Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Alhamisi, 8 Agosti 2019

TEKNOLOJIA YA NANO FILTER YAWAVUTIA VIONGOZI WA WIZARA JIJINI ARUSHA

- Hakuna maoni

Dkt. Askwar Hilonga akiwakaribisha Viongozi wa Wizara wakiongozwa na Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi na wengineo wakati walipotembelea Chuo Kikuu cha Nelson Mandela Jijini Arusha.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Nelson Mandela Prof. Emmanuel Luoga akiangalia tuzo ya ubunifu wa teknolojia ya maji aliyopewa Dkt. Askwar Hilonga kwenye kikao cha dunia cha masuala ya afya (World Health Assembly) kilichofanyika Jijini Geneva, Uswisi mwezi Mei mwaka huu.

Picha ya pamoja katika ofisi ya Kaimu Mkuu wa chuo cha Nelsona Mandela Jijini Arusha.


Mbunifu wa Teknolojia ya Nano Filter Dkt. Askwar Hilonga akiwaonesha viongozi sehemu ambayo ubunifu huo ulipoanzia katika chuo cha Nelson Mandela.

Mifupa ya wanyama inayotumika katika Teknolojia ya Nano Filter kuchuja na kutibu maji kwa ajili ya matumizi.

Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi akiangalia chengachenga za mifupa inayotumika na teknolojia ya Nano Filter katika kuchuja na kutibu maji ya kunywa.

Dkt. Hilonga akitoa maelezo kwa viongozi wa Wizara wakati walipotembelea maonesho ya Sabasaba kwenye banda la Nano Filter.

Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi akiwa na Dkt. Khalid Massa, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Wedson Sichalwe, mbunifu wa Teknolojia ya Nano Filter Dkt. Askwar Hilonga na wajumbe wengine wakiwa katika picha ya pamoja nje ya banda la Nano Filter katika maonesho ya Nanenane Jijini Arusha.


Teknolojia ya Nano Filter iliyofungwa katika moja ya Shule Jijini Arusha.

Baadhi ya Wananchi waliofika katika ofisi hiyo kwa ajili ya kujaziwa maji.

Picha ya pamoja ya viongozi wa Wizara wakiwa na Baadhi ya Wafanyakazi wa Nano Filter nje ya ofisi zao.
Teknolojia ya Nano Filter ikiwa imefungwa katika Maonesho ya Nanenane Jijini Arusha.
Na Emmanuel Malegi-Arusha


Viongozi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakiongozwa na Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi wamemtembelea mbunifu wa teknolojia ya kusafisha maji ambaye pia ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Nelson Mandela kilichoko Arusha Dkt. Askwar Hilonga.

Katika ziara hiyo Dkt. Hilonga amewaonesha viongozi hao Teknolojia iitwayo Nano Filter yenye uwezo wa kusafisha maji, kuondoa bacteria na virusi, huondoa fluoride na madini yote ambayo hayatakiwi kwa binadamu na kuyafanya maji kuwa safi na salama kwa watumiaji na kwa gharama nafuu zaidi.

Dkt. Hilonga ana tuzo 17 kutoka taasisi na mashirika mbalimbali kutokana na ubunifu huo huku tuzo yake kubwa ikiwa ni ile aliyoipata kwenye kikao cha dunia cha masuala ya afya (World Health Assembly) kilichofanyika Jijini Geneva, Uswisi mwezi Mei mwaka huu.

Jumatano, 7 Agosti 2019

HABARI PICHA : ZOEZI LA UTAYARI KUKABILIANA NA UGONJWA WA EBOLA KATIKA WILAYA YA BUHIGWE MKOANI KIGOMA.

- Hakuna maoni
Na Englibert Kayombo, Kigoma


Watoa huduma za afya kutoka Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma wakiwa wamembeba mgonjwa anayehisiwa kuwa na ugonjwa wa ebola tayari kumpatia huduma ya kwanza katika zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo usiingie nchini.

Kufuatia nchi ya jirani (DRC) kuendelea kukabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola tangu Agosti mwaka 2018. Serikali ya Tanzania imeendelea kuchukua tahadhari za ugonjwa huo kwa kupima utayari wa Watoa huduma za Afya kwa mikoa iliyomo hatarini kuathiriwa na ugonjwa huo.

Serikali kupitia uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Menejimenti ya Maafa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, pamoja na wadau wa maendeleo; WHO, FAO, USAID, HRH2030, Shirika la Msalaba Mwekundu (RED CROSS), na USAID Global Health Supply Chain Programu, inaendelea na zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo katika Wilaya za Mkoa wa Kigoma.

