Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Ijumaa, 14 Februari 2020

“TANZANIA NI SALAMA HAKUNA UGONJWA WA CORONA” - DKT. NDUGULILE

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, jisnai, Wazee na watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na Waandishi wa Habari (Hawapo kwenye picha) wakati wa ziara yake Jijini Arusha,



“TANZANIA NI SALAMA HAKUNA UGONJWA WA CORONA” -  DKT. NDUGULILE

Na Englibert Kayombo, WAMJW, Arusha.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewahakikisha Watanzania kuwa nchi bado iko salama na hakuna mgonwjwa yeyote mwenye ugonjwa wa Virusi vya Corona.

Dkt. Ndugulile ametoa kauli hiyo akiwa Jijini arusha katika Ziara zake za kikazi ambapo waandishi wa habari walimuuliza juu ya tetesi za uwepo wa ugonjwa huo nchini, pamoja na kutaka kufahamu ukweli wa taarifa za mtu anayedai kuwa na dawa za ugonjwa huo.

“Niseme tuu kuwa Tanzania mpaka sasa hivi bado tuko salama na hakuna mgonjwa yeyoteambaye ameripotiwa na amethibitika kuwa na ugonjwa” amesema Dkt Ndugulile.

Amesema kuwa Serikali imekuwa ikifuatilia taarifa mbalimbali za washukiwa na watu wote ambao tunawahisi kuwa na ugonjwa huo na tumeweza kuwapima na kubaini kuwa hawana ugonjwa.

“Sambamba na hilo tumeendelea kuchukua tahadhari mbalimbali na mimi niko katika Mkoa huu wa Arusha na nitaenda Kilimanjaro kwenda kuangalia utayari” amesmea Dkt. Ndugulile na kuendelea kusema “ Nimepita hapa leo nimeongea na uongozi na nimeridhika na maandalizi ambayo tunayo hapa katika Mkoa huu wa Arusha katika kudhibiti ugonjwa huo” Ameeleza Dkt. Ndugulile.

Akijibu kuhusu mtu ambaye anasema kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa huo ambaye anajulikana kwa jina la Mosses Mollel maarufu kwa jina la “Nabii namba saba” aliyetoa taarifa za kuwa na dawa yenye uwezo wa kutibu virusi vya corona, Dkt Ndugulile amesema kuwa anazo taarifa za mtu huyo ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari akijitangaza kuwa anayodawa ya kutibu ugonjwa huo na kumtaka athibitishe kauli yake.

“Kimsingi nimeiona hiyo taarifa ya huyo mtu  anayejiita Nabii Saba kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa wa Corona ,ila hapa kwetu Tanzania hatuna maambukizi yoyote ya ugonjwa huyo ,tunachotaka huyo mtu  atuthibitishie uwezo wake wa kutibu huo ugonjwa wa Corona” Amesema Ndugulile

Ameongeza kuwa iwapo atashindwa kuthibitisha atachukuliwa hatua Kali za kisheria.
Amesema hadi sasa Serikali imetuma wataalamu wake kwenda kumsaka na kumhoji kama anavyo vibali Vya kutoa huduma ya Tiba na kujitangaza kuwa anatoa Huduma ya kutibu ugonjwa huo  hatari ambao hadi sasa mataifa bado yanahaha kusaka  Tiba ya ugonjwa huo.

Nabii Namba Saba ambaye ni mkazi wa Ngaramtoni Wilayani Arumeru,Mkoani Arusha amekuwa akijitangaza kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa huo wa virusi vya corona na kuweka mawasiliano yake  kwenye mitandao .

Dkt. Ndugulile amesema kuwa mtu yeyote anayetoa tiba asili na mbadala kwanza ni lazima asajiliwe na mamlaka husika ambayo ni Wizara ya Afya, pili lazima dawa zake ziwe zimesajiliwa na Wizara ya Afya na kusisitiza kuwa nabii huyo pia anapaswa kuthibitisha amesajiliwa wapi na lini.

“Tuepuke kutoa kauli ambazo zinakwenda kuchanganya jamii, na endapo tutabaini mtu huyu hana sifa ambazo anasema kuwa nazo tutamchukulia hatua za kisheria” Amesema Dkt. Ndugulile.

TANZANIA KUKABILIANA NA MAGONJWA YA MILIPUKO

- Hakuna maoni
 Mkurugenzi wa huduma za tiba Dkt. Grace Magembe akionesha jinsi ya unawaji mikono kwenye mpaka wa rusumo.

 Katibu Mkuu Dkt. Chaula akiingia kwenye hema la mapumziko lililopo kwenye mpaka wa rusumo





Maafisa afya wa mpaka wa Rusumo wakitayarisha kifaa cha kupima joto la binadamu cha kutembea ambacho wasafiri kabla ya kuingia kwenye jengo hilo hupita na kufanyiwa uchunguzi.


