Like us on Facebook

Inaendeshwa na Blogger.

Tafuta katika Blogu Hii

Instagram

visitors

display number of visitors

Popular Posts

Pages

Flickr Images

Jumatatu, 27 Aprili 2020

SERIKALI YAPOKEA MSAADA WA SHILINGI BILIONI 14.9

- Hakuna maoni









 
Na WAMJW-Dar es Salaam

Serikali  imepokea msaada wa shilingi bilioni 14.9 kutoka Global Fund, Airtel Tanzania, Rotary Club Tanzania ambazo sehemu kubwa zitatumika kununua vifaa kinga kwa watumishi wa afya na vifaa tiba kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wenye maambukizi ya COVID-19.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ameyasema hayo leo wakati akipokea msaada wa fedha na lita 1,250 za vitakasa mikono ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kupambana na maambukizi ya virusi vya Corona.

Waziri Ummy amefafanua kwamba Global Fund imetoa shilingi bilioni 14, Airtel Tanzania shilingi milioni 700 na Rotary Club Tanzania shilingi milioni 250.

“Tumepokea shilingi bilioni 14 kutoka Global Fund, shilingi bilioni 9.6 tumezitoa kwa ajili ya kununua vifaa kinga kwa ajili ya watumishi wa Afya, lakini pia fedha zilizotolewa na Airtel na Rotary Club Tanzania tutazielekeza huko. Kipaumbele chetu ni kuwalinda watumishi wa afya,” amesema Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu.

“Natumia fursa hii kuwashukuru watumishi wa afya ambao wamekuwa wakijitoa usiku na mchana katika kutoa huduma kwa watu waliopata maambukizi ya virusi vya Corona (Covid-19) pamoja na wale wahisiwa.

"Kipaumbele cha Serikali ni kuwalinda watumishi wa Afya kwa kununua vifaa kinga kwani fedha tulizozipata hapa tutazielekeza kwenye ununuzi wa vifaa kinga.  Niendelee kuwaisistiza Watumishi wa Afya wazingatie miongozo ya magonjwa ya kuambukiza,” Amesema Waziri Ummy .

Amesema watumishi wa afya ambao wamepatiwa mafunzo katika vituo vya kutoa huduma kwa wenyr maambukizi ya  ugonjwa huo,  hakuna aliyepata maambukizi kwa kuwa wanazingatia miongozo ya Serikali ya kutoa matibabu kwa wagonjwa wa Covid-19 pamoja na miongozo ya magonjwa ya kuambukiza.

Waziri amesema ushiriki wa kila mdau katika mapambano dhidi ya maambikizi ya virusi vya Corona ni muhimu na kwamba msaada uliotolewa na kampuni hizo ni mkubwa katika mapambano ya maambukizi ya ugonjwa wa Corona.

“Napenda kurudia tena kwa niaba Mhe. Rais Dkt. John Magufuli, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, nawashukuru Airtel Tanzania, Serengenti Breweries na Rotary Club kwa hiki mlichotupatia. Asanteni sana,” amesema Waziri Ummy.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Airtel Tanzania, Bw. Gabriel Malata amesema Airtel Tanzania imetoa shilingi milioni 700 ikiwa ni sehemu ya  kuunga mkono juhudi za Serikali za kupambana na janga la Corona.

“Sisi bodi ya wakurugenzi wa Airtel na kwa niaba ya Airtel Tanzania, tunatambua juhudi za Serikali katika kupambana na ugonjwa wa Corona, lakini pia tumejitathimini na kutambua kuwa sisi kama 

Airtel hatuwezi kuendelea bila kuwepo watu wanaotumia huduma zetu. Watu hawa ndio mtaji wa Kampuni,” amesema Bw. Gabriel.

Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kampuni ya Bia ya Serengenti, Bw. John Wanyancha amesema kuwa kampuni hiyo imetoa lita 1,250 ya vitakasa mikono nyenye thamani ya shilingi milioni 15  kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kupambana na maambukiza ya virusi.

Mwenyekiti wa Rotary Club, Bi. Agnes Batenga amesema Rotary imetoa shilingi milioni 250 kwa ajili ya kupambana na ugonjwa wa homa ya mapafu (COVID-19).

“Shilingi milioni 183 zitatumika kutoa msaada wa vifaa vya kujikinga (PPE), vifaa vya maji safi ambavyo vitasambazwa katika vituo maalumu vya kuhudumia wagonjwa wa Corona jijini Dar es Salaam, Hospitali ya Amana, Zanzibar, Hospitali ya Mawenzi na Hospitali ya Mount Meru,” amesema Bi. Agnes.

Amesema shilingi milioni 67 zitatumika katika kutekeleza miradi ya kudhibiti ugonjwa wa Corona nchini kupitia Club za Rotary.