Zoezi hilo linalenga kuwaimarisha watumishi hao katika maeneo maalum ikiwemo ya uratibu, utambuzi na ufuatiliaji wa wagonjwa iwapo atagundulika, matibabu ya wagonjwa, uchukuaji na usafirishaji wa sampuli na kuthibitisha maabukizi pamoja kuimarisha mifumo ya utambuzi wa masuala ya Afya kwa kila abiria wanaopita kwenye mipaka ya mkoa wa Kigoma.


Mwezeshaji wa zoezi la upimaji wa utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Dkt. Christopher Mnzava akifafanua umuhimu wa kuzingatia muda wakati wa maandalizi ya kumhudumia mgonjwa anaehisiwa kuwa na ugonwja wa ebola kwa watoa huduma za afya Katika Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma.

Watoa huduma za afya mara baada ya kumhudia mgonjwa wa ebola wakiwa wamebeba mifuko maalum kwa ajili ya utunzaji wa mavazi na vifaa vilivyovyotumika kuhumdumia mgonjwa kabla ya kuyateketeza.

Dkt. Refaya Ndyamuba kutoka Shirika la Afya Duniani akielekea kukagua kituo kitachokutumika kuhudumia wagonjwa wa ebola katika Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma katika zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa ebola usiingie nchini linaloendelea Mkoani Kigoma.

Bi. Consolata Felix Muuguzi kutoka Wizara ya Afya(aliyesimama kulia) akikagua watoa huduma za afya katika Kituo cha hudumia wagonjwa wa ebola katika Wilaya ya Buhigwe namna wanavyosafisha kitanda kilichotumika kumbeba mgonjwa wa ebola katika zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa ebola usiingie nchini linaloendelea kufanyika mkoani humo.

"Mahema ya kuhudumia wagonjwa wa ebola yanatakiwa kuwa na hewa safi muda wote" Dkt. Refaya Ndyamuba kutoka Shirika la Afya Duniani akifungua sehemu ya kuingiza hewa kwenye hema linalotumika kuhudumia wagonjwa wa ebola wakati wa zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo katika Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma. 

Mtoa huduma za afya katika Wilaya ya Buhigwe akinawa kwa maji safi yaliyochanganywa na kemikali ya "Chroline" mara baada ya kutoka kumhudumia mgonjwa wa ebola wakati wa zoezi la tayari wa kukabiliana na ugonjwa huo


Jumatatu, 5 Agosti 2019

WATOA HUDUMA ZA AFYA KIGOMA KUPIMWA UTAYARI KUKABILIANA NA EBOLA

- Hakuna maoni
Consolata Felix kutoka Wizara ya Afya (aliyesimama kushoto) akifuatilia zoezi la vitendo la utayari wa kukabiliana ugonjwa wa ebola kwa watoa huduma za afya katika jamii.
Washiriki wa zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa ebola Mkoa wa Kigoma wakiwa kwenye mazoezi ya mezani kujadili mikakati ya kudhibiti ugonjwa huo usiingie nchini mapema leo Mjini Kigoma.

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Bw  Daniel Machunda akisema jambo kwa washiriki wa kikao kazi katika zoezi la upimaji wa utayari wa kukabiliana na ugonjwa ebola (hawapo pichani) mapema leo Mjini Kigoma.

Picha ya pamoja ya mgenu rasmi Bw . Daniel Machunda (aliyeketi kati kati) wadau wa maendeleo na washiriki wa zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa ebola nchini katika Mkoa wa Kigoma


Na Englibert Kayombo, Kigoma.

SEREKALI ya Tanzania kupitia uratibu wa wa ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  zitafanya zoezi la kupima utayari kwa watoa huduma za afya katika kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika Mkoa wa Kigoma.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Maafa  Ofisi ya Waziri Mkuu Bwana Bashiru Taratibu wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha wadau kutoka ndani nan je ya nchi kujadili mikakati iliyopo kudhibiti ugonjwa huo usiingie nchini.

Amesema kuwa zoezi hilo litazingatia dhana ya afya moja ambayo hujumuisha sekta ya afya ya mifugo,binadamu,mifugo,wanyamapori na mazingira katika kujiandaa,kufuatilia na kukabili magonjwa ambayo huambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda binaadamu.

"Zoezi hili litapima uelewa wa jamii kuhusu namna ambavyo wanapaswa kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa ebola, hivyo wakati wa zoezi watoa huduma za afya na sekta zingine watakuwa wakifanya zoezi hilo kwa vitendo"alisema

Bw. Taratibu amesema kuwa zoezi hilo litafanyika kuanzia tarehe 5 hadi 9 Agosti katika vituo vya kutolea huduma za afya na maeneo ya mipaka ya Mkoa wa Kigoma. Aliendelea kwa kusema kuwa katika zoezi hilo watoa huduma wa afya watakuwa wakifanya zoezi hilo kwa vitendo namna ya kumuhudumia mgonjwa wa ebola atakapogundulika.