TANZANIA KUKABILIANA NA MAGONJWA YA MILIPUKO

Na. Catherine Sungura-Kagera

Katika kukabiliana na magonjwa ya milipuko nchini wizara ya afya inajipanga kuboresha hali ya mipaka yake ili kuzuia magonjwa hayo yasiingie kwa kuboresha miundombinu ya kutolea huduma endapo itatokea muhisiwa.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula wakati wa alipotembelea mpaka wa manyovu mkoani kigoma na mpaka wa risumo mkoani kagera

"Tumefika mipaka hii kubwa ikiwa ni kuangalia utayari wetu wa kujikinga na maradhi haya ya kuambukiza ambayo yanaweza kuingia nchini"

Kwa upande wa manyovu katibu mkuu  alibainisha mapunguvu ikiwemo ya eneo dogo hivyo  kukubaliana kuweza kutatua mapungufu hayo ikiwemo namna ya kujenga jengo la pamoja na bora kwa huduma zote za mpaka huo.

“Tumeona eneo walilopo, wanakutana moja kwa moja na msafiri, ni dogo, watu wote wakishuka, wanaingia moja kwa moja mule ndani na kuonana na mtoa huduma,” alisema.

Aidha Dk. Chaula aliweza kuingia nchi ya Burundi na kuona jinsi walivyojiandaa alisema kwa upande wa Burundi ameona namna walivyojiandaa ikiwamo kuandaa hema maalum kwa ajili ya kuwaweka watu ambao watahisiwa kuwa na ugonjwa huo.

Hata hivyo alisema kuwa hapa nchini mambo makubwa yamefanyika, wataalamu wanafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha magonjwa haya hayaingii nchini, tumeongeza idadi ya watumishi mipakani hapa manyovu kutoka mmoja hadi watano, tumewapa pia vifaa vya ukaguzi na kujikinga lakini pamoja na juhudi hizi bado tuna changamoto zinatukabili ila watazifanyia kazi.

Sambamba na hilo, Katibu Mkuu huyo alifika pia katika eneo la na kujionea njia nyingi za mipaka isiyo rasmi ambapo wenyeji walimueleza wazi kwamba watu wa pande zote mbili (Tanzania na Burundi) huitumia kuingia na kutoka baina ya nchi hizo mbili.

Dk. Chaula alisema kupata ufumbuzi wa jambo hili, watajadiliana kwa kina na watendaji wa Wizara hizo mbili  kupata ufumbuzi wa kuitatua changamoto hiyo, akitoa rai kwa watumishi wa afya kuendelea kutoa elimu kwa jamii, wajue namna bora ya kujikinga dhidi ya magonjwa hayo.

Kwa upande wa Rusumo Dkt.Chaula alisema ameridhishwa na utayari  wa kukabiliana na magonjwa ambapo mpaka huo wana aina mbili za vifaa vya upimaji joto la binadamu ikiwepo 'thermo scanner' na 'walk through'


MWISHO

HOSPITALI YA WILAYA MWANGA YAPEWA WIKI MBILI KUJA NA MKAKATI WA UPATIKANAJI WA VIPIMO MUHIMU VYA AFYA

- Hakuna maoni
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua kadi ya bima ya afya ngazi ya jamii iliyoboreshwa kutoka kwa mgonjwa aliyefika hospitali ya Wilaya ya Mwanga kupata huduma za afya.

 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kulia) akifafanua jambo kwa watumishi  wa Wilaya ya Mwanga (hawapo pichani) kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bw. Thomas Apson.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto)  akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bw. Thomas Apson (kulia) mara baada ya kuwasili katika ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Mwanga.



HOSPITALI YA WILAYA MWANGA YAPEWA WIKI MBILI KUJA NA MKAKATI WA UPATIKANAJI WA VIPIMO MUHIMU VYA AFYA

Na WAMJW - Mwanga, Kilimanjaro.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameutaka uongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Mwanga kuandaa mkakati madhubuti utakaowawezesha kuwa na vipimo muhimu vya afya.

Dkt Ndugulile ametoa agizo hilo leo alipotembelea Hospitali ya Wilaya ya Mwanga kujionea hali ya utoaji huduma na kubaini kuwa hospitali hiyo haina vipimo vya damu, vipimo vya kemia pamoja vipimo vya CD4.

”Kwa miaka miwili sasa hakuna vipimo vya msingi katika hospitali hii, tunawakosesha huduma wananchi” amesema Dkt. Ndugulile

”Haiwezekani Hospitali kubwa ndani ya Wilaya kukosa vipimo vya msingi, haiwezekani mtu hapa sasa hivi anahitaji kipimo cha damu atoke hapa aende Hospitali ya Mawenzi Moshi kwa ajili ya vipimo” amesema Naibu Waziri Ndugulile.

Katika hatua za kutafuta ufumbuzi wa changamoto hiyo, Waziri Ndugulile ameushauri uongozi wa afya ndani ya Wilaya kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga kuhakikisha wanatenga fedha kwa ajili ya kununua vifaatiba hivyo ili wananchi waweze kupata huduma za vipimo ndani ya Wilaya ya Mwanga.

