Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatano, 27 Novemba 2019

SERA MPYA YA AFYA KUJIKITA ZAIDI KWENYE KINGA.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. @umwalimu akifungua Kongamano la 6 la mwaka la Afya lenye lengo la kuwaleta pamoja Wadau mbali mbali katika Sekta ya Afya, ili kujadili maendeleo na changamoto ambazo nchi inakabiliana nazo.

Wadau mbali mbali wa Sekta ya Afya wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Kongamano la 6 la mwaka la Afya lenye lengo la kuwaleta pamoja Wadau mbali mbali katika Sekta ya Afya, ili kujadili maendeleo na changamoto ambazo nchi inakabiliana nazo, lenye kauli mbiu ya "ufanisi na matokeo " katika utoaji huduma za Afya.

Wadau mbali mbali wa Sekta ya Afya wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Kongamano la 6 la mwaka la Afya lenye lengo la kuwaleta pamoja Wadau mbali mbali katika Sekta ya Afya, kauli mbiu ya "ufanisi na matokeo " katika utoaji huduma za Afya.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa @umwalimu akiwa na Wadau wa masuala ya Afya kutoka Sekta mbali mbali za Kiserikali na Binafsi wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 6 la mwaka la Afya lenye kauli mbiu ya "ufanisi na matokeo " katika utoaji huduma za Afya.


SERA MPYA YA  AFYA KUJIKITA ZAIDI KWENYE KINGA.

Na Rayson Mwisemba, WAMJW- DOM

Sera Mpya ya Afya ya Mwaka  2019 - 2020 itajikita katika Kinga ili kukabiliana na mzigo wa gharama za matibabu ambazo zinawatesa Wananchi katika ngazi ya Jamii na nchi kwa ujumla.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu jiji hapa wakati akifungua kongamano la 6 la mwaka la Afya lenye lengo la kuwaleta pamoja Wadau mbali mbali katika Sekta ya Afya, ili kujadili maendeleo na changamoto ambazo nchi inakabiliana nazo, lenye kauli mbiu ya "ufanisi na matokeo " katika utoaji huduma za Afya.

"Ukiangalia Sera ya Afya ya Mwaka 2007, tulijikita zaidi kwenye mambo ya Tiba, sio kinga, kwahiyo Sera hii mpya ya Afya ya mwaka 2019 - 2020 itajiwekeza zaidi katika masuala ya Kinga sio Tiba, kwa sababu wote tunaamini Kinga ni bora kuliko tiba" alisema Waziri Ummy.

Hata hivyo alisema Sera hiyo inapendekeza kwamba, Serikali kwa kushirikiana na Wadau iweke miundombinu ya kutoa huduma za Afya kwa kuzingatia vigezo vya jografia ya eneo husika, idadi ya watu waliopo katika eneo, na kuangalia mzigo wa magonjwa katika eneo hilo.

"Serikali kwa kushirikiana na Wadau tutaweka miundombinu ya kutoa huduma za Afya kwa kuzingatia vigezo vitatu, vigezo vya kijografia ya eneo husika, vigezo vya idadi ya watu waliopo katika eneo, na vigezo cha tatu tutaangalia mzigo wa magonjwa katika eneo hilo ili kumpatia mwananchi huduma stahiki na kwa wakati kulingana na vigezo hivi" Alisema.

Aidha , amesema Sera hiyo mpya inayotarajia kuanza kutumika mwaka huu wa fedha , Serikali itaendelea kutambua mchango wa Sekta Binafsi katika utoaji wa huduma za Afya kwa wananchi, jambo litalosaidia kupunguza mzigo wa utoaji huduma.

Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Kongamano la Afya Omary Nchili amesema kuwa, lengo la Mkutano huo, ni kujadili changamoto na matokeo chanya katika Sekta ya Afya, ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za Afya kwa wananchi.

"Tumekutana hapa Wadau mbali mbali kuweza kujadili, changamoto pamoja na matokeo chanya katika Sekta ya Afya, kwa ufanisi, hivyo tutakuwa hapa kwa siku mbili ambazo tutapembua kwa undani kuhusu upatikanaji wa huduma kwa gharama ndogo na upatikanaji wa huduma kwa ujumla " alisema.