Mgeni rasmi katika kikao hicho Daniel Machunda Kaimu katibu Tawala Msaidizi rasilimali watu kwaniaba ya katibu wa Mkoa wa Kigoma Rashid Mchata alisema Mkoa wa Kigoma una njia nyingi zisizo za halali za mipakani(panya road)ambazo zinachangia hatari ya ugonjwa wa Ebola kuingia nchini.

Aliwataka wananchi kuchukua tahadhari hasa wale wanaovuka mipaka kwenda nchi za jirani."Ikumbukwe kuwa zoezi linahusu upimaji wa utayari kwa Mkoa wa Kigoma na hakuna mgonjwa yeyote wa ebola aliyeripotiwa hadi sasa nchini"alisema Machunda

Mganga mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt Paul Chawote alisema kuwa nchi ya jirani ya DRC(Congo)imeendelea kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola tangu kulipotiwa mlipuko wa ugonjwa huo mnamo mwezi Agosti mwaka 2018.

Dkt Chawote amesema kuwa idadi ya vifo vilikuwa 1823 ikiwa ni sawa na asilimia 67 ya idadi watu walioathiriwa na ugonjwa huo huku nchi ya Uganda ambayo inapakana na DRC na Tanzania imekuwa na wagonjwa 3 wa Ebola kwa mujibu wa taarifa maambukizi hayo yametoka DRC.

"Kwenye mipaka yetu ya DRC na Burundi kuna mwingiliano mkubwa wa watu unaochangiwa na shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi hivyo vinachangia hatari zaidi ya ugonjwa wa Ebol kuingia nchini"alisema Dkt Chawote

Remidius Kakulu Afida Afya mwandamizi toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto amesema mpaka sasa mipaka iliyorasmi yote imedhibitiwa na tayati Serikali imefunga vipima joto vya kisasa katika mipaka yote iliyo rasmi.

"Kuna ile mipaka ambayo siyo rasmi ambayo ipo kwenye vijiji na maeneo mengine tunawaomba Viongozi wa Vijiji pamoja na wananchi kutoa taarifa pale mgeni anapoingia au kumpeleka kituo cha afya ili aweze kupimwa"alisema

Mwisho

WIZARA YA AFYA KUDHIBITI KIFUA KIKUU MAGAREZA 15 NCHINI

- Hakuna maoni
Meneja Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma Dkt.Beatrice Mutayoba akiongea na washiriki wa mafunzo hayo(hawapo pichani) kwenye bwalo la Magereza Ukonga

Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Jeshi la Magereza Owesu Ngalama akifungua mafunzo ya tathimini ya udhibiti wa TB katika Magereza 15 nchini

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza mgeni rasmi(hayupo pichani) kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo


Picha ya pamoja ya mgeni rasmi na washiriki wa mafunzo hayo ambayo yana lengo la kuyafikia magereza kumi na tano hapa nchini katika kutathimini hali ya huduma ya TB kwenye magereza nchini