Aliendelea kushauri kuwa kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wao wanatoa mkopo wa majengo na vifaa kwa taasisi za umma na binafsi, mnaweza kuwafikia NHIF na kujadili kuhusu suala hili.

”Huko kwingine wanazitumia hizo fursa, kaeni na watu wa NHIF, Meneja wa NHIF kaa na viongozi wa Hospitali hii ikiwezekana mkubaliane hivyo vitu vipatikane kwa haraka” ameshauri Dkt. Ndugulile.

”Naamini mna wadau wa maendeleo ambao mnashirikiana nao katika mambo mbalimbali, timu ya afya ndani ya mkoa, wilaya pamoja na hospitali nawaombeni sana tuwe tunaomba vitu ambavyo vina manufaa kwa wananchi” amesisitiza Dkt. Ndugulile.

Awali akitoa salamu za wananchi wa Wilaya ya Mwanga, Mbunge wa Jimbo la Mwanga Profesa Jumanne Maghembe amesema kuwa changamoto ya kijiografia ndani ya Wilaya hiyo inachangia wananchi kukimbilia hospitali za Wilaya jirani ili kuweza kupata huduma.

”Wilaya yetu hii ina upande wa mlimani na huku tambarare, wananchi wengi walio huku tambarare wanaona ni bora kwenda Moshi kwa ajili ya matibabu kuliko kwenda juu mlimani iliko Hospitali” amesema Prof. Maghembe.

Hata hivyo Prof. Maghembe amesema kuwa tayari ndani ya Wilaya wameshaanza taratibu za kujenga Hospitali nyingine eneo la chini (tambarare) ili wananchi wanaoishi maeneo hayo waweze kupata huduma za afya ndani ya Wilaya ya Mwanga.

-Mwisho-

“TANZANIA NI SALAMA HAKUNA UGONJWA WA CORONA” - DKT. NDUGULILE.

- Hakuna maoni


Dkt. Faustine Ndugulile
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto 

Na Englibert Kayombo, WAMJW, Arusha.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewahakikisha Watanzania kuwa nchi bado iko salama na hakuna mgonwjwa yeyote mwenye ugonjwa wa Virusi vya Corona.
Dkt Ndugulile ametoa kauli hiyo akiwa Jijini arusha katika Ziara zake za kikazi ambapo waandishi wa habari walimuuliza juu ya tetesi za uwepo wa ugonjwa huo nchini, pamoja na kutaka kufahamu ukweli wa taarifa za mtu anayedai kuwa na dawa za ugonjwa huo.
“Niseme tuu kuwa Tanzania mpaka sasa hivi bado tuko salama na hakuna mgonjwa yeyoteambaye ameripotiwa na amethibitika kuwa na ugonjwa” amesema Dkt Ndugulile.
Amesema kuwa Serikali imekuwa ikifuatilia taarifa mbalimbali za washukiwa na watu wote ambao tunawahisi kuwa na ugonjwa huo na tumeweza kuwapima na kubaini kuwa hawana ugonjwa.
“Sambamba na hilo tumeendelea kuchukua tahadhari mbalimbali na mimi niko katika Mkoa huu wa Arusha na nitaenda Kilimanjaro kwenda kuangalia utayari” amesmea Dkt. Ndugulile na kuendelea kusema “ Nimepita hapa leo nimeongea na uongozi na nimeridhika na maandalizi ambayo tunayo hapa katika Mkoa huu wa Arusha katika kudhibiti ugonjwa huo” Ameeleza Dkt. Ndugulile
Akijibu kuhusu mtu ambaye anasema kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa huo ambaye anajulikana kwa jina la Mosses Mollel maarufu kwa jina la “Nabii namba saba” aliyetoa taarifa za kuwa na dawa yenye uwezo wa kutibu virusi vya corona, Dkt Ndugulile amesema kuwa anazo taarifa za mtu huyo ambazo zimesambaa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari akijitangaza kuwa anayodawa ya kutibu ugonjwa huo na kumtaka athibitishe kauli yake.
“Kimsingi nimeiona hiyo taarifa ya huyo mtu  anayejiita Nabii Saba kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa wa Corona ,ila hapa kwetu Tanzania hatuna maambukizi yoyote ya ugonjwa huyo ,tunachotaka huyo mtu  atuthibitishie uwezo wake wa kutibu huo ugonjwa wa Corona” Amesema Ndugulile
Ameongeza kuwa iwapo atashindwa kuthibitisha atachukuliwa hatua Kali za kisheria.
Amesema hadi sasa Serikali imetuma wataalamu wake kwenda kumsaka na kumhoji kama anavyo vibali Vya kutoa huduma ya Tiba na kujitangaza kuwa anatoa Huduma ya kutibu ugonjwa huo  hatari ambao hadi sasa mataifa bado yanahaha kusaka  Tiba ya ugonjwa huo.
Nabii Namba Saba ambaye ni mkazi wa Ngaramtoni Wilayani Arumeru,Mkoani Arusha amekuwa akijitangaza kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa huo wa virusi vya corona na kuweka mawasiliano yake  kwenye mitandao .
Dkt. Ndugulile amesema kuwa mtu yeyote anayetoa tiba asili na mbadala kwanza ni lazima asajiliwe na mamlaka husika ambayo ni Wizara ya Afya, pili lazima dawa zake ziwe zimesajiliwa na Wizara ya Afya na kusisitiza kuwa nabii huyo pia anapaswa kuthibitisha amesajiliwa wapi na lini.
“Tuepuke kutoa kauli ambazo zinakwenda kuchanganya jamii, na endapo tutabaini mtu huyu hana sifa ambazo anasema kuwa nazo tutamchukulia hatua za kisheria” Amesema Dkt. Ndugulile.