Kongamano hilo la siku mbili limeandaliwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Wizara ya Afya Zanzibar, Tume ya huduma ya Kijamii ya Kikristo, Bakwata na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Tindwa Medical Services inayofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete .

Mwisho.

Jumanne, 26 Novemba 2019

DKT. CHAULA AFUMUA MFUMO WA UONGOZI WA VYUO VYA MAFUNZO VYA AFYA

- Hakuna maoni
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula akifungua Mkutano wa wakuu wa vyuo vya Afya 37 vilivyo chini ya wizara hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtumba, Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Deodata Makani akifuatilia busara za Katibu Mkuu Wizara ya Afya (Hayupo kwenye picha) wakati wa mkutano wa wakuu wa vyuo vya Afya 37 vilivyo chini ya wizara hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtumba, Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Grace Magembe akifuatilia, ufunguzi wa mkutano wa wakuu wa vyuo vya Afya 37 vilivyo chini ya wizara hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtumba, Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu Dkt. Saitore Laizer akiwa na Mkurugenzi wa Sera na Mipango Edward Mbanga katika mkutano wa wakuu wa vyuo vya Afya 37 vilivyo chini ya wizara hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtumba, Jijini Dodoma.

Prof. Andrea Pembe, wakwanza kushoto akiwa na baadhi ya Wakuu wa vyuo vya Afya na baadhi ya Viongozi katika Sekta ya Afya wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wakuu wa vyuo vya Afya 37 vilivyo chini ya Wizara ya Afya, uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtumba, Jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakuu wa vyuo vya Afya vilivyo chini ya wizara wakifuatilia maelekezo kutoka kwa Katibu mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula (hayupo kwenye picha)wakati wa ufunguzi wa  mkutano wa wakuu wa vyuo vya Afya 37 vilivyo chini ya wizara ya Afya.

Wakuu wa Vyuo vya Afya 37 pamoja na baadhi ya viongozi katika Sekta ya Afya, wakifuatilia taarifa kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya,  wakati wa mkutano wa wakuu wa vyuo vya Afya uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtumba, Jijini Dodoma.

DKT. CHAULA AFUMUA MFUMO WA UONGOZI WA VYUO VYA MAFUNZO VYA AFYA

Na WAMJW-DOM

Katibu mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula amefumua mfumo  wa uongozi katika vyuo vya Afya nchini na kuunganisha  vyuo vyote vilivyokaribu na hivyo kufanya vyuo kupungua idadi kutoka vyuo 37 hadi kufikia vyuo 9, hali itayosaidia matumizi mazuri ya rasilimali chache zilizopo katika kuzalisha rasilimali watu.

Hayo yamejiri wakati wa mkutano wa wakuu wa vyuo vya Afya 37 vilivyo chini ya wizara hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mtumba, Jijini Dodoma.

“Wizara imeona ili kuboresha utoaji taaluma katika vyuo vyake ni vyema kubadilisha mfumo uliopo wa kuendesha vyuo vidogovidogo na kutengeneza mazingira ya kuwa na vyuo vikubwa vichache vyenye mfumo mzuri wa kiuongozi ili kuzalisha Wataalamu sahihi”, alisema.

Dkt. Chaula amesema kuwa, lengo la mkutano huo ni kupanga jinsi ya  kuboresha taaluma ndani ya vyuo vya Afya nchini ili kutoa Watumishi bora zaidi jambo litakalosaidia kupunguza vifo visivyokuwa vya lazima kwa kiasi kikubwa.

Mbali na hayo Dkt. Chaula amesema kuwa, mfumo bora wa utawala vyuoni  ni muhimili mkubwa na wa msingi katika kuhakikisha mafunzo bora yanatolewa katika vyuo vyetu na wahitimu wanaozalishwa kutoka vyuo hivyo wana umahiri unaokusudiwa katika kutoa huduma za Afya kwa wananchi.

Aliendelea kusema, Wizara imekiri kupokea changamoto za uendeshaji wa mafunzo vyuoni, ikiwemo uchache wa watumishi vyuoni, vifaa vya kufundishia, viwango vya ubora wa wahitimu kushuka, huku akisisitiza mabadiliko ya mfumo wa uongozi yatakuwa chachu ya utatuzi wa changamoto hizo.