Na. Catherine Sungura, WAMJW-DSM
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti kifua kikuu na Ukoma kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza nchini wanaanza afua ya ufuatiliaji wa kutathimini hali ya huduma za kutokomeza kifua kikuu katika magereza nchini.
Hayo yamesemwa na Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Jeshi la Magereza (CP) Owesu Ngalama wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa maofisa wa jeshi hilo yanayofanyika kwenye bwalo la magereza ukonga jijini hapa.
CP Ngalama alisema kuwa afua hiyo itasaidia jeshi la magereza kuweza kubaini hali ya TB kwenye magereza kwani wanaoingia kwenye magereza ni wana jamii hivyo itasaidia kubaini ugonjwa huo kwa wafungwa na kwa jamii kwa ujumla
“Ugonjwa huu unaambukizwa kwa hewa hivyo kwa tathimini hii itasaidia kuleta utaalam mkubwa kwa wataalam wetu wa tiba waliopo kwenye jeshi kwani hali ya TB sio kubwa kwenye magereza  ila lengo ni kuhakikisha hakuna maambukizi makubwa kwani wafungwa wanaingia na kutoka”.Alisema CP Ngalama
Aidha,ameishukuru wizara ya afya kwa kuendelea kushirikiana nao kwa muda mrefu hususan kwenye utoaji huduma za afya ikiwemo utoaji wa dawa,vifaa na vifaa tiba pamoja na masuala ya lishe kwenye vituo vya afya vilivyopo kwenye magereza nchini.
Naye Meneja Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma (NTLP) kutoka Wizara ya Afya Dkt. Beatrice Mutayoba alisema ugonjwa wa Kifua Kikuu bado ni jangwa kwani bado kuna takribani watu laki moja na elfu hamsini na nne wanakadiriwa kuugua kifua kikuu kila mwaka na inakadiriwa vifo elfu ishirini na saba  kila mwaka nchini.
Dkt. Mutayoba alisema kifua kikuu kinaweza kumpata mtu yeyote kwani maambukizi yake ni ya njia ya hewa hivyo yapo makundi hatarishi zaidi ikiwemo magereza hivyo wanaweka jitihada zaidi kuyafikia makundi hayo ili kutokomeza kifua kikuu ifikapo 2030.
“kama nchi tumepiga hatua kubwa sana kutokomeza ugonjwa huu hivyo tunaongeza juhudi zaidi kwenye makundi hatarishi ikiwemo magereza,migodini,wavuvi ili kuwafikia kwa karibu na kuhakikisha tunapunguza maambukizi ndani ya magereza na maeneo haya”.Alisisitiza
Hata hivyo alisema mkakati wa kudhibiti kifua kikuu upo kwa wananchi wote hivyo  kama mpango wanaendelea kutoa elimu kwa watanzania wote mara waonapo dalili waende kwenye vituo vya afya kwani wizara ya afya inatoa dawa,vipimo  na huduma za kifua kikuu bila malipo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya “Magerezani tunaweza utaratibu kwa wanaoingia kuwe na taratibu za uchunguzi ili anapokutwa na kifua kikuu waanze matibabu kwani unapoanza matibabu ndani ya wiki mbili huwezi kuambukiza wengine”.Alisema Dkt. Mutayoba
Mikoa kumi na tano itakayoanza na utekelezaji  huo ni pamoja na Dar es salaam, Dodoma, Iringa, Kagera, Kilimanjaro, lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Mwanza, Pwani, Shinyanga, Singida, Tabora na Tanga.
Mwisho

PREPARING THE HEALTH WORKFORCE TO MAKE THE MOST OF DATA

- Hakuna maoni
DataUseForHealth


Health workers exchange learnings about Tanzania's electronic immunization registry. Photo: PATH/Trevor Snapp. For nearly thirty years as a health worker in Tanzania, Salome has used pen and paper to record patient data. A digital transformation promises to streamline her work and improve patient care. 

Digital health solutions increase data quality and accessibility, but to be effective and improve patient outcomes, health workers must know how to make the most of the information. For many like Salome, Tanzania’s digital transformation will require retraining and developing new digital literacy skills. 



Building the workforce of the future 
The Data Use Partnership—a collaboration between the Government of Tanzania and PATH—aims to equip Tanzania’s health sector and workforce with skills for the country’s changing digital landscape. This includes training existing and future generations of health workers to make better use of digital platforms and data. 

To facilitate trainings, the Data Use Partnership established the Capacity Building Consortium (CBC). Made up of three universities, two health research and training institutes, and zonal health training centers around the country, the CBC fosters a culture of data use and builds the capacity of health workers to identify and solve problems, measure performance, allocate resources, track patients, support clinical decisions, and streamline service delivery. 



Making the most of data 
“In the health sector, a lot of data are collected, but aren’t necessarily put into efficient use when making crucial decisions,” explains Professor Flora Lucas Kessy, Secretariat Chairperson of the CBC and instructor at the Tanzania Training Center for International Health. “The consortium was formed to build the capacity of health workers through both in-service and pre-service training.” 

The consortium is building the health workforce’s capacity by: 
• Developing trainings and innovative platforms: The Data Use Partnership is developing a new series of short-term trainings, using costeffective and innovative platforms. Trainings will be offered in person through zonal health resource centers to ensure greater accessibility, and through eLearning modules that the CBC aims to integrate under a single government-owned National Health eLearning platform.



 • Establishing new delivery methods: eLearning platforms can help deliver trainings to rural health providers, where long distances, limited resources, and poor transportation may otherwise be a barrier to education. “There are lots of current innovations in this country in terms of mobile phone and smartphone use,” explains Professor Kessy. “We can use digital platforms to deliver critical courses even to health providers that are very far away.” 

• Increasing focus on data use and analytics: The CBC will review, develop, and standardize curricula for data analytics training, so that the workforce is operating from a place of common experience. With more than 136 institutions offering certificates and diplomas in health and allied sciences programs, it’s critical that students graduate with a shared skillset, understanding, and appreciation for data use. 