HOSPITALI YA WILAYA MWANGA YAPEWA WIKI MBILI KUJA NA MKAKATI WA UPATIKANAJI WA VIPIMO MUHIMU VYA AFYA

- Hakuna maoni
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bw. Thomas Apson (kulia) mara baada ya kuwasili katika ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Mwanga.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kulia) akifafanua jambo kwa watumishi wa Wilaya ya Mwanga (hawapo pichani) kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Bw. Thomas Apson.

Mbunge wa Jimbo la Mwanga Prof. Jumanne Maghembe akisema jambo kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani) wakati wa Ziara ya Dkt. Ndugulile Wilayani Mwanga.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akionyesha alama ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika dawa zote ambazo zinatolewa Serikali kwa Mbunge wa Jimbo la Mwanga Prof. Jummane Maghembe.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua uwekaji wa kumbukumbu za taarifa za jotoridi la jokofu la dawa katika Hospitali ya Wilaya ya Mwanga.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua kadi ya bima ya afya ngazi ya jamii iliyoboreshwa kutoka kwa mgonjwa aliyefika hospitali ya Wilaya ya Mwanga kupata huduma za afya.

Na WAMJW – Mwanga, Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ameutaka uongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Mwanga kuandaa mkakati madhubuti utakaowawezesha kuwa na vipimo muhimu vya afya.
Dkt Ndugulile ametoa agizo hilo alipotembelea Hospitali ya Wilaya ya Mwanga kujionea hali ya utoaji huduma na kubaini kuwa hospitali hiyo haina vipimo vya damu, vipimo vya kemia pamoja vipimo vya CD4.
”Kwa miaka miwili sasa hakuna vipimo vya msingi katika hospitali hii, tunawakosesha huduma wananchi” amesema Dkt. Ndugulile
”Haiwezekani Hospitali kubwa ndani ya Wilaya kukosa vipimo vya msingi, haiwezekani mtu hapa sasa hivi anahitaji kipimo cha damu atoke hapa aende Hospitali ya Mawenzi Moshi kwa ajili ya vipimo” amesema Naibu Waziri Ndugulile.
Katika hatua za kutafuta ufumbuzi wa changamoto hiyo, Waziri Ndugulile ameushauri uongozi wa afya ndani ya Wilaya kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga kuhakikisha wanatenga fedha kwa ajili ya kununua vifaatiba hivyo ili wananchi waweze kupata huduma za vipimo ndani ya Wilaya ya Mwanga.
Aliendelea kushauri kuwa kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wao wanatoa mkopo wa majengo na vifaa kwa taasisi za umma na binafsi, mnaweza kuwafikia NHIF na kujadili kuhusu suala hili.
”Huko kwingine wanazitumia hizo fursa, kaeni na watu wa NHIF, Meneja wa NHIF kaa na viongozi wa Hospitali hii ikiwezekana mkubaliane hivyo vitu vipatikane kwa haraka” ameshauri Dkt. Ndugulile.
”Naamini mna wadau wa maendeleo ambao mnashirikiana nao katika mambo mbalimbali, timu ya afya ndani ya mkoa, wilaya pamoja na hospitali nawaombeni sana tuwe tunaomba vitu ambavyo vina manufaa kwa wananchi” amesisitiza Dkt. Ndugulile.
Awali akitoa salamu za wananchi wa Wilaya ya Mwanga, Mbunge wa Jimbo la Mwanga Profesa Jumanne Maghembe amesema kuwa changamoto ya kijiografia ndani ya Wilaya hiyo inachangia wananchi kukimbilia hospitali za Wilaya jirani ili kuweza kupata huduma.
”Wilaya yetu hii ina upande wa mlimani na huku tambarare, wananchi wengi walio huku tambarare wanaona ni bora kwenda Moshi kwa ajili ya matibabu kuliko kwenda juu mlimani iliko Hospitali” amesema Prof. Maghembe.
Hata hivyo Prof. Maghembe amesema kuwa tayari ndani ya Wilaya wameshaanza taratibu za kujenga Hospitali nyingine eneo la chini (tambarare) ili wananchi wanaoishi maeneo hayo waweze kupata huduma za afya ndani ya Wilaya ya Mwanga.