Jumapili, 26 Aprili 2020

TUENDELEE KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA CORONA - ASP SWEBE

- Hakuna maoni
Mrakibu mwandamizi wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam ASP Edith Swebe akieleza jambo mbele ya timu ya uhamasishaji wa elimu juu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona katika kituo cha polisi Pangani Ilala.

Timu ya uhamasishaji kutoka Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau kutoka Shirika lisilo Lakiserikali la Project CLEAR wakiendelea na uhamasishaji jinsi  ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa abilia na bodaboda katika kituo cha daladala cha Mbezi kwa Msuguli.

Sfaff sergeant (S/Sgt ) Valentine Ngowi akiongea na madereva boda boda wa kituo cha Mbezi mwisho Jijini Dar es Salaam juu ya tahadhari za kuchukua ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo Flavour) Banana Zolo akinawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka, ishara ya kuunga mkono kampeni ya kusafisha mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka kama moja ya nyenzo ya kupambana dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Mkazi wa Mbezi Mwisho Jijini dar es salaam aliyeweka uzio wa kamba kwenye duka lake kujitenganisha na mteja, inayosaidia kumzuia mteja kuingia dukani kabla ya kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka na kuzuia mteja asikae karibu nae wakati anamhudumia, ikiwa ni muitikio chanya kutoka Wizara ya Afya wa kukaa mita moja au zaidi baina ya mtu mmoja na mwingine na kusafisha mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka kabla ya kupata huduma yoyote ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.

Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba), pamoja na askari polisi kituo cha polisi Pangani Ilala wakinyoosha mikono, ishara ya kuunga mkono kampeni ya mikono safi, Tanzania salama inayohamasisha kunawa mikono kwa sabuni  na maji safi yanayotiririka.



TUENDELEE KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA CORONA - ASP SWEBE

Na WAMJW- DSM

Mrakibu mwandamizi wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam ASP Edith Swebe ametoa wito kwa wananchi, hususan Wana Dar es Salaam kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

Ameyasema hayo wakati akiwa katika majukumu yake ya ukaguzi wa namna gani kituo cha Polisi Pangani kilichopo Ilala Jijini Dar es Salaam kimechukua hatua ya kukabiliana dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

"Tunaendelea kukumbusha Wananchi wa hususan Wanaotoka Jijini Dar es Salaam kunawa mikono na kuchukua hatua zote za tahadhari zinazotakiwa, tunaendelea kusisitiza kila mmoja katika familia yake aendelee kuchukua hatua ambazo Wizara ya Afya inapendekeza" alisema

Kwa upande mwingine, ASP Swebe ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kuja na kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" inayohamasisha wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona, hali inayoonesha jinsi gani Serikali imewekeza kwenye Afya ya wananchi.

"Kwanza nitoe shukrani kwa Serikali kupitia Wizara ya Afya, kwa Kampeni inayoendelea ya "Mikono safi, Tanzania salama", hii inaonesha ni jinsi gani Serikali imewekeza kwenye Afya ya wananchi" alisema.

Aidha, ameishukuru Wizara ya Afya kwa kuendelea kulisaidia Jeshi la polisi vifaa vya kujikinga dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona ikiwemo vitakasa mikono na Barakoa (mask).

Kwa upande wake, Sfaff sergeant (S/Sgt ) Valentine Ngowi, amewataka madereva wote wa vyombo vya moto hususan bodaboda na bajaj kuhakikisha wanavitakasa vyombo vyao vya usafiri kwa sabuni mara kwa mara ili kuua maambukizi ya virusi vya Corona endapo vitakuwepo.

Uhamasishaji huu unafanywa kupitia kampeni hii ya “Mikono safi, Tanzania salama” inaratibiwa na Wizara ya Afya, kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Project CLEAR kwa kushirikiana na Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) kutoka Mjomba Theatre Gallery unaendelea katika Jiji la Dar es Salaam.

Mwisho

Ijumaa, 24 Aprili 2020

WAGONJWA 37 WA CORONA WAPONA NA KURUHUSIWA HUKU 71 WAKISUBIRI VIPIMO VYA MWISHO

- Hakuna maoni


Na.WAMJW-Dar es Salaam

Wagonjwa 37 waliokuwa wameambukizwa virusi vya Corona (COVID-19) wamepona na kuruhusiwa kurejea nyumbani baada ya vipimo vya mwisho kuthibitisha kwamba hawana maambukizi ya COVID-19.

Hayo yamesemwa leo  na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akipokea msaada wa sabuni na fedha kutoka kampuni ya Azania group ya jijini hapa

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amesema kuwa wagonjwa hao 37 ni kati ya wagonjwa 108 waliothibitika kuwa na maambukizi ya virusi vya Corona lakini hivi sasa hawana dalili zozote za ugonjwa kama homa, mafua na kikohozi.