• Fostering government ownership and peer learning: The CBC also recognizes the importance of ensuring that trainings are delivered by their own peers and experts, instead of an outside institution or implementing partner. “Health workers have to feel that they’re being trained by one of their own,” explains Mr. Tumaini Macha, Assistant Director, Monitoring & Evaluation from the Ministry of Health. “This mentorship model is even more efficient and ensures that trainers understand the need in different areas.” 

Achieving digital transformation 
"Having a curriculum that’s strong in data use ensures that whoever graduates from universities and other academic institutions, goes home with knowledge on how to deliver on data use,” explains Professor Kessy. “We've been able to bring together five different prime institutions that have their own different ways of operating. It’s so unique that we can work together, forget our own university boundaries, and build an open consortium that’s focused on data use.” 


The CBC is critical to Tanzania achieving digital transformation. By educating and training the existing workforce and preparing a pipeline of future talent, the health workforce will be able to make optimal use of digital tools, ultimately leading to better patient care and more equitable access to health services.

Jumamosi, 3 Agosti 2019

WAZIRI UMMY AKABIDHI MASHINE YA UPULIZIAJI DAWA ZA KUDHIBITI WADUDU MKOANI TANGA

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati wa hafla ya makabidhiano ya mashine ya kupulizia dawa za kudhibiti wadudu wadhurifu yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano Jijini Tanga.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa afya wa jiji la Tanga jinsi wanavyowanasa mbu kwa ajili ya kuwafanyia tafiti mbalimbali wakati wa hafla ya makabidhiano ya mashine ya upuliziaji dawa za kuangamiza wadudu wadhurifu iliyofanyika katika viwanja vya Tangamano jijini Tanga.

Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi akiongelea mkakati wa wizara hiyo wa kudhibiti mbu na wadudu wadhurifu ambao utatekelezwa nchi nzima, hapo ni katika makabidhiano ya mashine ya kupulizia dawa za kudhibiti wadudu wadhurifu yakiyofanyika katika viwanja vya Tangamano Jijini Tanga.


Viongozi wa Jiji la Tanga wakifurahia makabidhiano ya Mashine ya upuliziaji dawa za kudhibiti wadudu wadhurifu kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu. Makabidhiano hayo yalifanyika katika viwanja vya Tangamano jijini humo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapa na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Bw. Mustafa Mhina wakiangalia jinsi mashine ya upuliziaji inavyofanya kazi.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (katikati), Mkurugenzi wa kinga wa Wizara hiyo Dkt. Leonard  Subi (wa kwanza kushoto) wakiwa pamoja na Mabwana Afya wa Jijini Tanga wanaotekeleza mkakati wa kudhibiti mbu na wadudu wadhurifu mkoani humo.

Na Emmanuel Malegi-WAJMW, Tanga

Jiji la Tanga limekua la pili kupata mashine za kupulizia dawa za kuua mbu na wadudu wadhurifu waenezao magonjwa mbalimbali ikiwa ni mkakati wa Wizara ya Afya kwa kushirikiana na TAMISEMI katika kudhibiti wadudu hao.

Akikabidhi mashine hiyo kwa uongozi wa Jiji la Tanga, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema mkakati huo ni wa miaka mitano (2019-2024) na unalenga kuhakikisha mbu na wadudu wadhurifu wanadhibitiwa kwa njia ya utengamano na ameiomba jamii ishiriki kikamilifu katika kupambana na wadudu hao.

“Wizara yangu imeagiza mashine nane za kisasa(foggig mashine) zenye uwezo mkubwa wa kupulizia na zinabebwa na magari na kupuliza eneo kubwa kwa wakati mmoja, hivyo naomba jamii ihakikishe inashiriki kikamilifu katika kupambana na wadudu hawa dhurifu”. Amesema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy ameongeza kuwa katika kuhakikisha mkakati huo unafanikiwa ni vema mikoa ikawekeza katika maeneo ya msingi am bayo ni pamoja na ushiriki wa jamii, sekta binafsi na wadau  kushiriki katika kudhibiti wadudu kwa njia shirikishi zinazolenga kuharibu mazalia ya wadudu. Mikoa kuimarisha mfumo wa ufuatiliaji wa mbu na wadudu wadhurifu katika ngazi zote na kupanga njia madhubuti za udhibiti wa wadudu hao.

Waziri Ummy amesema katika kuhakikisha mkakati huu unatekelezwa, Wizara ya afya kwa kushirikiana na TAMISEMI imetoa maagizo kwa kila Mkoa, Wilaya na Halmashauri zote ziweze kuyatekeleza ikiwa ni pamoja na kuandaa mipango ya utekelezaji wa udhibiti wa mbu na wadudu wadhurifu ambayo itakua mtaa kwa mtaa, Halmashauri kuhakikisha zinaishirikisha jamii katika ngazi zote za mapambano haya ya mbu na wadudu wadhurifu.