Alhamisi, 13 Februari 2020

NARUDISHA HUDUMA ZA CHAKULA CHUONI - DKT.CHAULA

 Katibu Mkuu Dkt. Zainab Chaula na Watumishi wengine kutoka Sekta ya Afya wakimpiga jeki moja kati ya mwanachuo wa mwaka wa tatu wa chuo cha afya ya mazingira Kagemu.

Baadhi ya wanachuo wa chuo cha afya mazingira Kagemu wakimsikiliza Katibu Mkuu ambapo anewaahidi kurudisha huduma ya chakula na kufanya ukarabati jiko la chuoni hapo.

Katibu Mkuu Dkt. Zainab Chaula akiwa kwenye picha ya pamoja na Wanachuo wa mwaka wa tatu wa chuo cha afya ya mazingira Kagemu.


NARUDISHA HUDUMA ZA CHAKULA CHUONI - DKT.CHAULA

Na. Catherine Sungura-Kagera

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula ameahidi kurudisha chakula kwa wanachuo wote ili kuondoa kupoteza muda wa kujipikia.

Dkt. Chaula ameyasema hayo mara baada ya kukitembelea chuo cha afya mazingira-Kagemu kwenye ziara ya usimamizi shirikishi akishirikiana na  TAMISEMI ambao wamefika chuoni hapo kuona mazingira ya chuo hicho ambacho kilipata madhara ya tetemeko la ardhi  lililotokea mkoani hapa mwaka 2016.

"Nitaanza ukarabati wa jiko na darasa,ninamwagiza  mkuu wa chuo afanye tahimini ili kila mwanafunzi awe na utulivu wa mwili na roho".

Aidha,Dkt. Chaula amekitaka chuo hicho kuanza mara moja kusafisha eneo la chuo hicho ili waanze kutengeneza matuta kwa ajili ya kulima bustani ambayo itasaidia kupunguza gharama ya kununua mahitaji mengine nje ya nchi.

"Uzalendo unaanzia vyuoni hivyo nitatoa fedha kwa ajili ya vibarua wasafishe eneo la shamba lote  na muanze kulima bustani,lazima mjifunze ujasiliamali mkiwa chuoni".

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera Dkt. Hasan Kawia  amesema wamepokea maagizo yote na kuahidi kuyafanyia kazi ikiwemo tatizo la gari la kuwapeleka mafunzo kwa vitendo wanafunzi hao mipakani

Dkt. Kawia amesema atamfikishia Katibu Tawala wa mkoa suala hilo kwani serikali  bado inawahitaji maofisa afya katika kulinda jamii isipate magonjwa hususani yale ya milipuko na vile vile kudhibiti magonjwa kutoka nchi jirani yasiingie nchini.

MWISHO

KITENGO CHA MAGONJWA YA DHARURA KANDA YA KATI CHAZINDULIWA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge akiongoza zoezi la kukata utepe, ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Kitengo cha matibabu ya Magonjwa ya Dharura na Majeruhi kanda ya kati katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Jijini Dodoma.

Muonekano wa vitanda na vifaa vya matibabu ndani ya Kitengo cha matibabu ya Magonjwa ya Dharura na Majeruhi kanda ya kati katika Hospitali ya Benjamini Mkapa iliyopo Jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge, akisalimiana na Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya Dkt. Leonard Subi baada ya tukio uzinduzi wa Kitengo cha matibabu ya Magonjwa ya Dharura na Majeruhi kanda ya kati katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Jijini Dodoma.

Baadhi ya Watumishi wa Hospitali ya Benjamini Mkapa waliojitokeza kushuhudia tukio la uzinduzi wa Kitengo cha matibabu ya Magonjwa ya Dharura na Majeruhi kanda ya kati katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Jijini Dodoma.

Picha ya pamoja ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge baada ya  uzinduzi wa Kitengo cha matibabu ya Magonjwa ya Dharura na Majeruhi kanda ya kati katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Jijini Dodoma.

Muonekana wa Jengo la Kitengo cha matibabu ya magonjwa ya dharura na majeruhi kanda ya kati katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Jijini Dodoma.



KITENGO CHA MAGONJWA YA DHARURA KANDA YA KATI CHAZINDULIWA.

Na Rayson Mwaisemba, WAMJW-DOM

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge, leo amezindua Kitengo cha matibabu ya Magonjwa ya Dharura na Majeruhi kanda ya kati katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Jijini Dodoma.

Katika uzinduzi huo Mhe. Dkt. Binilith Mahenge amesema kuwa, kitengo hiki ni mkombozi kwa wanachi wa Kanda ya kati hasa ukizingatia kuwa ujio wa Serikali hapa Dodoma umechagiza ongezeko na muingiliano wa watu jambo linaloweza kuongeza matukio ya ajali na magonjwa ya dharura.

“Kitengo hiki ni mkombozi kwa Wanachi wa Kanda hii hasa ukizingatia kuwa ujio wa Serikali hapa Dodoma umechagiza ongezeko na muingiliano wa watu jambo linaloweza kuongeza matukio ya ajali na magonjwa ya dharura jijini na maeneo yanayozunguka jiji la Dodoma,” alisema.

