Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 16 Desemba 2019

MAOFISA AFYA WATAKIWA KUWAKINGA WANANCHI DHIDI YA MAGONJWA-DKT. SUBI

Mkurugenzi wa Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akieleza jambo mbele ya Maafisa Afya wa Mikoa na Halmashauri, wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya usafi wa mazingira.

Afisa kutoka Idara ya Mazingira Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee naWatoto Bw. Anyitike Mwakitalima akieleza mafanikio mbali mbali yaliyopatikana kutokana na afua mbali mbali za usafi wa mazingira zinazotekelezwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau.

Maafisa Afya kutoka Mikoa, Halmashauri na Wadau wakifuatilia kwa makini neno kutoka kwa Mkurugenzi wa Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi.


MAOFISA AFYA WATAKIWA KUWAKINGA WANANCHI DHIDI YA MAGONJWA-DKT. SUBI

Na Catherine Sungura, WAMJW - Dodoma

Maofisa afya wa mikoa na halmashauri wametakiwa kusimamia afya ya jamii kwenye maeneo yao ili wananchi wajikinge dhidi ya magonjwa yakuambukiza na yele yasiyoambukiza.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa kinga Dkt. Leonard Subi wakati akiongea na maofisa hao ambao wanakutana jijini hapa  kwa  kikao kazi cha siku tatu wakijadili utekelezaji wa maazimio yaliyotolewa kwenye mkutano mkuu wa kwanza mwaka jana  na  Waziri Mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.

“Mkutano huu ni wa pili mwaka huu,ni mkutano muhimu kwa maofisa afya kwani ndio wasimamizi wa shughuli za afya katika ngazi za jamii kwa kuhakikisha wananchi wanajikinga na maradhi, kula chakula bora kuishi makazi bora,usafi wa mazingira pamoja na kuwa vyoo bora”.Amesema Dkt. Subi

Aidha, amesema katika mkutano huu mambo mbali mbali yatajadiliwa ikiwemo  afya mazingira,usafi na uchafuzi wa mazingira na kila kinachotumiwa na kumzunguka  mwananchi ,pia wataangalia mabadiliko ya tabia nchi na kupata taarifa kutoka ngazi za mikoa ni jinsi gani walivyotekeleza majukumu yao.

“Maafisa afya muendelee kuishauri wizara kwa kutumia takwimu kwani tunatarajia mkutano huu mtabadilishana uzoefu  kutoka sehemu zenu za kazi,kama wizara tumekua tukitengeneza sera na miongozo mbali mbali ya kudhibiti maradhi yote yanayoweza kuathiri afya za binadamu hivyo kazi ya wizara ni kukusanya taarifa,kuchakata na kuzitolea miongozo na maelekezo”. Aliongeza Dkt. Subi.

Hata hivyo amesema maofisa hao wana majukumu ya kusimamia na  kulinda afya mipakani ili kusiingie magonjwa ya milipuko kutoka nje hususan  nchi za jirani pamoja na utoaji wa chanjo ambapo Tanzania ipo vizuri.

Mkutano huo ambao utafunguliwa kesho na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu umebeba Kauli mbiu isemayo “Huduma bora za afya mazingira na usafi ni kichocheo muhimu cha uchumi endelevu.


Jumamosi, 14 Desemba 2019

KITUO CHA AFYA KOME CHAFANYA UPASUAJI WA KWANZA

Bango la Kituo cha Afya Kome, linalotoa maelekezo ya Huduma zinazotolewa katika kituo hicho.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiongea na moja kati ya mama aliyefika kupata huduma katika kituo cha Afya Kome, Halmashauri ya Buchosa, Sengerema Mwanza.


KITUO CHA AFYA KOME CHAFANYA UPASUAJI WA KWANZA

Na.Catherine Sungura

Kituo cha afya Kome kilichopo halmashauri ya buchosa wilayani Sengerema kimefanikiwa kufanya upasuaji wa kwanza  wa dharura wa kumtoa mtoto tumboni na hivyo kumuokoa mama na mtoto wake.

Akiandika kwenye mtandao wa kijamii Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema kuwa kwa mara ya kwanza kituo hicho kimeweza kufanya upasuaji huo baada ya serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  kujenga “theatre” na kuweka vifaa tiba kwenye kituo hicho.