“Watu hawa 108 hawana dalili zozote za ugonjwa kama vile homa au mwili kuchoka isipokuwa wapo katika vituo vya matibabu kusubiri vipimo vya mwisho ili kuthibika kwamba hawana virusi vya corona kabla ya kuruhusiwa kutoka vituoni, hivyo wamepona na wameruhusiwa kurejea nyumbani,” amesema Waziri wa Afya.

Waziri Ummy Mwalimu amewataka watu waliopona ugonjwa huo kuzingatia maelekezo ya wataalamu wa afya ili kujikinga na maambukizi mapya ya COVID-19 kwani zipo tafiti zilizofanyika nchi mbalimbali ikiwamo China zimeonyesha kuwa watu wanaweza kupata  maambukizi mapya kama asilimia 14.

“Tunapenda kuwahimiza watu waliopona watoe elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona (COVID-19) kwa jamii. Pia, Nitumie fursa hii kwa niaba ya Serikali  kutoa shukrani zetu za thati kwa watumishi wa afya kwa kuendelea kutoa huduma kwa watu wenye maambukizi ya COVID-19. Asanteni sana watumishi wa afya,” amesema Waziri.

Waziri pia ametoa wito kwa watumishi wa afya kuendelea kutoa huduma za afya kwa watu wote wanaohitaji huduma za matibabu wakiwamo wenye dalili za ugonjwa wa Corona.

“Tumeona kumeanza tabia ambayo ni kinyume na taratibu za afya, hatutakiwi kuwakataa wagonjwa wenye dalili za maambukizi ya virusi vya Corona. Nasisitiza kwamba watumishi wa afya wanakumbushwa kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia nwongozo wa Taifa wa kudhibiti maambukizi (National Infection Prevention and Control Guidelines for Health care Services in Tanzania) wa Juni, 2018 pamoja na mwongozo wa Menejimenti ya Matibabu ya Ugonjwa wa COVID-19 wa Januari, 2020 ili kujikinga na maambukizi wakati wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa,” amesema Waziri Ummy Mwalimu.

Wakati huo  Waziri Ummy Mwalimu ameishukuru kampuni ya Azania group kwa msaada wa sabuni 300 na fedha shilingi milioni 50 kwa ajili ya mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Msaada huo utatumika kwa chakula cha wagonjwa na usafi kwenye vituo vya tiba cha Temeke,Amana na Kisoka-Mloganzila.

Jumatano, 22 Aprili 2020

WAZAZI TUWAKINGE WATOTO WETU DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA

Wakazi wa eneo la Keko Jijini Dar es Salaam wakisikiliza elimu kuhusu mbinu za kujikinga wao na Watoto wao kupata maambukizi ya virusi vya Corona kutoka kwa timu ya uhamasishaji kutoka Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau kutoka Shirika lisilo Lakiserikali la Project CLEAR.

Dereva boda boda wa eneo la Kariakoo Jijini Dar es Salaam wakisikiliza elimu kuhusu mbinu za kujikinga kupata maambukizi ya virusi vya Corona.

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima akikabidhi vitakasa mikono kwa askari wa jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani ili viwasaidie kujilinda dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona wakati wa kutoa huduma kwa wananchi, katika eneo la Kariakoo Jijini Dar es Salaam.

Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba), akikabidhi boksi la vitakasa mikono (sanitizer) Mrakibu msaidizi wa polisi (ASP) Angelica, makao makao makuu ndogo ya jeshi la polisi, Posta Jijini Dar es Salaam.

Afisa kutoka jeshi polisi kitengo chaushrikishaji jamii Stafu Sajenti Valentino Ngowi akiongea na Dereva boda boda na Bajaji, kuhusu elimu ya kujikinga kupata maambukizi ya virusi vya Corona.

Mkurugenzi wa Lemutuz Brand, vyombo vya utoaji habari za kwa njia ya mtandao, Ndg. Lemutuz akinawa mikono yake kwa sabuni na maji safi yanayotiririka ikiwa ni sehemu ya uhamasishaji kwa wananchi juu ya kunawa mikono, kama moja ya njia ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Timu ya uhamasishaji kutoka Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wadau kutoka Shirika lisilo Lakiserikali la Project CLEAR na kampuni ya Mjomba Gallery ikiendelea na utoaji elimu kwa wafanyabiashara wa Kariakoo Jiji la Dar es Salaam kuhusu kuchukua tahadhari za kujikinga dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.



WAZAZI TUWAKINGE WATOTO WETU DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA

Na WAMJW- DSM

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa wito kwa wazazi na walezi nchini kuwalinda Watoto wao dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa kuhakikisha wanajikinga vizuri na kuwakinga watoto wao dhidi ya virusi hivyo,

Wito huo ameutoa, Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima wakati akitoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kuhusu kuchukua tahadhari za kujikinga dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona

Ndg. Anyitike Mwakitalima amesema kuwa, Watoto wanaweza kuwa chanzo cha kusambaa kwa maambukizi ya virusi vya Corona katika jamii na familia, hivyo amesisitiza wazazi na walezi kuhakikisha wanawadhibiti watoto kuzulula mitaani katika kipindi hiki cha mlipuko wa virusi hivyo.