Aliendelea kusema kuwa, Hospitali ya Benjamin Mkapa pamoja na huduma zingine za afya ilianzishwa ili kutoa huduma za Kibingwa, hivyo Serikali inategemea  kuona kitengo hiki kikitoa huduma za kibingwa  kwa magonjwa ya dharura na majeruhi.

Aidha, Dkt. Binilith Mahenge amesema, Serikali iliingia makubaliano na Shirika la misaada la Israel (MASHAV- ISRAEL AGENCY FOR INTERNATIONAL DEVELOPMENT COOPERATION) kwa ajili ya kuboresha huduma za afya zinazotolewa BMH hususan wagonjwa wa dharula na majeruhi,

Mbali na hayo amesema kuwa, Shirika hilo limekubali kutoa  msaada wa vifaa vya kutoa huduma za dharula na kwa majeruhi na kutoa mafunzo kwa wataalamu wa afya wa Hospitali ya Benjamin Mkapa  juu ya utoaji wa huduma  hizo.

“Serikali iliingia makubaliano na Shirika la misaada la Israel (MASHAV- ISRAEL AGENCY FOR INTERNATIONAL DEVELOPMENT COOPERATION) kwa ajili ya kuboresha huduma za afya zinazotolewa hususan wagonjwa wa dharula na majeruhi, kwa kuboresha eneo la kutolea huduma pamoja na kutoa  msaada wa vifaa vya kutoa huduma za dharula na kwa majeruhi. Vilevile kutoa mafunzo kwa wataalamu wa afya” alisema.

Kwa upande mwingine amempongeza Mkurugenzi wa Hospitali ya benjamini mkapa na Watumishi  wake wote kwa jitihada kubwa mnazozifanya katika kuhudumia wananchi wa Kanda ya Kati na Tanzania kwa ujumla.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa wa Dkt. Alphonce Chandika amesema kuwa, mpaka sasa kitengo hiki cha dharura na majeruhi kimeshahudumia zaidi ya wagonjwa  3,000.

“Kwa Kanda ya Kati, Kitengo hiki kiko  hapa Hospitali ya Benjamin Mkapa pekee. Na mpaka sasa zaidi ya wagonjwa 3,000 wamepata huduma kutoka katika kitengo hiki,” alisema Dkt. Chandika.

Aidha, Dkt. Chandika amemuomba Naibu Balozi kuendelea kutoa msaada wa  mafunzo mbalimbali kwa watumishi wa Benjamin Mkapa ili kuwajengea uwezo zaidi katika kitengo hiki cha dharula na kwenye maeneo mengine ya kibingwa, katika huduma ambazo zinatarajiwa kuanzishwa ikiwemo huduma za matibabu ya moyo, matibabu ya saratani, upandikizaji wa viungo.

Nae Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi ameishukuru amemuomba Naibu balozi Mheshimiwa Eyal David pamoja na madaktari alioambatana nao wasisite kuendelea kuisaidia Hospitali hii pale watakapohitaji msaada toka kwenu, huku akisisitiza kuwa, huu ni mwanzo mzuri wa ushirikiano kati ya Hospitali ya Benjamin Mkapa na Serikali ya Israel.

Jumatano, 12 Februari 2020

ONGEZENI KASI YA KUWAHUDUMIA WANANCHI:DKT. CHAULA

 Dkt. Zainab Chaula akiangalia vifaa vilivyowekwa kwenye wodi hiyo maalum ya kuwahudumia wagonjwa wa milipuko endapo watatokea.

Mganga mfawidhi wa zahanati ya Bangwe akimuelezea Katibu Mkuu Dkt. Zainab Chaula jinsi walivyojipanga kutoa huduma endapo atatokea muhisiwa wa magonjwa ya mlipuko kwenye jengo maalum lililotengwa na manispaa ya kigoma,




Jengo la wazazi ambalo limejengwa kutokana na fedha za malipo kwa ufanisi(RBF) ambapo imesaidia kuongezeka kwa akina mama kujifungulia kwenye zahanati kutoka akina wajawazito 10  kwa mwezi mwaka 2018 hadi akina wajawazito 30 kwa mwezi mwaka 2019



ONGEZENI KASI YA KUWAHUDUMIA WANANCHI:DKT. CHAULA

Na. Catherine Sungura-Kigoma

Watumishi wa afya nchini wametakiwa kuongeza kasi ya kuwahudumia wananchi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini

Rai hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto-Idara kuu Aftlya Dkt. Zainab Chaula wakati akiongea na watumishi wa zahanati ya Kigoma jijini hapa.

"Tunaboresha huduma za afya kote nchini ili watu wasisafiri umbali mrefu kwenda kutafuta huduma za afya,zahanati ni ngazi ya awali ya afya ya msingi hivyo inasaidia wagonjwa wasio na shida kubwa kupata huduma karibu na maeneo yao".Amesema Dkt. Chaula

Aidha, ameongeza kuwa kabla ya kuboresha huduma za afya nchini asilimia 80 ya akina mama walikuwa wakijifungulia majumbani,hivyo kwa hali.ya sasa akina mama  wanafika vituoni kwa sababu ya kufuata huduma zilizoboreshwa.

