Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumanne, 13 Agosti 2019

WATOA HUDUMA ZA AFYA MWANZA WAFUNDWA

- Hakuna maoni
Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora wa Huduma za Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Joseph Hokororo akieleza jambo mbele ya Watoa Huduma na Watumishi wa Sekta ya Afya wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), inayoendelea Jijini Mwanza.

Afisa Afya ya Mazingira kutoka Taasisi ya JBHN Said Chibwana akitoa Elimu kwa Wataalamu wa Huduma za Afya na baadhi ya  Watumishi wa Sekta ya Afya  wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Afisa kutoka Kitengo cha Uhakika Ubora wa Huduma Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Radenta Bahegwa akijibu hoja kutoka kwa Wataalamu wa Huduma za Afya na baadhi ya  Watumishi wa Sekta ya Afya  wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Mtaalamu wa Maabara Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikikishi MUHAS Akili Mawazo Mwakabhana akisisitiza jambo mbele ya Watoa Huduma na Watumishi wa Sekta ya Afya wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), Semina hiyo inaendelea Jijini Mwanza.

Afisa kutoka Kitengo cha Dharura na Maafa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Alex Sanga akifafanua jambo mbele ya Watoa Huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), inayoendelea Jijini Mwanza

Baadhi ya Watoa Huduma za Afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando wakifuatilia mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Baadhi ya Watoa Huduma za Afya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Seketoure wakifuatilia mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline).

Baadhi ya Watoa Huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya wakifuatilia kwa makini  Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), mafunzo yanaendelea Jijini Mwanza.

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Wataalamu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto sambamba na Watoa Huduma za Afya na Watumishi wa Sekta ya Afya baada ya kumaliza Wiki ya kwanza ya Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa (IPC guideline), Jijini Mwanza.



WATOA HUDUMA ZA AFYA MWANZA WAFUNDWA

Na Rayson Mwaisemba WAMJW-MWANZA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yawafunda Watoa Huduma za Afya Jijini Mwanza  kuwakumbusha namna ya utoaji huduma kwa kufuata misingi na taratibu za utoaji huduma kwa Wagonjwa ili kupunguza maambukizi mapya na vifo visivyo na ulazima.

Hayo yamejiri wakati wa Semina ya mafunzo juu ya njia bora ya namna ya kujikinga na kudhibiti magonjwa (Maambukizi) kwa kufuata kanuni, miiko na taratibu za utoaji huduma kwa mgonjwa, iliyofanyika Jijini Mwanza ikiwa ni moja kati ya mikoa iliyo katika hatari ya kupata ugonjwa wa Ebola.

Katika Mafunzo hayo yaliyo andaliwa na Wizara ya Afya imedaiwa kuwa Tanzania ipo kwenye hatari ya kupata wagonjwa wa Ebola kutokana na mwingiliano mkubwa wa watu na ukaribu na Nchi ya Uganda na Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo ambako Mlipuko unaendelea.

Kwa taarifa za Shirika la Afya Duniani (WHO) inakadiriwa kuwa Wagonjwa 2577 wamethibitika kuwa na Ugonjwa wa Ebola, huku Wagonjwa 1790 wakipoteza maisha tokea mlipuko huo ulipojitokeza Agosti 2018, huku Wataalamu wa Afya 131 walipata maambukizi, ambapo 41 kati yao wamepoteza maisha.

Aidha, Serikali ya Tanzania imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha utayari wa kukabiliana na tishio la Ugonjwa huo ili kuhakikisha hauingii nchini, ikiwemo kuelimisha jamii njia za kujikinga na Ugonjwa ili kuzuia usiingie nchini, na kutoa Elimu kwa Watoa huduma za Afya juu ya kumuhudumia mtu mwenye dalili za Ebola endapo atatokea.

Watoa huduma wanatakiwa kuzingatia taratibu za kujikinga na kudhibiti maambukizi (IPC Standard precautions) kwa kadri Miongozo inavyoelekeza wakati wote watoapo huduma kwa Wagonjwa, jambo litalosaidia kuwaepusha kupata maambukizi, au kumsaidia mgonjwa kupata maambukizi mapya wakati wa matibabu.

Afisa Mkuu Uhakiki Ubora kutoka Wizara ya Afya Dkt. Joseph Hokololo amesema kuwa zaidi ya watu milioni 1.4 Duniani wanaugua magonjwa yanayosababishwa na kupata maambukizi mapya wakati wakupata huduma ya afya, hii hutokana na Watoa huduma za Afya kutofuata taratibu za namna ya kutoa huduma.