Waziri Ummy ameendelea kuandika kuwa chumba hicho cha upasuaji ambacho kipo kituoni hapo kitawasaidia akina mama wajawazito wa kisiwa cha kome watakaopata uzazi pingamizi na hivyo kutokufuata huduma hizo wilayani sengerema na hivyo kutokuvuka tena maji.

“Hakika tumedhamiria kuokoa maisha  ya akina mama wajawazito na watoto wachanga,tutaendelea kuchukua hatua ili kuhakikisha huduma za uzazi  za dharura ikiwemo ya upasuaji wa kumtoa mtoto tumboni(CEmONC) zinapatikana katika vituo vyote vya afya vya umma ,mama na mtoto huyo mwenye uzito wa kilo 3 na nusu wanaendelea vizuri”Amesema waziri Ummy

Naye Mganga Mkuu wa halmashauri ya buchosha Dkt. Ernest Chacha amesema walimpokea mama huyo kituoni hapo siku ya ijumaa ambaye alikua akihudhuria kliniki kwenye zahanati moja huko kisiwani hakuweza kujifungua kawaida kwani alikua akikabiliwa na uchungu pingamizi kwani nyonga zake  hazikuwa zinapanuka hivyo ili kumuokoa ilibidi afanyiwe upasuaji kuweza kumuokoa mama pamoja na mtoto .

Dkt. Chacha ameishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa uboreshaji wa vituo vya afya nchini ikiwemo kituo cha afya cha kome ambacho kipo kisiwani kwa kuboresha miundombinu kwa kujengewa chumba cha upasuaji pamoja na kuwekewa vifaa tiba hivyo kusaidia kuokoa maisha ya akina mama wajawazito na watoto wachanga hususan visiwani humo.

“Wananchi walikua wanapata adha kubwa sana ya kuvuka maji kutoka kisiwani na kufuata huduma kwenye hospitali ya wilaya iliyopo sengerema,tunamshukuru Waziri Ummy Mwalimu kwa kuiagiza MSD kutufungia taa kwenye chumba cha upasuaji wakati wa ziara yake hivi karibuni visiwani hapa kwani tumeweza kuokoa maisha ya huyu mama muda mfupi baada ya taa hizo kufungwa”Amesema Dkt. chacha

Hivi karibu waziri wa afya alitembelea kisiwa hicho na kuwaahidi  kuwapatia xray mashine ya kidigitali  kwenye kituo hicho cha afya na kuwataka MSD kufunga taa kwenye chumba hicho cha upasuaji mara moja.

Kisiwa cha kome kimeongeza  idadi ya akina mama wanaojifungulia  kwenye vituo vya afya  kwa  asilimia 80  kwa mwaka ambapo wastani akina mama  50 wanajifungulia kwa mwezi

Ijumaa, 13 Desemba 2019

TAASISI BINAFSI ZAOMBWA KUSHIRIKIANA NA WIZARA YA AFYA KATIKA KUBORESHA HUDUMA NCHINI

- Hakuna maoni


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya vitanda vya wodi ya watoto wanaohitaji uangalizi maalumu (PICU) ya Hospitali ya Taifa Muhimbili, vitanda hivyo vimetolewa na Benki ya NMB.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya NMB Bw. Juma Kimoli, Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala wa Wizara ya Afya Bi. Deodatha Makani (Mwisho) wakiwa katika hafla ya upokeaji wa Vitanda vitano vya chumba cha watoto wagonjwa mahututi (PICU) katika Hospitali ya Muhimbili vilivyotolewa na NMB.


 Mwakilishi wa Benki ya NMB Bw. Juma Kimoli akikabidhi rasmi vitanda hivyo kwa Waziri Ummy Mwalimu.
Mwakilishi wa NMB Bw. Juma Kimoli (kushoto) akiwa na Waziri Ummy Mwalimu, Kaimu mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi Bi. Zuhura Mawona wakimuangalia mmoja wa watoto aliyelazwa katika chumba cha uangalizi maalumu Muhimbili.

Waziri Ummy Mwalimu akiongea na baadhi ya wazazi walioleta watoto kwa ajili ya matibabu katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili kitengo cha watoto.

Waziri Ummy Mwalimu akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Madaktari na Wauguzi wa wodi ya watoto wenye kuhitaji uangalizi maalumu (PICU), pamoja na wawakilishi wa Benki ya NMB.

Na Emmanuel Malegi-DSM

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ameziomba sekta binafsi ikiwamo benki ya NMB kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuboresha huduma za Sekta ya Afya nchini.