Pia Waziri Ummy amezitaka Halmashauri kufanya tathmini ya utekelezaji wa mkakati huu katika kipindi cha mwaka mmoja na kutoa taarifa ya mafanikio, changamoto na mipango ya Halmashauri katika utekelezaji ikiwa ni pamoja na kununua mashine za upuliziaji (Fogging Machine) angalau moja katika kipindi cha kufikia Januari 2020.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tanga ambae ni Kaimu Mkuu wa Mkoa Bw. Thobias Mwilapa amemshukuru Waziri Ummy na Wizara ya Afya kwa ujumla kwa kuupatia mkoa huo mashine hiyo ambayo itasaidia katika utekelezaji wa mkakati wa kudhibiti mbu na wadudu wadhurifu ambao wanaeneza magonjwa huku akiitaja Tanga kushika namba mbili kitaifa kwa ugonjwa wa Homa ya Dengue baada ya Dar Es Salaam.

MWISHO

Ijumaa, 2 Agosti 2019

WAKAZI WA TANGA KUPATA HUDUMA ZA DHARURA NA MAHUTUTI KATIKA HOSPITALI YA BOMBO

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiteta na Makamu wa Rais wa Taasisi ya ABBOTT Bw. Andy Wilson wakati wa uzinduzi wa huduma za dharura na mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tanga.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea jambo wakati wa uzinduzi wa huduma za dharura na mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga mapema leo.
Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya ambaye alimuwakilisha Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Leonard Subi akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma za dharura na mahututi kartika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizindua huduma za dharura na mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Tanga Bw. Thobias Mwilapa.




Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (Kushoto) akioneshwa kifaa cha kusaidia mapigo ya moyo na Daktari bingwa wa huduma za dharura Dkt. Juma Ramadhan wakati Waziri alipozindua huduma za dharura na mahututi katika Hospitali ya Bombo mkoani Tanga.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisikiliza maelezo kutoka kwa mtaalamu wa chumba cha wagonjwa mahututi wakati alipotembelea chumba hicho baada ya uzinduzi wa huduma za dharura na mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga.


Chumba cha wagonjwa mahututi (ICU)
Baadhi ya Wafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Tanga wakifuatilia Hotuba za uzinduzi wa huduma za dharura na mahututi Hospitalini hapo.
Na Emmanuel Malegi-WAJMW-Tanga

Wakazi wa Jiji la Tanga sasa wataanza kupata huduma za uhakika za dharura pamoja na huduma za wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga (Bombo).

Huduma hizo zimefunguliwa rasmi leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati ziara yake ya siku mbili mkoani humo huku akiwahakikishia wananchi wa Tanga kutolazimika kupewa rufaa kwa ajili ya kufuata huduma hizo Muhimbili na KCMC.

“Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli inaendelea kuboresha huduma za afya katika Hospitali za mikoa kwa kujenga jengo la huduma za dharura lililogharimu Tsh. Milioni 211.6 na jingo la kuwahudumia wagonjwa mahututi Tsh. Milioni 350 katika kipindi cha mwaka 2018/19”. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy ameongeza kuwa kuanzishwa kwa huduma hizo za dharura na mahututi zitatatua changamoto zilizokuwepo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga na kuongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2018/19 Serikali iliipatia Hospitali hiyo ya Mkoa Tsh. Milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa mtambo wa kutengeneza Oksijeni (Oxygen Implantation).

Aidha, Waziri Ummy amesema kuanzishwa kwa huduma za dharura na mahututi zinategemewa kupunguza vifo vitokanavyo na dharura kwa asilimia 50, huku akiongeza kuwa Serikali inatarajia kuhakikisha kuwa dawa zinapatikana kwa asilimia 100 Hospitalini hapo, kutengeneza lifti katika wodi ya Galanos, kujenga kituo cha uchunguzi na vipimo pamoja na kujenga jengo la tiba shufaa kwa wateja walioathirika na matumizi ya madawa ya kulevya.

Pamoja na hayo Waziri Ummy ameishukuru taasisi ya ABBOTT chini ya makamu wake wa Rais Bw. Andy Wilson kwa kusaidia ukarabati wa jengo la huduma za dharura kwa wagonjwa pia Waziri amewashukuru Wafanyabiashara wa Mkoa wa Tanga kwa kuchangia kuboresha huduma za afya katika Hospitali hiyo.