Aliendelea kusema kuwa Asilimia 15 ya Wagonjwa hupata maambukizi ya magonjwa mapya pindi waendapo kupata huduma za Afya katika Vituo vya kutolea Huduma za Afya, kutokana na kutofuatwa kwa taratibu, kanuni za miongozo ya kutoa huduma za Afya (IPC Guideline, SOP).

Kwa Upande wake Afisa kutoka Kitengo Uhakiki Ubora Wizara ya Afya Dkt. Chrisogane Justine amesema kuwa kufuata taratibu za utoaji huduma kama kanuni za uoshaji sahihi wa mikono kutamsaidia Mtoa huduma kuzuia kusambaza maambukizi ndani ya Kituo cha kutolea huduma za Afya na nje.

Licha ya changamoto za upatikanaji wa huduma za maji safi kwa baadhi ya Vituo vya Afya, Dkt. Chrisogone Justine German amesisitiza kuwa ni muhimu kwa Mtoa huduma za Afya kuhakikisha ananawa mikono yake vizuri kwa sabuni na maji safi ili kuepuka kusambaza maambukizi kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Akitoa Elimu juu ya namna ya kujikinga dhidi ya maambukizi mapya yanayotokea wakati wa matibabu kutokana na baadhi ya Watoa huduma kutofuata taratibu na miongozo Dkt. Radenta Bahegwa amesema kuwa asilimia 40 ya magonjwa yanayopatikana katika vituo vya kutolea huduma za Afya nayosababishwa na kutofuata kwa taratibu za miongozo ya utoaji huduma.

“Asilimia 40 ya ya magonjwa yanayopatikana katika Vituo vya kutolea huduma za Afya husababishwa na kutofuata miongozo (IPC Guidline), ndiomaana asilimia 80 ya UTI zinazoibuka katika Vituo vya Afya zinatokana na kukosea kuweka kifaa cha kupitisha haja ndogo” alisema Dkt. Radenta.

Mtaalamu kutoka Kitengo cha Dharura na Maafa Dkt. Alex Sanga amesema kuwa katika watu 100, watu 5 hadi 10 wanakuwa katika hali mbaya ya ugonjwa wa kipindu pindu, hivyo ametoa wito kwa Watoa huduma kuhakikisha wanafuata miongozo na taratibu wakati wa kutoa huduma ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi mapya katika jamii.

“Tafiti za Shirika la Afya Duniani zinonesha kuwa ndani ya miaka 3 (2015-2018) kati ya watu 33,421, watu 542 walipoteza maisha, huku katika watu 100, watu 5 hadi 10 wanakuwa katika hali mbaya ya ugonjwa wa kipindu pindu, hivyo juhudi za makusudi zinatakiwa kuchukuliwa” alisema Dkt. Sanga.

Naye Mtaalamu wa Maabara kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi MUHAS Akili Mawazo Mwakabhana amesisitiza umuhimu wa kufuata taratibu na miongozo wakati wa kutoa huduma kwa mgonjwa kuzuia maambukizi mapya kwa Mgonjwa au Mtoa huduma za Afya jambo ambalo litasaidia kupunguza idadi ya Wagonjwa na kuokoa fedha ambazo zingetumika katika matibabu. 

Kwa upande wake Mfamasia kutoka Hospitali ya Kanda Bugando Francisco Chibunda ametoa wito kwa watoa huduma za Afya kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwa kufuata miiko na taratibu na miongozo inavyoelekeza jambo litalosaidia kuondoa tatizo la usugu wa magonjwa (Wadudu) kutokana na matumizi mara kwa mara ya dawa, ambayo daktari angeweza kuyazuia kwa kufuata taratibu na miongozo wakati wakutibu ugonjwa.

“Tunapoteza nguvu kubwa, tunapoteza rasilimali nyingi kwenye dawa na matibabu, mwisho wa siku tunasababisha maambukizi mapya, nah ii hupelekea usugu wa magonjwa , kwa hiyo tubadilike” Alisema Chibunda.

Mwisho.

Jumatatu, 12 Agosti 2019

WAZIRI UMMY ASHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA ZOEZI LA KUTAMBUA MAITI NA KUJULIA HALI MAJERUHI

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akimjulia hali mmoja wa majeruhi wa moto aliyelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.


Waziri Ummy akizungumza na baadhi ya wananchi waliojitokeza katika chumba cha kuhifadhia maiti ili kutambua miili ya ndugu zao.