Waziri Ummy amesema hayo leo wakati akipokea msaada wa vitanda vitano kutoka Benki ya NMB vyenye thamani ya shilingi Milioni 35 kwa ajili ya wodi ya watoto wanaohitaji huduma ya uangalizi maalumu (ICU) katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na vitanda 10 pamoja na magodoro 10 kwa Hospitali ya Muhimbili-Mloganzila vyenye thamani ya shilingi milioni 10. 

Amesema sekta binafsi zina wajibu mkubwa katika kuchangia shughuli za maendeleo ikiwamo huduma za afya kama ilivyofanya Benki ya NMB.

“Nawapongeza NMB kwa jitihada zao kwani msaada wa vitanda vya ICU ni msaada mkubwa kwa watoto na pia benki hii inafanya vizuri kurejesha fedha zake kwa jamii ikiwemo na kutoa gawio Serikalini”. Amesema Waziri Ummy.

Pia, Waziri Ummy amesema kutokana na juhudi za Serikali ya awamu ya tano, Muhimbili inaendelea kutoa huduma za kibingwa za hali ya juu zikiwemo huduma ya kupandikiza figo pamoja na huduma ya kupandikiza vifaa vya usikivu kwa watoto wenye matatizo ya kusikia.

Naye mwakilishi wa Benki ya NMB, Bw. Juma Kimoli ameipongeza Muhimbili na serikali ya awamu ya tano kwa kuboresha huduma za afya huku akisisitiza kuwa NMB imeweka utaratibu wa kuisaidia sekta ya afya kwa kutenga fedha kwa ajili ya kutoa misaada mbalimbali kwa jamii.

Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi katika Hospitali ya Muhimbili, Bi. Zuhura Mawona ameishukuru NMB kwa msaada huo kwa kuwa umekuja wakati ambapo Hospitali hiyo kwa kushirikiana na wahisani imejenga wodi za uangalizi maalumu kwa watoto wenye umri kati ya siku 1 hadi siku 28 (NICU) na wenye umri wa siku 29 hadi miaka 14 (PICU), hivyo kuwa na uhitaji wa vitendea kazi mbalimbali ikiwemo vitanda.

 “Vitanda hivi vya kisasa vinatumia umeme na vinaweza kutumika kwa kupandishwa juu na kushushwa  kulingana na uhitaji,  hivyo vinasaidia mgonjwa kulazwa katika mlalo unaofaa na pia kupunguza maumivu ya mgongo kwa wauguzi na madaktari wakati wa kutoa huduma”. Amesema Bi. Zuhura.

Mkurugenzi huyo amesema kuwa vitanda hivyo pia vimesaidia wauguzi kutoa huduma kwa urahisi na ufanisi zaidi ikiwamo kumwezesha mgonjwa kupumua (Intubation) kwa urahisi.

Kwa niaba ya Hospitali ya Muhimbili, Bi. Zuhura ameishukuru NMB kwa kutoa msaada huu na pia ameiomba kuongeza vitanda vingine kwani mahitaji ya vitanda ni makubwa kwa watoto wanaohitaji uangalizi maalumu.

WAZIRI UMMY AITAKA BODI MPYA YA WADHAMINI KUSIMAMIA VYEMA TAASISI YA MOI

- Hakuna maoni

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa bodi mpya ya wadhamini wa Taasisi ya MOI mapema leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya MOI Dkt. Respicious Boniface akizungumza wakati wa uzinduzi wa bodi mpya ya wadhamini iliyozinduliwa rasmi mapema leo na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akimkabidhi Mwenyekiti wa bodi wadhamini wa Taasisi ya MOI Prof. Charles Mkony sheria pamoja mpango mkakati wa Taasisi hiyo kwa ajili utekelezaji.

Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi ya MOI Prof. Charles Mkony akiongea jambo wakati wa uzinduzi wa bodi ya mpya ya wadhamini ya Taasisi hiyo ambayo imezinduliwa rasmi leo na Waziri Ummy Mwalimu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na Bodi mpya ya wadhamini wa Taasisi ya MOI aliyoizindua mapema leo.
Na Emmanuel Malegi-DSM

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu Leo amezindua bodi mpya ya wadhamini  ya taasisi ya mifupa (MOI ) na kuitaka bodi hiyo kusimamia vizuri utekelezaji wa majukumu ya kila siku ya Taasisi hiyo ili kuiwezesha kuendelea kutoa huduma bora kwa viwango vya juu.