Hali kadharika Dkt. Chaula aliupongeza Mpango wa Malipo kwa Ufanisi(RBF) kwa kuwajengea wodi ya wazazi kwenye zahanati na kuwapatia motisha watumishi

"Kigoma imeingia katika mpango huu mwaka 2017 na hivyo niwapongeze kwa kuweza kuboresha huduma pamoja na kufanya makubwa ,kwa maboresho haya lazima wananchi wapate  huduma bila manyanyaso yeyote".Alisisitiza

Naye Mganga mfawidhi wa zahanati hiyo Godlove Myinga amesema kuwa kwa kipindi cha mwezi julai hadi septemba 2018 zahanati hiyo ilipokea kiasi cha shilingi milioni  7,924,214  ambazo asilimia 25 zitatumika kama motisha kwa watumishi na asilimia 75 itatumika kwa ajili ya ukarabati na vifaa tiba.

Kwa upande wa akina mama wanaojifungulia kwenye zahanati hiyo Mganga mfawidhi huyo amesema kumekuwa na ongezeko tangu wodi ya wazazi ilipozinduliwa  mwaka 2018 kutoka akina mama 10 kwa mwezi  hadi kufikia akina mama 30 mwaka 2019.

Mpango wa Malipo kwa Ufanisi (RBF) ni mfumo wa malipo ya fedha kwa vituo vya afya mara baada ya kufanyika uhakiki wa majukumu na viashiria vilivyowekwa na hivyo malipo hutokana na kiwango cha utendaji ,RBF ilianza kutekelezwa hapa nchini mwaka 2015 na kutarajia kuisha mwaka huu. 

Fedha za Mpango huu zimesaidia kuinua kiwango cha utoaji huduma katika vituo vya afya ambapo utumika katika kufanya ukarabati mdogomdogo wa vituo, ununuzi wa vifaa tiba, dawa na mahitaji mengine ya kituo. 

MWISHO

WANANCHI KIJIJI CHA KALENGE WAISHUKURU SERIKALI KUWAJENGEA ZAHANATI

Katibu Mkuu Wizara Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula akiwa na Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya Dkt. Grace Magembe, wakati wa ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma katika  Mkoa wa Kigoma.

Baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Kalenge wilayani Uvinza wakifurahia ujio wa Katibu Mkuu Wizara Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainab Chaula, kwa kuwajengea Zahanati na hivyo kuwahepusha na vifo vitokanavyo na uzazi.




Zahanati iliyojengwa katika Kijiji cha Kalenga Wilaya ya Uvinza ikiwa tayari kuanza kutoa huduma



WANANCHI KIJIJI CHA KALENGE WAISHUKURU SERIKALI KUWAJENGEA ZAHANATI

Na.Catherine Sungura-Uvinza

Wananchi wa kijiji cha Kalenge wilayani hapa wameishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kuwajengea zahanati na hivyo kuwahepusha na vifo vitokanavyo na uzazi.

Hayo yamebainishwa jana  na wakazi wa kijiji hicho wakati walipotembelewa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto-Idara Kuu Afya  Dkt. Zainab Chaula ambaye ameanza ziara ya usimamizi shirikishi mkoani kigoma ambayo inafanywa na wizara ya afya pamoja na TAMISEMI.

Akiongea kwa furaha bi. Marystela Chishako alisema kuwa wanaishukuru serikali ya awamu ya tano kwani kwa kupata zahanati hiyo imewasaidia kupata huduma za afya ikiwemo huduma ya kujifungua ambayo awali walikua wakiifuata kigoma mjini.

"Tunashukuru kwa serikali hii kutukumbuka mkoa wa kigoma,siku za nyuma mama akitaka kujifungua ilibidi aende kigoma mjini,ila hivi sasa tunajifungulia hapa hapa kwenye zahanati na tunapata huduma muhimu hapa hapa".

Aidha, alisema zahanati hiyo imewasaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto kwani kipindi cha nyuma walikua wakipata matatizo njiani kwa sababu walikua wakisafiri umbali mrefu na kupelekea kupata matatizo wakiwa njiani.

Katika Ziara hiyo Katibu Mkuu Dkt.Chaula aliwahidi kulifanyia kazi ombi lao la kupatiwa kituo cha afya kwani wameshaomba kwa kufuata utaratibu kupitia mkoa.

"Ninawapongeza kwa sababu mmejua umuhimu wa kuwa na kituo cha afya,kwahiyo maombi yataletwa wizara ya afya kutoka TAMISEMI,na katika ziara yangu nimeongozana nao hapa na nimepokea ombi hili najua ukitoa ahadi lazima utimize".Alisema Dkt. Chaula

Hata hivyo Katibu Mkuu huyo amesema atahakikisha wanapata fedha ili kutimiza ndoto za wananchi hao"mmefanya wajibu wenu na uzalendo mkubwa wa kuipenda nchi yenu kwa kujituma mpaka mmetenga eneo na kuweka mawe na mchanga, hivyo serikali itaongezea nguvu pale mlipoanzisha.