 

Picha mbalimbali zikionesha Waziri Ummy akishiriki katika kuhakikisha wananchi wanatoka salama katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Morogoro kwa kuweka dawa ili wananchi wakanyage wakati wa kutoka mara baada ya kuaga kuondoa madhara wanayoweza toka nayo katika chumba hicho.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula akiwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Kambi pamoja viongozi wengine wakiwa nje ya chumba cha kuhifadhia maiti katika Hopitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro katika kuhakikisha zoezi la kutambua maiti linaenda vizuri.

Na.WAMJW - Morogoro

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu (Mb), leo ameshiriki katika zoezi la utambuzi na uhifadhi wa miili ya marehemu wa ajali ya lori la mafuta lilioanguka na kuwaka moto katika eneo la Msamvu Itigi mjini Morogoro.

Pamoja na shughuli hizo, Mhe.Waziri Ummy Mwalimu amewatembelea majeruhi na kuwajulia hali, kuwapa pole na kuona mwendelezo wa huduma za matibabu wanazopata na kuwatakia kheri ya kupona haraka na kurejea katika shughuli za ujenzi wa Taifa majeruhi wote ambao bado wanapata matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Aidha, mara baada ya kuwajulia hali alizungumza na ndugu, jamaa na rafiki wa walioathirika na ajali hii iliyopoteza maisha wa wananchi 69 na kusababisha majeruhi 65 ambao maziko ya awamu ya kwanza yanafanyika leo katika makaburi ya Mlima Kolla mjini Morogoro huku majeruhi wakiendelea na tiba Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Morogoro.

Aidha, amezidi kuwasihi na kuwahimiza wananchi kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu katika hali ya kawaida kibinaadamu na kuwahakikishia kuwa Serikali inazidi kuweka nguvu zaidi katika kuokoa maisha ya majeruhi wote katika Hospitali walizopo ikiwemo Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar Es Salaam.

"Naomba kuwathibitishia wataalamu wetu kwa pamoja wameunganisha nguvu kutoka Kitengo cha Dharura Muhimbili, Amana, Mwananyamala, Benjamin Mkapa Dodoma, wote wako hapa ili kuokoa maisha ya ndugu zetu. Na wenzetu wa MSD pamoja na wadau wengine hapa mkoani wamehakikisha kila kinachohitajika kwa waathirika wetu kimepatika na kiko hapa ili huduma muafaka itolewe kwa wakati kulingana na mahitaji ya aina ya janga lenyewe," amesema Waziri Ummy.

Ajali hii ilitokea siku ya Jumamosi Agosti 10, 2019 mida ya saa 2 asubuhi baada ya lori la mafuta lililokua limebeba shehema ya mafuta aina ya petrol na dizeli likielekea Mafinga mkoani Iringa kumkwepa mwendesha pikipiki aliyekatisha ghafla barabarani hivyo gari kupoteza uelekeo na kuanguka kisha kuwaka moto.

Mwisho.

Alhamisi, 8 Agosti 2019

TEKNOLOJIA YA NANO FILTER YAWAVUTIA VIONGOZI WA WIZARA JIJINI ARUSHA

- Hakuna maoni

Dkt. Askwar Hilonga akiwakaribisha Viongozi wa Wizara wakiongozwa na Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi na wengineo wakati walipotembelea Chuo Kikuu cha Nelson Mandela Jijini Arusha.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Nelson Mandela Prof. Emmanuel Luoga akiangalia tuzo ya ubunifu wa teknolojia ya maji aliyopewa Dkt. Askwar Hilonga kwenye kikao cha dunia cha masuala ya afya (World Health Assembly) kilichofanyika Jijini Geneva, Uswisi mwezi Mei mwaka huu.

Picha ya pamoja katika ofisi ya Kaimu Mkuu wa chuo cha Nelsona Mandela Jijini Arusha.


Mbunifu wa Teknolojia ya Nano Filter Dkt. Askwar Hilonga akiwaonesha viongozi sehemu ambayo ubunifu huo ulipoanzia katika chuo cha Nelson Mandela.

Mifupa ya wanyama inayotumika katika Teknolojia ya Nano Filter kuchuja na kutibu maji kwa ajili ya matumizi.

Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi akiangalia chengachenga za mifupa inayotumika na teknolojia ya Nano Filter katika kuchuja na kutibu maji ya kunywa.

Dkt. Hilonga akitoa maelezo kwa viongozi wa Wizara wakati walipotembelea maonesho ya Sabasaba kwenye banda la Nano Filter.

Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi akiwa na Dkt. Khalid Massa, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Wedson Sichalwe, mbunifu wa Teknolojia ya Nano Filter Dkt. Askwar Hilonga na wajumbe wengine wakiwa katika picha ya pamoja nje ya banda la Nano Filter katika maonesho ya Nanenane Jijini Arusha.