Mbali na hayo, Dkt. Chaula amewaasa Viongozi wapya kushughulikia changamoto ya malalamiko kutoka kwa wazazi na wanafunzi wanaosoma vyuoni ikiwemo kukosa kwa baadhi ya haki zao, hali iliyopelekea kwa baadhi ya vyuo kupoteza uaminifu kwa wanafunzi na wazazi.

Nae, Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasiliamali  Watu Dkt. Saitore Laizer ametoa wito kwa Wakuu wapya wa vyuo hivyo kufanya kazi kwa ushirikiano baina yao, jambo litalosaidia matumizi mazuri ya rasilimali chache zilizopo katika kuzalisha rasilimali watu.

MWISHO.

Ijumaa, 22 Novemba 2019

“TUNAZO FEDHA ZA KUKAMILISHA HOSPITALI YA UHURU” - RAIS MAGUFULI

- Hakuna maoni
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi (hawapo pichani) mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Hospitali ya Uhuru inayojengwa Wilayani Chamwino, Dodoma.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  akimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Hospitali ya Uhuru inayojengwa wilayani Chamwino, Dodoma.

Na Englibert Kayombo, WAMJW – Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewahakikishia wananchi kuwa Serikali inayo fedha za kutosha kukamilisha ujenzi wa Hospitali ya Uhuru.

Rais Magufuli amesema hayo leo alipokuwa akizungumza na wananchi mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali hiyo inayojengwa wilayani Chamwino, Dodoma.
“Fedha ya ujenzi wa hospitali ipo, tunayo Billioni 3.4” amesema Rais Magufuli ambaye ameonyesha kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wa Hospitali hiyo.

Mafundi ujenzi wakiendelea na kazi ya ujenzi wa Hospitali ya Uhuru Wilayani Chamwino, Dodoma.

Rais Magufuli amesema kuwa mwanzoni TBA ilipewa kazi ya ujenzi wa hospitali hiyo lakini hawakusimamia vizuri ujenzi kupelea Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo kuchukua maamuzi ya kukabidhi kazi kwa Jeshi la Kujenga Taifa ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akitizama ramani ya mchoro sanifu wa kengo la Hospitali ya Uhuru inayojengwa Wilayani Chamwino, Dodoma.

Naye Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenarali Charles Mbuge aliyepewa jukumu la kusimamia ujenzi wa Hospitali hiyo amesema kuwa Jeshi lake linauwezo wa kufanya kazi hiyo na kuikamilisha ndani ya muda uliopangwa.

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia General Charles Mbuge akifafanua jambo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Bombe Magufuli mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali ya Uhuru wilayani Chamwino, Dodoma.

“Mheshimiwa Amiri Jeshi Mkuu, Jeshi letu lina nguvu ya kutosha na tutamaliza kwa muda kazi hii, sina mipango mingine ni kumaliza tuu” amesema Brigedia Jenerali Mbuge.

Mnamo tarehe 9 Desemba, 2018, Rais Magufuli alitoa maagizo ya fedha zilizotengwa kugharamia sherehe za uhuru kiasi cha Shilingi Milioni 995 kutumika kujenga hospitali katika Mkoa wa Dodoma. Kukamilika kwa hopitali hiyo kutatatua kero waliyokuwa wanaipata wananchi ya umbali wa kufuata huduma za afya.


Picha ya Mchoro sanifu wa jengo la Hospitali ya Uhuru inayojengwa Wilayani Chamwino, Dodoma.

Mwisho

Jumatano, 20 Novemba 2019

BILIONI 127 ZATOLEWA KUCHANGIA MFUKO WA AFYA WA PAMOJA NCHINI TANZANIA

 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza jambo na Wadau wa Maendeleo wanaochangia Mfuko wa Pamoja wa Afya-HBF (hawapo pichani) walipotembelea Kituo cha Afya Hombolo Jijini Dodoma.