Wakazi wa kijiji hicho wametenga eneo la hekari ishiriki,kukusanya mawe pamoja na mchanga kwa kujitolea ili kuweza kujenga kituo cha afya ikiwa ni juhudi za kuiunga mkono serikali kwa kutatua changamoto za huduma za afya karibu na wananchi.

MWISHO

Jumatano, 5 Februari 2020

MAAMBUKIZI MAPYA YA MALARIA YAMEPUNGUA KWA ASILIMIA 27

 Katibu wa Chama cha TAPAMA Mhe. Raphael Chegeni akionesha kadi ya tathmini ya Malaria, wakati wa kikao cha uraghabishaji kwa Wakurugenzi na Wakuu wa vitengo wa Wizara ya Afya.

Mkurugenzi wa Kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi akisikiliza maoni ya washiriki, wakati kikao na umoja wa wabunge wa kupambana na malaria na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Tanzania(TAPAMA) na Alma (African Leaders Malaria Alliance).

Mwakilishi wa Alma Tanzania Bw. Diego akiwasilisha mada kuhusu namna namna ya kuingia kwenye mfumo wa simu/kompyuta ya kadi ya tathmini ya Malaria ili kujionea utendaji wa Mkoa au hatua zinazochukuliwa kutatua matatizo ya eneo husika.

Picha ya pamoja kati ya Watumishi wa Wizara ya Afya na wabunge wa kupambana na Malaria na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Tanzania(TAPAMA) na viongozi wa Alma (African Leaders Malaria Alliance) waliofika Wizara ya Afya kufanya uraghibishaji wa  kadi ya tathimini ya malaria  kwa ajili ya uwajibikaji na utendaji kwa viongozi wa wizara jijini hapa.


MAAMBUKIZI MAPYA YA MALARIA YAMEPUNGUA KWA ASILIMIA 27

Na WAMJW - Dodoma.

Maambukizi mapya ya ugonjwa wa malaria yamepungua nchini   kwa asilimia 27 na hiyo ni kutokana na kuboreka kwa utoaji huduma za mapambano ya ugonjwa huo ukilinganisha na waginjwa 164 kati ya watu 1000 mwaka 2015 hadi wagonjwa 119 kati ya watu 1000 mwaka 2018.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Kinga Dkt. Leonard Subi wakati akitoa taarifa kwa umoja wa wabunge wa kupambana na malaria na magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Tanzania(TAPAMA) na Alma (African Leaders Malaria Alliance) waliofika wizara ya afya kufanya uraghibishaji wa  kadi ya tathimini ya malaria  kwa ajili ya uwajibikaji na utendaji kwa viongozi wa wizara jijini hapa.

Dkt. Subi amesema kuwa mafanikio hayo yametokana na jitahada za viongozi wa Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na muhimili wa Bunge katika ushirikiano mzuri na wadau pamoja ma wananchi katika kupambana na ugonjwa huo.

Amesema kuwa viongozi wa nchi za afrika wanawajibika kwa afya za wananchi na hivyo kwa Tanzania vifo vitokanavyo na Malaria vimepungua  kwa asilimia 63 kutoka vifo 6,737 mwaka 2015  hadi 2,540 mwaka 2018.

“Ingawa hivi sasa tupo kwenye kudhibiti ila  tunalengo la kutokomeza,hivyo tuna imani kwamba tanzania tunao uwezo mkubwa wa kufikia huko kwani kuaniza Mh. Rais Wetu hadi muhimbili kama Bunge nao wako mstari wa mbele kuondosha malaria nchini”.

Aidha, amesema kuwa hivi sasa kumekuwa na mabadiliko makubwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini kwa kupungua kwa wagonjwa wanaougua malaria kupungua pia hata kwa watoto chini ya miaka mitano vifo vimepungua.

“Tanzania tumeamua kupambana na wadudu dhurifu kuanzia ngazi ya viluilui hadi mbu wapevu waenezao maradhi, hivyo kila mwananchi anawajibu wa  kuchukua hatua, hivyo ni vyema tukaungana ili kuiondosha Malaria nchini”.Amesema Dkt. Subi

Naye Katibu wa TAPAMA Mhe. Raphael Chegeni amesema kuwa msingi wa taifa ni kuwa na afya ,hivyo wanafarijika na afua zinazochukuliwa na wizara ya afya katika kupambana na malaria nchini “Malaria inaua hivyo tunajivunia kuona tanzania inazidi kupambana kutokomeza ugonjwa huu.

Kadi ya tathimini ya malaria ni kitendea kazi cha usimamizi kilichotolewa na wizara ya afya kinachoonyesha takwimu za utendaji wa viashiria vya malaria vilivyopewa kipaumbele katika ngazi ya mikoa na wilaya  ambayo inaleta urahisi katika kutambua wapi kuna tatizo ili hatua za kuokoa maisha ziweze kuchukuliwa.

Mwisho