Teknolojia ya Nano Filter iliyofungwa katika moja ya Shule Jijini Arusha.

Baadhi ya Wananchi waliofika katika ofisi hiyo kwa ajili ya kujaziwa maji.

Picha ya pamoja ya viongozi wa Wizara wakiwa na Baadhi ya Wafanyakazi wa Nano Filter nje ya ofisi zao.
Teknolojia ya Nano Filter ikiwa imefungwa katika Maonesho ya Nanenane Jijini Arusha.
Na Emmanuel Malegi-Arusha


Viongozi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakiongozwa na Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi wamemtembelea mbunifu wa teknolojia ya kusafisha maji ambaye pia ni mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Nelson Mandela kilichoko Arusha Dkt. Askwar Hilonga.

Katika ziara hiyo Dkt. Hilonga amewaonesha viongozi hao Teknolojia iitwayo Nano Filter yenye uwezo wa kusafisha maji, kuondoa bacteria na virusi, huondoa fluoride na madini yote ambayo hayatakiwi kwa binadamu na kuyafanya maji kuwa safi na salama kwa watumiaji na kwa gharama nafuu zaidi.

Dkt. Hilonga ana tuzo 17 kutoka taasisi na mashirika mbalimbali kutokana na ubunifu huo huku tuzo yake kubwa ikiwa ni ile aliyoipata kwenye kikao cha dunia cha masuala ya afya (World Health Assembly) kilichofanyika Jijini Geneva, Uswisi mwezi Mei mwaka huu.

Jumatano, 7 Agosti 2019

HABARI PICHA : ZOEZI LA UTAYARI KUKABILIANA NA UGONJWA WA EBOLA KATIKA WILAYA YA BUHIGWE MKOANI KIGOMA.

- Hakuna maoni
Na Englibert Kayombo, Kigoma


Watoa huduma za afya kutoka Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma wakiwa wamembeba mgonjwa anayehisiwa kuwa na ugonjwa wa ebola tayari kumpatia huduma ya kwanza katika zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo usiingie nchini.

Kufuatia nchi ya jirani (DRC) kuendelea kukabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola tangu Agosti mwaka 2018. Serikali ya Tanzania imeendelea kuchukua tahadhari za ugonjwa huo kwa kupima utayari wa Watoa huduma za Afya kwa mikoa iliyomo hatarini kuathiriwa na ugonjwa huo.

Serikali kupitia uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Menejimenti ya Maafa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, pamoja na wadau wa maendeleo; WHO, FAO, USAID, HRH2030, Shirika la Msalaba Mwekundu (RED CROSS), na USAID Global Health Supply Chain Programu, inaendelea na zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo katika Wilaya za Mkoa wa Kigoma.

Zoezi hilo linalenga kuwaimarisha watumishi hao katika maeneo maalum ikiwemo ya uratibu, utambuzi na ufuatiliaji wa wagonjwa iwapo atagundulika, matibabu ya wagonjwa, uchukuaji na usafirishaji wa sampuli na kuthibitisha maabukizi pamoja kuimarisha mifumo ya utambuzi wa masuala ya Afya kwa kila abiria wanaopita kwenye mipaka ya mkoa wa Kigoma.


Mwezeshaji wa zoezi la upimaji wa utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Dkt. Christopher Mnzava akifafanua umuhimu wa kuzingatia muda wakati wa maandalizi ya kumhudumia mgonjwa anaehisiwa kuwa na ugonwja wa ebola kwa watoa huduma za afya Katika Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma.

Watoa huduma za afya mara baada ya kumhudia mgonjwa wa ebola wakiwa wamebeba mifuko maalum kwa ajili ya utunzaji wa mavazi na vifaa vilivyovyotumika kuhumdumia mgonjwa kabla ya kuyateketeza.

Dkt. Refaya Ndyamuba kutoka Shirika la Afya Duniani akielekea kukagua kituo kitachokutumika kuhudumia wagonjwa wa ebola katika Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma katika zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa ebola usiingie nchini linaloendelea Mkoani Kigoma.

Bi. Consolata Felix Muuguzi kutoka Wizara ya Afya(aliyesimama kulia) akikagua watoa huduma za afya katika Kituo cha hudumia wagonjwa wa ebola katika Wilaya ya Buhigwe namna wanavyosafisha kitanda kilichotumika kumbeba mgonjwa wa ebola katika zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa ebola usiingie nchini linaloendelea kufanyika mkoani humo.