Waziri Ummy amesema mchakato wa upatikanaji wa wajumbe wa bodi mpya ya MOI ulikua mgumu kwani majina yalikua mengi lakini  lengo ikiwa ni kupata wajumbe makini watakaoisimamia vyema Taasisi hiyo.

“Ndugu Mwenyekiti, Prof. Mkony pamoja na wajumbe, ni ukweli kwamba wajumbe wa bodi hii wamechelewa kupatikana kutokana na mchujo uliokua unafanyika miongoni mwa majina yaliyokua yamependekezwa, nitumie fursa hii kuwapongeza mliokidhi vigezo na ni matarajio yangu mtaisimamia vyema Taasisi hii ambayo ni tegemeo kubwa hapa nchini”. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli imefanya uwekezaji mkubwa katika Taasisi ya MOI jambo ambalo limepelekea huduma za afya kuimarika na kupunguza kwa kiasi kikubwa rufaa za kupeleka wagonjwa nje ya nchi.

“Uboreshwaji wa miundombinu umepelekea kuongezekaa idadi ya wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji hapa MOI, mwaka 2015 idadi ya wagonjwa waliokua wanafanyiwa upasuaji hapa MOI kwa mwezi ilikua kati ya 400 mpaka 500 lakini sasa hivi imeongezeka na kufikia 700 mpaka 900 kwa mwezi.” Waziri Ummy.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface amesema kutokana na maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali  ya awamu ya Tano katika Taasisi ya MOI, huduma nyingi mpya zimeanzishwa na katika kipindi cha miaka 4 Taasisi imewafanyia upasuaji zaidi ya wagonjwa 43,200.

“Mh. Waziri katika kipindi cha Miaka 4 ya Serikali ya awamu ya Tano, kupitia usimamizi wa Wizara yako tumeweza kuanzisha huduma za upasuaji wa magoti na mabega kwa njia ya matundu, upasuaji wa kunyoosha vibiongo kwa watoto, upasuaji wa kuondoa vivimbe vya mishipa ya damu kwenye ubongo, upasuaji wa kuondoa uvimbe kwenye ubongo kupitia puani, upasuaji wa mgongo kwa kufungua eneo dogo, hii ni hatua kubwa sana kwetu.” Amesema Dkt. Boniface.

Akitoa neno la shukrani Mwenyekiti mpya wa Bodi mpya ya Wadhamini MOI Prof. Charles Mkony ameshukuru kwa kupewa dhamana ya kusimamia Taasisi hiyo muhimu  na kuahidi kendelea kuisimamia MOI ili iendelee kutoa huduma bora na za viwango vya juu kwa wananchi.

-MWISHO-

Alhamisi, 12 Desemba 2019

SERIKALI YAAGIZA HOSPITALI ZOTE NCHINI KUANZISHA MFUKO WA FEDHA ZA DAWA.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akieleza jambo wakati wa kikao cha kuzindua Bodi ya ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou-Toure.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akiteta  jambo na Mwenyekiti mpya wa Bodi ya ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou-Toure  Prof. Abel Makubi wakati wa kikao cha kuzindua Bodi hiyo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akikata  utepe ikiwa kama ishara ya uzinduzi wa Bodi mpya ya ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou-Toure, Kulia kwake ni Mwenyekiti mpya wa Bodi Prof. Abel Makubi, kushoto kwake ni Kaimu RMO Mkoa Mwanza Dkt. Silas Wambura.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu na Mwenyekiti mpya wa Bodi ya ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou-Toure wakiwa wamebeba kitabu cha mwongozo wa Bodi ya ushauri,  wakati wa kikao cha kuzindua Bodi hiyo.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akimkabidhi mwongozo mmoja kati  ya wajumbe wa Bodi mpya ya ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou-Toure, katikati ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Silas Wambura.

Baadhi ya Watumishi wa Hospitali  ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou-Toure waliofika kushuhudia uzinduzi wa Bodi mpya ya ushauri ya Hospitali hiyo, uliofanywa na Waziri wa Afya Mhe.@umwalimu katika ukumbi wa RMO Mkoa wa Mwanza.

Baadhi ya Watumishi wa Hospitali  ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou-Toure na Wajumbe wa Bodi ya zamani  ya ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou-Toure, waliofika kushuhudia uzinduzi wa Bodi mpya ya ushauri ya Hospitali hiyo, uliofanywa na Waziri wa Afya Mhe.@umwalimu katika ukumbi wa RMO Mkoa wa Mwanza.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya Mhe.@umwalimu, akiwa na wajumbe wa Bodi mpya ya ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou-Toure baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo.