Jengo la upasuaji katika Kituo cha Afya Hombolo lililojengwa kutoka fedha za Mfuko wa Pamoja wa Afya (HBF)

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wa tatu lutona kushoto) akimuonyesha Balozi wa Denmark nchini Tanzania Bi. Mette Spandet maboresho ya mioundombinu yaliyofanyika katika Kituo cha Afya Hombolo Jijini Dodoma.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (wa pili upande wa kulia) akiongea jambo na Balozi wa Denmark nchini Tanzania Bi Mette Norgaard Dissing Spandet mapema leo walipotembelea Kituo cha Afya Hombolo kujionea hali ya utoaji huduma.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akizungumza na wananchi waliokwenda kupata huduma katika Kituo cha Afya Hombolo Jijini Dodoma.

"Ukiwa mkubwa unawake kuwa nani?; Nataka kuwa kama wewe" (Utani) Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisalimiana na mtoto Agatha Daniel alipotembelea Kituo cha Afya Hombolo leo Jijini Dodoma

Na Englibert Kayombo – WAMJW, Dodoma.

Wadau wa mfuko wa Afya wa pamoja (HBF) wanaofadhili upatikanaji wa huduma za afya ngazi ya jamii wachangia Shilingi Bilioni 127 ili kuboresha huduma za afya nchini.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu alipofaya ziara na wadau wa maendeleo wanaochangia mfuko wa afya wa pamoja walipotembelea Kituo cha Afya Hombolo Jijini Dodoma.

“Tumekuja hapa na wenzetu hawa wanaochangia mfuko wa afya wa pamoja ambapo kwa mwaka huu wa fedha 2019/20 wametupatia Bilioni 127 kwa ajili ya kuboresha huduma za afya” Amesema Waziri Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy amesema kuwa kiasi cha Shilingi BIlioni 104 zitapelekwa kwenye Halmashauri za Wilaya na Sekretarieti za Mikoa kwa ajili ya kuboresha huduma za afya ngazi ya Jamii huku kiasi cha Shilingi Bilioni 23 kikitarajiwa kutumika kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za Afya zinazolenga kuboresha huduma za afya.

“Kwa hiyo tunaona hapa fedha nyingi zitakuja huku chini kwenye Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitli za Wilaya, nawashukuru sana wadau wetu wa maendeleo kwa kutupatia Bilioni 127 kwa ajili kuboresha huduma za Afya Tanzania” amesema Waziri Ummy Mwalimu.

Kwa upande wake Balozi wa Denmark nchini Tanzania Bi Mette Norgaard Dissing Spandet amesema kuwa mfuko huo umekuwa ukisaidia uboreshaji wa huduma za afya ngaza ya jamii kwa miaka 20 sasa na wanajivunia kuwa na uhusiano wa karibu na kusaidia katika upatikanaji wa bora huduma za afya nchini.

“Tunafuraha kufikia miaka 20 ya kusaidia katika kuboresha huduma za afya nchini Tanzania na tutaendelea kufanya hivyo zaidi kwa miaka mingi inayokuja” amesema Balozi Mette Spandet.

Naye Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Bw. Godwin Kunambi ambaye Jiji lake ni mnufaika wa mfuko huo wa pamoja wa afya amesema kuwa walipokea fedha kiasi cha Shilingi Milioni 500 na walizitumia vizuri kwa kuboresha na kujenga miundombinu katika Kituo cha Afya hapa Hombolo.

“Kwa shilingi Milioni 500 tumeweza kujenga nyumba ya mganga, jengo la kuhifadhi maiti, jengo la upasuaji pamoja na jengo la wodi ya kina mama” anasema Mkurugenzi Kunambi.

Mkurugenzi Kunambi amesema kuwa kwa kutumia mapato ya ndani ya Jiji la Dodoma wamefanikiwa kujenga wodi ya wototo iliyogharimu kiasi cha Shilingi Milioni 63.

Mfuko wa pamoja wa afya unaoratibiwa na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais TAMISEMI  huku wadau wa maendeleo wakiwa ni Nchi ya Switzerland, Canada, Denmark na Korea ya Kusini, Shirika la UNFPA, UNICEF na Benki ya Dunia umekuwa ukichangia kuboresha huduma za afya nchini Tanzania kwa miaka 20 sasa toka mwaka 1999 ambapo huduma za afya ngazi ya jamii zimekuwa zikiimarika mwaka hadi mwaka.