"Mahema ya kuhudumia wagonjwa wa ebola yanatakiwa kuwa na hewa safi muda wote" Dkt. Refaya Ndyamuba kutoka Shirika la Afya Duniani akifungua sehemu ya kuingiza hewa kwenye hema linalotumika kuhudumia wagonjwa wa ebola wakati wa zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo katika Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma. 

Mtoa huduma za afya katika Wilaya ya Buhigwe akinawa kwa maji safi yaliyochanganywa na kemikali ya "Chroline" mara baada ya kutoka kumhudumia mgonjwa wa ebola wakati wa zoezi la tayari wa kukabiliana na ugonjwa huo


Jumatatu, 5 Agosti 2019

WATOA HUDUMA ZA AFYA KIGOMA KUPIMWA UTAYARI KUKABILIANA NA EBOLA

- Hakuna maoni
Consolata Felix kutoka Wizara ya Afya (aliyesimama kushoto) akifuatilia zoezi la vitendo la utayari wa kukabiliana ugonjwa wa ebola kwa watoa huduma za afya katika jamii.
Washiriki wa zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa ebola Mkoa wa Kigoma wakiwa kwenye mazoezi ya mezani kujadili mikakati ya kudhibiti ugonjwa huo usiingie nchini mapema leo Mjini Kigoma.

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Bw  Daniel Machunda akisema jambo kwa washiriki wa kikao kazi katika zoezi la upimaji wa utayari wa kukabiliana na ugonjwa ebola (hawapo pichani) mapema leo Mjini Kigoma.

Picha ya pamoja ya mgenu rasmi Bw . Daniel Machunda (aliyeketi kati kati) wadau wa maendeleo na washiriki wa zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa ebola nchini katika Mkoa wa Kigoma


Na Englibert Kayombo, Kigoma.

SEREKALI ya Tanzania kupitia uratibu wa wa ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  zitafanya zoezi la kupima utayari kwa watoa huduma za afya katika kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika Mkoa wa Kigoma.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Maafa  Ofisi ya Waziri Mkuu Bwana Bashiru Taratibu wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha wadau kutoka ndani nan je ya nchi kujadili mikakati iliyopo kudhibiti ugonjwa huo usiingie nchini.

Amesema kuwa zoezi hilo litazingatia dhana ya afya moja ambayo hujumuisha sekta ya afya ya mifugo,binadamu,mifugo,wanyamapori na mazingira katika kujiandaa,kufuatilia na kukabili magonjwa ambayo huambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda binaadamu.

"Zoezi hili litapima uelewa wa jamii kuhusu namna ambavyo wanapaswa kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa ebola, hivyo wakati wa zoezi watoa huduma za afya na sekta zingine watakuwa wakifanya zoezi hilo kwa vitendo"alisema

Bw. Taratibu amesema kuwa zoezi hilo litafanyika kuanzia tarehe 5 hadi 9 Agosti katika vituo vya kutolea huduma za afya na maeneo ya mipaka ya Mkoa wa Kigoma. Aliendelea kwa kusema kuwa katika zoezi hilo watoa huduma wa afya watakuwa wakifanya zoezi hilo kwa vitendo namna ya kumuhudumia mgonjwa wa ebola atakapogundulika.

Mgeni rasmi katika kikao hicho Daniel Machunda Kaimu katibu Tawala Msaidizi rasilimali watu kwaniaba ya katibu wa Mkoa wa Kigoma Rashid Mchata alisema Mkoa wa Kigoma una njia nyingi zisizo za halali za mipakani(panya road)ambazo zinachangia hatari ya ugonjwa wa Ebola kuingia nchini.

Aliwataka wananchi kuchukua tahadhari hasa wale wanaovuka mipaka kwenda nchi za jirani."Ikumbukwe kuwa zoezi linahusu upimaji wa utayari kwa Mkoa wa Kigoma na hakuna mgonjwa yeyote wa ebola aliyeripotiwa hadi sasa nchini"alisema Machunda

Mganga mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt Paul Chawote alisema kuwa nchi ya jirani ya DRC(Congo)imeendelea kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola tangu kulipotiwa mlipuko wa ugonjwa huo mnamo mwezi Agosti mwaka 2018.

Dkt Chawote amesema kuwa idadi ya vifo vilikuwa 1823 ikiwa ni sawa na asilimia 67 ya idadi watu walioathiriwa na ugonjwa huo huku nchi ya Uganda ambayo inapakana na DRC na Tanzania imekuwa na wagonjwa 3 wa Ebola kwa mujibu wa taarifa maambukizi hayo yametoka DRC.