Kwa upande Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Serikali  ambaue ni Mkurugenzi huduma za Kinga a Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Leonard Subi amesema uzinduzi huo wa huduma za dharura na chumba cha wagonjwa mahututi ni katika utekelezaji wa mkakati wa Wizara ya Afya kuhakikisha huduma hizo zinapatikana katika Hospitali zote za rufaa nchini.

MWISHO

Alhamisi, 1 Agosti 2019

TANZANIA YAPIGA HATUA KUDHIBITI MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE

- Hakuna maoni
Mgeni rasmi wa mkutano huo wa NTD ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Elias Kwesi akifungua mkutano huo ambao unawakilishwa na waratibu wa mpango huo kutoka mikoa mbalimbali,wadau wa ndani na nje ya nchi

Mkurugenzi wa huduma za Kinga kutoka wizara ya afya Dkt.Leonard Subi akiongea na vyombo vya habari mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo

Mratibu wa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele(NTD) Dkt.Upendo Mwingira akifanya utambulisho wa wageni walioshiriki mkutano wa mwaka wa mapitio na kutengeneza mpango kazi wa mwaka unaofanyika jijini Dar es Salaam

Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani(WHO) Dkt. Christine Musanhu akipeana mkono na Mgeni rasmi wa mkutano huo mwakilishi wa Katibu Mkuu wizara ya afya Dkt.Elias Kwesi

Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa mapitio ya shughuli za kitaifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele

Kaimu Mwakilishi mkazi wa shirika la afya duniani(WHO)Dkt. Christine Musanhu akiongea kwenye mkutano huo.

Mratibu wa NTD Dkt.Upendo Mwingira akisalimiana na mgeni rasmi Dkt.Elias Kwesi

 Picha ya pamoja ya mgeni rasmi na washiriki wa mkutano huo.


TANZANIA  YAPIGA HATUA KUDHIBITI MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE

Na.Catherine Sungura,WAMJW-DSM

Serikali kupitia wizara ya afya imepiga  hatua katika kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele nchi.

Hayo yamesemwa na mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mkurugenzi wa Huduma za Dharura na Maafa wa Wizara hiyo, Dk. Elius Kwesi wakati akifungua mkutano wa mwaka wa mapitio ya shuguli wa mpango wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele na mpango kazi wa mwaka.

Dkt.Kwesi alisema mkutano huo ni muhimu kwani watajadiliana na wadau hao kuona namna watakavyoshirikiana na Wizara hiyo kwa upande wa rasilimali fedha.

"Tuna pengo la rasilimali  mbalimbali  na tumewaita hapa Wadau kujadiliana nao Mpango kazi wetu  na kuangalia namna gani watatusaidia kuziba pengo na kutakavyosaidiana kutekeleza," alisema Dkt.Kwesi

Alisema tangu utekelezaji wa Mpango huo ulipoanza nchini umefanikiwa kupunguza magonjwa hayo kwa kiwango cha asilimia 80.

Awali Mkurugenzi wa huduma za Kinga wizarani hapo Dkt.Leonard Subi alisema magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele yasipodhibitiwa yatapelekea watu wengi kuugua siku zijazo kwani yana athari kubwa na kusababisha upofu na ulemavu kwa jamii.

“mfano ugonjwa wa kichocho kwa watoto huathiri ukuaji na wengine wanaweza kupata saratani katika maisha yao".Alisema Dkt.Subi

Alisema wizara kushirikiana na wadau wa maendeleo imefanya jitihada kubwa na hivyo kufanikiwa kudhibiti magonjwa hayo kwa kiwango kikubwa

"Wilaya ambazo zilikua zimeathirika sana na matende na mabusha miaka kumi iliyopita zilikua takribani 120 lakini hivi sasa zimebaki wilaya 24 ambazo bado tunaendelea na ugawaji kingatiba na trakoma kulikuwa na wilaya 71 na sasa zimebaki wilaya sita tu".

Naye Mratibu wa Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele(NTD) Dkt.Upendo Mwingira amesema kwa upande wa kichocho na minyoo ya tumbo bado inahitajika   kuendelea kuwakinga watoto na baadhi ya wilaya wanaendelea kugawa kingatiba za matende na mabusha pamoja na usubi.

Mwisho

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WAAJIRI WANAOWANYIMA HAKI WANAWAKE LIKIZO YA UZAZI.