SERIKALI YAAGIZA HOSPITALI ZOTE NCHINI KUANZISHA MFUKO WA FEDHA ZA DAWA.

Na Rayson Mwaisemba, WAMJW- MWANZA

Serikali kupitia Wizara ya Afya imeagiza Waganga Wakuu wa Vituo vya Afya na Hospitali zote nchini kuanzisha mfuko wa fedha za Dawa kupitia makusanyo ya fedha za ndani, ili kuweza kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa dawa nchini endapo itatokea.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu katika kikao cha uzinduzi wa Bodi mpya ya ushauri ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza.

"Kuanzia Vituo vya Afya, Hospitali zote za Halmashauri, za Mikoa , kuanzisha mfuko wa fedha za dawa, na vyanzo vikuu vya mifuko hii ni mapato yatokanayo na mauzo ya dawa, huduma za Maabara, huduma za mionzi" alisema Waziri @umwalimu.

Amesema, Bodi hiyo ya ushauri lengo lake kubwa ni kuhakikisha inaboresha huduma za kinga na tiba katika Hospitali, huku ikihakikisha huduma hizo zinaifikia wananchi kwa ubora na gharama nafua.

Aliendelea kusema, Sera ya Afya nchini inawataka Wananchi kuchangia huduma kwa gharama nafuu isipokuwa kwa makundi yote ya msamaha, wakiwemo Wazee, Watoto walio chini ya miaka mitano na mama wajawazito, hivyo kuwataka kuweka mifumo mizuri ili kurahisisha utoaji huduma.

Mbali na hayo, Waziri Ummy ameiagiza Bodi hiyo kuhakikisha inaboresha huduma za dharura na ajali, ili kuokoa vifo vitokanavyo weza kuepukika kupitia huduma za dharura, keisha kuwashauri kujenga jengo jipya la wagonjwa wa nje (OPD) ili kuboresha huduma kwa wananchi.

"Watu wengi wanakufa wakiwa getini Mwa Hospitali, wakati utaalamu upo, kwamba mkiboresha huduma za dharura na ajari, tunaweza kuokoa maisha ya watu wengi " alisema Waziri @umwalimu.

Aidha, Waziri Ummy ameeleza majukumu ya Bodi hiyo ni kushauri, kutengeneza, kusimamia na kupitisha miongozo, malengo na mipango mikakati ya Hospitali kulingana na Sera na miongozo ya Serikali.

Nae Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sekou-Toure Dkt. Dkt. Graham Mtui ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kuendelea kuboresha huduma za Afya katika Hospitali hiyo kwa kuleta mashine ya uchunguzi wa figo na ini, mashine ya kusafisha figo ambazo zinatarajia kuanza kutoa huduma Januari 2020.

Kwa upande mwingine amesema, Hospitali inatarajia kupokea mashine sita ikiwemo CT Scan, X- ray yakidigitali, vifaa vya mifupa na mashine zinazosaidia kupumulia kutoka MSD.

Hata hivyo, amesema kuwa, idadi ya Wagonjwa wanaofika kupata huduma, kutoka wastani wa wagonjwa 350 kwa siku kwa mwaka 2015 hadi kufikia wagonjwa kati ya 500 mpaka 700 kwa Mwaka huu 2019, huku akiweka wazi kupunguza Rufaa za kwenda Hospitali ya Rufaa ya kanda ya Bugando kwa asilimia 50.

"Kutokana na mafanikio hayo, idadi ya wagonjwa wanaopata huduma katika Hospitali imeongezeka, kutoka wastani wa wagonjwa 350 kwa siku ambayo ilikuwa mwaka 2015, na kufikia wastani wa wagonjwa kati ya 500 hadi 700 kwa mwaka huu 2019", alisema Dkt. Graham Mtui.

Mwisho.

TUHUMA ZA KUDAIWA RUSHWA YA NGONO MADAKTARI WA MAZOEZI KWA VITENDO (INTERNS) KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA.


Jumatano, 11 Desemba 2019

SAMPULI 5106 ZIMEFANYIWA UCHUNGUZI NA MAABARA YA MKEMIA KANDA YA KATI




Picha mbalimbali zikionesha Meneja wa mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kanda ya kati Bw. Musa Kuzumila akizungumza na Maafisa Mahusiano na Mawasilino wa Wizara ya Afya na Taasisi zake wakati walipotembelea mamlaka hiyo kujionea mafanikio yaliyofanywa katika kuboresha sekta ya afya nchini chini ya kipindi cha miaka minne ya Rais Magufuli akiwa madarakani.