"Serikali kupitia Wizara ya Afya inatoa wito ambao inautoa ni kwamba wazazi na walezi tukumbuke kuwalinda watoto wetu, wakae na watulie majumbani kwa kipindi hiki shule zimefunga, msiwaruhusu waende kuzulula maeneo mbali mbali, kwani wanaweza kupata maambukizi huko wanakoenda kucheza" alisema.

Mbali na hayo, alisisitiza kuwa, wazazi watoe elimu kwa watoto kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona kwa kuhakikisha wananawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka, huku akisisitiza waepuke kushika macho, pua na mdomo ili kuzuia kupata maambukizi hayo.

"Wazazi na walezi tuwakumbushe Watoto kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka, tuwakumbushe Watoto kuepuka kushika pua, mdomo na macho kwa mikono kwa kufanya hivyo tutakuwa tumewalinda watoto watoto wetu na tutajilinda sisi wenyewe kupata maambukizi ya virusi vya Corona " alisema

Kwa upande wake, Afisa kutoka jeshi polisi kitengo chaushrikishaji jamii Stafu Sajenti Valentino Ngowi amewaagiza madereva na makondakta wao kuhakikisha kila siku jioni wanapokuwa wamemaliza kazi zao Kutakasa magari yao kwa dawa maalum aina ya jiki, ili kuua virusi vinavyoweza kuwepo na kupelekea maambukizi ya ugonjwa wa Corona.

Nae Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba), amewakumbusha Watanzania kufuata maelekezo ya Wataalamu wa Afya ikiwemo kuepuka msongamano katika maeneo yote, huku akisisitiza kama hakuna sababu yakutoka nje ni watulie majumbani.

“Nitumie fursa hii kuwakumbusha Watanzania kuendelee kufuata maelekezo ya wataalam wa afya, ikiwemo kuepuka misongamano isiyo na ulazima, na kama huna sababu ya kutoka nyumbani ni vyema ukabaki nyumbani" alisema

Mwisho.

Jumanne, 21 Aprili 2020

SERIKALI YAPONGEZWA KATIKA KUKABILIANA NA UGONJWA WA CORONA

- Hakuna maoni






Na WAMJW – Dar es Salaam

Serikali imepongezwa kwa jitihada inazozifanya katika kukabiliana na ugonjwa unaosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19) hapa nchini.

Pongezi hizo zimetolewa leo jijini Dar es Salaam na mwakilishi wa Ubalozi wa Pakistani hapa nchini Muhammad Saleem wakati akikabidhi vifaa vya kujikinga na ugonjwa huo kwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Saleem alisema tangu ugonjwa huo ulipoingia  hapa nchini mwezi uliopita kasi ya maambukizi ni ndogo ukilinganisha na nchi zingine, hiyo yote ni kutokana na hatua thabiti zinazofanywa na Serikali katika kukabiliana na ugonjwa huo.

“Nchi yetu ya Pakistani imekuwa na ushirikiano mzuri na Tanzania, hivyo basi  tumeona nasi tutoe msada wa vifaa kinga. Tunaomba mpokee mchango wetu ambao ni kidogo ili watoa huduma wa afya waweze kutumia vifaa hivi wakati wanawahudumia wagonjwa kwani ugonjwa huu ni janga la Dunia”, alisema Saleem.

Mwakilishi huyo wa Ubalozi wa Pakistani aliishauri Serikali kuendelea kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii katika kutoa elimu ya ugonjwa wa COVID-19  ili wananchi waendelee kupata elimu ya kutosha ambayo itawasaidia kujikinga na ugonjwa huo.

Kwa upande wake mganga mkuu wa Serikali Prof. Muhamad Bakari Kambi aliushukuru Ubalozi wa Pakistani kwa msaada walioutoa na kusema kuwa utasaidia kwa kiasi kikubwa katika kukabiliana na ugonjwa huo.

Prof. Kambi alisema ugonjwa wa COVID -19 ni janga la Dunia,  watu wengi wamepata madhara kutokana ugonjwa huo hivyo basi hakuna msaada mdogo. "Msaada wowote unaotolewa kwa Serikali utanasaidia kwa kiasi kukubwa katika kukabiliana na ugonjwa".

Ubalozi wa Pakistani umetoa msaada wa barakoa za upasuaji 1800, kofia ambazo zinavaliwa na  wahudumu wa afya wakati wanahudumia wagonjwa 1800, kava za viatu za kuvaliwa wodini 800, barakoa za N95 zipatazo 500, magauni ya kuvaa watoa huduma za afya 100, glovu 8000 pamoja na miwani ya kujikinga na virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Corona  60. Thamani ya vifaa hivyo ni zaidi ya milioni 11.