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Waandishi wa Habari na Watumishi wa Sekta ya Afya(hawapo kwenye picha), wakati uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji Duniani yaliyofanyika Jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  akieleza jambo mbele ya Waandishi wa Habari na Watumishi wa Sekta ya Afya (hawapo kwenye picha), wakati uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji Duniani yaliyofanyika Jijini Dodoma. Wakwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Dkt. Germana Leyna, na wa mwisho kulia ni Kaimu Katibu mkuu Wizara ya Afya, ambae pia ni Meneja Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma Dkt. Beatrice Mutayoba.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizindua maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji Duniani mbele ya Waandishi wa Habari na Watumishi wa Sekta ya Afya   yaliyofanyika Jijini Dodoma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji Duniani yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma, kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Chakula na Lishe Dkt. Germana Leyna wa mwisho Kulia ni Mwakilishi kutoka UNICEF James Gitau.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akifuatilia maelezo kuhusu huduma ya unyonyeshaji katika maeneo ya kazi kutoka Afisa kutoka Wizara  ya Afya Bi Tufingene Malambugi wakati uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji Duniani yaliyofanyika Jijini Dodoma.


SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WAAJIRI WANAOWANYIMA HAKI  WANAWAKE  LIKIZO YA UZAZI. 

Na Rayson Mwaisemba, WAMJW- DODOMA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imetangaza kuanza kuwachukulia hatua Waajiri wote ambao wanavunja Sheria kwa kugandamiza haki ya kupata likizo ya uzazi kwa wanawake pindi anapojifungua. 

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji Duniani yaliyofanyika katika ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma, yenye kauli mbiu ya “Wawezeshe wazazi kufanikisha unyonyeshaji”.

"Haki ya Mwanamke Kuzaa na kupata likizo ya uzazi ni haki yake ya asili, haitakiwi kuwekewa vikwazo au changamoto yoyote, kwahiyo nitoe wito kwa wanawake ambao wanafanya kazi, ni haki yako kupata likizo, asije mtu anakwambia anaijaza kazi yako kwakuwa umetoka likizo ya kujifungua, tuambie sisi, tutachukua hatua, na huyo Mwajiri  tutamtangaza kuwa ni adui wa Wanawake na Watoto wa Tanzania ".Amesema Waziri Ummy. 

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa Serikali ipo katika mpango wa kuanzisha dawati la kutoa malalamiko litaloshughulikia kupigania na kutetea haki za wanawake kupata likizo ya uzazi, jambo litalosaidia kudhibiti tabia za baadhi ya Waajiri kukandamiza haki za wanawake baada ya kujifungua.

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amesema kuwa takribani asilimia 97 ya watoto wenye umri chini ya miaka miwili wananyonyeshwa maziwa ya mama, hii inaonesha kuwa hali ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama imepungua ikilinganishwa na takwimu ya mwaka 2015/2016 ambayo ilikuwa ni asilimia 98.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa idadi ya watoto wanaoanzishiwa kunyonyeshwa maziwa ya mama kwa wakati sahihi (ndani ya saa moja baada ya kuzaliwa) ni asilimia 53 ikilinganishwa na asilimia 51 ya mwaka 2015/2016

Aliendelea kusema kuwa, idadi ya watoto wanaonyonyeshwa maziwa ya mama pekee bila kupewa maji, vinywaji na vyakula vingine katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo baada ya kuzaliwa ni asilimia 58 ikilinganishwa na asilimia 59 ya mwaka 2015/2016.

Hata hivyo, Waziri Ummy amesema kuwa Idadi ya watoto wenye umri wa miezi 6 hadi 23 wanaolishwa chakula kinachokidhi vigezo vya ubora kilishe ni 35%, huku kiwango kikionekana kuongezeka ikilinganishwa na asilimia 10 kwa mwaka 2015/2016. 

Mbali na hayo, Waziri Ummy amesema kuwa, takwimu za utafiti wa hali ya lishe nchini za mwaka 2018 zinaonyesha kuwa asilimia 31 ya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano wamedumaa ikilinganishwa na asilimia 34 ya mwaka 2015/2016, huku sababu kubwa ya ikiwa ni ulishaji usio sahihi ambao huchangiwa na majukumu mengi yanayomkabili mama na hivyo kukosa muda wa kutosha wa kumtunza mtoto.

Naye Mwakilishi kutoka UNICEF Bw. James Gitau amesema kuwa, unyonyeshaji ni moja ya njia muhimu kuhakikisha Afya Bora kwa maisha ya mtoto, hivyo kutoa wito kwa wanahabari kuhakikisha wanapeleka Elimu kwa wananchi hususan wanawake kuhakikisha wanafahamu umuhimu wa kunyonyesha Watoto mfululizo miezi sita ya mwanzo,

Pia, Bw. James Gitau ametoa wito kwa Serikali kuongeza nguvu katika uhamasishaji juu ya umuhimu na haki ya Watoto kunyonyeshwa, amesema jambo hili litasaidia kuokoa watoto kupata magonjwa yanayotokana na kukosa virutubisho kutoka kwa maziwa ya mama.

Mwisho.