Dodoma

Jumla ya sampuli 5106 zimefanyiwa uchunguzi katika maabara zikiwemo za masuala ya kijamii na kijinai katika mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali kanda ya kati.

Hayo yamesemwa na Meneja wa mamlaka hiyo kanda ya kati Musa Kuzumila wakati wa ziara ya maofisa habari wa wizara ya afya na taasisi zake wakati wa kutembelea mamlaka hiyo kujionea mafanikio yaliyofanywa katika kuboresha sekta ya afya nchini.

Kazumila amesema kwamba tangu kuanzishwa kwa kanda hiyo miaka miwili na nusu sasa ,kanda yake imefanikiwa kupima sampuli hizo ambazo zimefanyiwa uchunguzi katika maabara na kuzitolea ushahidi mahakamani

"Mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu inasimamia sheria na kudhibiti kemikali hivyo tumeweza kufanyia uchunguzi sampuli na hivyo kupunguzia wateja  umbali na hivyo kusaidia wananchi kupata haki na kutoa ushahidi kwa wakati".Amesema Kazumila.

Kwa upande wa vinasaba Kazumila amesema kati ya sampuli walizopokea jumla ya sampuli 36 zilizowasilishwa asilimia 90 zilikua zinaangalia uhalali wa baba wa mtoto.

Hata hivyo amesema kwamba mamlaka hiyo imeweza kukagua maeneo yanayojihusisha na kemikali zipatazo 360 pamoj na kutoa vibali 139 za kuingiza na kusafirisha kemikali nchini kwa kanda ya kati.

Kwa upande wa wajasiriamali wadogo wadogo mamlaka hiyo imewapatia mafunzo wajasiriamali 315 namna ya matumizi salama ya kemikali pamoja na kutoa elimu kwa wachenjuaji wa dhahabu wanaotumia kemikali aina ya sodium cyanide.

Mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali kanda ya kati inahudumia mikoa ya morogoro,iringa,dodoma,singida na tabora na ilianzishwa mwaka 2017.


-Mwisho-

Jumanne, 10 Desemba 2019

BILIONI 1.9 KUJENGA JENGO LA MAMA WAJAWAZITO NA WATOTO GEITA

- Hakuna maoni


Waziri wa Afya, Maendeleo  ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akielekeza jambo wakati wa ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita uliofikia 86%. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mmwalimu akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel pamoja na Mhandisi kutoka TBA Glady Jefta, wakiwa katika ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.

 Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel pamoja na Mhandisi kutoka TBA Glady Jefta, wakiwa katika ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu, akiwa na Mhandisi kutoka Wizara ya Afya Eng. Francis Mbuya, pamoja na Mhandisi kutoka TBA Eng. Glady Jefta wakikagua jengo la wagonjwa wa nje (OPD) wakati wa ziara ya Waziri kukagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.



Baadhi ya Majengo ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita

Na.Rayson Mwaisemba, WAMJW- GEITA 

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa kiasi cha shilingi Bilioni 1.9 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la huduma za mama wajawazito na Watoto Mkoani Geita. 

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya Mh.  Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita ambayo imefika zaidi ya asilimia 80 ya ujenzi 

"Habari njema kwa Wananchi, Serikali kupitia Wizara ya Afya tuna Bilioni 1.9 kwa ajili ya kujenga jengo la akina mama wajawazito pamoja na Watoto wachanga, tunakamilisha taratibu tayari kuanza ujenzi huo" alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy aliendelea kusema, Hospitali hiyo inajengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la upasuaji (thieta), jengo la mionzi (radiolojia), huku akisisitiza kuwa majengo hayo ya wodi yaliyokamilika yataanza kutoa huduma ili kuendelea kuwasaidia wananchi. 

Waziri Ummy amesema, Serikali tayari imepeleka Milioni 400 kwa ajili ya ujenzi na uboreshaji wa kituo cha Afya vya Katoro, ikiwa ni azma ya Serikali ya kuboresha huduma za Afya katika ngazi ya chini, ili kuzipunguzia mzigo Hospitali za Rufaa za Wilaya na Mikoa. 

