokuja wanaulizia kuhusu wodi za kulala wagonjwa " amesema Mhe. Mtaka.

#tunaboreshaafya


Mwisho .

RAIS MAGUFULI AMWAGIZA WAZIRI UMMY KUFUATILIA MALIPO YOTE YA SERIKALI KWA WAGONJWA WA NJE YA NCHI

- Hakuna maoni
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuonesha ishara ya uzinduzi rasmi wa miradi 7 yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando. Kulia kwake ni Baba Askofu Mhashamu Askofu Renatus Nkwande huku kushoto kwake ni Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu akifuatiwa na Waziri wa Nishati Medard Kalemani na mwisho ni Naibu  Waziri wa Ardhi Mhe. Angelina Mabula

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimpa mkono Baba Askofu Mhashamu Askofu Renatus Nkwande baada ya kuzindua mradi wa NHIF ikiwa ni moja kati ya miradi 7 iliyozinduliwa yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akieleza jambo wakati wa uzinduzi rasmi wa miradi 7 yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitoa taarifa ya Wizara ya utekelezaji mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (hayupo kwenye picha) wakati wa uzinduzi rasmi wa miradi 7 yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando.

Baadhi ya viongozi wa Serikali wakifuatilia Maelekezo kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (hayupo kwenye picha) wakati wa uzinduzi rasmi wa miradi 7 yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando.

Wananchi waliojitokeza kumsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wwakati wa uzinduzi wa miradi 7 yenye jumla ya shilingi Bilion 15 katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya ziwa Bugando.


Na WAMJW-MWANZA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli amemwagiza Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kufuatilia malipo yote ya Wagonjwa wanoenda kutibiwa nje ya nchi ili kubaini ubadilifu unaofanywa na baadhi ya watu wasiowaaminifu.

Rais Magufuli ameagiza hilo leo wakati akizindua miradi Saba ya huduma za Afya katika Hospitali ya Rufaa ya kanda ya Ziwa Bugando yenye thamani ya shilingi Bilion15, jambo litalosaidia kurahisisha upatikanaji wa huduma bora kwa ukaribu pamoja na kuokoa kiasi cha fedha miongoni mwa wanaohitaji huduma. 

"Na kwasababu Waziri wa Afya yupo hapa, akafuatilie malipo yote ambayo tunatakiwa kulipa, kule nje , akikuta kunamalipo yakulipa mtu ambae hakuwa mgonjwa aliyejihifadhi huko, akazilipe mwenyewe " alisema Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 

Rais Magufuli amesema kuwa baadhiya Watendaji waliona kupeleka Wagonjwa nje ya nchi kwaajili ya matibabu ni fursa yakujipatia kipato, jambo lililokuwa linapelekea hasara kubwa kwa nchi ya Tanzania kutokana na malipo kwa baadhiya watu wasiostaholi.

" Hata kupeleka kwa wagonjwa nje kwa Watanzania ilikuwa ni dili, ilikuwa ni fursa kwa Watendaji, wapo watu waliokuwa wanapewa vibali kwenda kutibiwa India lakini anaumwa mafia, ilikusudi apate safari na msindikizaji, bill zote zinaletwa kwa Serikali " alisema Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 

Dkt. Magufuli aliendelea kusema kuwa ni lazima tujenge nidhamu katika nchi, huku akisisitiza kuwa Serikali haijakataza kupeleka wagonjwa nje ya nchi, huku akisisitiza kuwa wagonjwa wanaostahili kupelekwa kwa matibabu nje ya nchi ni wale walioshindikana ndani ya nchi.

Aidha, Waziri Ummy ameagiza kuboresha uzalishaji wa oksijeni ili kuhakikisha zinazalishwa kwa wingi jambo litalosaidia kuokoa kiwango kikubwa cha mapato kinachopotea kwa kuagiza nje ya nchi, pia itasaidia kuongeza ajira kwa wananchi wa Tanzania. 

"Ninawaomba ndugu zangu, tengenezeni oksijeni nyingi, panueni uzalishaji ili Wizara ya Afya iagize hapa hapa Bugando ili vijana wanaomaliza famasi hapa hapa Bugando wapate ajira hapa yakutengeneza Oksijeni " alisema Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 

Nae, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu amesema kuwa hadi kufikia juni 30, 2019 Serikali ina jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya vya umma 5756 (71%),Taasisi za Dini 923 (11%) na vituo vya watu binafsi ni 1440 (18%). 

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa, pia Serikali, ina Jumla ya Vituo vya Afya vya Mashirika ya Dini ikiwemo Hospitali Teule za Wilaya vipatavyo 43, ambazo zinapata ruzuku (OC) kiasi cha shilingi 30,704,000/= kwa mwezi na mishahara kiasi cha Tshs.1.8 bilioni kwa mwezi kwa ajili ya watumishi 2600. 

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali imepunguza malalamiko ya upatikanaji wa dawa kwa Wananchi na katika hospitali ya rufaa ya Bugando hii ni kufuatia ongezeko la bajeti ya dawa hadi kufikia Tshs.270 bilioni, huku Serikali ikitoa kiasi cha Tshs. milioni 100 kila mwezi kwa ajili ya kununulia dawa, huku Mwaka 2015/16 walikuwa wanapata Tshs.534 milioni na Mwaka 2018/19 wanapata Tshs.1.5 bilioni.