Mwisho

Ijumaa, 15 Novemba 2019

WANAUME ZAIDI YA MILIONI 4 NCHINI WAFANYIWA TOHARA.

- Hakuna maoni
Katibu Mkuu Dkt. Zainab Chaula akifafanua jambo wakati wa semina hiyo
.


 
 Wabunge wa Kamati ya Bunge ya masuala ya Ukimwi, Kamati ya kudumu ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya Jamii pamoja na kamati ya  Katiba na Sheria walioshiriki semina ya kujengewa uelewa wa masuala ya mpango wa taifa wa kudhibiti UKIMWI.

Waheshimiwa wabunge wakifuatilia uwasilishwaji wa mada wakati ya semina hiyo

NA Catherine Sungura -Dodoma

JUMLA ya wanaume milioni 4,456,511 wamefanyiwa tohara kinga ya kitabibu tangu 2009 ilipoanza kutolewa hadi kufikia Septemba, 2019.

Hayo yamesemwa na Afisa Mpango kutoka Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi (NACP), Dk. Sasan Mmbando wakati wa semina ya kuwajengea uelewa wabunge wa Kamati ya Bunge ya masuala ya Ukimwi, Kamati yabkudumu ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya Jamii pamoja na kamati ya  Katiba na Sheria kuhusu mpango huo.

Dk. Mmbando alisema kuwa lengo la kwanza la afua hiyo lilikuwa kuwafikia wanaume na vijana milioni 2.8 kufikia Septemba, 2017.

“Hadi kufikia Septemba, 2017 tumeweza kuwafikia milioni 3,303,940 na kuwatahiri,” alisema.

Aidha, alisema katika lengo la pili kuanzia mwaka 2017 hadi 2022 wana mpango wa kuwafikia wanaume milioni 2.7.

Alisema hadi kufikia Septemba, 2019, tayari wameweza kuwatahiri jumla ya wanaume 1,681,070 ikiwa ni sawa na asilimia 60 ya lengo.

Alisema afua hiyo inatekelezwa katika mikoa 17 yenye kiwango kikubwa cha maambukizi ya HIV na kiwango kidogo cha utahiri nchini.

“Hata hivyo, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ili kuwa na huduma endelevu na kupunguza matatizo ya njia ya mkojo, mfano UTI, ilianza kutoa huduma ya tohara kwa watoto wachanga wenye umri kuanzia siku moja hadi 60, 2013, kama utafiti wa kujifunzia (pilot study), katika mkoa wa Iringa hadi sasa imefikia mikoa 15 nchini,” alibainisha.

Alisema hadi kufikia Septemba, 2019 jumla ya watoto wachanga 13,603 wametahiriwa.

“Tohara ya watoto wachanga inafanyika katika mikoa 15, Iringa Njombe, Morogoro, Singida, Tabora, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Geita, Kagera, Rukwa, Katavi, Songwe, Mbeya na Kigoma,” alisema.
MWISHO

Alhamisi, 14 Novemba 2019

WAZIRI MKUU AWAASA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA KUFANYA MAZOEZI.


WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amewaasa Wananchi kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi kwa dakika 30 angalau mara tatu kwa wiki.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo, wakati akizindua Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yasiyo ya kuambukiza katika viwanja vya Jamhuri, Jijini Dodoma.

"Tujenge utamaduni wa kufanya mazoezi angalau dakika 30 mara tatu kwa kila wiki, niweke msisitizo kwa sekretarieti ya Mkoa na mamlaka ya Serikali za mitaa, kuendeleza utaratibu wa mazoezi uliowekwa na mama yetu Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ", amesema Waziri Mkuu. 


Mbali na hayo, Waziri Mkuu, amesisitiza juu ya kupunguza matumizi ya vilevi, kama vile Pombe na sigara pamoja na kinywaji vyenye sukari, ambavyo kwa kiasi kikubwa uchangia magonjwa kama vile kisukari na Kansa jambo linalopelekea mzigo wa matibabu kwa wananchi.