"Kwenye mipaka yetu ya DRC na Burundi kuna mwingiliano mkubwa wa watu unaochangiwa na shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi hivyo vinachangia hatari zaidi ya ugonjwa wa Ebol kuingia nchini"alisema Dkt Chawote

Remidius Kakulu Afida Afya mwandamizi toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto amesema mpaka sasa mipaka iliyorasmi yote imedhibitiwa na tayati Serikali imefunga vipima joto vya kisasa katika mipaka yote iliyo rasmi.

"Kuna ile mipaka ambayo siyo rasmi ambayo ipo kwenye vijiji na maeneo mengine tunawaomba Viongozi wa Vijiji pamoja na wananchi kutoa taarifa pale mgeni anapoingia au kumpeleka kituo cha afya ili aweze kupimwa"alisema

Mwisho

WIZARA YA AFYA KUDHIBITI KIFUA KIKUU MAGAREZA 15 NCHINI

- Hakuna maoni
Meneja Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma Dkt.Beatrice Mutayoba akiongea na washiriki wa mafunzo hayo(hawapo pichani) kwenye bwalo la Magereza Ukonga

Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Jeshi la Magereza Owesu Ngalama akifungua mafunzo ya tathimini ya udhibiti wa TB katika Magereza 15 nchini

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza mgeni rasmi(hayupo pichani) kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo


Picha ya pamoja ya mgeni rasmi na washiriki wa mafunzo hayo ambayo yana lengo la kuyafikia magereza kumi na tano hapa nchini katika kutathimini hali ya huduma ya TB kwenye magereza nchini

Na. Catherine Sungura, WAMJW-DSM
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti kifua kikuu na Ukoma kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza nchini wanaanza afua ya ufuatiliaji wa kutathimini hali ya huduma za kutokomeza kifua kikuu katika magereza nchini.
Hayo yamesemwa na Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Jeshi la Magereza (CP) Owesu Ngalama wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa maofisa wa jeshi hilo yanayofanyika kwenye bwalo la magereza ukonga jijini hapa.
CP Ngalama alisema kuwa afua hiyo itasaidia jeshi la magereza kuweza kubaini hali ya TB kwenye magereza kwani wanaoingia kwenye magereza ni wana jamii hivyo itasaidia kubaini ugonjwa huo kwa wafungwa na kwa jamii kwa ujumla
“Ugonjwa huu unaambukizwa kwa hewa hivyo kwa tathimini hii itasaidia kuleta utaalam mkubwa kwa wataalam wetu wa tiba waliopo kwenye jeshi kwani hali ya TB sio kubwa kwenye magereza  ila lengo ni kuhakikisha hakuna maambukizi makubwa kwani wafungwa wanaingia na kutoka”.Alisema CP Ngalama
Aidha,ameishukuru wizara ya afya kwa kuendelea kushirikiana nao kwa muda mrefu hususan kwenye utoaji huduma za afya ikiwemo utoaji wa dawa,vifaa na vifaa tiba pamoja na masuala ya lishe kwenye vituo vya afya vilivyopo kwenye magereza nchini.
Naye Meneja Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma (NTLP) kutoka Wizara ya Afya Dkt. Beatrice Mutayoba alisema ugonjwa wa Kifua Kikuu bado ni jangwa kwani bado kuna takribani watu laki moja na elfu hamsini na nne wanakadiriwa kuugua kifua kikuu kila mwaka na inakadiriwa vifo elfu ishirini na saba  kila mwaka nchini.
Dkt. Mutayoba alisema kifua kikuu kinaweza kumpata mtu yeyote kwani maambukizi yake ni ya njia ya hewa hivyo yapo makundi hatarishi zaidi ikiwemo magereza hivyo wanaweka jitihada zaidi kuyafikia makundi hayo ili kutokomeza kifua kikuu ifikapo 2030.
“kama nchi tumepiga hatua kubwa sana kutokomeza ugonjwa huu hivyo tunaongeza juhudi zaidi kwenye makundi hatarishi ikiwemo magereza,migodini,wavuvi ili kuwafikia kwa karibu na kuhakikisha tunapunguza maambukizi ndani ya magereza na maeneo haya”.Alisisitiza
Hata hivyo alisema mkakati wa kudhibiti kifua kikuu upo kwa wananchi wote hivyo  kama mpango wanaendelea kutoa elimu kwa watanzania wote mara waonapo dalili waende kwenye vituo vya afya kwani wizara ya afya inatoa dawa,vipimo  na huduma za kifua kikuu bila malipo kwenye vituo vya kutolea huduma za afya “Magerezani tunaweza utaratibu kwa wanaoingia kuwe na taratibu za uchunguzi ili anapokutwa na kifua kikuu waanze matibabu kwani unapoanza matibabu ndani ya wiki mbili huwezi kuambukiza wengine”.Alisema Dkt. Mutayoba
Mikoa kumi na tano itakayoanza na utekelezaji  huo ni pamoja na Dar es salaam, Dodoma, Iringa, Kagera, Kilimanjaro, lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Mwanza, Pwani, Shinyanga, Singida, Tabora na Tanga.
Mwisho