Mwisho

Jumapili, 19 Aprili 2020

TUACHE MZAHA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA CORONA

- Hakuna maoni
Wafanya biashara ndogo ndogo katika kituo cha mabasi Makumbusho wakipata mafunzo juu ya namna yakunawa mikono kwa sabuni na maji yanayotiririka wakati,   elimu ya kujikinga dhidi ya Corona ilipokuwa ikitolewa kituoni hapo.

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira kutoka Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima akiwaelekeza madereva bajaji namna ya kunawa  kwa kufuata taratibu za unawaji mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka kwa usahihi kulingana na miongozo ya Wizara.

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira kutoka Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima akielekeza  jambo wakati wa kampeni ya uhamasishaji kwa Jamii juu ya namna ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba), akisisitiza jambo kwa wafanyabiashara katika eneo la Coco Beach Dar es salaam juu ya umuhimu wa kuchukua tahadhari wakati wote ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) akisisitiza kukaa umbali wa mita moja au zaidi ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona pindi watu wanapoongea au mtu anapopiga chafya au kukohoa.


TUACHE MZAHA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA CORONA

Na WAMJW- DSM

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ndg. Anyitike Mwakitalima ametoa wito kwa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kuacha mzaha na kufuata taratibu kutoka kwa Wataalamu wa Afya ili kujikinga dhidi ya virusi vya Corona.

Ameyasema hayo leo, wakati akitoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kuhusu kuchukua tahadhari za kujikinga dhidi ya maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona

"Watanzania tusifanye mzaha, huu ugonjwa sio wakufanyiwa mzaha, wenzetu wa nchi zilizoendelea pamoja na uchumi wao kuwa mkubwa na sayansi yao kubwa, lakini wamefika mahali wameshindwa, hizi tahadhari za msingi ambazo tunaelekeza ni muhimu kuzizingatia " alisema.

Alisema kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Afya, inaendelea kutoa elimu ya Corona kwa jamii kupitia vyombo vya habari, lakini pia kuwafuata wananchi walipo ili kuwapa elimu hiyo na kujibu maswali yanayowatatiza, hali itayosaidia watu kufahamu njia zote za kujikinga na kuepuka kupata maambukizi ya virusi hivyo.

"Tunafahamu kwamba , bado suala la elimu halijaweza kufika kwa Jamii vyakutosha, kwahiyo tunatumia njia mbali mbali, tunatumia vyombo vya habari kama tv na redio, lakini tumeona tunakila sababu yakushuka na kwenda ambako Jamii hipo ili tuweze kuzungumza nao, na kujibu maswali ya msingi yanayowatatiza" alisema.

Aidha, alisema kuwa, kwa sehemu kubwa Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wanachukua tahadhari, kwa kuweka vifaa vya kunawia mikono na sabuni, na kusafisha mikono ya abiria kabla yakupenda usafiri.

"Kwa sehemu kubwa tumeona wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wanachukua tahadhari, ikiwemo kutengeneza jiki kwaajili yakutakasa chombo chake cha usafiri, lakini katika sehemu za biashara watu wameweka vyombo vya kunawia mikono na wanaelekezwa kunawa kabla ya kufanya manunuzi" alisema

Nae Balozi wa kampeni ya Mikoni safi, Tanzania salama, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) amewaasa wananchi kunawa mikono mara kwa mara kwa kufuata hatua tano muhimu, kama ifuatavyo moja ni kulowanisha mikono, pili kupakaa sabuni kwenye mikono ili kuua virusi vyote, tatu ni sugua mikono yako kwenye kucha, viganja, vidole na sehemu zote, nne ni kusuuza mikono kwa maji yanayotiririka, na hatua ya tano ni kufuta mikono kwa kitambaa safi.

Aliendelea kusisitiza kuwa, kulingana na miongozo kutoka kwa Wataalamu wa Afya, hairuhusiwi kufuta mikono kwenye nguo baada ya kunawa mikono kwenye hatua tano, kwani kufanya hivyo hupelekea kurudisha maambukizi mikononi endapo vitakuwepo katika nguo hizo.

Uhamasishaji huu unafanywa kupitia kampeni hii ya “Mikono safi, Tanzania salama” inaratibiwa na Wizara ya Afya, kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Project CLEAR kwa kushirikiana na Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) kutoka Mjomba Theatre Gallery unaendelea katika Jiji la Dar es Salaam.

Mwisho

Jumatano, 15 Aprili 2020

TUEPUKE MSONGAMANO KATIKA MAENEO YETU YA KAZI

- Hakuna maoni
 Mkuu wa Mkoa wa Songwe Breg. Jen. Nicodemus Mwengela akisisitiza jambo wakati akiongea na wahamasishaji kutoka Wizara ya Afya, Shirika lisilo Lakiserikali la Project CLEAR na Mjomba Theatre Gallery katika ofisi zake Vywawa Mkoa wa Songwe. 

Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi, Wizara ya Afya Ndg. Anyitike Mwakitalima akieleza jambo kuhusu ugonjwa wa Corona mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe Breg. Jen. Nicodemus Mwengela wakati walipoenda kukabidhi vifaa vya kunawa mikono na vitakasa mikono kwaajili ya Mkoa huo.

Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) kutoka Mjomba Theatre Gallery akifafanua jambo mbele ya mkuu wa Mkoa wa Songwe Breg. Jen. Nicodemus Mwengela (hayupo kwenye picha).

Waratibu wa kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" kutoka Wizara ya Afya Shirika lisilo Lakiserikali Project CLEAR na Mpoto Gallery wakifuatilia neno kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe Breg. Jen. Nicodemus Mwengela juu ya namna Mkoa unavopambana na ugonjwa wa Corona. 

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Breg. Jen. Nicodemus Mwengela akinawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka, ikiwa ni sehemu ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo kutoka Wizara ya Afya na washirika wake, pembeni yake ni Katibu tawala wa Mkoa huo.

Mwenyekiti wa Machifu Mkoa wa Songwe akinawa mikono yake kwa sabuni na maji safi yanayotiririka ikiwa ni moja ya njia ya kupambana dhidi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

Mwananchi wa Ichenjezya Vywawa Songwe akinawa mikono yake kwa sabuni na maji safi yanayotiririka ikiwa ni moja ya njia ya kupambana dhidi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) kutoka Mjomba Theatre Gallery akikabidhi vitakasa mikono na vifaa vingine vya kupambana dhidi ya ugonjwa wa Corona kwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe Breg. Jen. Nicodemus Mwengela, kulia ni Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi, Wizara ya Afya Ndg. Anyitike Mwakitalima.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Breg. Jen. Nicodemus Mwengela katika picha ya pamoja na Waratibu wa kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" kutoka Wizara ya Afya Shirika lisilo Lakiserikali Project CLEAR na Mpoto Gallery baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo kwaajili ya kupambana dhidi ya ugonjwa wa Corona Mkoani Songwe.

Afisa kutoka makao makuu jeshi la polisi kitengo cha ushirikishaji Stafu Sajenti Valentino Ngowi akihamasisha wananchi katika kituo cha mabasi Vwawa juu ya umuhimu wa kukaa zaidi ya mita moja kati ya mtu mmoja hadi mwingine ikiwa ni moja ya njia ya kupambana dhidi ya ugonjwa wa Corona katika Mkoa wa Songwe.

Afisa kutoka makao makuu jeshi la polisi kitengo cha ushirikishaji Stafu Sajenti Valentino Ngowi akikagua moja ya daladala ili kujionea kama wanafuata maelekezo ya Serikali ya kuepuka msongamano ndani ya daladala (level sit) katika kituo cha mabasi Vwawa Mkoa wa Songwe.
 
Wafanyabiashara katika Soko la Ichenjezya Vwawa Songwe wakifuatilia Elimu juu ya njia za kupambana dhidi ya ugonjwa wa Corona kutoka timu ya uhamasishaji Wizara ya Afya ikiwemo kunawa mikono kwa maji safi yanayotiririka na sabuni, au kutumia vitakasa mikono (sanitizer) na kuepuka msongamano isiyo na ulazima. 



TUEPUKE MSONGAMANO KATIKA MAENEO YETU YA KAZI.

Na Rayson Mwaisemba, WAMJW-SONGWE

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Breg. Jen. Nicodemus Mwangela ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Songwe kuepuka misongamano katika maeneo yote, ikiwa ni moja ya njia ya kupambana na ugonjwa wa Corona usisambae endapo utaingia Mkoani hapo.

Ameyasema hayo, wakati akipokea vifaa vya kunawia mikono pamoja na vitakasa mikono kutoka Wizara ya Afya na Shirika la Project CLEAR, ikiwa ni mwendelezo wa kampeni ya uhamasishaji kwa wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona.

“Serikali imetoa maagizo mbali mbali, ambayo sisi kama Serikali ya Mkoa tunayasimamia na kuhakikisha yanatekelezwa, ikiwemo kusisitiza kuepuka msongamano na mikutano isiyokuwa yalazima katika maeneo mbali mbali na hili linatekelezwa vizuri kabisa” alisema.

Mbali na hayo, amesema kuwa, maambukizi ya ugonjwa wa Corona yameleta madhara makubwa kwa maisha ya binadamu hasa katika upande wa kiuchumi, huku akisisitiza kuwa nchi nyingi duniani zimeathirika kutokana na janga hili la Corona.

“Ni kweli kabisa huu ugonjwa sasahivi, umeleta madhara makubwa kwa Maisha ya binadamu, lakini pia kiuchumi, nan chi nyingi zenye uwezo mkubwa kiuchumi na kiafya zimeahirika kutokana na janga hili”alisema.