"Tujitahidi sana kupunguza matumizi ya vilevi, hususan Pombe na Sigara, pamoja na vinywaji vilivyo na sukari  kama vile soda, juisi na chokoreti, tunajua wengi tunakunywa, basi wewe kama ni mshiriki mzuri basi pata kwa kiasi". Amesema Mhe. Kassim Majaliwa.



Ameendelea, kusisitiza kwa kuwaagiza viongozi wa maeneo mbali mbali kuhamasisha wananchi wa maeneo yao kufanya mazoezi angalau kila Jumamosi, na kuwataka kupunguza matumizi ya magari kila mara.

Aidha, Mhe. Majaliwa ameagiza viongozi kuendelea kuhamasisha wananchi kujiunga katika vikundi vya kufanya mazoezi, na kusisitiza kuvifufua vikundi vyote vya mazoezi vilivyo kufa, huku akieleza umuhimu wa kutoa taarifa kwa wananchi ili washiriki katika mazoezi.  



Amesema Halmashauri zote zihakikishe zinatenga na kuyaendeleza maeneo ya wazi katika kila kata au mitaa ili pamoja na shughuli nyingine wananchi pia watumie maeneo hayo kwa ajili ya kufanya mazoezi.

Waziri Mkuu amesema  wanafunzi kuanzia sasa kabla ya kuingia darasani wawe wanakimbia mchakamchaka ili waweze kujiimarisha kiafya jambo ambalo litawaepusha na magonjwa yasiyoambukiza. 


Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa, katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita Tanzania ilishuhudia ongezeko la idadi ya watu waliopatiwa huduma za magonjwa yasiyoambukiza kutoka wagonjwa milioni 3.4 kwaka 2016 hadi wagonjwa milioni 4.2 mwaka 2018, ilkiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 24.

Hata hivyo, Waziri Ummy ameyataja magonjwa hayo ni kama vile, pumu, shinikizo la juu la damu, kisukari, saratani, siko seli, magonjwa ya akili, ajali, magonjwa mengi ya macho, kinywa, masikio, pua na koo, huku akidai kuwa magonjwa haya yamekuwa yakiongezeka duniani kote na kuathiri nyanja zote za kimaisha.

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa akiwa na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu, pamoja na viongozi wengine wa Kitaifa katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.

#TunaboreshaAfya.

Jumatatu, 11 Novemba 2019

WATAALAMU WA SEKTA YA AFYA WEKEZENI KWENYE TAFITI-DKT. NDUGULILE

 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewaagiza Wataalamu wa Sekta ya Afya nchini kuwekeza katika kufanya tafiti ili kutatua changamoto za Magonjwa yasiyoambukiza nchini.

Ameyasema hayo leo wakati akifungua Kongamano la Kwanza la Kitaifa Kuhusu Udhibiti wa Magonjwa Yasiyoambukiza, lililohudhuriwa na Wataalamu mbali mbali wa masuala ya Afya, katika ukumbi wa chou cha UDOM, Jijini Dodoma.

Dkt Ndugulile amesema kuwa, Licha ya kuwa na tafiti mbali mbali za Magonjwa yasiyoambukiza, bado kuna haja yakufanya tafiti zakutosha, ili kuendana na kasi ya matatizo ya magonjwa haya ambayo yanazidi kuwa tishio katika jamii yet una Dunia kwa ujumla.

“Tunapoanza mpango huu, mimi niwaombe sana Wanazuoni na Wanataaluma wengine tuwekeze kwenye tafiti, mpango huu hautakuwa na maana, kama hatukuwa na takwimu, zitazosaidia kujua kama tunapiga hatua au la”, amesema Dkt. Ndugulile.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Tiba, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Grace Magembe amesema Alisema, awali Serikali ilijikita katika kukabili magonjwa ya kuambukiza kama vile malaria, kifua kikuu, ukimwi na mengineyo lakini sasa hali inaonesha kasi ya magonjwa yasiyoambukiza ni kubwa.

“Ndiyo maana sasa Serikali imeona kuna ulazima wa kuwa na mpango wa kuyashughulikia haya magonjwa kwa pamoja, utaangalia upande wa matibabu na kujikita zaidi katika kuzuia watu wasiugue,” alisisitiza.