PREPARING THE HEALTH WORKFORCE TO MAKE THE MOST OF DATA

- Hakuna maoni
DataUseForHealth


Health workers exchange learnings about Tanzania's electronic immunization registry. Photo: PATH/Trevor Snapp. For nearly thirty years as a health worker in Tanzania, Salome has used pen and paper to record patient data. A digital transformation promises to streamline her work and improve patient care. 

Digital health solutions increase data quality and accessibility, but to be effective and improve patient outcomes, health workers must know how to make the most of the information. For many like Salome, Tanzania’s digital transformation will require retraining and developing new digital literacy skills. 



Building the workforce of the future 
The Data Use Partnership—a collaboration between the Government of Tanzania and PATH—aims to equip Tanzania’s health sector and workforce with skills for the country’s changing digital landscape. This includes training existing and future generations of health workers to make better use of digital platforms and data. 

To facilitate trainings, the Data Use Partnership established the Capacity Building Consortium (CBC). Made up of three universities, two health research and training institutes, and zonal health training centers around the country, the CBC fosters a culture of data use and builds the capacity of health workers to identify and solve problems, measure performance, allocate resources, track patients, support clinical decisions, and streamline service delivery. 



Making the most of data 
“In the health sector, a lot of data are collected, but aren’t necessarily put into efficient use when making crucial decisions,” explains Professor Flora Lucas Kessy, Secretariat Chairperson of the CBC and instructor at the Tanzania Training Center for International Health. “The consortium was formed to build the capacity of health workers through both in-service and pre-service training.” 

The consortium is building the health workforce’s capacity by: 
• Developing trainings and innovative platforms: The Data Use Partnership is developing a new series of short-term trainings, using costeffective and innovative platforms. Trainings will be offered in person through zonal health resource centers to ensure greater accessibility, and through eLearning modules that the CBC aims to integrate under a single government-owned National Health eLearning platform.



 • Establishing new delivery methods: eLearning platforms can help deliver trainings to rural health providers, where long distances, limited resources, and poor transportation may otherwise be a barrier to education. “There are lots of current innovations in this country in terms of mobile phone and smartphone use,” explains Professor Kessy. “We can use digital platforms to deliver critical courses even to health providers that are very far away.” 

• Increasing focus on data use and analytics: The CBC will review, develop, and standardize curricula for data analytics training, so that the workforce is operating from a place of common experience. With more than 136 institutions offering certificates and diplomas in health and allied sciences programs, it’s critical that students graduate with a shared skillset, understanding, and appreciation for data use. 



• Fostering government ownership and peer learning: The CBC also recognizes the importance of ensuring that trainings are delivered by their own peers and experts, instead of an outside institution or implementing partner. “Health workers have to feel that they’re being trained by one of their own,” explains Mr. Tumaini Macha, Assistant Director, Monitoring & Evaluation from the Ministry of Health. “This mentorship model is even more efficient and ensures that trainers understand the need in different areas.” 

Achieving digital transformation 
"Having a curriculum that’s strong in data use ensures that whoever graduates from universities and other academic institutions, goes home with knowledge on how to deliver on data use,” explains Professor Kessy. “We've been able to bring together five different prime institutions that have their own different ways of operating. It’s so unique that we can work together, forget our own university boundaries, and build an open consortium that’s focused on data use.” 


The CBC is critical to Tanzania achieving digital transformation. By educating and training the existing workforce and preparing a pipeline of future talent, the health workforce will be able to make optimal use of digital tools, ultimately leading to better patient care and more equitable access to health services.

Jumamosi, 3 Agosti 2019

WAZIRI UMMY AKABIDHI MASHINE YA UPULIZIAJI DAWA ZA KUDHIBITI WADUDU MKOANI TANGA

- Hakuna maoni
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati wa hafla ya makabidhiano ya mashine ya kupulizia dawa za kudhibiti wadudu wadhurifu yaliyofanyika katika viwanja vya Tangamano Jijini Tanga.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa afya wa jiji la Tanga jinsi wanavyowanasa mbu kwa ajili ya kuwafanyia tafiti mbalimbali wakati wa hafla ya makabidhiano ya mashine ya upuliziaji dawa za kuangamiza wadudu wadhurifu iliyofanyika katika viwanja vya Tangamano jijini Tanga.