Aidha, Mhe. Alisema kuwa, Serikali inaendelea kutoa elimu na tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Corona kwa wananchi, hii inafuatia sababu kuwa, Mkoa wa Songwe upo mpakani mwa nchi za Malawi na nchi ya Zambia ambayo inapokea pia watu kutoka nchi ya DR Congo.

“Songwe ipo kwenye mlango, tusipotoa tahadhari ya kutosha kwa wananchi kuna hatari kubwa ya ugonjwa kuingia, Mkoa wa Songwe upo mpakani, tuna KM 135 tunapakana na Zambia, KM 45 tunapakana na Malawi, nchi zote hizo tayari zina maambukizi ya ugonjwa wa Homa kali ya mapafu, huku nchi ya DR Congo ikiongoza kuwa na wagonjwa wengi zaidi” alisema

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira kutoka Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima amesema kuwa katika kupambana na ugonjwa huo Serikali kupitia Wizara ya Afya inakabidhi vifaa vya kunawa mikono (sanitizer) lita 150 , Dispensa 30 na vifaa maalum vya kunawia mikono Mkoa  wa Songwe na mikoa yote ya mipakani kama sehemu ya kupambana na maambukizi ya ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu.

Nae, Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) amesema kuwa, vita dhidi ya ugonjwa huu ni vita inayohitaji ushirikiano na umoja baina ya watu wote katika jamii, huku akiweka wazi kuwa baadhi ya silaha za kupambana dhidi ya ugonjwa huu ni kunawa mikono kwa sabuni na maji yanayotiririka na kuepuka msongamano isiyo na ulazima.

“Tupo katika kipindi ambacho tunahitajiana sana, kila mtu kwa nafasi yake anamuhitaji mwingine, kwahiyo tushirikiane kwa pamoja tunaweza kukabiliana na ugonjwa huu, janga hili haliitaji vifaru, janga hili haliitaji jeshi la anga, janga hili linatuhitaji sisi na utayari wet utu, na nguvu pekee tulionayo ni kunawa mikono, na kuepuka misongamano isiyo yalazima, na utamaduni huu uwe endelevu”, alisema

Uhamasishaji huu unafanywa kupitia kampeni hii ya “Mikono safi, Tanzania salama” inaratibiwa na Wizara ya Afya, kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Project CLEAR kwa kushirikiana na Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) kutoka Mjomba Theatre Gallery unaendelea katika Mkoa wa Songwe, kisha kuelekea Mkoa wa Rukwa.

MWISHO.

Jumanne, 14 Aprili 2020

MADEREVA CHUKUENI TAHADHARI DHIDI YA CORONA

- Hakuna maoni
Mratibu wa kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" kutoka Wizara ya Afya Ndg. Anyitike Mwakitalima akitoa maelekezo kutoka kwa moja kati ya dereva boda boda katika eneo la kituo cha daladala cha Kabwe Jijini Mbeya ikiwa ni mwendelezo wa kampeni maalum ya uhamasishaji jamii kuchukua hatua za tahadhari dhidi ya maambukizi ugonjwa wa Corona Jijini Mbeya. 

Kondakta wa basi linalofanya safari ya Kyela akimsaidia abilia wake kutaka mikono kwa sanitizer kabla ya kuingia kwenye gari katika kituo cha mabasi Nanenane Jijini Mbeya, ili kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa Corona yasisambae kwa abilia wengine endapo yatatokea.

Mkazi wa Mbalizi Jijini Mbeya akisafisha mikono kwa maji safi yanayotiririka na sabuni kabla yakuingia dukani kufanya manunuzi ikiwa ni sehemu ya kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Corona.

Mratibu wa kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" kutoka Wizara ya Afya Ndg. Anyitike Mwakitalima akinawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka katika chuo cha MUST Jijini Mbeya, ikiwa ni sehemu ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona nchini.
Waratibu wa kampeni ya "Mikono safi, Tanzania salama" kutoka Wizara ya Afya Shirika lisilo Lakiserikali Project CLEAR na Mpoto Gallery wakitoa Elimu kwa madereva bodaboda wa Mbalizi Mbeya wakati wa kampeni maalum ya uhamasishaji jamii kuchukua hatua za tahadhari dhidi ya maambukizi ugonjwa wa Corona.

Kushoto ni Meneja wa Peter Hoteli Jijini iliyopo Jijini Mbeya, akikabidhiwa zawadi ya sabuni na vitakasa mikono (sanitizer) kutoka kwa mfanya kazi wa Shirika lisilo Lakiserikali Project CLEAR Bi Viola baada ya Waratibu wa Kampeni hiyo kutoka Wizara ya Afya kuridhishwa na hatua zinazochukuliwa na Hoteli hiyo kupambana dhidi ya ugonjwa wa Corona. 