Naye, Mkurugenzi wa Hospitali ya kanda ya Bugando Prof. Abel Makubi akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, amesema  kwa  kipindi cha miaka minne wamefanikiwa kuboresha huduma za afya na kukamilisha miradi saba ambayo ni  kitengo cha  saratani, mahututi, upasuaji, oksijeni na viwanda vidogo ambavyo vitakuwa vinazalisha dawa kwa ajili ya wagonjwa.

Ameongeza kuwa asilimia 70 ya wagonjwa wa saratani ambao walikuwa wanakwenda katika Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam walikuwa wanatoka Kanda ya Ziwa, hivyo imewapunguzia gharama na usumbufu wa kusafiri kutafuta huduma hiyo.

#tunaboreshaafya

Jumapili, 14 Julai 2019

ZIARA YA MAFUNZO 5S-KAIZEN KWA WAGENI KUTOKA WIZARA YA AFYA NA WATUMISHI YA BANGLADESH

- Hakuna maoni
Muuguzi Mkuu - Hospital ya Rufaa ya Mkoa- Amana,Beauty Mwambebule akitoa maelezo kwa wageni kutoka nchi ya  Bangladesh namna mfumo wa KAIZEN  unavyofanya kazi katika Hospital hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Mratibu wa Hospitali za Rufaa za Mikoa kutoka Wizara ya Afya -Idara ya Tiba -Kitengo cha Uratibu wa Hospitali za Rufaa za Mikoa,Dkt. Angelina Clarisa Sijaona (kushoto) akiwa na wageni kutoka nchi ya Bangladesh akiwaonesha mambo mbalimbali yanayo tumika kwenye  mfumo wa KAIZEN  katika Hospital Amana  jijini Dar es Salaam.

Wangeni kutoka Bangladesh wakiwa katika Hospital ya Amana iliyopo Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam

Picha ya pamoja ya maofisa kutoka wizara ya afya,hospitali ya rufaa ya mkoa Amana pamoja na wageni kutoka Bangladesh baada ya kutembelea hospitali ya Amana

Na.WAMJW,Dsm
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mradi wa Kuimarisha Hospitali za Rufaa za Mikoa (RRHMP) katika kuendelea kuziwezesha Hospitali za Rufaa za Mikoa  ilipanga kukaribisha wageni kutoka katika nchi mbalimbali za Afrika ili kubadilishana uwezo katika utekelezaji wa 5S-KAIZEN katika kuboresha utoaji wa huduma za afya nchini.

Kulingana na mpango kazi wa mwaka huu, Mradi ukishirikiana na Wizara ya Afya ulitarajia kupokea wageni kutoka Wizara ya Afya na watumishi wa sekta hiyo kutoka nchini Ghana  (7) na Bangladesh (7) kwa ajili ya ziara ya mafunzo ya Falsafa ya 5S-KAIZEN-TQM pamoja na wawakilishi wa JICA wawili kutoka kila nchi.  Pamoja na hao, tulitegemea kupokea watumishi wa Afya 14 kutoka nchi za kiafrika zikiwemo Uganda, Kenya, Malawi, Liberia, Siera Leoni, Sudan, Zambia, Zimbabwe na Benin.

Tayari wageni wote hawa waliishafika na kupata mafunzo kutoka haya.

Wiki hii, tumewapokea wageni kutoka Katika Wizara ya Afya na watumishi 7 wa sekta na wawakilishi wawili wa JICA-Bangladesh. Wageni hawa watakuwepo hapa nchini kwa wiki moja  Katika kipindi hicho watapata mafunzo ya KAIZEN na leo wametembelea Hospitali za Rufaa ya Mkoa Amana na kesho wanategemewa kutembelea Hospitali za Taifa Muhimbili.

Lengo la ziara hii ni kubadilishana uzoefu katika utekelezaji wa 5S-KAIZEN-TQM katika hospitali zetu kwa ajili ya kujifunza na kuiga mazuri ya kujifunza watakaporejea nchini kwao. Aidha, Timu zetu zinategemewa kupata nafasi ya kupata uzoefu kutoka kwa nchi zinazotutembelea.

Falsafa ya 5S-KAIZEN-TQM hii inalenga kuboresha mazingira ya kutoa huduma za afya  na kukidhi mahitaji ya wateja wetu, wale wa ndani na wa nje.

Kwa ujumla wake, falsafa ya 5S-KAIZEN-TQM hii inarahisha kazi, inahakikisha usalama kwa wateja wa ndani na nje na inapunguza upotevu wa rasilimali, napunguza makosa na inapunguza gharama za uendeshaji.

Kwa Hospitali za Rufaa za Mikoa ambayo wanaitimia falsafa hii wameweza kufanya vizuri katika kutoa huduma bora, kuongeza katika mapato na wafanyakazi kufurahia mazingira yao ya kazi.

Ni falsafa inayoweza kutumika katika maeneo mbalimbali pamoja na viwandani.