Mkurugenzi wa Kinga kutoka Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi akiongelea mkakati wa wizara hiyo wa kudhibiti mbu na wadudu wadhurifu ambao utatekelezwa nchi nzima, hapo ni katika makabidhiano ya mashine ya kupulizia dawa za kudhibiti wadudu wadhurifu yakiyofanyika katika viwanja vya Tangamano Jijini Tanga.


Viongozi wa Jiji la Tanga wakifurahia makabidhiano ya Mashine ya upuliziaji dawa za kudhibiti wadudu wadhurifu kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu. Makabidhiano hayo yalifanyika katika viwanja vya Tangamano jijini humo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. Thobias Mwilapa na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Bw. Mustafa Mhina wakiangalia jinsi mashine ya upuliziaji inavyofanya kazi.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (katikati), Mkurugenzi wa kinga wa Wizara hiyo Dkt. Leonard  Subi (wa kwanza kushoto) wakiwa pamoja na Mabwana Afya wa Jijini Tanga wanaotekeleza mkakati wa kudhibiti mbu na wadudu wadhurifu mkoani humo.

Na Emmanuel Malegi-WAJMW, Tanga

Jiji la Tanga limekua la pili kupata mashine za kupulizia dawa za kuua mbu na wadudu wadhurifu waenezao magonjwa mbalimbali ikiwa ni mkakati wa Wizara ya Afya kwa kushirikiana na TAMISEMI katika kudhibiti wadudu hao.

Akikabidhi mashine hiyo kwa uongozi wa Jiji la Tanga, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema mkakati huo ni wa miaka mitano (2019-2024) na unalenga kuhakikisha mbu na wadudu wadhurifu wanadhibitiwa kwa njia ya utengamano na ameiomba jamii ishiriki kikamilifu katika kupambana na wadudu hao.

“Wizara yangu imeagiza mashine nane za kisasa(foggig mashine) zenye uwezo mkubwa wa kupulizia na zinabebwa na magari na kupuliza eneo kubwa kwa wakati mmoja, hivyo naomba jamii ihakikishe inashiriki kikamilifu katika kupambana na wadudu hawa dhurifu”. Amesema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy ameongeza kuwa katika kuhakikisha mkakati huo unafanikiwa ni vema mikoa ikawekeza katika maeneo ya msingi am bayo ni pamoja na ushiriki wa jamii, sekta binafsi na wadau  kushiriki katika kudhibiti wadudu kwa njia shirikishi zinazolenga kuharibu mazalia ya wadudu. Mikoa kuimarisha mfumo wa ufuatiliaji wa mbu na wadudu wadhurifu katika ngazi zote na kupanga njia madhubuti za udhibiti wa wadudu hao.

Waziri Ummy amesema katika kuhakikisha mkakati huu unatekelezwa, Wizara ya afya kwa kushirikiana na TAMISEMI imetoa maagizo kwa kila Mkoa, Wilaya na Halmashauri zote ziweze kuyatekeleza ikiwa ni pamoja na kuandaa mipango ya utekelezaji wa udhibiti wa mbu na wadudu wadhurifu ambayo itakua mtaa kwa mtaa, Halmashauri kuhakikisha zinaishirikisha jamii katika ngazi zote za mapambano haya ya mbu na wadudu wadhurifu.

Pia Waziri Ummy amezitaka Halmashauri kufanya tathmini ya utekelezaji wa mkakati huu katika kipindi cha mwaka mmoja na kutoa taarifa ya mafanikio, changamoto na mipango ya Halmashauri katika utekelezaji ikiwa ni pamoja na kununua mashine za upuliziaji (Fogging Machine) angalau moja katika kipindi cha kufikia Januari 2020.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tanga ambae ni Kaimu Mkuu wa Mkoa Bw. Thobias Mwilapa amemshukuru Waziri Ummy na Wizara ya Afya kwa ujumla kwa kuupatia mkoa huo mashine hiyo ambayo itasaidia katika utekelezaji wa mkakati wa kudhibiti mbu na wadudu wadhurifu ambao wanaeneza magonjwa huku akiitaja Tanga kushika namba mbili kitaifa kwa ugonjwa wa Homa ya Dengue baada ya Dar Es Salaam.

MWISHO