Aidha Dkt. Maghembe amesema, gharama za matibabu dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza unazidi kuielemea jamii na Serikali, huku akidai kuwa, Magonjwa yasiyoambukiza yanachukua zaidi ya asilimia 40 ya bajeti ya sekta ya afya.


“Mtu anayekabiliwa na magonjwa ya kuambukizwa anaweza kutibiwa na kuondoka zake, lakini kwa upande wa magonjwa yasiyoambukiza ikiwamo figo, moyo, shinikizo la damu, kisukari, mtu huyo anatibiwa milele na milele,”.

Aliendelea kusema, “Bajeti yetu yote ya afya inaingia kwenye magonjwa haya, ni gharama kubwa kuyatibu, kuanzia ugunduzi, dawa, vifaa tiba ni ghali, kuyatibu ni tofauti na yale ya kuambukiza.

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Afya Dkt. Faustine Ndugulile.

Ijumaa, 8 Novemba 2019

TANZANIA YAPUNGUZA MAAMBUKIZI YA MALARIA KWA ASILIMIA 50

- Hakuna maoni
Serikili kupitia Wizara ya Afya imefanikiwa kupunguza maambukizi ya malaria kwa takribani asilimia 50% kutoka 14.8% mwaka 2015 mpaka kufikia 7.3% mwaka 2017.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wakiongozana na Mawaziri kutoka nchi za SADC ziarani Mkoa wa Pwani, Kibaha walipotembelea Kiwanda cha Viuadudu wa kibaiolojia cha TBPL.

 Waziri Ummy Mwalimu amesema, mafanikio haya ni kutokana na kuwekeza rasilimali fedha, utashi wa viongozi, wadau mbalimbali na jamii kwa ujumla katika kutekeleza mikakati ya udhibiti wa malaria.

Mojawapo ya afua zilizochukuliwa na Serikali ya Tanzania katika kudhibiti ugonjwa wa malaria ni kujenga kiwanda cha viuadudu vya kibailojia kwa ajili ya kuua mazalia, alibainisha Waziri Ummy.

 Aliendelea kusisitiza kuwa matumizi ya viuadudu hivyo vya kibailojia ni kwa ajili ya kuangamiza viluilui vya mbu wanavyoeneza magonjwa mbalimbali yakiwemo; malaria, homa ya dengue, zika, homa ya manjano, matende, giri-majihoma ya bonde la ufa na chikungunya.

Aidha, Waziri Ummy amesema  kuwa ili kuendeleza mafanikio na hatimae kutokomeza kabisa malaria katika nchi zote za SADC tunahitaji kuongeza wigo na kuhakikisha nchi wanachama wanaongeza rasilimali fedha ili kutekeleza afua  mbalimbali za udhibti wa malaria, alisema.



Aidha, Waziri Ummy akiongozana na Mawaziri wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya nchi Kusini mwa Afrika (SADC) alifanya ziara katika Bohari ya Dawa MSD, huku kwa kiasi kikubwa kuonekana kuridhishwa na hali ya utendaji kazi wa Bohari ya Dawa nchini (MSD), kutokana na mfumo mzuri wa manunuzi na usambazaji wa dawa, vifaa, vifaatiba na vitendanishi.

Waziri Ummy ambae pia ni, Mwenyekiti wa baraza hilo la Mawaziri amesema wameridhishwa na utendaji kazi wa bohari hiyo na kwamba sasa wanasubiri hatua za mwisho zikamilike manunuzi yaanze.

“Wameshuhudia MSD wana uwezo, utaalamu, vifaa kwa hiyo mawaziri wameridhika na hali waliyoikuta hapa  na tunaamini kwa kununua dawa kwa pamoja kama nchi za Sadc bei pia itashuka,” amesema Ummy Mwalimu.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amesema kuwa, MSD ina uwezo na utaalamu unaokidhi viwango katika manunuzi na usambazaji wa dawa, hali iliyopelekea kushinda zabuni ya usambazaji wa dawa kwa nchi wanachama wa SADC.


#SADC
#TunaboreshaAfya