"Tulianza kujenga vituo vya Afya zaidi ya 352 katika Halmashauri mbali mbali, muelekeo tunazungumzia huduma za Afya kwa wote, kupitia kuwekeza katika vituo vya Afya na Zahanati, ndio maana wiki iliyopita tulileta Milioni 800 kwa ajili ya kuongeza majengo katika kituo cha Afya Katoro na Buseresere" amesema Waziri Ummy

Licha ya kuridhishwa na ujenzi huo, Waziri Ummy amemuagiza Mkandarasi kutoka TBA kuhakikisha unamaliza unakamilisha ujenzi wa Hospitali hiyo mapema, huku akisisitiza ifikapo mwaka kesho Mwezi Machi 31, Hospitali hiyo ianze kutoa huduma za Afya kwa Wananchi. 

"Mipango ya Serikali, tunategemea ifikapo tarehe 31 Machi, nikija hapa anikabidhi Hospitali, sitokuja kukagua Hospitali, mimi nitatimiza wajibu wangu wa kutafuta fedha, nataka ifikapo tarehe hiyo tuanze kutoa huduma kwa Wananchi " amesema. 

Aidha, Waziri Ummy, amewatoa hofu wananchi wa Mkoa wa Geita kuwa ,Serikali imejipanga kuhusu Watumishi wataohudumu katika Hospitali hiyo, huku akiwatoa wasi wasi kuhusu upatikanaji wa vifaa vya kutolea huduma katika Hospitali hiyo. 

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kupitia Wizara ya Afya kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya uboreshaji wa huduma za Afya katika Mkoa wa Geita. 

"Naomba niendelee kumshukuru Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kwa kuendelea kutenga fedha katika Mkoa wetu kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wanyonge, huu ni Mkoa mpya una watu wengi, na una changamoto nyingi, lakini changamoto zote Wizara imezichukua na kutekeleza" alisema 

MWISHO.

Jumapili, 1 Desemba 2019

MAAMBUKIZI YA VVU YASHUKA NCHINI

Logo ya Siku ya UKIMWI.

Hadi sasa Watanzania milioni.1.4 wanaoishi na VVU ambapo kiwango cha maambukizi kikiwa ni asilimia 4.7 ikilinganishwa na asilimia 7.0 ya mwaka 2014.

Hayo yamesemwa leo na Mgeni rasmi wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya UKIMWI duniani  na Waziri wa Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemevu Mhe. Jenista Mhagama jijini Mwanza.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu.
Waziri Mhagama amesema kuwa maambukizi mapya na vifo  vitokanavyo na UKIMWI pia vimepungua.
 "Tumeweza kupata mafanikio haya kufuatia kuboreshwa kwa huduma.za ART na afua za kinga kama vile utahiri wa kitabibu wa wanaume na kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto"Alisema Waziri Mhagama.

Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Jenister.

Aidha, amesema kiwango  cha watu wanaoishi na VVU walioko kwenye mpango wa ARV kimeongezeka kutoka asilimia 22 mwaka 2009 hadi kufikia asilimia 57 ya mwaka 2017.

Naye Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema mpaka kufikia mwezi Septemba 2019 takribani watu 1,252,205 kati ya wananchi 1,600,000 wanaokadiriwa kuishi na VVU nchini walikuwa wamepima na kufahamu hali zao za maambukizi ya VVU. 
"Hii ni sawa na asilimia 78.3 ya lengo la 90 ya kwanza.
Miongoni mwao wanaume walikuwa 413,985 sawa na asilimia 33, na wanawake walikuwa 838,220 sawa na asilimia 77".

Mhe. Jenister akiwa na Mhe. Ummy Mwalimu.
Kwa upande wa vijana Waziri Ummy amesema kuwa Vijana balehe (umri wa miaka 10 – 19) walikuwa 57,167 sawa na asilimia 4.6, na vijana (umri wa miaka 15 – 24) walikuwa 96,006 sawa na asilimia 7.7.

Aidha, amesema kati ya waliopima na kutambua afya zao watu 1,221,799 sawa na asilimia 97.6 wanatumia ARV. 

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella.

 Hata hivyo alisema Lengo la 90 ya pili ambalo ni asilimia ya kuwa watu waliopimwa na kugundulika kuwa wana maambukizi ya VVU wanatumia dawa za kupunguza makali ya VVU (yaani ARV’s), tayari tumefikia takriban asilimia 98 wanatumia zawa za kupunguza makali ya VVU yaani ARV.