Mkazi wa Mbalizi Jijini Mbeya aliyejishindia zawadi wa kitenge baada ya timu ya kampeni maalum ya uhamasishaji jamii kuchukua hatua za tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Corona kutoka Wizara ya Afya kumkuta akichukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo kwa kunawa mikono kwa maji safi yanayotiririka.

Timu ya kampeni maalum ya uhamasishaji jamii kuchukua hatua za tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Corona kutoka Wizara ya Afya ikiendelea na kazi ya uhamasishaji katika eneo la kituo kikuu cha mabasi ya Mkoani Jijini Mbeya ili wananchi waendelee kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Corona.


MADEREVA CHUKUENI TAHADHARI DHIDI YA CORONA

Na Rayson Mwaisemba, WAMJW- MBEYA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeendelea kuwaasa madereva wa vyombo vya usafiri kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona.

Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Kitengo cha Maji na Usafi wa Mazingira kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ndg. Anyitike Mwakitalima wakati wa uhamasishaji kwa wananchi wa kuchukua hatua za tahadhari dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Corona katika Mikoa ya Mbeya na Songwe.

Amesema kuwa, kila dereva na kondakta wake ni lazima wahakikishe gari linakuwa na vitakasa mikono (Sanitizer) kwa ajili ya matumizi yao na abiria. Aidha, vituo vyote vya mabasi viwe na sehemu za kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni kwa hii ni hatua muhimu sana ya kujikinga na virusi vya Corona. Aliyasema hayo alipotembelea Stendi Kuu ya mabasi katika Jiji la Mbeya iliyopo eneo la Nane Nane.

"Kondakta hakikisha kila anaepanda gari lako amenawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka au ametakasa mikono yake kwa Sanitizer ndio aruhusiwe kuingia kwenye gari, huu ugonjwa jamani ni hatari na umeua watu wengi" alisema.

Aidha, amewaagiza madereva na makondakta wao kuhakikisha kila siku jioni wanapokuwa wamemaliza kazi zao wahakikishe wanasafisha magari yao kwa dawa maalum aina ya Jiki, ili kuua virusi vinavyoweza kuwepo na kupelekea maambukizi ya ugonjwa wa Corona.

"Madereva na makondakta wote kila siku jioni, hakikisha mnasafisha magari yenu kwa dawa maalum, wote mnaifahamu Jiki hapa, dawa hii inatumika Kutakasa magari, bajaji au pikipiki. Changanya kipimo kimoja cha Jiki na vipimo Sita (6) vya maji ili kupata mchanganyiko unaotakiwa kisha osha chombo chako cha kusafirisha abiria, utajikinga wewe na abiria wako " alisema.

Nae, Afisa kutoka Makao Makuu Jeshi la Polisi Kamisheni ya Ushirikishaji Jamii Stafu Sajenti Valentino Ngowi, amewataka madereva bodaboda kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi endapo watakutana na mtu alieingia nchini kwa njia za panya, ikiwa ni moja ya jitihada za kupambana na ugonjwa wa Corona, huku akiwataka wasiingie katika vishawishi vya kutaka pesa ya haraka ambayo inaweza kuwagharimu wao na taifa kwa jumla.

"Sasa hivi kuna abiria wengi ambao wanaingia mkoani Mbeya kwa kupita njia za panya, na njia rahisi wanayotumia ni watu wa Bodaboda, hivyo tunawata msiingie kwenye vishawishi vya kutafuta hela ya haraka kwa kuwapitisha watu hao, jambo ambalo ni kinyume na Sheria" alisema

Mbali na hayo, Stafu Sajenti Valentino Ngowi amewataka madereva wote wa vyombo vya moto kuhakikisha wanafuata Sheria bila shurti, ikiwemo kuhakikisha abiria hawasimami kwenye magari (level seat), huku kwa upande wa Bajaj wapande abiria watatu tu.

Kampeni hii ya "Mikono safi, Tanzania salama" inaratibiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana ya Shirika lisilo la kiserikali la Oroject CLEAR. Katika kuchagiza ufikishaji wa elimu ya tahadhari dhidi ya Corona, Wizara inashirikiana na Msanii Mrisho Mpoto (Mjomba) kutoka Mjomba Theatre Gallery, ambae aliwakumbusha wakazi wa Jiji la Mbeya hususani maeneo ya Uyole, Sae, Ilomba, Mwanjelwa, Stendi Kuu, Meta, Nzovwe na Mbalizi kuzingatia unawaji wa mikono kwa maji na sabuni na vile vile kuepuka kushikana mikono na misongamano isiyokuwa na lazima. Ziara hii ya utoaji wa elimu ya tahadhari dhidi ya Corona inaendelea katika Mkoa wa Songwe ambao unapakana na nchi ya Zambia.

Mwisho.