"Lengo la 90 ya tatu, ambalo ni kuhakikisha kuwa asilimia 90 ya wanaotumia ARV’s wamefanikiwa kupunguza wingi wa VVU mwilini Waziri huyo alisema wamefanya vizuri sana,"ni kuwa tumekuwa tukifuatilia kwa karibu hali za watu wanaotumia dawa za kupunguza makali ya VVU".Alisema 

Mhe. Jenister Mhagama akiwa na Mhe. Ummy Mwalimu, wakipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa TACAIDS Leonard Maboko.

Waziri Ummy alitaja mafanikio mengine ya kujikinga dhidi ya maambukizi ni tohara kwa wanaume ambapo kuanzia mwaka 2009 hadi Agosti 2019 jumla ya wanaume 4,456,511 wamefanyiwa tohara kupitia njia za mkoba na huduma katika vituo vya huduma.

Takwimu zinaonesha kwamba watu 953,973 sawa na asilimia 89 ya watu 1,072,650 waliopimwa wingi wa VVU wamefanikiwa kupunguza wingi wa VVU mwilini jambo ambalo ni muhimu katika kinga dhidi ya UKIMWI.Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "Jamii ni chachu ya mabadiliko,tuungane kupunguza maambukizi mapya ya VVU"

Wananchi waliojitokeza katika viwanja vya Rock City Mall leo, kushuhudia Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani, mgeni rasmi akiwa Waziri Jenister Mhagama, aliyemwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Kassim Majaliwa.

Picha ya Pamoja ikiongozwa na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Jenister Mhagama, aliyemwakilisha Mgeni rasmi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Mhe. Kassim Majaliwa.


#TunaboreshaAfya.
#WAMJW









Jumamosi, 30 Novemba 2019

KITUO CHA AFYA KOME KUPEWA X-RAY YA KIDIGITALI







Na.Catherine Sungura,Buchosa

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ameahidi kuwapatia mashine ya x-ray ya kisasa ya kidigitali kituo cha afya kome kilichopo halmashauri ya Buchosha wilayani Sengerema.

Waziri Ummy ametoa ahadi hiyo akiwa kwenye ziara ya kikazi kisiwani hapo ya kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

“Ninawaahidi wananchi nitaleta x-ray mashine ya kidigitali kwenye kituoa hichi cha afya ili msivuke maji kwenda kupata huduma za vipimo wilayani sengerema".Alisema Waziri Ummy

Aidha, alimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buchosha Crispian Luanda pamoja na Mganga Mkuu wake Dkt. Ernest Chacha  kwa jitihada kubwa wanazofanya za kuboresha huduma za afya kwenye halmashauri hiyo"Nimefurahi kumuona daktari wa upasuaji kwenye kituo hiki na hongereni kwa kumpatia mafunzo ya mwaka mzima kwenye eneo hili,sasa mnatakiwa kuweka vifaa na huduma za mtoto njiti ili kusiwepo na vifo vya watoto hao endapo itatokea".

Hata hivyo Waziri Ummy aliwataka akina mama wa kisiwa hicho kuhudhuria kliniki mara nne mara wanapokuwa wajawazito ili kuepukana na vifo vya wajawazito na watoto pamoja na kuepusha kuzaa watoto walemavu.

"Tumeanzisha huduma za upasuaji kwenye kitua hiki cha afya tunataka mama mjamzito wa Kome akipata tatizo la mtoto kukaa vibaya tumboni au mama akipata kifaa cha mimba asaidiwe hapa hapa"Alisisitiza Waziri Ummy.

Naye Mbunge wa Buchosa Dkt. Charles Tizeba ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya kuwajengea jengo la upasuaji pamoja na vifaa hivyo kuondoa tatizo kubwa la upasuaji lililokuwa linawakabili wananchi wa Kome na kuomba wizara kuwapatia vifaa vya vipimo katika vituo vya huduma za afya kwenye halmashauri hiyo kwani wananchi wameanzisha ujenzi wa zahanati 30 kwa nguvu zao hivyo wakikamilisha miundombinu huduma za afya zitakuwa zimeboreshwa kwenye jimbo lake.

Kisiwa cha Kome kimeongeza idadi ya akina mama wanaojifungulia kwenye vituo vya huduma za afya kutoka asilimia 42 mwaka 2015 kati ya akina mama 100 hadi kufikia asilimia 80 kwa mwaka  ambapo wastani wa akina mama 50 wanajifungua kwa mwezi.
-Mwisho-